Wapo wapi watetezi wa Watanzania, wamesusa au wanalamba asali?

Wapo wapi watetezi wa Watanzania, wamesusa au wanalamba asali?

Mkuu Mimi Ni miongoni mwa Watanzania wachache walioonja Cha mtema kuni kwenye siasa za kuwa mpinzani!!
Ukitaka uwe adui wa umma Tanzania,toa mawazo yaliyo kinyume na Yale ya serikali au chama Tawala!

Narudia tena Tanzania Ni kosa kutofautiana mawazo na kiongozi wako,na ikitokea hivyo wewe utakuwa adui wa umma na siyo uliyetofautiana naye pekee!

Hofu? Tufanye je sasa? Tusalimu amri?

Tuwatambue wenye kutaka kutuaminisha kuwa tu waoga
 
Ukimya umekuwa mkubwa kwa wanaharakati na wanasiasa ,ukimya ambao unashtusha na kutia hofu kubwa.

Leo hii yupo wapi Zitto Kabwe tuliyemzoea kukosoa serikali kwa hoja zenye mashiko, yupo wapi Freeman mbowe na tindu lissu wasemaji hodari wa kuwasemea wanachi pale Mambo serikalini yanapoenda mrama, wapo wapi wale wakereketwa wa CCM waliokuwa wanamshambulia mwenda zake na serikali yake kipindi Mambo yalipokuwa hayaeleweki wapo wapi wale wakina kigogo 2014 na Mange Kimambi watu waliokuwa wakifichua maovu ya serikali ya awamu ya tano, vipi Tweeter ya kina chaali na wapazaji sauti wengine mbona kimya hapa jamii forum hatuwasikii Tena kina mzee Mwanakijiji na Faizafox.

Je, ukimya huu ni kielelezo kuwa Mambo yapo shwari?

Au ukimya huu ni kwamba watu wamechoka kuongea ukweli na wamesusa Sasa kila mtu apambane na hali yake?

Au ukimya huu ni kwamba wamefungwa midomo kwa kupewa asali warambe?

Kipindi ambacho ufisadi na ubadhilifu upo waziwazi, kipindi ambacho tozo zimepitiliza, kipindi ambacho vitu vimependa bei kupitiliza, kipindi ambacho uchumi wa nchi umeshuka sana, kipindi ambacho miradi mikubwa imesimama, kipindi ambacho umeme wetu sio wa uhakika, kipindi ambacho tunakopa hela kupitiliza, kipindi ambacho matumizi ya serikali ya mekuwa makubwa kuliko makusanyo, kipindi ambacho wenye nacho wanaongezewa na maskini wanapokonywa hadi kidogo walichonacho, kipindi ambacho wamachinga wananyanyaswa.

Je, ni sahihi watu tunaowategemea watusemee kukaa kimya je ukimya huu na kutokupaza sauti ni kwamba hawayaoni yanayoendelea au wameridhika na machozi ya Watanzania kila kukicha. Nani wakutusemea wananchi wanyonge tumebaki kulalamika tu nani wa kukosoa utendaji mbovu wa serikali nani wa kumwajibisha waziri wa nishati na waziri wa fedha kwa utumbo wanaotufanyia Nani wa kukemea ubadhilifu yupo wapi au tukamfufue magu?[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
Kuwatetea wabongo ni sawa na kubeba zigo la misumari,wakati wanapambana kazi yenu ilikuwa ni kuwatukana na kuwakejeli, sasa Kila mtu abebe zigo lake mwenyewe ,lipa tozo kwa lazima
 
Nimesikia ka clip humu JF Mbowe akijaribu kusimama na wananchi japo ninkama kajirecord kwenye simu ya tochi ili akiulizwa asali alokula aruke kimanga na kama sikosei inaishiria ndo maana anajibaraguza kishikaji
 
Kwani uliowataja hao wote ni wabunge?ubunge umpe mtu mwingine afu kukusemea umuite mtu mwingine🙄

Tanzania,CCM haipendwi lakini hakuna upinzani wa kweli.
Upinzani wa kweli wewe unaujua?.
Unapenda wenzio wakutetee ukiwa umelala halafu wao waumie.
Pambana mwenyewe.
 
Nimesikia ka clip humu JF Mbowe akijaribu kusimama na wananchi japo ninkama kajirecord kwenye simu ya tochi ili akiulizwa asali alokula aruke kimanga na kama sikosei inaishiria ndo maana anajibaraguza kishikaji
Anajikosha tu hakuna Cha maana
 
Narina tu wengine wanalamba wengine baba
Hakuna mrinaji mwenye kushangilia uozo huu:

IMG_20220901_085859_867.jpg


Kwani hujui hata Mwigulu, vibaraka na chawa wao hujiita warina asali kana itasaidia kutupoteza watudhaniao wajinga sisi, maboya?
 
Hakuna mrinaji mwenye kushangilia uozo huu:

View attachment 2341804

Kwani hujui hata Mwigulu, vibaraka na chawa wao hujiita warina asali kana itasaidia kutupoteza watudhaniao wajinga sisi, maboya?
Mkuu nadhani ninayo hasira kuzidi ya kwako . Siku nikiungana na hawa wapuuzi wanaotufanya nyumbu kulamba asali zitakuwa siku za mwisho naturally nachukia wanaodhani sisi tunawajibika kuishi maisha haya wao wakilamba asali so I just have to give it a break maana maisha ni.mafupi .ila kuona hizi kelele ni bit of light at the end of tunnel mwisho wao unakuja
 
Mkuu nadhani ninayo hasira kuzidi ya kwako . Siku nikiungana na hawa wapuuzi wanaotufanya nyumbu kulamba asali zitakuwa siku za mwisho naturally nachukia wanaodhani sisi tunawajibika kuishi maisha haya wao wakilamba asali so I just have to give it a break maana maisha ni.mafupi .ila kuona hizi kelele ni bit of light at the end of tunnel mwisho wao unakuja

Hadi kufikia kuandika uzi huu:

"Walamba asali wanapoufurahia "ujinga" wetu"

Tungali kwenye makasiriko tu?
 
Back
Top Bottom