Muwe makini pia mtakao enda kununua msije pigwa mkaja kulalamika huku jf
Ushauri kwa ambaye atavutiwa katika hilo dili hakikisha una servilance ya kutosha na hata uwe na tails kibao au ma sniper , hii biashara kwetu sisi haina tofauti na zile biashara za ngada.. Point ni kwamba hutakiwi kuamini hata kama utapewa pesa mpaka vyote vi balance.
Lazima useme hivyo sababu hujawahi kuishika na wala hujui inapatikana katika mazingira gani kwa utaratibu upi yaani kwa ufupi You know nothing...... Tunazungumzia Ruby umeshaingiza na mambo ya rupia. Kuna mwingine ukikwambia mambo ya rupia anakuambia hivyo vitu havipo ni hadithi tu so tunatofautiana ufahamu katika mambo mengi. Jukumu la kuamini ama kutokuamini ni la kwako msomaji hujashikiwa bastola ukubaliane na hoja hii and vice versa
Kaka unadhani biashara hii inafanyikaje?? Unaamini kuwa madini haya yapo na yanafanyiwa biashara??Ni bishara ya kimafia ? Je kitu cha m10 unaweza fanyia mkononi? Beware
Kwa dhana hii ni wazi nina kazi kubwa sana kuhakikisha kama madini haya ni yenyewe nayauza!!Umemshauri vizuri sana Kiongozi maana hii biashara sitakagi kuisikia tena maishani mwangu!!
Amani kwenu wadau wa biashara.
Ndugu zangu huko kijijini wamefanikiwa kuchimba madini ya ruby kwa walivyo niambia, yanakadiriwa kufikia robo tatu ya KG. Ila hawajui wapi wayauze na pia hawana vibali vya uchimbaji maana kwa uwezo wao hawawezi kuwa nao. Pia natambua utata wa kisheria uliopo juu ya umiliki wa madini. maana kwa sheria ya madini iliyopitishwa miaka michache iliyopita hata ukiokota madini uko kwenye kosa kisheria.
Naomba msaada wenu, ni wapi ndugu zangu hawa wanaweza kuuza madini yao kisheria na walipe kodi huku wakipata stahili zao bila kupunjwa??
Nimepitia mitandaoni na kupata bei za kimataifa na inaonesha madini haya yanathamani si haba.... Ila ni wapi wanapoweza kuuza na wasikutana na matatizo ya kisheria?? ni kipi wafanye??
Naweza kuwa nimechanganya madesa katika uandishi wa hoja yangu.... Nisameheni!! Ila dhamira yangu ni kuwasaidia ndugu zangu hawa wasije uza at black market au wakayauza kwa bei ya hovyo kama wazee wetu wakati wa ukoloni walipobadilisha kwa shanga!!
nategemea majibu yatayonisaidia.
Bro hivi akili zako zinafanya kazi?? Unatuhumu na kutoa hukumu. stu pid kabisa.... we umeona mimi nimeomba nini?? Ji.nga kweli wewe. Unanijua mimi na unahakika gani kuwa natapeli??Acha utapeli , nyie ndo mnatafuta wa kuwapiga unajua rubb wew , ngoja nimshtue mod . Maana mmezoea kutapeli watu kwenye JF
Kaka unadhani biashara hii inafanyikaje?? Unaamini kuwa madini haya yapo na yanafanyiwa biashara??
Ndugu wanajamii forum huyu jamaa ni tapeli kuweni makini na hawa matapeli kuna siku alikuja humu eti anauza Green tomalin eti akanieleza ana nusu kiroba kitu ambacho sio rahisi kupata hata gram 300 ni shida. baada ya kumbana jamaa akapotea maana mimi ni mtaalam wa hayo madude
Hicho ndicho nachotaka kusubiri nikione.... Na pia kwakuwa si mimi wala wao wanaojua ruby yenye quality ni ipi ndipo hapo ugumu unapokuja.Biashara ya madini haitaki kuambiwa kitu ambacho hujakiona. Jamaa wa vijijini wepesi sana kusema wana mawe ukija yaona unakuta ni uchafu.. Makapshon yaliyoziba kabsaa au hata sio ruby.
Kwa kiasi cha Ruby waliyosema wanayo 3/4 kgs bila kupepesa macho na utakuja nithibitishia hapa sio Gem quality.. Hzo wakijitahidi sana ni kapshon na sio high.
Pocket ya Ruby inaweza ikawa na kilo 100 lakini ukaotea kaGem quality 0.8grams tuu au usipate kabisa.
.......
Ahsante kwa ushauri wakotunduru utauza maana ndiko watu wanakochimba na kuuza.kuna wa sri lanka wengi sana wanao nunua
Sijawekeza hata senti... waliochimba ni ndugu zangu wa ukoo... wameniomba niwasaidie katika mchakato wa kuyauza na nitakuwa nao kila hatua mpaka watapoyauza.Halahala usiwekeza hata senti moja katika biashara hiyo.
Kama huna uzoefu nayo huku ukitegemea Wataalam wa JF.
Usije-sema hukuonywa!