ITR
JF-Expert Member
- Sep 22, 2022
- 6,096
- 16,390
Kuna baadhi ya wanawake wenye tabia ya kutothamini jasho wala kuhurumia nguvu za waume zao.
Watanzania walio wengi kipato chetu ni cha kuunga unga ili kipato chako kikuwezeshe kutimiza mahitaji ya familia yako na wakati huo uweke akiba kwa ajili ya kesho kunahitaji mahesabu ya hali ya juu sana.
Mfano mwanaume unaamuwa ununue kilo 50 za mchele,mafuta lita 10, tambi box 2, ngano mfuko 1, sukari mfuko wa kg 25 na mahindi labda gunia moja. Huku matumaini yako yakiwa kuwa kwa familia yako ya watoto 2 na mkeo mahitaji hayo yatachukua miezi miwili hivyo pesa utakazo kuwa unapata wakati huo unazielekeza kwenye uwekezaji meingine kwa ajili ya familia.
Lakini cha kushangaza baada ya wiki mbili unaambiwa mahitaji yote yameisha ,kumbe ww baada ya kuleta mahitaji hayo mkeo anajigeuza masihi wa misaada mtaani kwako kwa kuwagawia mashosti na dada zake ,na mbaya zaidi hao mashosti na dada zake nao wana waume zao majumbani.
Hii tabia alikuwa nayo shemeji yangu mke wa kaka yangu na kaka alikuja kuniomba ushauri juu ya hilo lakini mm nikosa cha kumshauri kwakweli, lakini baada ya muda alikuja kumdhibiti mkewe kwa njia moja ya kimafia sijui alifundishwa na nani.
Baada ya kuona mkewe haachi hiyo tabia licha ya kumuonya ,alicho kifanya alienda sokoni akanunua gunia la viazi vitamu.
Ikawa ni mwendo wa viazi asubuhi kama chai ,mchana ugali na mboga za majani ,na usiku wanarudia viazi , walienda mwendo huo mpaka miezi 2 nakwambia mwanamke alinyooka kisawa sawa na mwanamke alipo taka kuleta fyoko alimuambia wazi kabisa kuwa kama huwezi maisha ya viazi na ugali ya kila siku mlango uko wazi inaweza ukaondoka.
Sasa brother akawa ananisimulia njia aliyo tumia kuidhibiti tabia ya shemeji kugawa gawa vitu , sasa nikamuuliza kuwa huoni hiyo njia ulikuwa una watesa watoto akiniambia maneno ambayo yalinifikirisha sana.
Akiniambia mdogo wangu siku hizi wanawake wamekuwa wakiwatumia watoto kama kinga ya kufanya mambo ya kijinga ,na wanaume wengi kwa sasa wanaishi kwa mateso ndani ya ndoa kwa sababu falisafa hiyo ya nikifanya hivi watoto watateseka.
Akaniambia kuwa saa nyingine unatakiwa kuwa mnonko kupitiliza ili uweze kuishi na mwana mke.
Watanzania walio wengi kipato chetu ni cha kuunga unga ili kipato chako kikuwezeshe kutimiza mahitaji ya familia yako na wakati huo uweke akiba kwa ajili ya kesho kunahitaji mahesabu ya hali ya juu sana.
Mfano mwanaume unaamuwa ununue kilo 50 za mchele,mafuta lita 10, tambi box 2, ngano mfuko 1, sukari mfuko wa kg 25 na mahindi labda gunia moja. Huku matumaini yako yakiwa kuwa kwa familia yako ya watoto 2 na mkeo mahitaji hayo yatachukua miezi miwili hivyo pesa utakazo kuwa unapata wakati huo unazielekeza kwenye uwekezaji meingine kwa ajili ya familia.
Lakini cha kushangaza baada ya wiki mbili unaambiwa mahitaji yote yameisha ,kumbe ww baada ya kuleta mahitaji hayo mkeo anajigeuza masihi wa misaada mtaani kwako kwa kuwagawia mashosti na dada zake ,na mbaya zaidi hao mashosti na dada zake nao wana waume zao majumbani.
Hii tabia alikuwa nayo shemeji yangu mke wa kaka yangu na kaka alikuja kuniomba ushauri juu ya hilo lakini mm nikosa cha kumshauri kwakweli, lakini baada ya muda alikuja kumdhibiti mkewe kwa njia moja ya kimafia sijui alifundishwa na nani.
Baada ya kuona mkewe haachi hiyo tabia licha ya kumuonya ,alicho kifanya alienda sokoni akanunua gunia la viazi vitamu.
Ikawa ni mwendo wa viazi asubuhi kama chai ,mchana ugali na mboga za majani ,na usiku wanarudia viazi , walienda mwendo huo mpaka miezi 2 nakwambia mwanamke alinyooka kisawa sawa na mwanamke alipo taka kuleta fyoko alimuambia wazi kabisa kuwa kama huwezi maisha ya viazi na ugali ya kila siku mlango uko wazi inaweza ukaondoka.
Sasa brother akawa ananisimulia njia aliyo tumia kuidhibiti tabia ya shemeji kugawa gawa vitu , sasa nikamuuliza kuwa huoni hiyo njia ulikuwa una watesa watoto akiniambia maneno ambayo yalinifikirisha sana.
Akiniambia mdogo wangu siku hizi wanawake wamekuwa wakiwatumia watoto kama kinga ya kufanya mambo ya kijinga ,na wanaume wengi kwa sasa wanaishi kwa mateso ndani ya ndoa kwa sababu falisafa hiyo ya nikifanya hivi watoto watateseka.
Akaniambia kuwa saa nyingine unatakiwa kuwa mnonko kupitiliza ili uweze kuishi na mwana mke.