dear lizzy kwanza hongera kwa taji la umalkia.
Pia wapo watu ambao wakifanikiwa kidogo tu wanaanza kujenga imani kuwa watu wanawaonea wivu kumbe wala watu hata hawana habari.Na kwa vile tayari umeshajijenga iman kuwa unaonewa wivu hata watu wakikukosea au kukufanyia vitu vya kuudhi utatafsiri kuwa hawanipendi sbb nimefanikiwa kuwazidi kumbe hata ungekuwa bado hujafanikiwa wangekukosea sbb kukoseana ni kawaida.
Mim naona kauli za mfano wa WANAWAKE HAWAPENDANI ni moja ya kauli nyingi zinazoonesha jinsi gani wanawake tunaonekana ni chanzo cha matatizo ktk jamii na chanzo cha kukwamisha maendeleo sbb eti tunaambiwa mwenzetu akifanikiwa tunajaribu kumrudisha nyuma badala ya kumsaidia kusonga mbele,wakati wako wanawake wengi sana wanaosaidiana.
Wapo wanaume pia ambao wana wivu mkali na mbaya kwa wao kwa wao au kwa wanawake,tena wanaume wakizidiwa kimaendeleo na mwanamke huwa wana chuki mbaya sana sbb wamejijengea akilini kwamba wao ni lazima watuzidi.Tena wanaume wanawaonea wivu hadi wanawake waliowaoa,unakuta mke akiwa na mafanikio tu kumzidi mume,mume kauli yake ya kwanza utasikia mke wangu tokea aongezwe mshahara haniheshimu tena,kuna mathread kibao juu ya hili hapa MMU.
Watu wenye kuonea wenzao wivu wapo lakini sio wanawake tu hata wanaume wenye kuonea wenzao wivu na kutopenda maendeleo ya wenzao wapo.
Wanawake tuache kudhani kuwa ukifanikiwa kidogo tu eti watu wanakuonea wivu sababu ukiwaza kuwa watu wanakuonea wivu wewe mwenyewe ndio utaanza kuwabadilikia wenzio na wenzio wakiona umebadilika nao watabadilika halafu wakibadilika akili zitakwambia "unaona sasa hivi wanaonesha wivu wao wazi wazi"