Wapiga debe 30 wakamatwa stendi ya Magufuli

Wapiga debe 30 wakamatwa stendi ya Magufuli

WATU WA ARUSHA TANGA UPARENI NAO WAJENGEWE STAND YA KWAO WANAPATA SHIDA SANA
 
Hao so ndio wanyonge alioongea bwana mkubwa.
...Ndipo na Mimi ninaposhangaa
Si ndio alisema hawa boda bofa na mama na baba ntilie ni wanyonge wake wasifukuzwe stendi hapo.
Sasa hawa wapiga debe si nao wanatafuta tu kipato chao halali hapo kwa kuwabughudhi Abiria! Si nao wapi kundi LA wanyonge na waachwe ili kupata riziki zao??
 
Ninashauri hao wapigadebe wote 30 waishie jela, na huko jela wakafundishwe kulima na wakirudi waelekee vijijini wakalime.
Wapiga debe 30 wamekamatwa katika Kituo cha Mabasi cha Magufuli kilichozinduliwa siku mbili zilizopita na Rais John Magufuli.

Akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa Februari 26,2021 Meneja wa kituo hicho, Maira Mkama amesema wapiga debe waliokuwa Ubungo, Riverside na Mbezi wamevamia na kusababisha usumbufu kwa abiria.

"Leo tumeanza operesheni ya kuwakamata, hadi kufikia saa nne tumewakamata wapiga debe zaidi ya 30 na hapa Mbezi palikuwa na wapiga debe zaidi ya 100 bado waliokuwa Ubungo na wengine Riveside wote waliposikia kinafunguliwa wamevamia huku ndani,"amesema

Mkama amesema wameliomba Jeshi la polisi Kanda Maalum kuongeza askari na gari kwaajili ya doria ili kuwakamata wapiga debe watakaoendelea na shughuli hiyo.

Amesema wapiga debe hao wanasababisha usumbufu kwa abiria pamoja na kuhatarisha usalama wao hivyo viongozi wa kituo hicho watashirikiana na wamiliki wa mabasi kuangalia hatua za kuzichukua ili kuwaondoa wapiga debe.

Mwenyekiti wa Chama cha Kutetea Abiria (Chakua) Maulid Masalu amesema wanaweza kutoa ushauri lakini Serikali ndiyo yenye mkakati wa kuwaondoa wapigadebe.

"Hawa wapigadebe hawapo ndani ya stendi hii tu, wapo kuanzia stendi ya daladala wakati abiria anaposhushwa wanamvamia na kusababaisha usalama wake kuwa ndogo,"amesema Masalu.

Chanzo: Mwananchi
 
...Ndipo na Mimi ninaposhangaa
Si ndio alisema hawa boda bofa na mama na baba ntilie ni wanyonge wake wasifukuzwe stendi hapo.
Sasa hawa wapiga debe si nao wanatafuta tu kipato chao halali hapo kwa kuwabughudhi Abiria! Si nao wapi kundi LA wanyonge na waachwe ili kupata riziki zao??
Kabisa mkuu manake hao wapiga debe wa Riverside walikuwa wanadalalia abiria waliokuwa wanaenda kupanda mabasi hapo ibungo Sasa kituo kimeamishiwa mbezi so lazima na wao wahame
 
Ongea ila shukuru Mungu hayajakukuta
Au unadhani mpiga debe anapenda lile lyf

Kwani kazi ni moja ya upiga debe tu?? Kwanza mimi nawachukia sababu nishakua muhanga wa uwepo wao hapo Ubungo.
 
Ila Bongo bwana. Eti Chama cha Kutetea Abiria (CHAKUA).

Hii kitu sijui ata kama ina exist ndio naisikia leo.
 
vyombo vya ulinzi vinao wajibu kuhakikisha kituo hicho cha kimataifa na kilicho beba heshima ya Rais wetu mpendwa kinakuwa na heshima iliyo kusudiwa.
chonde chonde tusimuangushe Rais wetu kwa kuachilia mambo yasiyo faa yatokee ktk kituo hicho.
 
On contrary hao jamaa ni wa muhimu pia endapo wakiwekewa utaratibu mzuri.
Mimi pale ubungo kila nikienda kukata tiketi naongozana na mmoja mpaka ofisi ya basi naloenda kukakata tiketi.sio kwamba ofisi siijui no! Ila waliniambia wakipeleka mtu mmoja basi anapewa buku naye anasogesha maisha. Hivyo huwa siwakatai japokuwa sijui kama kuna wezi na matapeli kati yao
 
On contrary hao jamaa ni wa muhimu pia endapo wakiwekewa utaratibu mzuri.
Mimi pale ubungo kila nikienda kukata tiketi naongozana na mmoja mpaka ofisi ya basi naloenda kukakata tiketi.sio kwamba ofisi siijui no! Ila waliniambia wakipeleka mtu mmoja basi anapewa buku naye anasogesha maisha. Hivyo huwa siwakatai japokuwa sijui kama kuna wezi na matapeli kati yao
Wewe una moyo wa kusaidia pia ni mwerevu pia unaishi maisha mazuri na yenye amani

Binafsi huwa sipendi usumbufu, maana nilikutana nao wawili kila mmoja kwa wakati na sehemu tofauti

Mmoja nilikutana nae Tanga,
huyu jamaa alikua ni mstaarabu sana maana nilikua na mizigo pia nilikua naongozana na mzee 80yrs, mbaya zaidi nilikua nimevunjika mkono, pia nilikuta watu kibao wanasubiri dala dala ya mwisho kuelekea pangani, jamaa alichokifanya dala dala ilipofika tu akawahi kunikamatia siti mbili nikamlipa buku ilikua 2014 huko, jamaa akaniambia, akaniomba nimuonge nikamwambia hapa nimebaki na nauli tu
Akaniambia, "Poa naamini siku nyingine tukionana utanipa"
Nami nikamjibu, "Poa"
Baadae ikawa kila nikitembelea Tanga nikawa najaribu kupepesa macho pale nimtoe japo 10k sikuwahi kumuona


Kuna mwingine huyu wa Ubungo,
Nadhani huyu ndo kasababisha nimejikuta nawachukia hawa jamaa, yaani basi ninaloenda kupanda nalijua lakini jamaa ananifata tu afu nikakata tiketi nataka kuingia kwenye basi ananidai buku la kunipeleka nikamwangalia hadi akajishtukia akaondoka kimya kimya

Sa hv huwa nawaambia tu, "nimeshafanya Booking tayari" nikiwajibu hivyo hawanifati

Kuna baadhi ni wastaarabu na waelewa ila wengine wanakera sana
 
Back
Top Bottom