Waraka kwa mitandao ya simu (Vodacom, yas, airtel, halotel, etc)

Waraka kwa mitandao ya simu (Vodacom, yas, airtel, halotel, etc)

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Habari zenu enyi makampuni ya huduma za mawasiliano. Nakuja kwenu kwa lengo la kuwapa wazo la kibiashara ambalo litaweza kuboresha huduma zenu kwa wateja, haswa kwa upande wa intaneti. Changamoto ambayo nyie makampuni mnayo ni urasimu haswa linapokuja suala la mtu mwenye nia ya kufanya kazi na nyie. Inafahamika mnaogopa sana suala la hakimiliki na kesi zinazohusiana na kipengele hicho kwa kuwa tayari mmeshapata sana changamoto maeneo hayo. Lakini tayari mnao wanasheria na sijui wanafanya kazi gani kuhakikisha maslahi yenu hayapati shida. Au ndio wanawashauri muweke urasimu kiasi hicho?

Kwa njia hiyo mtakosa sana ideas mpya katika soko hata kama mna wadau/agents mnaofanya nao kazi. Nao pia wana limitations zao kama hawatapata mawazo mapya, mradi tu wasiweke nao urasimu kama nyie. Nitawapatia wazo hapa na kama litakuwa muafaka kwenu ni vyema mkanitafuta inbox kwa ajili ya kujua tunayajenga vipi. Hii nayo itasaidia sana kuondoa usumbufu ambao mnaukimbia pale ambapo hapatakuwa na makubaliano rasmi.

Here is the Deal!

WAZO LA KIMKAKATI

HUDUMA YA KUMPUNGUZIA MTEJA BANDO LA INTANETI KATIKA MITANDAO YA SIMU

19/10/2024

UTANGULIZI

Kumekuwepo na uhitaji wa matumizi ya intaneti kwenye simu janja kwa kiasi kikubwa kwa miaka ya karibuni. Hii kwa kiasi kikubwa imechangiwa na kampuni za simu kuboresha vifurushi vyao vya intaneti. Pili ni kutokana na watu wengi kumiliki simu janja. Kadhalika ni kutokana na kuwepo kwa watengenezaji maudhui wengi kuona fursa iliyopo kupitia mitandao mbalimbali Pamoja na application mbalimbali kama Tiktok, facebook, Instagram, WhatsApp, X, n.k. yote haya pamoja na mengine yamefanya matumizi ya intaneti kuongozeka.

Sambamba na matumizi hayo kuongezeka, kumekuwa na changamoto moja ambapo sio kila mmoja anaweza kumudu kununua bando ambalo litamtosha kutumia na kukamilisha mahitaji yake ya kimtandao. Hivyo wakati wa matumizi, mteja hujikuta anaishiwa bando na pengine asiwe na kiasi cha hela ambacho angeweza kununua bando kwa wakati huo. Wakati huo huo wapo watu ambao wana uwezo wa kuwa na bando la kutosha na ziada juu. Ndipo wazo la kumpunguzia mteja mwingine bando la intaneti likaja. Wazo tuliite NIBANDIKE TAFADHALI.

UHAMISHAJI WA SALIO LA KIFURUSHI CHA INTANETI KWENYE SIMU


Kwa sasa mteja anapoishiwa kifurushi cha intaneti, atamwomba mtu wake wa karibu amuunganishe kwa njia ya tethering, na mlengwa atapata huduma hiyo kwa muda huo na kwa eneo hilo alipo kutegemea na uwezo wa wi-fi. Changamoto ya njia hii ni kwamba mhitaji ni lazima awe Jirani sana na msaidizi wake. Lakini kwa huduma ya NIBANDIKE, ujumbe utatumwa kama wa kawaida kwenye huduma zingine na mhitaji atapunguziwa kiasi cha bando aliloomba bila kujali yuko wapi.

NINI KIFANYIKE

Kwa mara nyingine mteja anapoishiwa bando la intaneti atatuma ujumbe kwa mtu wake wa karibu kuomba ampunguzie kiasi cha data ili akamilishe hitaji lake. Ili zoezi zima lisiathiri biashara ya kampuni na pia kuleta usumbufu kwa msaidizi, ni lazima pawepo na taratibu zitakazopaswa kufuatwa, kwa maana ya vigezo na masharti kuzingatiwa. Hii ni kama ifuatavyo;

  • Kiasi cha juu cha mteja kuomba kupunguziwa bando kisizidi MB 1000
  • Muombaji ataomba mara moja kwa siku.
  • Ili pia kampuni iweze kufaidika na zoezi hili, itaweza kutoza kiasi kidogo cha gharama ya hamisho la bando.
  • Njia zingine ambazo kampuni inaweza kuona ni sahihi katika kuboresha huduma hii.
FAIDA

Mpango huu utaleta faida kwa kampuni kama ifuatavyo;

  • Pale ambapo wateja wataona kampuni imewajali katika hali zao na kuwawezesha kutatua shida zao za matumizi ya intaneti kwa muda huo bila kujali umbali.
  • Kuiongezea kampuni kipato kupitia tozo za hamisho la bando
  • Kuongeza matumizi ya intaneti ambapo itapelekea kuongezeka kwa ununuzi wa bando za intaneti
  • Faida zingine ambazo kampuni inaweza kuziona kupitia mpango huu.


HASARA

Hakuna hasara.

HITIMISHO

Wateja wana michango yao katika kuboresha huduma za biashara za makampuni ambayo wanapata huduma na bidhaa. Ni wakati sasa wa kuyaangalia mahitaji ya wateja katika kona hii ili kuweza kuwaboreshea huduma zao, hasa katika matumizi ya intaneti pale ambapo wamefikwa na uhitaji sana na hawana suluhisho la haraka.

Pale mtakapoona wazo hili ni bora na linafaa kufanyiwa kazi, msisite kufanya hivyo, pakiwepo na makubaliano ya pande mbili kwenye utekelezaji wa wazo hili.


©2024
 
Pamoja sana kwa wale ambao wanapongeza kupitia PM
 
Habari zenu enyi makampuni ya huduma za mawasiliano. Nakuja kwenu kwa lengo la kuwapa wazo la kibiashara ambalo litaweza kuboresha huduma zenu kwa wateja, haswa kwa upande wa intaneti. Changamoto ambayo nyie makampuni mnayo ni urasimu haswa linapokuja suala la mtu mwenye nia ya kufanya kazi na nyie. Inafahamika mnaogopa sana suala la hakimiliki na kesi zinazohusiana na kipengele hicho kwa kuwa tayari mmeshapata sana changamoto maeneo hayo. Lakini tayari mnao wanasheria na sijui wanafanya kazi gani kuhakikisha maslahi yenu hayapati shida. Au ndio wanawashauri muweke urasimu kiasi hicho?

Kwa njia hiyo mtakosa sana ideas mpya katika soko hata kama mna wadau/agents mnaofanya nao kazi. Nao pia wana limitations zao kama hawatapata mawazo mapya, mradi tu wasiweke nao urasimu kama nyie. Nitawapatia wazo hapa na kama litakuwa muafaka kwenu ni vyema mkanitafuta inbox kwa ajili ya kujua tunayajenga vipi. Hii nayo itasaidia sana kuondoa usumbufu ambao mnaukimbia pale ambapo hapatakuwa na makubaliano rasmi.

Here is the Deal!

WAZO LA KIMKAKATI

HUDUMA YA KUMPUNGUZIA MTEJA BANDO LA INTANETI KATIKA MITANDAO YA SIMU

19/10/2024

UTANGULIZI

Kumekuwepo na uhitaji wa matumizi ya intaneti kwenye simu janja kwa kiasi kikubwa kwa miaka ya karibuni. Hii kwa kiasi kikubwa imechangiwa na kampuni za simu kuboresha vifurushi vyao vya intaneti. Pili ni kutokana na watu wengi kumiliki simu janja. Kadhalika ni kutokana na kuwepo kwa watengenezaji maudhui wengi kuona fursa iliyopo kupitia mitandao mbalimbali Pamoja na application mbalimbali kama Tiktok, facebook, Instagram, WhatsApp, X, n.k. yote haya pamoja na mengine yamefanya matumizi ya intaneti kuongozeka.

Sambamba na matumizi hayo kuongezeka, kumekuwa na changamoto moja ambapo sio kila mmoja anaweza kumudu kununua bando ambalo litamtosha kutumia na kukamilisha mahitaji yake ya kimtandao. Hivyo wakati wa matumizi, mteja hujikuta anaishiwa bando na pengine asiwe na kiasi cha hela ambacho angeweza kununua bando kwa wakati huo. Wakati huo huo wapo watu ambao wana uwezo wa kuwa na bando la kutosha na ziada juu. Ndipo wazo la kumpunguzia mteja mwingine bando la intaneti likaja. Wazo tuliite NIBANDIKE TAFADHALI.

UHAMISHAJI WA SALIO LA KIFURUSHI CHA INTANETI KWENYE SIMU


Kwa sasa mteja anapoishiwa kifurushi cha intaneti, atamwomba mtu wake wa karibu amuunganishe kwa njia ya tethering, na mlengwa atapata huduma hiyo kwa muda huo na kwa eneo hilo alipo kutegemea na uwezo wa wi-fi. Changamoto ya njia hii ni kwamba mhitaji ni lazima awe Jirani sana na msaidizi wake. Lakini kwa huduma ya NIBANDIKE, ujumbe utatumwa kama wa kawaida kwenye huduma zingine na mhitaji atapunguziwa kiasi cha bando aliloomba bila kujali yuko wapi.

NINI KIFANYIKE

Kwa mara nyingine mteja anapoishiwa bando la intaneti atatuma ujumbe kwa mtu wake wa karibu kuomba ampunguzie kiasi cha data ili akamilishe hitaji lake. Ili zoezi zima lisiathiri biashara ya kampuni na pia kuleta usumbufu kwa msaidizi, ni lazima pawepo na taratibu zitakazopaswa kufuatwa, kwa maana ya vigezo na masharti kuzingatiwa. Hii ni kama ifuatavyo;

  • Kiasi cha juu cha mteja kuomba kupunguziwa bando kisizidi MB 1000
  • Muombaji ataomba mara moja kwa siku.
  • Ili pia kampuni iweze kufaidika na zoezi hili, itaweza kutoza kiasi kidogo cha gharama ya hamisho la bando.
  • Njia zingine ambazo kampuni inaweza kuona ni sahihi katika kuboresha huduma hii.
FAIDA

Mpango huu utaleta faida kwa kampuni kama ifuatavyo;

  • Pale ambapo wateja wataona kampuni imewajali katika hali zao na kuwawezesha kutatua shida zao za matumizi ya intaneti kwa muda huo bila kujali umbali.
  • Kuiongezea kampuni kipato kupitia tozo za hamisho la bando
  • Kuongeza matumizi ya intaneti ambapo itapelekea kuongezeka kwa ununuzi wa bando za intaneti
  • Faida zingine ambazo kampuni inaweza kuziona kupitia mpango huu.


HASARA

Hakuna hasara.

HITIMISHO

Wateja wana michango yao katika kuboresha huduma za biashara za makampuni ambayo wanapata huduma na bidhaa. Ni wakati sasa wa kuyaangalia mahitaji ya wateja katika kona hii ili kuweza kuwaboreshea huduma zao, hasa katika matumizi ya intaneti pale ambapo wamefikwa na uhitaji sana na hawana suluhisho la haraka.

Pale mtakapoona wazo hili ni bora na linafaa kufanyiwa kazi, msisite kufanya hivyo, pakiwepo na makubaliano ya pande mbili kwenye utekelezaji wa wazo hili.


©2024
Hasara, unawapunguzia Faida wao, hilo wazo ni gumu sana kwa mfanyabiashara
 
Kutatua Tatizo ni kujua Tatizo au mzizi wa Tatizo..., na tatizo ni kujiuliza kwanini Bundle ni gharama je ni mitandao ya simu au ni lack of Ushindani ? Jibu tatizo ni Serikali ilipoweka Bei elekezi wote wakacheza kwenye uelekezi hence kukawa hakua ushindani (And why did Serikali do that ?, Sababu ya Tozo ni ili wapate Mapato) they care less about Mwananchi

 
Hasara, unawapunguzia Faida wao, hilo wazo ni gumu sana kwa mfanyabiashara
Bora kipi? Watu kufanya tethering au kukaa bila bundle? 80/20 rule applies. Hofu inaweza jengeka hadi pale kampuni itakapoamua kutekeleza. Waamuzi ni wateja. Walengwa ni wateja. Ukiacha mbali faida, pia ni sehemu ya CSR. Watoa huduma watajua namna ya kudhibiti hii NIBANDIKE.
 
Kutatua Tatizo ni kujua Tatizo au mzizi wa Tatizo..., na tatizo ni kujiuliza kwanini Bundle ni gharama je ni mitandao ya simu au ni lack of Ushindani ? Jibu tatizo ni Serikali ilipoweka Bei elekezi wote wakacheza kwenye uelekezi hence kukawa hakua ushindani (And why did Serikali do that ?, Sababu ya Tozo ni ili wapate Mapato) they care less about Mwananchi

Ukweli ni kwamba kampuni zinataka faida, tena kubwa. Serikali nayo inataka mapato, mengi iwezekanavyo. Ndio maana kama ulivyodadavua kwenye mada yako serikali imeweka msururu wa kodi na tozo kwa bodhaa/huduma moja hadi kumlemea mlaji.

Mfano mwingine ni saga ya starlink ambayo watoa huduma nchini hawataki kuisikia. Wanajua ikiingia watappteza wateja upande wa data. Sidhani kama serikali inaihofia starlink bali ni watoa huduma wanaofanya hizo lobbying kujihakikishia 'monopoly'.

Njia nzuri ya hizi kampuni kujihakikishia milki ya wateja ni kuwapa huduma stahili na rafiki wateja ili wajisikie aibu kuacha kutumia huduma husika. Njia mojawapo ni hii ya NIBANDIKE
 
Ukweli ni kwamba kampuni zinataka faida, tena kubwa.
That is nature of the Beast Kampuni ni Answerable kwa Shareholder wala haipo pale kufanya charity, hata ikitoa huduma hio ni by the way ila the core mission is to get as much money as possible, ndio maana the only way ya kuhakikisha hawa watu wanabanwa ni ushindani baina yao ili mmoja wapo akibana sana mnunuzi watu wapate alternative
Serikali nayo inataka mapato, mengi iwezekanavyo.
Hilo ni kosa sababu Dhima ya Serikali ni kuhudumia wenye nchi (as much affordable service as it can sustainable offer) na kosa ndio lipo hapo hawa watu wameguka kuwa Kero badala ya msaada na bila faida kwa mwananchi

Ndio maana kama ulivyodadavua kwenye mada yako serikali imeweka msururu wa kodi na tozo kwa bodhaa/huduma moja hadi kumlemea mlaji.
Yaani Serikali hata ingeamua kuacha mambo yaende yenyewe (sababu hata sasa ni kama wananchi (wenye nchi) wamekuwa Yatima mambo yangekuwa bora
Mfano mwingine ni saga ya starlink ambayo watoa huduma nchini hawataki kuisikia. Wanajua ikiingia watappteza wateja upande wa data. Sidhani kama serikali inaihofia starlink bali ni watoa huduma wanaofanya hizo lobbying kujihakikishia 'monopoly'.
Hata Starlink ikija hakuna tofauti sababu shida ni TCRA / Serikali ambayo inaogopa kukosa hizo senti za hapa na pale... kabla ya bei elekezi kulikuwa na mpaka bundle za bure husika kwa baadhi ya wato huduma..., ndio maana kuna kipindi ilivyokuja Skype Tanzania ilipigwa marufuku ili TTCL / Serikali isikose pesa kwa watu kupiga simu ulaya kwa kutumia Internet..., na ndio maana walisikika wabunge (waliogeuka kutetea serikali badala ya kuwakilisha mwananchi) waliposema waangalie ni jinsi gani wanaweza kuchaji matumizi ya kwenye whatsapp na other social media..., Tatizo ni Serikali wamegeuka kuwa wachumaji badala ya wasambazaji wa huduma
Njia nzuri ya hizi kampuni kujihakikishia milki ya wateja ni kuwapa huduma stahili na rafiki wateja ili wajisikie aibu kuacha kutumia huduma husika. Njia mojawapo ni hii ya NIBANDIKE
Njia rahisi ni kuwaachie wajinafasi kwa kufanya wanachotaka kufanya iwe nibandike, nipatie au nimwagie... (does not matter) na kuepusha cartels UMMA / Serikali tuna TTCL na share nyingi Airtel kama kweli Serikali ni vichwa wawekeze huko na kuwa shamba Darasa mnunuzi atachagua pa kwenda....
 
Hii kitu mbona tayari ipo? Kama siyo voda ni tigo nimeiona kwa macho yangu kwenye laini yangu
 
That is nature of the Beast Kampuni ni Answerable kwa Shareholder wala haipo pale kufanya charity, hata ikitoa huduma hio ni by the way ila the core mission is to get as much money as possible, ndio maana the only way ya kuhakikisha hawa watu wanabanwa ni ushindani baina yao ili mmoja wapo akibana sana mnunuzi watu wapate alternative

Hilo ni kosa sababu Dhima ya Serikali ni kuhudumia wenye nchi (as much affordable service as it can sustainable offer) na kosa ndio lipo hapo hawa watu wameguka kuwa Kero badala ya msaada na bila faida kwa mwananchi


Yaani Serikali hata ingeamua kuacha mambo yaende yenyewe (sababu hata sasa ni kama wananchi (wenye nchi) wamekuwa Yatima mambo yangekuwa bora

Hata Starlink ikija hakuna tofauti sababu shida ni TCRA / Serikali ambayo inaogopa kukosa hizo senti za hapa na pale... kabla ya bei elekezi kulikuwa na mpaka bundle za bure husika kwa baadhi ya wato huduma..., ndio maana kuna kipindi ilivyokuja Skype Tanzania ilipigwa marufuku ili TTCL / Serikali isikose pesa kwa watu kupiga simu ulaya kwa kutumia Internet..., na ndio maana walisikika wabunge (waliogeuka kutetea serikali badala ya kuwakilisha mwananchi) waliposema waangalie ni jinsi gani wanaweza kuchaji matumizi ya kwenye whatsapp na other social media..., Tatizo ni Serikali wamegeuka kuwa wachumaji badala ya wasambazaji wa huduma

Njia rahisi ni kuwaachie wajinafasi kwa kufanya wanachotaka kufanya iwe nibandike, nipatie au nimwagie... (does not matter) na kuepusha cartels UMMA / Serikali tuna TTCL na share nyingi Airtel kama kweli Serikali ni vichwa wawekeze huko na kuwa shamba Darasa mnunuzi atachagua pa kwenda....
Ukweli ni kwamba ttcl wala tusiwaweke kwenye consideration. Wameshabebwa sana, na kipindi cha Magu walibebwa sana ila bado tija haikuonekana. Pale watakapopewa monopoly au pendeleo na serikali ndio wanaongeza kujisahau. Sikatai kwamba intaneti yao ni nzuri. Wanayo nzuri kuliko Raha na wengine, shida ni maintenance.

Mfano mdogo tu tabata kule kuna waya wao umekatika tangu jana asubuhi. Upo kwenye lami na unakanyagwa. Umekatika sehemu kubwa sana na taarifa wamepewa ila hadi asubuhi ya leo waya wao upo chini. Hawa dawa yao ni kuwaacha ushindani uwaondoe maana hawategemei kipato kutokana na huduma wanayotoa bali ruzuku toka serikalini ambazo ni kodi na tozo mbalimbali.
Kwa hizi kampuni zingine ambazo hazina ruzuku ninachojua nao pia wanapata faida sana tu. Kubwa ninalowa challenge nalo ni wawe na open door policy. Wameweka vizingiti vingi sana kwa wateja kiasi kwamba hawafikiki, ila wao wakitaka kukufikia wanaweza. Utalijua hili pale ambapo una jambo nao
 
Ukweli ni kwamba ttcl wala tusiwaweke kwenye consideration. Wameshabebwa sana, na kipindi cha Magu walibebwa sana ila bado tija haikuonekana.
TTCL hatuwezi kuwasahau tena inabidi tuwabebe tatizo tusiangalie mambo as what it is but what is should be wakati tunaona kina HALOTEL wanafaa wakati wametokea Vietnam mali ya Huko na huku wamekuja wamebebwa na kuweza kusambaa kwanini na sisi TTCL tusiende mpaka huko..., Kumbuka badala ya kulalamikia Kampuni binafsi na kuzipangia mambo ya kufanya kwanini hayo mawazo mazuri tusiyaweke kwenye Kampuni yetu (Na kama hakuna Tija basi fukuza weka watu wenye Tija) Iwapo kama Taifa na wasomi wote tunashindwa kuendesha tu Kampuni ya Simu ambayo kila kitu kipo wazi, tuna infrastructure yote na tunaweza kufanya copy and paste kweli ndio tutaweza kupanga bajeti ya nchi na kuunganisha all the units kuwa kitu kimoja ?
Pale watakapopewa monopoly au pendeleo na serikali ndio wanaongeza kujisahau. Sikatai kwamba intaneti yao ni nzuri. Wanayo nzuri kuliko Raha na wengine, shida ni maintenance.
Ni kwamba hakuna teknolojia ya kuwapa watu target na kufuatilia kwanini hawafanyi ipasavyo ? Dunia hii ya Block Chain tunashindwa kujua nani anatakiwa afanye nini na kwa wakati gani na kwanini hafanya na kiasi gani kinaingia na kwanini hakiingizwi kwenye development ?

Bila TTCL ambayo ni ya UMMA na moja ya Mission yake ni huduma kwa wananchi kuwaachia watu ambao dhima yao ni profit at all costs ni rahisi sana kufanya cartels na mwisho wa siku wote kutoa service ya gharama ila kama TTCL yupo anaweza akawa alternative (yeye anajali Huduma sababu ni mali ya UMMA)
Mfano mdogo tu tabata kule kuna waya wao umekatika tangu jana asubuhi. Upo kwenye lami na unakanyagwa. Umekatika sehemu kubwa sana na taarifa wamepewa ila hadi asubuhi ya leo waya wao upo chini.
Kwahio hapo tatizo ni nini ? Kwamba tunashindwa kujua meneja wa sehemu husika ni nani na wafanyakazi wa sehemu husika ni kina nani ? Tatizo la kutokuwa na uwajibikaji sio kuuza wala kuachia mali ya UMMA bali ni kuhakikisha kuna uwajibikaji mbona rahisi sana kina mtu akipewa targets na kuangaliwa na kupimwa kwa performance na kuweza kufukuzwa kama hakajidhi hizo performances ?
Hawa dawa yao ni kuwaacha ushindani uwaondoe maana hawategemei kipato kutokana na huduma wanayotoa bali ruzuku toka serikalini ambazo ni kodi na tozo mbalimbali.
Ushindani upo na uendelee lakini mali kama hii ni muhimu kuhakikisha hakuna faulo.., kwanini TTCL isifike mpaka Huko Bara la Asia kama Halotel imeweza kufika huku ? Ukiongelea Tozo na Kodi unataka hizo Tozo zifanye nini kama mpaka dakika hii hakuna lolote linalofanyika na kwanza Kodi zinazidi huduma zinapungua (Hata Bundle kupanda ni sababu ya hizo Tozo)

Kwa hizi kampuni zingine ambazo hazina ruzuku ninachojua nao pia wanapata faida sana tu.
Naam na wasingepata faida wangeshaacha kufanya kazi na wapo hapa kutengeneza faida wala sio kutoa huduma au kutangaza Injili..., kwahio waache faida na wapate kutokana na uwekezaji wao na jinsi wao wanavyoona wanaweza kufanya makamuzi..., the only alternative ni wewe kutumia Kampuni yako ya UMMA kushindana nao na kuhakikisha unaboresha pale unapoona wewe pana kasoro
Kubwa ninalowa challenge nalo ni wawe na open door policy. Wameweka vizingiti vingi sana kwa wateja kiasi kwamba hawafikiki, ila wao wakitaka kukufikia wanaweza. Utalijua hili pale ambapo una jambo nao
Na mimi nakwambia kuna mambo mengi huwa wanafanya na yapo kwenye their Research and Development ingawa Serikali inawapiga sana pini kila wakichomoza kwa red tapes kibao as well as matozo..., Kila mwaka wanatenga fungu kubwa sana kwenda kwenye Promotion na R & D, ingawa sasa hivi kampuni nyingi kuna services zimeshuka kutokana na kwamba wanafanya outsourcing (kuongeza madalali) na mwisho wa siku madalali hao they dont care about company brand au mission...
 
Back
Top Bottom