Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,750
- Thread starter
- #121
MAELFU ya wanchi wa Kisiwa cha Pemba, wametishia kuwa kesho kutwa wataanza kujisalimisha katika vituo mbalimbali vya polisi nchini, kushinikiza wazee saba waliopeleka barua Umoja wa Mataifa (UN) kuomba kisiwa hicho kiwe na serikali yake, wafutiwe mashtaka ya uhaini.
Wananchi hao ambao wanaunga mkono harakati zilizoanzishwa na wazee hao, wanatarajiwa kujisalimisha katika vituo ambavyo wazee hao wamekuwa wakiripoti baada ya kuamriwa na polisi kufanya hivyo kila Alhamisi.
Amri hiyo ilitolewa na polisi baada ya wazee hao, kukamatwa na kushikiliwa kwa siku tano katika vituo tofauti vya polisi kwa tuhuma za uhaini.
Katibu wa Wazee hao, Hamad Ali Mussa, alithibitisha suala hilo na kuvitaja vituo ambavyo wananchi hao wanatarajiwa kujisalimisha keshokutwa, kuwa ni pamoja na Makao Makuu ya Polisi, yaliyoko Madungu, Mkoa wa Kusini na Makao Makuu ya Kilimandege, yaliyoko Wete, Mkoa wa Kaskazini, kisiwani humo.
Hamad ambaye alizungumza na mwandishi katika ofisi za gazeti hili jana alisema, watu hao ni miongoni mwa wananchi waliojiorodhesha na kuweka saini zao kwenye barua na nyaraka walizozipeleka UN.
''Tunachowaomba polisi wasiwaue tu, kwa sababu baadhi ya watu siku hiyo watakwenda katika vituo polisi na watoto wao wachanga,'' alisema Hamad.
Alisema uamuzi huo umefikiwa, kwa vile 'kosa' linalodaiwa kutendwa na wazee waliokamatwa, lilikuwa ni maelekezo waliyopewa na wananchi hao.
Alisema wanapinga amri ya kuwataka wazee hao kuendelea kuripoti polisi kila Alhamisi, kwa sababu kosa wanalotuhumiwa kulitenda halipo.
Naye Dk Gharib ambaye ni mmoja wa wazee waliokamatwa alisema, mbali mateso mengi waliyoyapata walipokuwa wakishikiliwa kwa siku tano mfululizo, walinyang'anywa pasi zao za kusafiria pamoja na vitambulisho vingine.
Wananchi hao ambao wanaunga mkono harakati zilizoanzishwa na wazee hao, wanatarajiwa kujisalimisha katika vituo ambavyo wazee hao wamekuwa wakiripoti baada ya kuamriwa na polisi kufanya hivyo kila Alhamisi.
Amri hiyo ilitolewa na polisi baada ya wazee hao, kukamatwa na kushikiliwa kwa siku tano katika vituo tofauti vya polisi kwa tuhuma za uhaini.
Katibu wa Wazee hao, Hamad Ali Mussa, alithibitisha suala hilo na kuvitaja vituo ambavyo wananchi hao wanatarajiwa kujisalimisha keshokutwa, kuwa ni pamoja na Makao Makuu ya Polisi, yaliyoko Madungu, Mkoa wa Kusini na Makao Makuu ya Kilimandege, yaliyoko Wete, Mkoa wa Kaskazini, kisiwani humo.
Hamad ambaye alizungumza na mwandishi katika ofisi za gazeti hili jana alisema, watu hao ni miongoni mwa wananchi waliojiorodhesha na kuweka saini zao kwenye barua na nyaraka walizozipeleka UN.
''Tunachowaomba polisi wasiwaue tu, kwa sababu baadhi ya watu siku hiyo watakwenda katika vituo polisi na watoto wao wachanga,'' alisema Hamad.
Alisema uamuzi huo umefikiwa, kwa vile 'kosa' linalodaiwa kutendwa na wazee waliokamatwa, lilikuwa ni maelekezo waliyopewa na wananchi hao.
Alisema wanapinga amri ya kuwataka wazee hao kuendelea kuripoti polisi kila Alhamisi, kwa sababu kosa wanalotuhumiwa kulitenda halipo.
Naye Dk Gharib ambaye ni mmoja wa wazee waliokamatwa alisema, mbali mateso mengi waliyoyapata walipokuwa wakishikiliwa kwa siku tano mfululizo, walinyang'anywa pasi zao za kusafiria pamoja na vitambulisho vingine.