Wapangaji AICC Arusha wapewa notisi ya kuhama ndani ya Siku 90

Wapangaji AICC Arusha wapewa notisi ya kuhama ndani ya Siku 90

Mtoa Taarifa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2024
Posts
213
Reaction score
671
Kituo cha Mikutano ya Kimataifa Arusha (AICC) kimeingia kwenye mgogoro mkubwa na wapangaji wake zaidi ya 450 baada ya kuwapatia notisi ya kutakiwa kuhama katika nyumba zao ndani ya siku 60 hadi 90.

Wapangaji hao walioishi ndani ya nyumba hizo zilizoko eneo la Kijenge jijini Arusha kwa zaidi ya miaka 40, wamedai kuwa hawatahama katika nyumba hizo kwa sababu ya muda waliopatiwa ni mdogo huku wakidai AICC haijawatendea haki.

Mwananchi imezungumza na Assah Mwambene ambaye ni Ofisa Uhusiano wa AICC na amethibitisha kuwa taarifa za wapangaji hao kutakiwa kuhama ni za kweli.

Mwambene amesema AICC imeshawakabidhi barua za notisi wapangaji wote ikiwataka kuhama ndani ya siku 60 mpaka 90 kupisha eneo hilo kwa ajili ya uwekezaji mpya.

MWANANCHI
 
Una panga town kwa tzsh 50000 ata me nisinge hama
Tena hy 50000 n nyingi sana unaweza kukuta wanalipa 15000 kwa mwezi, mm nilikuwa naishi daraja mbili Arusha, kata ya themi karibu na shule ya sekondari na msingi ya themi kulikuwa na nyumba za serikali wapangaji walikuwa wanalipa 20000 kwa mwezi zilibomolewa 2013 ardhi ikawa mali za shule.
 
Una panga town kwa tzsh 50000 ata me nisinge hama
Hizo nyumba unakuta hata wapangaji original aka wa awali hawapo au wametangulia mbele za haki na wengine wazee mno.,...niliwahi kuishi NHC yaani watu walikuwa wanabadilishana mpaka mara ya mwisho dada yangu akainunua nyumba wakati mkataba wa awali ulikuwa wa mzazi wetu alafu Kodi kitonga bei ya apartment nusu kwa mtu aliepanga chumba na sebule
 
Yaani Miaka 40 umepanga tu nyumba ya mtu🤔
Wajukuu wana-enyoy tu, hizo nyumba wanarithishana na of course kama Kodi inalipwa wala hawahangaiki kuwatoa (zamani kulikuwa na uungwana though siku hizi huwa wanapita pita maana wengine wamepangisha nyumba hizo kama zao)
 
Assah Mwambene kutoka Ikulu enzi ya JK mpaka AICC, kweli maisha ni kama gwaride
Sio alikuwa Mkurugenzi wa Idara Habari Maelezo akapelekwa Wizara ya Mambo ya Nje......ila mkwanja upo palepale labda posho inaweza ikawa mgogoro kutokana yupo kwenye taasisi ambayo ipo specific kwenye eneo maalumu tofauti na maelezo ilikuwa ni Kwa nchi nzima
 
Back
Top Bottom