Wapemba Waanza Kukamatwa

Wapemba Waanza Kukamatwa

Kukamata watu usiku wa manane kwa vile tu ni wafuasi wa CUF au kwa vile wanatokea visiwa vya pemba ni ufashisti kama wa Hitler and CCM should know better.
 
Mimi naomba kwa Serikali kutafuta suluhu na muafaka.Kuondoa ubaguzi ni mojawapo ya kuwafanya nao waonekane kuwa ni Wazanzibari au Watanzania halisi.

Wapemba wamebaguliwa tangu enzi za Sultani hadi mapinduzi.Wanadharauliwa nchi nzima na kubaguliwa katika nyanja mbalimbali.

Kama Kikwete ana nia nzuri inabidi ku address suala la Pemba kwa diplomasia ya hali ya juu kwa sababau kamata kamata inaharibu sifa ya nchi yetu.Mojawapo ya urithi ambao anaweza kutuachia baada ya uongozi wake katika nchi hii na Afrika nzima ni kuleta amani ya kweli Zanzibar.

Matatizo ya Zanzibar ni matatizo ya Tanzania.
Wewe nawe Mheshimiwa. Hivi unaposema Wapemba huwa una maana gani? Wapemba katika ujumla wao au Wapemba unaowapenda wewe? Hivi wewe hujapata kuwaona Wapemba walioshika nafasi kubwa tu za uongozi katika Nchi yetu? Waliokuwa Mabalozi? waliopo katika nafasi za |Utaalamu? Waliopo kufundisha mashuleni. Waliopo wanaotibu wananchi wenzao., Hivi wewe unamaanisha Wapemba gani hao? Unaowalilia? Hivi na sisi tumo humo? Maana na sisi pia tunayo nasaba ya Pemba.
 
Kukamata watu usiku wa manane kwa vile tu ni wafuasi wa CUF au kwa vile wanatokea visiwa vya pemba ni ufashisti kama wa Hitler and CCM should know better.

Ah Bi sho we. Sasa mtu akifanya vitendo vya uhaini umpigie dandaro au mahumbwa acheze au umsogezee mipasho asikilize? Waache wapate funzo.
 
386px-Zanzibaro%2C_divido.png

Kama Pemba wanalia kiasi hicho Tumbatu watakuwa nafanya nini..?
 
Ah Bi sho we. Sasa mtu akifanya vitendo vya uhaini umpigie dandaro au mahumbwa acheze au umsogezee mipasho asikilize? Waache wapate funzo.

Funzo? Hivi hata swala watu wanafanya za nini kama wamejaa mioyo ya chuki namna hii dhidi ya wenzio?
 
Funzo? Hivi hata swala watu wanafanya za nini kama wamejaa mioyo ya chuki namna hii dhidi ya wenzio?

mwafrika wa kike nadhani unapoteza muda kubishana na hawa wabaguzi ambao wanajiona wao ndio wana thamani na haki zote kwenye jamii kuliko raia wengine. Nadhani wengi wetu tunajua bughudha na manyanyaso wanayopata wapemba kutokana tu na uamuzi wao wa kuikataa CCM kwa nguvu zote. Maneno ya hawa vibaraka wachache wa CCM hayawezi kutuzuia kuongea ukweli kuhusiana na uvunjwaji mkubwa wa haki za binadamu unaoendelea kule Pemba. Mapambano ya kudai haki za wapemba yaendelee.
 
kwi kwi kwi.... kama wameshindwa kumkamata Chenge na Rostam Azizi basi inaonekana hicho kifua mbele kinatokana na kikohozi cha kifua kikuu na sio kupigwa ngumi mgongoni....

Kwa kweli sioni kama hawa Usalama wa Taifa unania nzuri na Serikali ya Kikwete ila inawezekana kabisa ndani ya huu usalama wa Taifa wamo vitimba kwiri ambao bado wanatumiliwa na mafisadi ili kumpaka matope Muungwana na serikali yake ,kama ni mbinu za kumwangusha kitaifa na kimataifa ndio zimeanza ,maana mafisadi wameapa kula sahani moja na Kikwete wakihakikisha kuwa havuki tena na kuendelea na ngwe ya miaka mitano iliyobakia. Na mbinu zipo za aina nyingi za kumchafua huwezi kujua.
Sasa Wapemba wanajitayarisha kuelekea vituo vyote vya polisi ili wakamatwe ili kuonyesha mshikamano na wenzao hao wanasema kubwa lijalo na itakuwa ni kibarua cha kila siku ilivyokuwa hawana kazi za kufanya.
 
Kwa kweli sioni kama hawa Usalama wa Taifa unania nzuri na Serikali ya Kikwete ila inawezekana kabisa ndani ya huu usalama wa Taifa wamo vitimba kwiri ambao bado wanatumiliwa na mafisadi ili kumpaka matope Muungwana na serikali yake ,kama ni mbinu za kumwangusha kitaifa na kimataifa ndio zimeanza ,maana mafisadi wameapa kula sahani moja na Kikwete wakihakikisha kuwa havuki tena na kuendelea na ngwe ya miaka mitano iliyobakia. Na mbinu zipo za aina nyingi za kumchafua huwezi kujua.
Sasa Wapemba wanajitayarisha kuelekea vituo vyote vya polisi ili wakamatwe ili kuonyesha mshikamano na wenzao hao wanasema kubwa lijalo na itakuwa ni kibarua cha kila siku ilivyokuwa hawana kazi za kufanya.

Hiyo itakuwa rasmi. Kwani Polisi nao watapata kazi ya kufanya, siyo kuweka nne tu kila siku.
 
Ah Bi sho we. Sasa mtu akifanya vitendo vya uhaini umpigie dandaro au mahumbwa acheze au umsogezee mipasho asikilize? Waache wapate funzo.

Sabri-bachani, japokuwa wewe huonyeshi kutoa hiki kitu, bado nina wajibu wa kuanza kwa kusema -heshima mbele.

Naomba kupinga kwa damu chemfu wazo lako kuhusu kuwapa funzo wahaini.

Twende taratibu. Kuna msingi mmoja wa kuendesha jamii, wa kuendesha nchi, unaitwa kizungu Due Process. Tumejaribu kuuiga kutoka kwa Waingereza ambako tulichukua sheria yetu ya Common Law.

Huu Utaratibu Stahili unasema kwamba raia ana haki ambazo zinabidi zifuatwe wakati anapo nyang'anywa uhuru, mali na maisha, ili kuhakikisha kwamba inatendeka haki na usawa. Moja ya uhalalisho wa huu utaratibu ni msingi mwingine wa haki unaitwa 'Haki Asili.' Kwamba bila hata kujiuliza mara tatu tatu, au kuwa na stashahada ya Sheria, unaweza kung'amua kwamba ukimhukumu mtu aliyesingiziwa makosa wakati kumbe si kweli alitenda makosa hiyo si sahihi. Ndio Haki Asili hiyo inayozaa Utaratibu Stahili. Moja ya mifano ya kwanza ya huo msingi wa Utaratibu Stahili ni kwamba huna hatia mpaka upatikane na hatia. Kudhaniwa hatia sio hatia. Kushutumiwa sio hatia. Hata kukamatwa makosani sio hatia mpaka upatikane na hatia katika utaratibu stahili.

Pia huwezi kamatwa bila shuku ya msingi. Mara nyingi yabidi umsomeshe hakimu akupe kibali kukuruhusu kumkamata unaye mdhania mkosaji. Na unapokamatwa yapasa uambiwe umekamatiwa nini ndani ya muda fulani wa kukamatwa, na usomewe mashitaka.

Pasipo hivyo, siku nikiwa na fitina na wewe, labda kwa jinsi ya lugha unayo tumia, au kwa sababu umemwangalia vibaya mme wangu, halafu na mimi nina nguvu fulani, labda polisi, au Hakimu, basi ninaweza nikasema wewe mhaini halafu nikakumaliza kwa fitina nyingine tu. Utaratibu Stahili na Haki Asili vinajikunja hilo likifanyika.

Sabri-bachani, hiyo ndio jamii tunayo jaribu, au tunayo takiwa tujaribu, kuijenga.

Wadhani jamii hiyo yafaa?
 
Lakini, mimi ninachojua ni kwamba, wapemba wanaotaka kujitenga wanatapatapa tu. hawataweza. nafikiri JK akiona mambo yanaenda namna hii,bora awe tu dictator. wewe jamaa unaesema selikali iko kama toiletpaper, hauna adabu.mimi sio mwana ccm lakini sipendezewi na manano ya mtu asokuwa na akili kama wewe. ILA, PEMBA WAJIFUNZE KWA MUHAMAD BAKAR. WA ANJOUN. ni sisi wenyewe tulienda kule kukomboa kile kisiwa. sasa wapemba wasijefikiri tutawaacha wao walete ujinga wao. Naomba kikwete awashughulikie kikamilifu,ndani ya sheria, hawa wahaini. chapa fimbo, hata wakijilipua na mabom,waache wajilipue tu, watachoka na watanyamaza wenyewe. period.

Bwana mdogo Kidzogolae kumbe wewe bado kinda hujui maana ya mapambano!Hakuna wa kuwasimamisha wapemba wakianza mapambano na hayataishia visiwani kama unavofikiri wewe bali tanzania nzima na yatakua ni mapamabano ya kujikomboa,tafadhali ndugu yangu ujue kwamba amani yapatikana kwa gharama kubwa blood is purification liquid ma daer!!.Na kumbuka wataanza pemba baaadae Bara ,damu ya binadamu ndivo ilivo!
 
nyuma ya tukio hili kuna chama cha CUF, hivi ni sawa wengine waumie kwa maslahi ya wachache?

wanachafua hali ya hewa kwa manufaa binafsi? huwageuzA kila siku wenzao ni kafara
 
nyuma ya hili kuna CUF kivipi wakati wenyewe wamesema kuwa halijahusiana na chama?
isitoshe, kila kitakachofanywa na mwananchi wa pemba basi ni rahisi kudhaniwa kuwa linahusiana na cuf kwa vile wananchi wa pemba takriban 99% ni wafuasi wa cuf.
kukamatwa saa sita usiku kwa vishindo hakukuwa na sababu ya msingi, kama imelazimika na wangewakamata mchana.
kwanza mohamed seif khatib kachemsha kuwafananisha wao na wa comoro kwa vile hawa wametumia njia za utaratibu kudai haki yao, na kwenda katika chombo kinachofaa pia.
kivipi wanafanana na comoro?
 
walipohojiwa wamethibitisha kuwa wamefadhiliwa nauli na pesa za chakula na malazi na wabunge na wawakilishi wa CUF nnaamini si muda MREFU UKWELI UTAJULIKANA.

kama wao vidume wASIMAME WENYEWE WASISIMAME KWA MIGUU YA WANYONGE
 
Lakini, mimi ninachojua ni kwamba, wapemba wanaotaka kujitenga wanatapatapa tu. hawataweza. nafikiri JK akiona mambo yanaenda namna hii,bora awe tu dictator. wewe jamaa unaesema selikali iko kama toiletpaper, hauna adabu.mimi sio mwana ccm lakini sipendezewi na manano ya mtu asokuwa na akili kama wewe. ILA, PEMBA WAJIFUNZE KWA MUHAMAD BAKAR. WA ANJOUN. ni sisi wenyewe tulienda kule kukomboa kile kisiwa. sasa wapemba wasijefikiri tutawaacha wao walete ujinga wao. Naomba kikwete awashughulikie kikamilifu,ndani ya sheria, hawa wahaini. chapa fimbo, hata wakijilipua na mabom,waache wajilipue tu, watachoka na watanyamaza wenyewe. period.

That sound exactly like CCM political analyst, fear and fear. Wewe unacho jali ni kutishia watu kwamba wachapwe viboko, sijui wafanywa nini. Kwani kuna ubaya gani wa kuwasikiliza maombi yao, Tanzania si nchi ya demokrasia bwana, tuwasikilize wapemba kwa nini wanataka kuwa nchi huru.

Kama wana qualify kuwa nchi huru, why not kuwaruhusu?
 
That sound exactly like CCM political analyst, fear and fear. Wewe unacho jali ni kutishia watu kwamba wachapwe viboko, sijui wafanywa nini. Kwani kuna ubaya gani wa kuwasikiliza maombi yao, Tanzania si nchi ya demokrasia bwana, tuwasikilize wapemba kwa nini wanataka kuwa nchi huru.

Kama wana qualify kuwa nchi huru, why not kuwaruhusu?

Baada ya Pemba, Kuna Kigoma, Mtwara, Mafia, n.k Wanadai kujitenga na Unguja kwani waliunganishwa lini?
 
Baada ya Pemba, Kuna Kigoma, Mtwara, Mafia, n.k Wanadai kujitenga na Unguja kwani waliunganishwa lini?

Cha muhimu sio kukataza watu wasilete hoja zao za msingi, cha muhimu ni kuangalia wapi kuna tatizo then kutafuta binding solution ya tatizo. Pemba matatizo yao hayafanani na kigoma wala songea wala mafia.

Hawa watu wa pemba hawana muwakilishi hata mmoja kwenye serikali ya mapinduzi zanzibar, wananchi wa pemba wanafanywa kama si raia wa Tanzania. Imagine supply ya maji imefanywa na wasamalia wema, sasa wewe unataka wafanye nini?

Kumbuka kwa miaka 15 sasa Pemba wapo kwenye kapu, hawana pa kukimbilia. Tumesikia miafaka kibao imeandaliwa na haijasaida, kuanzia wa yule mnageria sijui chief nani anyauku mpaka wa JK wa sasa. Sasa kama CCM wameshindwa kusolve mpasuko jee ni nini solution yake?
 
Wapemba wapatao kumi wanaoshikiliwa mahali pasipojulikana na wanausalama wameonesha ujasiri mkubwa kwa kitendo cha kupeleka barua ofisi za UN kuomba Pemba ijitenge. Nasema ni majasiri kwa vile hawakuogopa vitisho bali walilifanya jambo wanaloliamini bila kulazimishwa na mtu.

Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na malalamiko kutoka pande mbili za muungano kutokana na mambo ambayo pande zote zinaona si sawa. Watawala wamekuwa wakilazimisha watanzania waamini kwamba matatizo ya muungano ni madogo tu na yatashughulikiwa. Hatahivyo, imedhihirika kwamba hakuna dhamira ya dhati katika kushghulikia mapungufu hayo ya muungano wetu. Watanzania wengi hawaoni umuhimu wa muungano bali wanaona matatizo zaidi na Hapa kuna tatizo kubwa. Kwa muda mrefu sasa hakuna aliyeweza kusimama na kuonesha dunia kwamba kuna matatizo bali wengi husema chini chini tu.

Waasisi wa Taifa hili waliunganisha nchi hizi mbili lakini bila kushirikisha wananchi. Ilipasa kupata ridhaa ya wananchi wa pande zote mbili lakini hili halikufanyika hadi leo. Baada ya miaka yote hii ya muungano serikali ilitakiwa ichukue hatua madhubuti ama kuimarisha muungano au kuuvunja lakini hakuna juhudi za makusudi zilizofanyika hadi mwaka 2006 rais Kikwete alipojaribu kwa kuunda wizara ya muungano. Kwa mtazamo wangu nadhani hili lilipaswa lifanyike miongo miwili iliyopita.

Kitendo cha wananchi kufikia hatua ya kufunga safari hadi ofisi za UN Dar si cha kuchukuliwa juu juu. Wala si cha kutumia mabavu kuzima hisia za watu hao kwa sababu hii ni sampuli ndogo tu ya watu wenye msimamo kama huo. Ni wakati sasa tuwe na mjadala wa kitaifa kuhusu suala la muungano. Tanzania inapaswa kukabiliana na changamoto uso kwa uso na sio kuzikimbia au kutafuta njia za mkato kama kuwatisha wananchi waliomua kuzielezea hisia zao wazi.

Naomba kuwasilisha hoja
 
Hii tabia ya kujenga matabaka ya kimajimbo, kimkoa kiwilaya, katika kuwaletea maendeleo wananchi hilo ndiyo jibu lake. Kuna wakati utafika wilaya zitataka kujitenga na mikoa yao.
 
Back
Top Bottom