Warioba afichua siri nzito


Kampuni ya Umoja inamilikiwa na familia ya Warioba, kampuni ya VMB inamilikiwa na familiaya Mahalu, kampuni ya YM inamilikiwa Yussuf Mushi, kampuni ya CCM Trust wenye hisa ni Warioba na Yussuf Mushi na si wadhamini wa CCM. Kazi kwenu
 

Kwanza ujue mimi sina chuki na Mzee Wetu , bali nina chuki na Ufisadi, Pili inaonekana unatetea kitu kwa sababu labda ya maslahi yako moja kwa moja au indirectly, kwa sababu umeshindwa kuwa- objective, au kwa kuwa unamapenzi na mzee kama sisi sote tulivyo na mapenzi nae, kinacho tutatanisha ni kuwemo kwenye kundi la kenge wakati yeye ni samaki.

Msingi wa hili suala ni utata wa uanzishwaji wake, maana kama ni kitu cha srekali kinatakiwa kiwe published in Government Gazette, kuna azimio la serikali towards it, kama alitengeneza hiyo memo na articles , sasa iweje akaendelea kuwemo humo, kama mwenyekiti, na shareholder, tatu yeye kama Mwanasheria Mkuu wa Serekali anajua taratibu au articles na memo za BOT kuhusu kutoua mikopo , tatu alipoona serekali anayo dai ilianzisha na serikali, na serikali hiyo hiyo ikaamua wachimbaji or what ever wa export raw gold, si angeamua kujitoa kwenye kampuni kama hiyo, ili kulinda jina lake zuri na pensheni yake nzuri kama mstaafu.
 
Kampuni ya Umoja inamilikiwa na familia ya Warioba, kampuni ya VMB inamilikiwa na familiaya Mahalu, kampuni ya YM inamilikiwa Yussuf Mushi, kampuni ya CCM Trust wenye hisa ni Warioba na Yussuf Mushi na si wadhamini wa CCM. Kazi kwenu

hivi ndio vitu alitakiwa kuviongea kwa uwazi si kujificha ficha kwa nia nzuri ya serikali wakati nia halisi ni kujitajirisha yeye binafsi na kundi lake. kwa kuwapatia wananchi kiduchu ya kile atakacho pata
 
Kampuni ya Umoja inamilikiwa na familia ya Warioba, kampuni ya VMB inamilikiwa na familiaya Mahalu, kampuni ya YM inamilikiwa Yussuf Mushi, kampuni ya CCM Trust wenye hisa ni Warioba na Yussuf Mushi na si wadhamini wa CCM. Kazi kwenu

Mzee Warioba anahusika hapa, maelezo yake na sakata zima lilivyo inaonyesha bila shaka kwamba Mzee amefanya ufisadi. Namheshimu sana Mzee Warioba, lakini si katika hili. Mzee Warioba bora awe muungana wa kwanza kukubali kuhusika na ufisadi huu.

Pesa ni tamu aise, hata hawa majaji!
 
Kuna uwezekano mkubwa kampuni ya Mwananchi ilianzishwa kwania nzuri kabisa ila
ninapata wakati mgumu kuamini na kuheshimu kile anachosema mzee Warioba kwasababu kuu tatu.

{1}Jaji Warioba alihusika kupitia kampuni yake kutoa ushauri wa kuanzisha mwananchi.Mpaka hapo sina tatizo na mzee wetu Warioba kwasababu hiyo ni kazi yake.

{2}Jaji Warioba akawa mwanahisa wa mwananchi Gold.Hapa kiwingu kinaanza,naomba kuelimishwa hivi ukitoa ushauri wa kisheria kwa kampuni unakuwa mwanahisa au hii imekaa vipi.

{3}Jaji Warioba anakuwa chairman wa board.Sijui nani alimteua au labda alikuwa na hisa nyingi !!!!.

Conclusion Jaji Warioba ni mtu analiyebobea katika fani ya sheria na alikuwa anajua nini anafanya.Ajiandae kwenda kisutu asiwaambie waandishi wa habari yuko tayari kwenda mahakamani hizo ni dalili za woga,kama kweli yuko safi asubiri siku ifike.
 

Watanzania tungependa kufahamu ili kupata hisa za 15% toka Mwananchi, CCM ilitoa kiasi gani ili kuchangia mtaji wa kampuni hiyo?
 
Judge Warioba first says that Mwananchi Gold was the brainchild and is owned by the Government. Later on he says that CCM is the major shareholder!! Does the Judge expect us to believe that CCM and the Sirikali are the one and same thing? He needs to be reminded that the era of a one party state is long gone!

If indeed this company is Government owned, then the Controller and Auditor General should tell us that he has audited the accounts of Mwananchi Gold and as is the practice with other parastatals, these should be made public.
 

Mwanakijiji,

..Chief Justice Nyalali alifariki 2003.

..kwenye hiyo Law Firm ya kina Warioba, kama sijakosea, yuko Justice Lameck Mfalila[rtd].
 

SISI EMU Ni NANI? Mi nafikiri sisi emu ni pamoja na sisi wananchi. Ikifika uchaguzi wananchi ndiyo sisi emu, kwenye masuala ya pesa na miradi inayohusu pesa na maliasili yetu "wana sisi emu" wanakuwa wachache tu 'MAFISADI'. Wanatutenga wananchi wakishapata kura (kula). Mengi tutayajua nayakati hizi za mwisho, ndiyo maana kila mtu anakimbilia/anangángánia huko SISI EMU hata kama ni kwa kukopa saudi arabia.

Wanajua kuwa huko kuna biashara wanazozifanya bila kuwa na mtaji!!! Wanakula mpaka wanapasuka kwa kunyonya damu za wananchi. Laana ya Mungu iwajae, na panga la moto litawakata na kuwachoma. MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WALALA HOI.

NAOMBA WIMBO WA TAIFA UREKEBISHWE SASA HATUHITAJI KUWABARIKI VIONGOZI TENA!

Endeleeni kuleta nyanga hapa.
 

".... serikali ilikuja kwenye ofisi yetu ya uwakili ya Nyalali, Warioba & Mahalu Law Associates ili tuisaidie kuipatia huduma ya kisheria kabla na baada ya kuundwa kwa kampuni hiyo."

Nani alikuja kwenye ofisi yako, kivipi, ulichaguliwaje?

Ufisadi huwa unaanza asubuhi.

Wakina Mkono nao ilibidi waeleze walivyopata tenda ya BOT. Waziri Ngeleja juzi juzi nae akataka kwenda kujinunulisha mashine za Dowans bila kufuata tararibu za tenda kabla hawajamstopisha. Mramba-Mgonja-Yona axis of corruption nayo ilivunja taratibu za tenda. Huyu msomali wa Dowans aliyemalizwa jana Kisutu nae tunaambiwa alifoji affidavits katika procedure za kupata tenda. Railways nayo ilivyopewa wahindi wasiojulikana nayo hivyo hivyo, taratibu za tenda, sasa hivi tunaambiwa ATC na TAZARA wanataka kupewa sijui wachina gani sijui. Baadae tutaanza kulizana. Tenda, tenda, tenda, tenda!

 
...
{1}Jaji Warioba alihusika kupitia kampuni yake kutoa ushauri wa kuanzisha mwananchi.Mpaka hapo sina tatizo na mzee wetu Warioba kwasababu hiyo ni kazi yake.
.......hata kwenye hiyo namba {1} bado Warioba ana maswali mengi ya kujibu:

  • kwanini tangu awali hakumshauri mteja wake (Serikali) achapishe nia yake ya kutumia kodi ya wananchi kupitia Government Gazzete?
  • kwanini alikaa kimya ilhali akijua Serikali, ambayo tayari ilishakana Azimio la Arusha kupitia lile la siri la Zanzibar, inajiingiza kwenye biashara pasipo ridhaa ya wananchi?
  • Kwanini hakuwa muungwana kuweka bayana upatikanaji wa hisa za kampuni hiyo ili wananchi na vyama vingine vya siasa wapate hisa (kama anadai "CCM Trust Company" ni mali ya SSM?
Kama tutakuwa makini tutampata mbaya wetu kupitia kauli hii ya Warioba. Hata kama Serikali ikikaa kimya Warioba anapaswa kufikishwa Kisutu ili tumjue mdudu anayeimaliza Tanzania.
 
Huyu mzee ni JAJI mstaafu na ndo alikuwa Attorney General wa Jamhuri yetu, Kitu kinachonifanya niamini kwamba huyu mzee sheria anaijua vyema. Sasa kweli tangu lini Serikali/Dola ikaenda kuomba ushauri wa kuanzisha kampuni/mradi kwa Kampuni binafsi? (Yes its possible but in very rare and extreme case). Mwanasheria mkuu wa serikali na wanasheria wake wanalipwa pesa ya nini? This is pure comedy. Sioni sababu zozote zile kwa nini serikali iende kuomba msaada kwenye private Law firm wakati kuna substantial amount ya hela ya walipa kodi iko involved ($5M). I dont see compelling facts/reasons. Kwa sababu hii ni legal advice pure!

Ok, Assume Law Firm ya Warioba ilikuwa consulted kama experts wa sheria (which I think is wrong though because we have Attorney General who is supposed to be the Legal Advisor wa serikali)..sasa ilikuwaje Warioba akawa mwanahisa kwenye hiyo kampuni? I dont get it! Na anasema kabisa kwamba BOT WALITUKOPESHA DOLA MILLION TANO! Hakuona conflcit of interests hapa?

Well, hapa ukiangalia vyema this was a dirty deal na nadhani Warioba anataka kuplay VICTIM CARD kwamba anaonewa na wabaya wake kisiasa... Lakini kama wengine walivyosema, deal za chini ya meza matokeo yake ndo hayo. Huyu mzee he was in a position to know better. Na katika siasa, kila mtu anaubeba mzigo wake. Sana sana BOT itakuwa on the spot na ofcourse the usual suspect Mkapa atakuwa involved kwenye hili deal.

Hii kesi itaibua mengi, kama mwanakijiji alivyosema..CCM wataruka! na ndo yatatoka maswali mengi kuliko majibu...
 
Kampuni za sheria ziko nyingi, warioba anapaswa kuelezea kwa nini wao walipewa kazi ambayo hawajaomba?

Hivi warioba anatuona sisi ni watoto wa kuwadanganya kuwa wao walifuatwa na ''serikali'' kupewa deal ambayo ni nzuri na hawajaiomba na wao wakaamini kuwa huo ni utaratibu wa kawaida na kila kitu kikafanyika legally? warioba acha politics za miaka ya sabini this is 2009.
 
Naona kuwa Waryoba yuko matatani kabisa, na sidhani kama atakwepa. Ninaanza kuelewa kwa nini alikuwa akitetea watu wasimsakame Mkapa. Inaelekea Mkapa alimgawia kitu hiki ili anyamaze asiendelee kupiga kelele kuhusu ile ripoti yake ya rushwa halafu akaibugia bila hata kunawa mikono. Mkapa alikuwa na namna ya kuwanyamazisha wanasiasa wa aina yake kama akina Mzindakaya, na nadhani alitumia njia hiyo hiyo kumnyamazisha huyu Waryoba, lakini sasa atakuwa amekalia makaa ya moto.

Najaribu kufikiri jinsi gani Bwana Nalaila Kiula, George Mlingwa na Bwana Stephen Wassira (mgomvi wake wa kisiasa kwa kiti cha Bunda) watakavyofurahi kumwona jamaa akipelekwa keko!!

maelezo yake yamejikanganya sana halafu mtu ukipitia rekodi zilizoko kuhusiana na sakata hilo ndipo unagundua kuwa Mzee yuko matatani. Iweje kweli serikali "iiombe" kampuni yake binafsi ya sheria "kusaidia" uanzishaji wa kampuni hiyo ambayo baadaye ilipewa fedha na benki kuu katika "utaratibu usio wa kisheria" na baadaye kampuni hiyo inayeyuka bila kulipa fedha za umma kinyume cha sheria?

Halafu basi baada ya serikali "kumwomba" atoe huo ushauri wa kisheria kuisaidia kampuni hiyo mpya, inakuwaje kampuni hiyo iliyoanzishwa kwa maelekezo ya serikali inakuwa na wabia ambao ni makampuni ya watu binafsi tu, na tena mwenyekiti wa bodi yake akiwa ni yeye huyo huyo Waryoba?

Maswali ya kutatanisha yanazidi kuwa mengi, ngoja mimi niwahi kiti pale kisutu kusudi niweze kumsikiliza mzee wa sheria akijitetea.
 

Warioba?? former prime minister? mwanasheria mahiri?

Si mramba huyu au Yona, pia sijaona bado alipojichanganya wapi, labda nisaidie!
 
Warioba?? former prime minister? mwanasheria mahiri?

Si mramba huyu au Yona, pia sijaona bado alipojichanganya wapi, labda nisaidie!

Waberoya,
Hata mie nimeanza kusoma nilikuwa sijui lolote. Ila nilianzia ukurasa wa kwanza na hadi kufika mwisho, nimeshaelewa kila kitu. NA WEWE NENDA UKAFANYE HIVYO. Vinginevyo, basi unaona kile tu unataka wewe ukione. Mzee kweli maji ya shingo. Mwanzo nilifikiri akina Mtanzania wanadanganya juu ya huyu Mzee.

Ila sasa nimeelewa na kwa kweli siasa kitu kibaya. Mkapa kalisha watu wengi sumu na ukichunguza sana, utagundua kuwa kuanzia juu hadi wabunge wetu, walikula ASALI hiyo ya mti wa kati.

Mtanzania nakubali sasa maneno yako. USIMWAMINI MWANASIASA.
 
- Hakuna jipya hapa sisi tumeyasema sana hapa kwamba huyu mzee ni another fisadi, sasa anajaribu kuwatisha serikali wait and see watakavyomfumulia mambo yake, yaani aibu tupu huyu ni fisadi tu hivi hiyo kampuni yao ya sheria ilikuwa ni lazima ianzishwe na Waziri Mkuu Mstaafu, Mwanasheria Mkuu Mstaafu, na Balozi wetu Italy ambaye ni rafiki wa karibu wa rais wetu Mkapa?

- Ni wanasheria wangapi Tanzania toka tupate uhuru wanaweza kusimama mbele ya public na kutuambia kua serikali iliwahi kwenda kwenye ofisi zao na kuomba msaada? What a nonesense? Haoni hata aibu kusema haya! Wanasheria wote tulionao serikalini ambao wamesoma mpaka mwisho wa elimu hawafai ila yeye Mahalu na Nyalali ndio waliokuwa wanafaa? Warioba amewahi kusimamia kesi ngapi kwenye mahakama zetu toka awe mwanasheria wa kujitegemea? Au nyalali aliwahi kusimamia kesi gani ya wezi wa kuku na mbuzi? au Mahalu ni lini aliwahi kusimamia kesi yoyote kwenye mahakama zetu? Hilo shirika wanaliendesha kwa hela kutoka wapi?

- Usafi wa Warioba unatokea wapi? Ni nani aliyekua akimlipia Wassira kusoma kule USA ili asirudi kumsumbua Warioba kwenye jimbo lake la ubunge?, wakati Warioba akiwa waziri mkuu? Kwa nini hawa viongozi wanapenda kutuchezea wananchi? Hivi Warioba kweli anaamini kuwa wanasheria wa serikali yetu ni wajinga kwamba wanaweza kumzushia kesi bila sababu huku wakijua wazi kwamba ni mtafutaji wa cheap popularity? Kama kweli sio fisadi kwa nini alipoona tu Mramba na Yona wako Kisutu, akaanza kuwapigia simu viongozi wanaohusika na sheria na kuanza kuwatukana kua hiyo kamata kamata wanawatisha viongozi kutoifanyia kazi nzuri serikali? Haya ni maneno ya kusemwa na Warioba, asiye fisadi? Na ambaye amekua akilia sana kuwa rushwa imezidi? Yeye ni msafi sasa leo wanakamatwa viongozi mafisadi halafu anatishia viongozi na maneno ya hovyo hovyo, WHY?

- Warioba anyamaze asubiri tu zamu yake ifike atinge Kisutu kama inakuja, lakini asitishie nyau serikali, I mean ninawaomba serikali yetu kutojiingiza kabisa na huu mtego wa Warioba wa kutaka kuigeuza sheria kua siasa, that is all he is trying to do sasa dawa ni serikali kuendelea na kazi yake kama kawaida bila kumjali na siku ikifika atinge tu Kisutu, lakini asilete ngebe, huyu Warioba si ndie aliyehesabu kura za mazishi zilizompa urais Mkapa mwaka 1995, leo anaweza kusimama mbele ya public na kutuambia kua matokeo aliyoyatangaza baada ya kuhesabu zile kura na kumpa urais Mkapa over Kikwete yalikua ni ya kweli? Hana hata aibu dhahabu inachimbwa wapi halafu yeye anashauri ikasafishiwe wapi eti?

Hivi kwa nini amekua akihangaika sana toka Mramba na Yona watinge Kisutu? WHY? Serikali haina sababu ya kumjibu, wamalize uchunguzi wao kama kuna kesi atinge tu, sio yeye tu kiongozi yoyote yule, wa sasa au zamani kusiwe na msamaha wala huruma,

Warioba anajaribu kudanganya toto hapa kwamba hatujui kuwa ukiona moshi maana yake chini kuna nini? Tena huyu inaonekana kuwa anajua mengi sana, ikibidi apewe immunity kwa masharti kwamba aseme yote anayoyajua, lakini muamuzi wa mwisho tutakuwa ni sisi wananchi sio yeye!

Finally, inaonyesha serikali iko kwenye the right track na hawa mafisadi, sasa hivi utawasikia na wegine, ingawa huyu Warioba anastahili sifa kidogo kwa kutokimbilia kupiga kelele jimboni, lakini serikali ikamate hapo hapo mpaka kieleweke!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…