Wanawake mnatuharibia watoto wa kiume

Wanawake mnatuharibia watoto wa kiume

Nakuelewa! ILA

Wimbi la mzazi upande mmoja linazidi kuongezeka kwa kuwa na wanaume hamtizimi wajibu wenu wa malezi.

Huyu dada maskini wapi anajua Wanaume wanalelewaje, anajikuta tu anapaki lipshine mwanae akiamini ndo mapenzi!
Wewe unayejua Unamume HAUPO!
Hata wanaoshi na watoto wao ni absent fathers, nani atafundisha watoto wenu wa kiume kuwa wanaume?
Watoto hujifunza kwa kuona matendo, wapi nyie mnaojua UANAMUME mnadisplay huo uanamume?
MTOTO ANAJIFUNZA ANACHOKIONA!
inahitaji busara na ufahamu wa tofauti sana wa mama anayeelwa tofauti ya malezi ya mtoto wa kike na wa kiume!
WANAUME MSIPOCHUKUA HATUA ZA DHATI KABISA KUONESHA MWANAUME ANAPASWA KUWAJE!
aiseeeeh msiwalaumu hawa wanawake mnaozaa nao wakiwapakia lipstick watoto wenu!
thats the best way anajiona anapendeza, anaamini na mwanae anatakiwa kupendeza hivyo!
Hebu hata kama umeachana na mamake! BE THERE for your son!
hata mamake ni mwehu, wewe USIACHE KUWA BABA KWA MTOTO WAKO!
hali ni tete!
Rai kwa kina mama
HUMKOMOI MWANAUME ULIYEZAA NAE KWA KULEA MTOTO WAKO WA KIUME KIKE.
malezi ya kiyai yai sio kumpenda mtoto!
Mwanaume ajue tu maisha ni magumu, kutafuta ni kutafuta kwa jasho, chakula hakitupwi wala hakichaguliwi, mwanaume ni kuwajibika, mwanaume ni kulinda, mwanaume ni kuprovide, mwanaume ni kuongoza. Hizi ni vitu unapaswa kumjaza mtoto wako wa kiume mapema kabisa!
Mwanaume kama ni mlinzi atatamani kujifunza ulinzi, kama mwanaume ni kutafuta ili familia ile, atajikuta hana muda wa kujiremba remba afanane na Hanna Montana!
Acha kusihi matamanio yako ya kuwa na mtoto wa kike kwa kumvalisha mtoto wako wa kiume traits za kike!
HATA KAMA UMEACHANA NA BABAKE, aseeee usiache kumkumbusha mwanao wa kiume yeye ni MWANAMUME!
Kuna kaka yako mahali, rafiki yako and stuff! hebu hakikisha huyo mtoto ana Male figure anayoitazama.

idolize hata kuhusu BABU YAKE!
msimulie nyakati baba yako alikuwa brave, msimulie kuhusu mjomba wako alivyokulipia ada!
Hupotezi kitu KUISHI NA MWANAO AKITAMBUA NAFASI YA UBABA hata kama BABA hayupo!

narudia
HUMKOMOI EX WAKO KWA KUMUONDOLEA MWANAO DHANA YA UBABA KICHWANI, tumia hata picha za wanaume mashujaa, tumia masimulizi, tumia hadithi.
Pengine ndo baba hana time, aseee tumia hata mawe, kuwe na jiwe dume na jike.
mradi mwanao ASIJIKUTE MAHALI PA KUONA KUWA WA KIKE NDIO SAHIHI na alikosewa kuwa wa kiume!

[emoji1431]comment bora kabisa
 
Mbaya zaidi mtoto wa kiume ana miaka zaidi ya nane alafu mama yake anavua Nguo mbele yake uchi wa mnyama bila mama yake hata kuna kama hilo ni kosa kinyume na maadili ya kiafrika.
 
Tabia zenu mbovu ndo zinawakimbiza akina baba katika malezi ya watoto wenu.
Katika malezi ya watoto wenu! ?? Sasa hapo unamaanisha hao watoto ni wa mwanamke pekee?

Halafu kwanini always mwanamke ndio tumuhisi mwenye makosa inapotokea kutengana? kwani hakuna wanaume wanaozingua katika ndoa zao? Tuache double standard jamani wanawake nao ni binaadamu, wanaumia kama sisi.

Mwanamke ana asili ya huruma na upendo kupitiliza, ndio maana hekima ya Mungu iliamua yeye ndiye atabeba ujauzito 9 months,
Kuhusu kulea kwa kudekeza na kubembeleza hiyo ni asili yake kabisa na sio kosa, Tangu enzi na enzi mama zetu walionesha huruma na mapenzi kuzidi baba zetu ktk familia,
Utandawazi na mambo ya kuiga ndio umeharibu mambo kwa baadhi yao, wameanza kuvuka mipaka.

Umuhimu wa baba katika malezi upo mkubwa sana na ndio maana tunatakiwa kuwa mwili mmoja ndio tuzae yaani tuoane,

Haya ya single mother kulea vibaya tunalaumu tu bure maana ni sisi wenyewe tumetoka kwenye misingi,
Mimi ni shuhuda namba moja, nimelelewa na mama pekee mimi na wadogo zangu, Mama yetu alitulea vzr sana sijaona dosari popote hata kwa wadogo zngu, wakati mwingine ni kama tunavuka mipaka tunapowaongelea hawa wanawake maana sio wote wajinga,

Baba alikimbia familia akidai anaenda tafuta maisha na hakumuaga mtu, isipokuwa ndugu zake ndio walimwambia mama hayo, akaenda dar es saalam akaoa huko na kuishi huko, aliondoka nina miaka 9 mpaka sasa nina 32, japo nilishaendaga kumchek nikamuukiza mawili matatu khs kuondoka kwake home, siku moja alinambia maisha magumu ndio sababu na akanisihi nimuombee msamaha kwa kwani anapitia magumu mengi huwenda ni kinyongo cha bimkubwa.

Sio hilo tu, kuna wamama wengi sana wanapambana kulea peke yao na watoto wanakuwa vyema tu, hapa labda ungekuwa specific kuwa unaongelea hawa pisi kali wa mjini nitakuelewa.
 
Katika malezi ya watoto wenu! ?? Sasa hapo unamaanisha hao watoto ni wa mwanamke pekee?

Halafu kwanini always mwanamke ndio tumuhisi mwenye makosa inapotokea kutengana? kwani hakuna wanaume wanaozingua katika ndoa zao? Tuache double standard jamani wanawake nao ni binaadamu, wanaumia kama sisi.

Mwanamke ana asili ya huruma na upendo kupitiliza, ndio maana hekima ya Mungu iliamua yeye ndiye atabeba ujauzito 9 months,
Kuhusu kulea kwa kudekeza na kubembeleza hiyo ni asili yake kabisa na sio kosa, Tangu enzi na enzi mama zetu walionesha huruma na mapenzi kuzidi baba zetu ktk familia,
Utandawazi na mambo ya kuiga ndio umeharibu mambo kwa baadhi yao, wameanza kuvuka mipaka.

Umuhimu wa baba katika malezi upo mkubwa sana na ndio maana tunatakiwa kuwa mwili mmoja ndio tuzae yaani tuoane,

Haya ya single mother kulea vibaya tunalaumu tu bure maana ni sisi wenyewe tumetoka kwenye misingi,
Mimi ni shuhuda namba moja, nimelelewa na mama pekee mimi na wadogo zangu, Mama yetu alitulea vzr sana sijaona dosari popote hata kwa wadogo zngu, wakati mwingine ni kama tunavuka mipaka tunapowaongelea hawa wanawake maana sio wote wajinga,

Baba alikimbia familia akidai anaenda tafuta maisha na hakumuaga mtu, isipokuwa ndugu zake ndio walimwambia mama hayo, akaenda dar es saalam akaoa huko na kuishi huko, aliondoka nina miaka 9 mpaka sasa nina 32, japo nilishaendaga kumchek nikamuukiza mawili matatu khs kuondoka kwake home, siku moja alinambia maisha magumu ndio sababu na akanisihi nimuombee msamaha kwa kwani anapitia magumu mengi huwenda ni kinyongo cha bimkubwa.

Sio hilo tu, kuna wamama wengi sana wanapambana kulea peke yao na watoto wanakuwa vyema tu, hapa labda ungekuwa specific kuwa unaongelea hawa pisi kali wa mjini nitakuelewa.
wewe na alichoeleza mtoa mada ni vitu viwili tofaut
 
Cheki toto lilivyo zuri
Screenshot_20240722-000749_Google.jpg

Screenshot_20240722-000815_Google.jpg
 
Back
Top Bottom