Wankyo Nyigesa, RPC Kagera: Natamani kuwa IGP, aliyepo hajafanya makosa lakini mimi nitafanya mazuri zaidi

Hii ni kali ya mwaka. Sijawahi kuona Askari anaeomba cheo kisiasa kiasi hichi.
 
 

Attachments

  • insta_23_20211203_005533.mp4
    537.3 KB
Muache mzee akaoneshe uwezo wake anajiamini.
 
Anayo kadi ya chama? Amelipia ada zote? Yule kama marehemu kada mtiifu wa CCM afande Jonathan Shana nae aliutaka sana uIGP ila ndo hivyo tena mwendo aliumaliza
 
Sio kosa kusema ndoto zake, kama ingekuwa ni kosa asingesema katumia haki yake ya kikatiba kutangaza malengo yake, kila la kheri kamanda
 
Mama alidhani Jeshi la Magereza ndio wanahujumiana kumbe na Polisi nao wamo!
 
Wameamua kumchanganya hangaya ili asimshughulikie boss wao anayeonekana kupwaya. Janja janja za kitoto.
 
Salam tosha kwa Siro,maana yake amekumbushwa tena kua ajiuzulu na ile nafasi alipewa na marehemu pasi kustahili!!!

Siro haoni tu maneno ya hadi mkulu,"geshi lijitafakari,geshi tendeni haki"
 
Mama siku moja aniote tu halafu anitamke tu niwe IGP, Mimi nitamuomba nifanye miaka mitatu halafu nimwambie Mama Mimi nakukabidhi naondoka unaonaje hapo?,"

Huyu kazua jambo
 
No matter alikuwa anatania au alikuwa siriazi ,huyu bwana maadili!!
 
Hana kosa na Sirro ni mstaafu soon kama hamjui mtulie
 
Kijeshi si kiraia
 
Inaelekea kwenye hilo jeshi kuna wengi wasiompenda. Huyu aliyetamka hadharani naamini amefanya hivyo kuwaonyesha wananchi kwamba sio wananchi tu wanaomlalamikia Sirro bali hata askari ndani ya jeshi lake lenyewe. Kulingana na mwongozo wa jeshi mwanajeshi yeyote anatakiwa atii amri ya mkuu wake. Kwa hiyo, kusema yeye anaweza kazi kuliko Sirro ni kama kusema akimpa amri hataitii.

Kwa hiyo, huyu lazima atastaafishwa au "kurudishwa makao makuu akapangiwe kazi nyingine" (Na hiyo ni ya kusoma magazeti)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…