Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,030
- 20,391
WAPINZANI TAMBUENI KUWA TUNAYAHITAJI MAENDELEO ZAIDI KULIKO SIASA
Kwa mjibu wa kamusi ya Oxford, "Siasa ni shughuli zenye lengo la kustawisha ama kuongeza hadhi ya mtu fulani au kuongeza mamlaka ndani ya jumuiya ama shirika fulani".
Kwa mantinki hiyo unaweza kuona kuwa siasa ipo kwa ajili ya maslahi ya mtu ama jumuiya fulani. Na ndio maana haishangazi kumwona mwanasiasa akitengeneza taswira mbaya kwa mpinzani wake hata kama mpinzani huyo atafanya mambo ya kimaendeleo.
Hii ni kwa sababu hataki mtu yule ampite katika maslai ya kisiasa. Na daima mwanasiasa hajawahi kuwa na msimamo thabiti katika jambo fulani. Mfano mzuri ni pale Tundu Lissu kipindi cha utawala wa Kikwete pale alipotaja orodha ya mafisadi. Katika orodha yake jina la Edward Lowasa lilikua la juu kabisa. Si kwamba Lissu alimtaja katika orodha ile kwa sababu ya ufisadi wake, bali ni kwa sababu Lowasa alikua CCM hivyo moja kwa moja alihesabika kama mpinzani wa CHADEMA.
Na kwa kuwa alikua katika wakati mgumu kisiasa basi ilikua ni upenyo kwa wapinzani kutaka kujiinua kupitia maovu yake. Ni huyohuyo fisadi aliyetajwa na Lissu miaka kadhaa baadae bila aibu Lissu alipanda jukwaani na kutuambia kuwa Lowasa anastahili kuwa rais wa nchi hii. Hiyo ndio siasa ambayo hupendelea sana kuishi ndani ya kiota kiitwacho demokrasia.
Ukiwa kama kiongozi wa nchi ukaruhusu siasa zikutawale utashindwa kuleta maendeleo kwa kuwa miruzi itakua mingi na itakupotezea focus yako. Jambo hili hayati Jpm alilitambua na ndio maana hakutoa mwanya kwa siasa kutamalaki akiwa katika utekelezaji wa majukumu yake. Na hii ilimfanya awe huru kufanya kazi zake. Jpm aliwatambua vizuri sana wanasiasa na tabia zao ndio maana hawakuweza kukwamisha malengo yake. Hata mwanzo wa utawala wake walisema anatekeleza ilani yao lakini ni haohao walikuja wakabadirika na kumwita dikteta.
Lakini je, ni kweli dikteta anaweza kuliliwa kiasi hiki tunachoshuhudia? La hasha ila ni kwa sababu aliziba njia zao za kujiinua kisiasa kupitia yeye.
Hivi karibuni wapinzani wameibuka tena na kuanza kutoa maelekezo kwa rais mpya mama Samia wakimtaka alete umoja na mshikamano wa kitaifa. Ukweli ni kwamba Tanzania inao mshikamano wa kitaifa wakati wote ila wanachokitaka wana siasa ni kupata ule uwanja wao wa kujiinua kwa maslai yao. Nami sina shaka na mama Samia kwa kuwa amenithibitishia kuwa Jpm amemnoa vya kutosha. Hivyo mimi nasubiri awaonyeshe wanasiasa hao makali yake. Kwa maana kama ataruhusu wamtawale kifikra hataweza kuyafikia malengo.
Na kwa vile sisi sote ni watanzania nawashauri wanasiasa wafumbue macho yao na watambue kuwa, "Tunayahitaji maendeleo zaidi kuliko siasa"
Kwa mjibu wa kamusi ya Oxford, "Siasa ni shughuli zenye lengo la kustawisha ama kuongeza hadhi ya mtu fulani au kuongeza mamlaka ndani ya jumuiya ama shirika fulani".
Kwa mantinki hiyo unaweza kuona kuwa siasa ipo kwa ajili ya maslahi ya mtu ama jumuiya fulani. Na ndio maana haishangazi kumwona mwanasiasa akitengeneza taswira mbaya kwa mpinzani wake hata kama mpinzani huyo atafanya mambo ya kimaendeleo.
Hii ni kwa sababu hataki mtu yule ampite katika maslai ya kisiasa. Na daima mwanasiasa hajawahi kuwa na msimamo thabiti katika jambo fulani. Mfano mzuri ni pale Tundu Lissu kipindi cha utawala wa Kikwete pale alipotaja orodha ya mafisadi. Katika orodha yake jina la Edward Lowasa lilikua la juu kabisa. Si kwamba Lissu alimtaja katika orodha ile kwa sababu ya ufisadi wake, bali ni kwa sababu Lowasa alikua CCM hivyo moja kwa moja alihesabika kama mpinzani wa CHADEMA.
Na kwa kuwa alikua katika wakati mgumu kisiasa basi ilikua ni upenyo kwa wapinzani kutaka kujiinua kupitia maovu yake. Ni huyohuyo fisadi aliyetajwa na Lissu miaka kadhaa baadae bila aibu Lissu alipanda jukwaani na kutuambia kuwa Lowasa anastahili kuwa rais wa nchi hii. Hiyo ndio siasa ambayo hupendelea sana kuishi ndani ya kiota kiitwacho demokrasia.
Ukiwa kama kiongozi wa nchi ukaruhusu siasa zikutawale utashindwa kuleta maendeleo kwa kuwa miruzi itakua mingi na itakupotezea focus yako. Jambo hili hayati Jpm alilitambua na ndio maana hakutoa mwanya kwa siasa kutamalaki akiwa katika utekelezaji wa majukumu yake. Na hii ilimfanya awe huru kufanya kazi zake. Jpm aliwatambua vizuri sana wanasiasa na tabia zao ndio maana hawakuweza kukwamisha malengo yake. Hata mwanzo wa utawala wake walisema anatekeleza ilani yao lakini ni haohao walikuja wakabadirika na kumwita dikteta.
Lakini je, ni kweli dikteta anaweza kuliliwa kiasi hiki tunachoshuhudia? La hasha ila ni kwa sababu aliziba njia zao za kujiinua kisiasa kupitia yeye.
Hivi karibuni wapinzani wameibuka tena na kuanza kutoa maelekezo kwa rais mpya mama Samia wakimtaka alete umoja na mshikamano wa kitaifa. Ukweli ni kwamba Tanzania inao mshikamano wa kitaifa wakati wote ila wanachokitaka wana siasa ni kupata ule uwanja wao wa kujiinua kwa maslai yao. Nami sina shaka na mama Samia kwa kuwa amenithibitishia kuwa Jpm amemnoa vya kutosha. Hivyo mimi nasubiri awaonyeshe wanasiasa hao makali yake. Kwa maana kama ataruhusu wamtawale kifikra hataweza kuyafikia malengo.
Na kwa vile sisi sote ni watanzania nawashauri wanasiasa wafumbue macho yao na watambue kuwa, "Tunayahitaji maendeleo zaidi kuliko siasa"