Wapinzani waandaa hoja: Wamtaka Pinda kujiuzulu

...Aisee Taifa si ndiyo watu wenyewe?? sasa hebu fikiria Taifa lenye watu wasiyo na Vichwa wala miguu.... au anaye baka naye abakwe,huo uchumi una-priorities gani tena?
 
All in all, mimi najaribu tu kufikiria kwa nini tunaakuwa na viongozi amabao siku zote wanakuwa reactive. Alichotakiwa kusema kwa wananchi Pinda ni namna ya kuzuia mauaji hayo lakini si nini cha kufanya mauaji yakitokea.. That's the challenge the govt hasn't provided the solution so far. Hapa naanza kuikumbuka ile hotuba ya JK yeye alisema ikiwa proved umeua albino utanyongwa (Ikumbuke just naye alilaumiwa pia na wanaharakati wa haki za binadamu)...... Looks like these guys are on the same line isipokuwa huyu mwingine aliamua kuwa a bit diplomatic.

N wale mnaobishana kuhusu alisema au hakusema. Hv hamjui staili ya viongozi wetu? mnafikiri mkuchika angekaa kimya mpaka leo kama hayo magazeti yangekuwa yanamsingizia waziri mkuu? Let's try to use a common sense.
 

Ilikuwa hivi.

1. Alipoulizwa swali. Hakulijibu kwanza. Alianza kwa kutoa background ya ziara nzima ya lake zone. ... Maelezo haya yalijenga feelings na emotions kwa wabunge. Na Ninafikiri... alifanikuwa kuwaondoa wabunge kwenye fikra zao na kufanya wawe kwenye emotions kama yeye...

2. Then akaja kwenye issue yenyewe...alipoanzatu kuijadili....akakwama kwa srtong feelings...akaomba samahani...kalia...akamaliza kwa sekunde chance. Akaendela kusema kwa mtu amabaye hajifika huko kwenye matukio hawezi kuipata hali kamili...na kuwa alitoa yale matamshi (Hakuyarudia)...KUTISHIA TU. Na akaomba msamaha kuwa kama kafanya kosa Mungu amsaidie....Hakurudia alichosema. Na hakuomba msamaha kwa bunge au...

3. In a way..aliomba msamaha kwa Mungu...!!!

4. Baada ya Pale Hamad akasimama.... Hali ya Baba Mkuu wa Nyumba kulia ..ilimtisha kidogo ...nafikiri naye akanza kufikiri kwa feelings kidogo...but he managed to say ..Pamoja na mazuri yote hayoo ..Uongozi wa sheria ni vema ufuatwe.....

5. Sijui Wapinzani walijiiadaa Kufanyia nini swali walilouliza na sijui kuwa kama ndicho walichofanya baada ya Kujibiwa hoja yao kwa kiliocha hisia kali.

Lakini PM anahitaji to learn how to work with his strong emotions....vinginevyo hata huko mbele ya safari .. .
 

asante tutasoma hansards, atakayepata mapema aturushie hapa. By the way PM ameonyesha kutokuwa na uzoefu kabisa. Ndo maana naamini Taifa ndo linaanza kutambaa sasa.
 

Kama the best of upinzani tulionao ndio huu... Kweli nchi yetu itakua imechanganya priorities... Coz i thought lilikua ni tatizo la CCM tu. Priority ya juu iko chini ya chini juu. PM ameshatolea ufafanuzi alichomaanisha... YOU ARE KEEPING YOUR EYES OFF THE BALL, kwa kung'anga'na na vijimambo visivyokua na tija kwa taifa at this point in time. Wakuu angalieni priorities za mtanzania wa kawaida ili nchi ipige hatua haraka.
 
Totally agree.

While i think Pinda's statement is not beffiting a prime minister, i think these people are overeacting.

Wapinzani wanaofikiri statement ya Waziri Pinda ina utata wanafikra mbovu na mgando. Hivi hawaoni kuua viumbe kwa ukatili kama wanakata miti wao ndio wanavunja katiba. wapinzani tafuta sera ya maendeleo ACHA KULUMBANA KWA MABO YALIYO WAZI.
 

Gembe, Gembe, Gembe..... mkuu mbona unachelewa hivyo kutathmini uzito wa jambo?

Ona jinsi vile ulivyokuwa ukimjibu Mkjj alipokuwa aking'ang'ana na haja ya kupata tape ya hotuba ili kuthibitisha ukweli wa kauli:

Kutoka link hii: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-alisema-nini-hasa-post363610.html#post363610 ulithubutu hata kupinga wanunua habari...

Gembe, ikiwezekana umwombe msamaha Mkjj kabla ya kumuunga mkono 🙂 Nafikiri kufanya hivyo baada ya yale uliyoyasema hapa jamvini litakuwa jambo la busara kwa mtu makini kama wewe. Kwa sababu ume-derail effort zake kupata tape katika wakati mwafaka, lakini baada ya kuona uko-cornered (au kambi yako), umebadilisha msimamo ghafla.

Mifano zaidi:https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-alisema-nini-hasa-post363885.html#post363885

Si hayo tu bali kuna mengine zaidi:

Gembe, unajua Mkjj anaweza kuwa mwanasiasa na kuonekana kama wanasiasa wetu walio wengi tu... hata hivyo tofauti yake ni moja: ni mwanasiasa aliyeamua kuamusha/kuamsha hisia zetu kutoka pande mbalimbali katika mazingara yetu. Tumpe ushirikiano sometimes kabla ya ku-offer pingamizi tu at first instance we see his posts.

Pandisha dau Gembe, naweza kukutumia tape... 🙂 Take care.

SteveD.
 
Wapinzani wanaofikiri statement ya Waziri Pinda ina utata wanafikra mbovu na mgando. Hivi hawaoni kuua viumbe kwa ukatili kama wanakata miti wao ndio wanavunja katiba. wapinzani tafuta sera ya maendeleo ACHA KULUMBANA KWA MABO YALIYO WAZI.

Novatus, si wapinzani tu, hata mimi (ambaye sina chama) nafikiri kuwa kauli ya Mh. Pinda ina utata na kuna ulazima aikane, aithibitishe, au kuielezea. Maana tamko la Waziri Mkuu katika mkutano wa hadhara ni motisha kubwa kwa wananchi. Chakujiuliza ni kuwa motisha hiyo yaweza kuwa na madhara gani?!
 
Pandisha dau Gembe, naweza kukutumia tape... 🙂 Take care.

SteveD.
wewe unataka sh. Ngapi?

Mie siwezi kumuomba msamaha mtu Mzee kama Mwanakijiji!Mie mara ya kwanza nilikuwa nampinga sababu aliendeleza uhalisia wa jambo wakati hata Tape hana. Na mie baaada ya kuona speculations zimezidi... Naona ni bora na Mimi nipate Tape nisikie alichosema Waziri Mkuu
 

Kwa hiyo haja yake ya kuwa na tape katika kuthibitisha uhalisia wa jambo haina maana sana kulinganisha na haja yako ya kuthibitisha jambo hilo hilo?
 
Wapinzani wa Tanzania kiboko, inaonekana wanakaa wanasubiria nani achemshe wamlime(IMHO).

ndo kazi ya upinzani ma dia, kama hawaweze kukosoa na kuhitaji maeloze ili kurekebisha mambo hamna haja ya wao kutumia ruzuku zetu ati.... ndo maana wapinzani na ndo maana Pinda analia maana anajua wapinzani wake wameshaona udhaifu wake....
 


Well said!!

Ukiua albino, umekwenda na maji ... hao akina Hamad Rashid, W. Slaa, Zitto, n.k. mtakutana kuzimu. Tutakapokuwa tunakucharanga mapanga hawatakuwepo kukunusuru ...

Mizengo Pinda songa mbele, tunakuunga mkono katika hili ... achana nao hawa mafisadi ...
 
- Kama ninaelewa vizuri ni kwamba ni kweli alisema na ameomba msamaha, sasa what is next? as of kichwa cha hii mada?
 

nini maana ya upinzani sasa haya madogo mkiyadharau yatakuja kutoka makubwa mtashindwa kuya handle, wewe aliyekuambia wezi wa EPA walianzia BOT ni nani, walianza chini.... sisi wengine hapa ni WANACCM, TUMEZALIWA CCM, TUMESOMESHWA NA CCM, ILA INABIDI TUJUE KAMA HATUTAJITAHIDI KUKOSOANA WENYEWE KWA WENYEWE HATUTAFIKA, TUFIKIRI MI NADHANI TUWE TUNAREKODI NA UMRI WA WATU HUKU MAANA HOJA ZA WATU WENGINE NI KAMA ZA WATOTO ILI WAKATI WA KUWAJIBU TUJIBU KWA BUSARA TUSIJEKATISHA WATU TAMAA YANI WEWE HOJA YAKO NATAMANI KUKURUSHIA KIATU
 
(Ikumbuke just naye alilaumiwa pia na wanaharakati wa haki za binadamu)...... Looks like these guys are on the same line isipokuwa huyu mwingine aliamua kuwa a bit diplomatic.

100% Nyambala, Mie naenda mbali kidogo kuwa wa kwanza alimung'unya na alipoona watu hawajamuelewa huyo huyo wa kwanza akamtuma Pinda, Pinda ehhhh! nenda huko kawaambie tumechoka halafu gandamiza kuwa sasa ni jino kwa jino na wapinzani wataishia kupiga kelele ntakulinda A-Z,KWISHA, Nyie akina MKJJ na wengine mtaishia kutaka utawala wa sheria wakati hali halisi haitoi nafasi hiyo, Jambazi la ulaya linahojiwa likiwa limepewa kahawa huku kwetu pale Osterbay polisi anazungushwa kule nyuma uani anakabidhiwa acheze na mbwa wa polisi baada ya dakika chache bila kutumia gharama kubwa ya upelelezi taarifa muhimu wanazo inaanza kamatakamata...looks ugly but effective 99% .....Bravo Pinda
 
- Ya utoto na ukubwa ni irrelevant katika kuchambua hoja, dawa ni kukata ishu kiroho mbaya in the process utoto na ukubwa wa opposed hoja utaonekana, lakini name calling tulishakubaliana na dalili za kutokuwa na hoja.

- Wananchi tunawalipa ruzuku wapinzani ili waturekebishie serikali, kwa hiyo ni kazi yao kuishambulia serikali inaharibu, Pinda anaporopoka na maneno yake kuishia kuhatarisha amani ya taifa as what he did here ni lazima aambiwe ukweli, hapa natoa hongera kwa wapinzani, tafadhali mkuu Zitto, huyu Pinda angalau apewe verbal warning kwa hili maaan he is out of the line na pia apewe heshima kwa kukubali makosa maana wangekuwa wengine wangekimbilia jimboni kwao na kupokelewa kwa sherehe na vifijo vingi.

Kwa hili wapinzani tupo pamoja.
 

Kamanda Kasheshe, Taifa letu is a boiling pot, kila kitu kinafanyika na kutendeka katika wakati mmoja. Ni jamii yenye watu takribani millioni 40. Hatuwezi kuchota kikombe kimoja na kukiweka pembeni kipoe ili maji yaliyobakia chunguni yachemke kwa haraka kisha kuyarudisha yale yaliyokwenye kikombe kwenye chungu na kutegemea kuwa hayatapunguza joto lililofikiwa tayari.

Hatuwezi kuacha mengine yadumae kwa visingizio kuwa kuna uchumi unajengeka. Kwani matatizo haya ya uchumi yametokana na nini kama si kudharau na kutoyafatililia matamshi ya viongozi wetu na kuwafanya wawajike nayo kama walivyoyatoa?

Nina imani kuwa umeshajionea yale yanayoongelewa kwenye media za nchi tunazoziita 'zimeendelea'. Katika nchi hizo maneno kama yanavyosemekana kutolewa na Mh. Pinda hakika yangemfikisha pabaya bila kujali hali ya uchumi walionao. Mkuu, ufatiliaji wao wa kauli za viongozi walio wateua ndiyo huo unaotufanya hivi sasa kwenda kujiombeleza kwao kila kukicha hata kwa vitu tunavyoweza kuvifanya siye wenyewe, including kufatilia kauli za viongozi wetu!!

SteveD.
 

Afadhali amelia kuliko angewaka, yakamtokea ya Mkapa
 
That was excellent Nziku!!! Kweli una-tafakuri nzito.
 
Ustaarabu wa kujiuzulu haupo hapa Tz,wale akina Lowasa na wengine msifikiri walijiuzulu kwa kuwa kuna msukumo au wameona waliyotuhumiwa nayo hayana faida na wa kuendelea kuwepo.
Maana hadi leo mnawaona wanapeta na kupewa kazi zingine ,hivyo serikali ya Kikwete isituzungue,kuwa inafanya kweli na kutaka kutubabaisha wanaojiuzulu tunawaona nchi nyingine na wakisha kujiuzulu hawatokezi tena pua kwenye vyombo vya umma huendelea na biashala zao na kama walihitajiwa mahakamani tunaona wanaitwa mahakamani na kama wakikutwa na makosa sheria zinachukua mkondo wake na kama hawana wanaachwa huru na kuwa raia wa kawaida,sasa hapa TZ nani aliejiuzulu na kufikia au kufikishwa hatua zote ,walio jiuzulu hao hapo wanaendelea Bungeni wanashirikishwa kwenye kamati mbalimbali sasa na mishahara inaingia kama kabla hajajiuzulu au zaidi maana ukishakuwa ndani ya kamati kamati basi posho yake inashinda.
Na hapa JF naona mmekuwa waoga niliweka topik ....Pinda na adhabu ya Kifo ,kichwa cha habari kikabadilishwa ,sijui kwa nini ? Lakini ndio hivyo jinamizi bado linamwandama na ilikuwa ni heading ambayo ingelikuwa inakwenda kwa wakati.
Basi na Kikwete nae afikishwe au ahojiwe na kauli zake alizozitoa Zanzibar.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…