Wapi nikachangamkie fursa ya mazao kipind hiki cha uhaba wa chakula nchini.

Wapi nikachangamkie fursa ya mazao kipind hiki cha uhaba wa chakula nchini.

bwana rene jr huko songea mvua zilishakata na watu wamevuna tayari maanake kwa dar mvua zinarindima sana sasa sijui huko vipi maanake mimi nilikuwa napiga hesabu nijikusanye mwezi huu na wa sita wote kisha niingie kwenye hii biashara au nitakuwa nimepishana na nyakati na nauliza vipi siwezi kuifanya hii biz kuanzia mwezi wa saba au mambo yatakuwa yamebadilika sana ushauri wako plz niko serious na hii mambo nishawasumbua sumbua sana wadau fulani fulani kwa pm humu ila namshukuru huyu bwana napoleone kwa kuleta uzi kabisaa na wadau wameuchangia
Mvua zilishakata mkuu, wakulima wameshaanza kuvuna.
 
mkubwa nikushukuru kwa kuchangia lakini kaka tunaomba ungetutajia maeneo yenyewe kabisa maana kagera ni kubwa alaf na bei za huko kuhusu bei za masoko hizo wadau tunaweza tu kuzitafuta
Leo hii nimefika hapa Kyerwa Maharage yameanza kufurika kutoka mashambani na bei yake ni tshs 175000/= kwa bei ya madalali kwa gunia lenye kg 120. Na Maharage mengine kibao. Ukifika mwenyewe au kuna namba ya Dalali mmoja maarufu ninayo ukihitaji nitakupa kwa msaada zaidi juu ya Maharage mkuu.
 
Mi cjaelewa kitu hapa kwa hii mixhe ya songea.,inamaana mnazungumzia mzunguko Wa hapo hapo au unanunua na kusafirixha kwenda Dar...!!??
 
Katavi mahindi ni mengi sana tena cheap.Maeneo ya Majimoto na Inyonga huko ni kama unapewa bure.
Mkuu kunasoko LA karibu huko...,au ndo vle ununue usafirixhe upeleke dar...!!!!
 
Jamani toeni ABC za eneo husika mana unamuambia mtu nenda Songea mahindi yanalipa ni sawa mtu anakuambia njoo Dar kazi zipo na ukifika Ubungo ndio unaanza kushangaa. Toeni sehemu ambapo mahindi yako na pia mtoe msaada wa mwenyeji aliepo sehemu hizo ili hata kama mtu anaenda iwe vizuri kwake
 
Back
Top Bottom