Wapalestina wapata faraja,Saudia na Qatar wakataa mkono wa Israel

Wapalestina wapata faraja,Saudia na Qatar wakataa mkono wa Israel

Israel inarudisha maeneo yake, hao walikuwa wamiliki haramu. Saudi Arabia anazuga tu, anahitaji support ya Israel na USA kumkabili Iran. Lazima hadharani azungumze hivyo lakini moyoni anashangaa ni kwa nini wapelestina wasihamie maeneo mengine.
Sawa kila mmoja akidai maeneo ya asili yao dunia itakuwaje..
 
Saudia anajichafua mwenyewe kwa kujiondoa kwenye mikono ya rehma na kuwakumbatia maadui wa Mwenyezi Mungu.
Dah ila katika watu mwenyezi Mungu anawachukia ni Israel na wakristo...sijui walimfanya nini yani Quran nzima anawalalamikia tu dah

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa kila mmoja akidai maeneo ya asili yao dunia itakuwaje..
Kitu kigumu sana ila wanasiasa wakishindwa silaha zote hutumia hii.Nionavyo yule anayemiliki sasa na umiliki wake haukuwa wa kudhulumu basi ndiye mwenyewe na asiguswe.Inasemekana waisrael waliwahadaa kwa pesa wapalestina mwaka 1947 wakiwa na ajenda ya muda mrefu mbele wakanunua halafu wakajitanua.Sawa nawaendelee hapo.Lakini hii ya sasa wanachukua kwa nguvu na kujenga kwa nguvu kila binadamu lazima aipinge na awe upande wa Palestina.
 
Dah ila katika watu mwenyezi Mungu anawachukia ni Israel na wakristo...sijui walimfanya nini yani Quran nzima anawalalamikia tu dah

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio kweli,kwanza Qur'an haikuteteremshwa kuwalalamikia wakristo na waisrael na wala hawakutajwa kwa majina hayo.Waliotajwa ni wale wenye tabia ambazo wakristo na waisrael wa sasa kwa kupotea kwao wanazifanya.Na huko si kuwachukia lakini ni kuwaongoa kwa ajili ya kuwaepusha na adhabu iumizayo na ya milele ambapo hizi adhabu Mwenyezi Mungu amezirudia rudia mara nyingi kwa usisitizo.
Ukishindwa kuelewa na ukastahiki adhabu hizo usimlaumu Mwenyezi Mungu kwa kiburi chako.
 
Kitu kigumu sana ila wanasiasa wakishindwa silaha zote hutumia hii.Nionavyo yule anayemiliki sasa na umiliki wake haukuwa wa kudhulumu basi ndiye mwenyewe na asiguswe.Inasemekana waisrael waliwahadaa kwa pesa wapalestina mwaka 1947 wakiwa na ajenda ya muda mrefu mbele wakanunua halafu wakajitanua.Sawa nawaendelee hapo.Lakini hii ya sasa wanachukua kwa nguvu na kujenga kwa nguvu kila binadamu lazima aipinge na awe upande wa Palestina.
Histori ya unyanganyi wa ardhi ya palestina kwenda kwa wazungu wa ulaya, Ethiopia Russia , uk, us nk..imeanza mwaka 1917 kwa kiitwacho bafour declaration ..
Wapalestina kupewa rushwa kuiachia ardhi yao Ni jipya.
 
Sio kweli,kwanza Qur'an haikuteteremshwa kuwalalamikia wakristo na waisrael na wala hawakutajwa kwa majina hayo.Waliotajwa ni wale wenye tabia ambazo wakristo na waisrael wa sasa kwa kupotea kwao wanazifanya.Na huko si kuwachukia lakini ni kuwaongoa kwa ajili ya kuwaepusha na adhabu iumizayo na ya milele ambapo hizi adhabu Mwenyezi Mungu amezirudia rudia mara nyingi kwa usisitizo.
Ukishindwa kuelewa na ukastahiki adhabu hizo usimlaumu Mwenyezi Mungu kwa kiburi chako.
Quran 9:30. Na Mayahudi wanasema: Uzeir ni mwana wa Mungu. Na Wakristo wanasema: Masihi ni mwana wa Mungu. Hiyo ndiyo kauli yao kwa vinywa vyao. Wanayaiga maneno ya walio kufuru kabla yao. Mwenyezi Mungu awaangamize! Wanageuzwa namna gani hawa! 30

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Saudia anajichafua mwenyewe kwa kujiondoa kwenye mikono ya rehma na kuwakumbatia maadui wa Mwenyezi Mungu.
Dini zinzwadumaza san uwezo wa kufikiri.mwenye nguvu atasavaivu yule dhaifu atakuwa erased.hii ni kanuni inayoishi ktk nyanja zote za maisha.
 
Mwanamfalme mwengine leo ametoa kauli kali zaidi kuipasha Israel na haijawahi kutokea.Wale wanaosema Saudia ni wanafiki leo inabidi wajiulize upya.
Huyu ni yule mwanadiplomasia na muwakilishi wa Saudi Arabia kwa miaka mingi .Ni Turk Al Faisal kwenye kongamano lililofanyika Manama mji mkuu wa Bahrain.Waziri wa mambo ya nje wa Israel hakutarajia mashambulizi kama hayo akabaki kuduwaa na alipojaribu kujibu Turk akambamiza tena.
Alianza kwa kusema Israel inajigamba kama ni mpenda haki mkubwa kinyume na ukweli kwamba wamewafanya wapalestina waishi kama koloni lao. Wamewalazimisha wapalestina waishi kwenye maisha ya kambi za mateso kwa kisingizio cha kipuuzi kuhusu kitisho cha usalama.Wazee kwa vijana,wake kwa waume wanaozeana humo bila kujua kosa lao.Israel wanavunja majumba yao kama wapendavyo na kumuua yeyote wanayemtaka.
Mwanamfalme Turk akaendeleza mashambulizi kwa kusema Israel ina zana za nyukia ambazo haitaki kuzitangaza na huku ikitumia wanasiasa walio chini yake na mitandao yake ya kueneza habari ikiishutumu Saudia na baadhi ya misimamo yake.
Baada ya hapo akasema Saudi bado imeshikamana na maazimio ya siku za nyuma yanayotaka kuwepo kwa taifa la Palestina na Israel irudi kwenye mipaka yake kabla ya mwaka 1967.Akasema huwezi kutibu donda linalochirizika damu kwa kutumia dawa za kuuwa maumivu.
Waziri wa mambo ya nje wa Israel Gabi Ashkenazi alipofuatia kuzungumza akasikitishwa na matamshi ya Turk Alfaisal na kusema mashambulizi yake hayaendani na mabadiliko yanayotokea sasa hivi katika mashariki ya kati na akaendeleza lawama kwa wapalestina kwamba ndio kikwazo cha kufikiwa makubaliano ya amani.Akajigamba kwamba katika hali hiyo kuna uchaguzi jee yapatikane makubaliano au tuendeleze mchezo wa kulaumiana.Naye Dore Gold mwakilishi mwengine wa Benjamin Netanyahu katika mkutano huo akasema shutuma za mwanamfalme Turk ni za kizamani na nyingi si za kweli.Kauli hiyo ikazidi kumpandisha hasira Turk na kwa kukumbushiia mahojiano ya televisheni ya zamani akasema Dore Gold anaatkiwa awe mtu wa mwisho kuzungumzia misimamo ya zamani.
Mwanamfalme Turk ameshikilia nafasi ya mkuu wa usalama wa Saudia kwa miaka mingi na kuwa balozi wa nchi hiyo Marekani na Uiengereza kwa nyakati tofauti ambaye kwa sasa hana cheo maalum.Mawazo yake yanasemekana ndiyo msimamo wa mfalme wa nchi hiyo yaliyodhidi ya mrithi wa mfalme Mohammed bin Suleiman ambaye ni mtoto wake.

1607280249255.png



 
Back
Top Bottom