Warioba afichua siri nzito

Warioba afichua siri nzito

FMES,
Mkuu sijawahi kuona statement ya Warioba akisema majina ya Mafisadi ni kuligawa Taifa..isipokuwa nakumbuka alizungumzia kuwepo kwa hao untouchbles ndio tunaligawa taifa!

Nje ya Mwananchi Gold, mkuu wangu unaweza kunipa Ufisadi wa Warioba na vitu ambavyo kavuna kutokana na Ufisadi wake..(ukweli wa mwananchi sina haja tena kuufahamu unless serikali ijitokeze na kupinga manenoa yake) maanake wapo watu wanaweza hata kusema kina Kawawa, Malecela, Msuya wote ni mafisadi kwa sababu tu zinazowapendeza wao.
 
Mkuu sijawahi kuona statement ya Warioba akisema majina ya Mafisadi ni kuligawa Taifa..isipokuwa nakumbuka alizungumzia kuwepo kwa hao untouchbles ndio tunaligawa taifa!..

- Mkuu Bob, kwenye hii topic sijaona hoja zako, lakini kwa haya ni kwamba mimi nimeona maneno ya Warioba mara baada ya Dr. Slaaa kutoa majina ya mafisadi, ambao mimi nilikuwa mtu wa kwanza kuyaleta hapa JF, alisema kwamba kitendo cha Dr. Slaaa ni cha hatari sana na kinaweza kuligawa taifa, na besides Warioba hakuafiki kabisa kitendo cha kamati ya Mwakyembe na kutoa to the public uchunguzi wa Lowassa na Richimonduli, sasa wewe huenda hujawahi kuyaona haya lakini mimi nimeyaona na ndio maana sijawahi kumuamini Warioba hata siku moja, Salim aliposhindwa aliwatukana sana Mtandao na Mkapa, lakini within a week akawa mshauri wa Mtandao, ukitafuta utaziona picha za siku Kikwete, aliporuidi Dar toka Dodoma kama mgombea rasmi wa CCM, zilpigiwa nyumbani kwa Kikwete utamuona Warioba pembeni yake tena mwenye furaha sana!

Lakini bado ni haki yako kuamini kuwa Warioba ni malaika, na mimi ni haki yangu kuamini ninavyoamini kuwa ni fisadi na kama Warioba sio fisadi basi aitoe to the public ile ripoti ya kamati yake ya rushwa kama kweli anao ubavu wa usafi!


Nje ya Mwananchi Gold, mkuu wangu unaweza kunipa Ufisadi wa Warioba na vitu ambavyo kavuna kutokana na Ufisadi wake..(ukweli wa mwananchi sina haja tena kuufahamu unless serikali ijitokeze na kupinga manenoa yake)

- Binafsi ninaamini kwamba kama ni kweli Warioba angekua msafi na Mwananchi, angeshamshitaki Mengi kama alivyoahidi huko nyuma kwa kumuita fisadi kutokana na hii kampuni. Sihitaji kuumiza kichwa changu na hii ishu maana najua Warioba ana ufisadi nayo, look sasa inamhusisha mpaka Mahalu, kama balozi wetu Italy na kama mshiriki wake Warioba kwenye shirika lao la sheria. Na besides sina tatizo na kukiamini chanzo cha magazeti ya Mengi, maana hayawezi kusema uongo kuhusu ufisadi wa Mkapa na Lowassa, lakini yakamsingizia Warioba tu! Siamini kwamba serikali inahitaji kujibizana na Warioba kwenye media, hiyo sio kazi ya serikali hata siku moja kazi yao ni kutekeleza majukumu yao ambayo ndio yetu pia wananchi, kama ya kuwaburuza wakulu Kisutu.

Warioba angekwua msafi na Mwananchi, angesema mapema anayosema sasa hata kabla magazeti ya Mengi hayajasema kitu na serikali haijaanza kumchunguza, kuanza kulia saa hizi ni too late kwake, kina Mramba mbona hawakul;ia lia unafikiri hawakujua kua wako njiani kutinga Kisutu? Mimi niliesma one year mapema sasa ikawaje wao wasijue? Warioba anajarib u kutishia nyau tu lakini ninaamini serikali inajua inachokifanya, tunachoitaka ni ukweli na haki za Warioba ksiheria ziheshimiwe, lakini serikali ikamate hapo hapo wananchi kama mimi tupo nao! Lakini pia ni haki yako kuamini kuwa Warioba ni clean, good for you!


maanake wapo watu wanaweza hata kusema kina Kawawa, Malecela, Msuya wote ni mafisadi kwa sababu tu zinazowapendeza wao.

- Magazeti ya Mengi hayajatoa sababu za ufisadi wa Warioba, Mkapa na Lowassa zinaowapendeza wao, na wewe unajua vizuri sana kwamba huwezi kusema ukweli ukageuka kua uongo na huwezi sema uongo ukawa ukweli, fisadi ni fisadi tu hata akiwa waziri mkuu wa zamani, saaa ya ukweli sasa imefika, hatutaogopa kusema ukweli au kuuchambua ukweli, kama wewe Bob una ukweli kuhusu ufisadi wa Msuya, Kawawa na Malecela ni bora uuanzishie thread mapema, maana huu ni Warioba na tutaendelea kuuchambua bila wasi wasi, wakti wa hadithi umeanza kufika mwisho, sasa kazi!

Na kama kawaida kwenye kumkoma nyani huwa hatuwezi kumuangalia usoni!
 
Lakini bado ni haki yako kuamini kuwa Warioba ni malaika, na mimi ni haki yangu kuamini ninavyoamini kuwa ni fisadi na kama Warioba sio fisadi basi aitoe to the public ile ripoti ya kamati yake ya rushwa kama kweli anao ubavu wa usafi!

Kama una kumbukumbu nzuri, ripoti ya rushwa ya tume ya Warioba ilitolewa to the public na ilichapishwa kwenye magazeti karibu yote ya wakati huo. Hivyo, ripoti hiyo haijawahi kuwa siri. Mimi mwenyewe niliisoma kwenye magazeti.

Executive summary ya report yenyewe ninaiambatanisha hapa. Report nzima inapatikana kwenye maktaba ya utumishi maana ni two books volumes.
 

Attachments

Last edited:
FMES,
Mkuu naona sasa unachanganya vitu hapa. Ni Malecela aliyepinga sana list ya mafisadi tena bungeni na nakumbuka vizuri kuwa Warioba alikuwa mtu wa mwanzo kulaani wakafuata kina Mwinyi, Chevji, Butiku na wengineo, wewe uliwashambulia sana Butiku na Warioba kuwa nao ni mafisadi.. Warioba on Mwananchi na Butiku ktk mfumo wa Mwalimu...nakumbuka vizuri sana mkuu na naomba kama mada ile bado ipo ama imehifadhiwa irudishwe.

Kuhusu Warioba kuwepo ktk uteuzi wa Kikwete na furaha, mkuu wangu sijui nani hakuwa na furaha hiyo hata mimi hapa nilifurahi pamoja na kwamba kitu kimoja tu nilichofahamu na kunikera wakati ule ni kutorudishwa nyumba za serikali.. zaidi ya yote haya hakuna kati yetu aliyefahamu list ya mafisadi...hata iule ya Mafia ya kina Patel ilikuwa haijatoka bado. Zaidi sote tulihofia RA na Lowassa kama ulivyotufahamisha wewe.

Magazeti ya Mengi yame report wanachofahamu kaa sisi sote tuliofikiria kwamba Warioba ana share ndani ya Mwananchi na shirika hilo limekuwa na utata mkubwa kufahamu kinachoendelea ndani yake sawa na lile shirika linalomilikiwa na Jeshi..Mengi nampa kila heko kuweza kufukua swala hili na ukweli ndio huu sasa hivi tunao.

Je, serikali inapinga kwamba ni wao walianzisha hili shirika na baadaye kulifuta ktk mradi muhimu kama huo.. Licha ya hapo report ya Warioba inaonyesha wazi hakuna Ulaji ktk Mwananchi zaidi ya watu fulani kulitumia shirika hilo kwa manufaa yao kisha wakaingia mitini.

Hatufahamu ni kiasi gani serikali ilitenga kuanzisha shirika hilo, hesabu ya dhahabu iliyowekwa BoT na kadhalika jambo ambalo kutokana na statement ya Warioba leo hii tunaweza kuulizia..Kama Wakili hana uwezo wowote wa kuiba hata senti tofauti na maelezo tuliyopata awali..

Kisha basi kama shirika huru (Incorporated) sioni kosa kabisa la kiutendaji kumwajiri Warioba na zaidfi ya hapo wengi wetu tuliwekea mashaka Mwananchi tukidhani ni shirika la nje wakitumia wazawa kutumaliza kumbe ni serikali ile ile ya Mkapa.
 
"Following a request from the Chairman of the company's Board of Directors, former Prime Minister, Joseph Warioba, who is also one of the shareholders in the project, the BoT injected a further $ 95,000 (around 100m/-) as a loan to the private, commercial project contrary to its own law." From Thisday

Hiyo conflict of interest babu kubwa, mwenyekiti wa board, shareholder na kampuni yake ndio inatoa ushauri wa kisheria. Hivi judge Warioba kweli hilo hakuliona wala hakuona ni tatizo?
Exactly my questions
 
Mkuu naona sasa unachanganya vitu hapa.. Ni Malecela aliyepinga sana list ya mafisadi tena bungeni na nakumbuka

- Mkuu Bob, acha kuzunguka mbuyu fungua thread inayomuhusu Malecela na ufisadi wake, hii ni ya Warioba na madudu yake ambayo sio mimi niliyeyaanika waazi, walianza Magazeti ya Mengi, na mimi ninawaunga mkono, kama hamkutaka Warioba ajadiliwe kaam mnavyoonyesha hapa basi mngemsaidia kunyamaza, maana kwa kwenda kwenye media amefungua milango yeye mwenyewe.

- Lakini kama Malecela ana ufisadi, basi ufungue topic yake karibu sana tena anytime! Ila hapa ni WArioba tu mpaka kieleweke!

- Unajua mwananchi yoyote wa Tanzania kuna maswali mengi tu serious ya kujiuliza hivi Warioba alifikaje kwenye uwaziri mkuu na makamu wa kwanza wa rais? I mean ukitazama njia nzima ni madudu matupu!
 
Mkuu Mkandara...

Mimi huwa nimekuwa nikimpa huyu Mzee wetu heshima kubwa tu, pamoja na anavyosemekana anapenda sana "chupa". Siku zote huwa nafurahishwa kusoma jinsi anavyopiga vitu hujuma mbalimbali. Nimemshangaa sana alipoanza kusema Dr Slaa akae kimya! Nihivyo hivyo nawashangaa hawa wenye kusema hakuna haja kushitaki mafisadi kwa vile kila Mtanzania mkono wake ni mchafu (Mbatia na NCCR), na pia wenye kusema kutakuwa na machafuko kama watu wakiulizwa! Niko kwenye school of thought ambayo iko radhi kuonyesha kisheria ni kwa utaratibu upi Rais anaweza kushtakiwa - kiasi kwamba kama Rais amekuwa FISADI, basi lazima katika ito mwanya wa kumsimamisha Kizimbani. Hatuwezi Tanzania ya 21st century kuruhusu impunity kwa Rais wa nchi. Mihimili na Milingo ya nchi ndio inatakiwa ndio ifanye kazi, kuna Bunge, Mahakama, Wananchi/Wapiga kura na hiyo Executive Office. Kamwe hatuweze kusema tunajenga nchi ya usawa wakati kuna watu wa Presidents Club ambao eti hawatakiwi kuulizwa maswali?? That is very, very wrong. Ukifuatilia historia ya nchi, wakati huo Governor wa nchi (ambae ndio kama imeishia kuwa Rais) alikuwa ndio Chief Executive Officer wa Mkoloni na alipewa madara makubwa mno mno kwa vile kulikuwa inaonekana hatuko tayari kujitawala. Ni huko mbeleni akina Sir Horace Bhyatt walipokuja na kuanzisha kushirkisha wananchi via machief wao. Naenda off topic, ila nataka kuonyesha kuwa Raisi kuwa untouchable Tanzania ilikuwa about 60 plus years ago. Leo hii, hilo kamwe halitakiwi kulindwa. Wakati ule bila shaka hapakuwa na wachambuzi wa mambo. Leo wamejaa tele na tena wanatoa uchambuzi wa kina. Leo hii tutantakiwa kulinda Utawala wa Sheria yenye kuweka watu wote kabisa sawa. Raisi ni mtumishi wa UMMA sio Mkuu wa Umma kama Boss Untouchable. Ni mtumishi nambari moja wa UMMA na anatakiwa kuwajibika kwa UMMA sio kwake au kwa familia yake au kwa title ye Presidency. Hivyo hvi vitisho eti nchi itanda kombo kwa kuclear mafisadi ni the oldest trick in the book. Ogopesha watu and then fanya vurugu and them get in back and try to pretend you are restoring things, kumbe ndio unawamaliza with controlling! Ndio theory of chaos hawa mabwana wanatuletea along with scare tactics! Tuwe wote makini ya hayo.

Hivyo, kitendo na Mzee Warioba kukubali kujiingiza kwenye mchakato mzima huo hapo juu ni wazi akili zake za interests za mtu wa chini, zilienda likizo kwa muda huo au bila shaka alitegemea kukaa kimya kwani Serikali isingemgusa. Hata kama CCM hapa wamemchezea, hana mwingine wa kulaumu ila yeye. The conflict of interest kutokana na roles zilivyokaa ni very open and very clear bila wasiwasi wowote hata kwa mtu asiejua darasa la sheria! Na hilo swala la local - yes ni mihumi sana. Lakini kwanini wasiweke hicho kiwanda huko mkoani?? Si ndio tunajenga wananchi and great opportunity for EPZ etc??

Mbona hatusikii watu wakihoji sera za CCM zinazosema do not privatise what is makes profit? Au ilishabadilishwa hiyo?? Hapa hatusikii juu ya value adding jobs nyumbani kupigiwa debe? Ingawa hii ya Mzee ina contradiction hapa, hili Swala la kuacha kusafishia nyumbani ni kubwa sana tuu nalo?? Mbana halichambuliwi kwa kina na kuhoji hadi Bungeni?? Bila shaka muda umefika sasa.

Hapa kuna kazi and we better wait and see, ila maswali yote ya msingi ni wazi kabisa. Na vile ameleta wazi, waache basi watoe minutes zote za vikao (utasiskia hawana)....
 
Last edited:
Kama una kumbukumbu nzuri, ripoti ya rushwa ya tume ya Warioba ilitolewa to the public na ilichapishwa kwenye magazeti karibu yote ya wakati huo. Hivyo, ripoti hiyo haijawahi kuwa siri. Mimi mwenyewe niliisoma kwenye magazeti. Executive summary ya report yenyewe ninaiambatanisha hapa. Report nzima inapatikana kwenye maktaba ya utumishi maana ni two books volumes.

- Mkuu hii ripoti ni yale yale ya mchezo wa bongo, imepunguzwa sana mkuu na kama haikupunguzwa basi ni nonesense at best, kwamba eti katika miaka 47 ya uhuru wetu Tanzania, ni Kilula, Ngasongwa na Mlingwa tu ndio mafisadi wetu wengine wote wasafi!

- Sasa kweli unataka mimi nimaini hayo ya hiyo ripoti kama wewe unavyoiamini? Warioba mwenyewe anajua ukweli wa hiyo ripoti maana kama hiyo iliyotolea ingekua ni yote basi yeye na Mkapa wangekua bado marafiki mpaka leo.

Lakini ashante sana kwa kinikumbusha kuhusu kuwepo kwa hiyo ropit mkuu.
 
INaelekea katika kutafuta maendeleo ya haraka, serikali ilikiuka misingi mingi sana, ambayo sasa inaifanya (au kuwafanya viongozi wake) kuingia kwenye matatizo makubwa.

Nakubaliana na wengi kwamba, inawezekana kuwepo kwa utata katika uanzishwaji na uendeshaji wa Mwananchi Gold. Ila naamini kuwa kuwepo kwa mkono wa Serikali katika mchakato mzima, kulifanya walioshiriki katika uanzishwaji/uendeshaji huo, kuona kuwa kila kitu kilikuwa halali na sahihi kabisa (akiwemo Mzee Warioba). Kila baada ya chaguzi zinazosababisha kubadilika kwa Serikali, mambo mapya hufichuka. Mambo ya zamani huonekana hayafai, labda kwa kuwa yalikiuka taratibu ama hayakuwa na maslahi kwa watu au taasisi mpya zinazokuja na Serikali mpya. Yote yanawezekana.

Katika issue ya Mwananchi Gold, sijui nani atamshitaki nani. Maana Serikali, CCM, BoT na baadhi ya Kampuni zinaonekana kumiliki Mwananchi Gold. Labda wamiliki wote washitakiwe. Ila kumshitaki mmiliki mmoja, sijui kama itatosheleza mahitaji ya kisheria (naomba msaada hapo).

Itakapofika wakati ambapo Serikali ya awamu hii ikabadilika (kwa uchaguzi) baada ya kumaliza muda wake, watakaoingia nao wataanza kufukuafukua mambo yao vile vile. Nao watatueleza mengi sana.
 
INaelekea katika kutafuta maendeleo ya haraka, serikali ilikiuka misingi mingi sana, ambayo sasa inaifanya (au kuwafanya viongozi wake) kuingia kwenye matatizo makubwa.

Nakubaliana na wengi kwamba, inawezekana kuwepo kwa utata katika uanzishwaji na uendeshaji wa Mwananchi Gold. Ila naamini kuwa kuwepo kwa mkono wa Serikali katika mchakato mzima, kulifanya walioshiriki katika uanzishwaji/uendeshaji huo, kuona kuwa kila kitu kilikuwa halali na sahihi kabisa (akiwemo Mzee Warioba). Kila baada ya chaguzi zinazosababisha kubadilika kwa Serikali, mambo mapya hufichuka. Mambo ya zamani huonekana hayafai, labda kwa kuwa yalikiuka taratibu ama hayakuwa na maslahi kwa watu au taasisi mpya zinazokuja na Serikali mpya. Yote yanawezekana.

Katika issue ya Mwananchi Gold, sijui nani atamshitaki nani. Maana Serikali, CCM, BoT na baadhi ya Kampuni zinaonekana kumiliki Mwananchi Gold. Labda wamiliki wote washitakiwe. Ila kumshitaki mmiliki mmoja, sijui kama itatosheleza mahitaji ya kisheria (naomba msaada hapo).

Itakapofika wakati ambapo Serikali ya awamu hii ikabadilika (kwa uchaguzi) baada ya kumaliza muda wake, watakaoingia nao wataanza kufukuafukua mambo yao vile vile. Nao watatueleza mengi sana.

Nashukuru kwa kuliona tatizo la uwazishwaji au uendeshwaji wa Mwananchi Gold, sasa hayo mengine ulio zungumzia nani wa kumshtaki nani tuwaachie wachunguzi , maana nionavyo kunawengine wanajificha nyuma ya hizo institution, kama ni CCm, BOT etc. itajulikana huko mbeleni.
Napenda tena kukupongeza kwa kuwa Objective na muelewa, na ujue sisi sote tunampenda warioba , lakini tunashangazwa na alichofanya au kilicho tokea, sasa akifika kisutu au what ever ndio tutakapo elewa vizuri ushiriki wake au kutoshiriki kwake
 
Wakati wa utawala wa BWM role ya central bank ilikuwacompromised; badala ya kujishuhuklisha na mambo ya kuthibiti mfumuko wa bei ili kustabilize uchumi wa nchi BOT walianza kufaya kazi ya kukopesha[guaratee] wateja kazi ambayoi hufanywa na commercial banks; hapa ndipo watu binafsi kama Mzindakaya wakapata upenyo wa kukopa mabilioni ya shilingi kutoka benki kwa guarantee ya BOT kuanzisha ranch ambayo katika uhai wa huyu bwana hawezi kumaliza deni na mwishowe BOT/wadanganyika itabidi tuje tulipe. Kwa misingi hiyo hiyo MWANANCHI GOLD iliingiza BOT kufanya shuhuri za kusafisha dhahabu kazi ambayo kisheria si kazi yake; nia ya kuongeza thamani kwa mali yetu ghafi ni nzuri tatizo ni jinsi tunavyozihusisha taasisi sizizohusika kufanya kazi hizo!! Warioba na team yake wasingeitumia BOT kubankroll mradi wao bali wangekwenda benki kukopa na kule kama mradi ungeonekana unalipa wangekopeshwa; walitumia siasa na si utaalamu kuanzisha hiyo kampuni ya kasafisha dhahabu na ndio maana wameingia hasara!! Haikufanyika thorough feasibility study ya kampuni hiyo bali utashi wa kisiasa ndio ulitawala na mwenyekiti wa CCM wakati huo nadhani alibaliki mradi huo!! Sinde Warioba should have known this better before he got into this Jam!!
 
- Mkuu hii ripoti ni yale yale ya mchezo wa bongo, imepunguzwa sana mkuu na kama haikupunguzwa basi ni nonesense at best, kwamba eti katika miaka 47 ya uhuru wetu Tanzania, ni Kilula, Ngasongwa na Mlingwa tu ndio mafisadi wetu wengine wote wasafi!

- Sasa kweli unataka mimi nimaini hayo ya hiyo ripoti kama wewe unavyoiamini? Warioba mwenyewe anajua ukweli wa hiyo ripoti maana kama hiyo iliyotolea ingekua ni yote basi yeye na Mkapa wangekua bado marafiki mpaka leo.

Lakini ashante sana kwa kinikumbusha kuhusu kuwepo kwa hiyo ropit mkuu.


Hii vita dhidi ya ufisadi ni "kitumbua kimeingia mchanga". Watu walikuwa wanapiga kelele kwa malengo ya kisiasa tu na wala siyo kutaka sheria ichukue mkondo wake. Kwa maneno mengine huu ulikuwa ni "MTAJI WA KISIASA" wakijua kwamba ni business as usual!!

Ama basi hawakujua kwamba ndugu zao nao wamehusika katika ufisadi wa aina mbalimbali.

Kutokana na hayo hapo juu, ndiyo maana unaona mwelekeo wa mapambano umekuwa hivi. Na bado tutaona na kusikia mengi.

(a) Moja: Tayari wale waliokuwa mstari wa mbele kuorodhesha majina ya "mafisadi" (list of shame), sasa hivi nao wamegawanyika baada ya kugundua kwamba kumbe ile list waliyokuwa nayo ni cha mtoto. Na wameanza kuwa na wasiwasi kwamba nao inawezekana wamo.
Usishangae kusikia wameanza kutoa mwito wa "Kuundwa kwa Tume ya Usuluhishi". NONSENSE!! Mbona hatuundi tume za kusuluhisha wezi wa kuku, majambazi yanayoteka magari ya abiria, n.k. Yaani kwa vile tu wafadhili wenu wametiwa nguvuni ndipo mnaanza kuwaonea huruma???

(b) Pili: Safari za Kisutu zilipoanza, ndio hao hao wameenda kuwadhamini "mafisadi", ambao hawako kweli list of shame na wako tayari kuwadhamini wengine pia, maana kwa njia moja ama nyingine wamefaidika na ufisadi walioutenda. (Wanatenda kinyume na wanayohubiri). Wanapoulizwa imekuwaje, basi jibu ni "aaa yule ni mjomba wangu, sijui mtoto wa shangazi yangu, etc."

Sasa hii vita ilipofikia ni patamu, maana "chui" waliovaa ngozi za "kondoo" ni lazima wazivue na wabaki kuwa chui ....

Hii kamata kamata imesaidi sana ... na ni vizuri ikaendelea ... na wale wanaofikisha ujumbe kwa wale walio kwenye list ya kuelekea Kisutu waendelee kufanya hivyo. Ikiwezekana wajihukumu wenyewe kwa kujinyonga, maana wanaendeleza uchungu kwetu sisi wananchi kwa kutumia mali walizochuma kwa ufisadi.
 
Nashukuru kwa kuliona tatizo la uwazishwaji au uendeshwaji wa Mwananchi Gold, sasa hayo mengine ulio zungumzia nani wa kumshtaki nani tuwaachie wachunguzi , maana nionavyo kunawengine wanajificha nyuma ya hizo institution, kama ni CCm, BOT etc. itajulikana huko mbeleni.
Napenda tena kukupongeza kwa kuwa Objective na muelewa, na ujue sisi sote tunampenda warioba , lakini tunashangazwa na alichofanya au kilicho tokea, sasa akifika kisutu au what ever ndio tutakapo elewa vizuri ushiriki wake au kutoshiriki kwake

- Mawazo yako mkuu ni sabuni ya roho, tupo pamoja hapa!
 
Serikali: Hatumchunguzi Warioba
Exuper Kachenje
SERIKALI imesema haina taarifa za kuchunguzwa na mpango wa kufikishwa mahakamani kwa waziri mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba na kwamba wala haihusika na suala hilo.

Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe alisema hayo jana alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari katika mkutano maalum aliouitisha kuelezea mafanikio ya wizara yake katika miaka mitatu ya serikali ya awamu ya nne.

Warioba amekuwa akibashiriwa na vyombo vya habari kuwa angefikishwa mahakamani kuhusu kampuni ya Mwananchi Gold ambayo inahusishwa na usafidi na ubashiri ulipozidi, kiongozi huyo wa zamani aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kufafanua kuhusu kampuni hiyo.

Warioba alisema alilazimika kuzungumzia suala hilo baada ya kuona uvumi unazidi kukomaa huku hadhi yake kwenye jamii ikitetereka, lakini Waziri Chikawe aliripotiwa baadaye akihoji sababu za waziri huyo mkuu wa zamani kuwa na wasiwasi kama anajiona hana hatia.

Jana, Waziri Chikawe alisema: "Sijui lolote kuhusu tuhuma za Jaji Warioba. Wizara yangu haijatamka wala haijamtuma mtu ama taasisi yoyote kumchunguza au kumtisha wala haihusiki na upelelezi.

"Kwa sasa mimi sina taarifa kuhusu hilo na kwanza ofisini kwangu hatuna utaratibu wa kutisha watu."

Alisema kuwa anamfahamu na kumheshimu Jaji Warioba kwa kuwa ndiye alimpokea na kufundisha kazi alipojiunga na Wizara ya Sheria mwaka 1975, wakati huo Warioba alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Alisema kuwa hajawahi kumkejeli Jaji Warioba na kwamba hiyo si tabia yake maishani akisisitiza kuwa hajawahi kumkejeli mtu, kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari mapema wiki hiii.

Waziri Chikawe alisema kuwa taarifa zinazomhusu yeye kuzungumzia Jaji Warioba zilizoandikwa na gazeti moja la kila siku (si Mwananchi) kuwa si za kweni na zimejaa ushabiki.

Hata hivyo, alisema si jukumu lake kumchunguza mtu bali vipo vyombo vinavyohusika, ambavyo vinastahili kuulizwa kuhusu suala la Jaji Warioba kuchunguzwa, na kwamba iwapo vitafanya hivyo Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), ndiye mwenye mamlaka ya kuamua kumfikisha mtu mahakamani ikiwa ataridhishwa na ushahidi alionao.

Wakati huohuo, Waziri Chikawe amesema serikali itatoa taarifa kuhusu ufumbuzi wa suala la kuwepo au kutokuwepo kwa Kadhi Mkuu hivi karibuni.

"Kuhusu suala la kuwepo au kutokuwepo Kadhi Mkuu, utafiti tayari umefanyika na umekabidhiwa serikalini. Serikali itatoa taarifa yake punde," alisema Chikawe katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.

Alisema hatua hiyo itatoa ufumbuzi kuhusu suala hilo lililogonga vichwa vya viongozi wa serikali, kisiasa na kidini huku Waislamu wakidai kuwepo kwa Kadhi Mkuu ni haki yao ya msingi kiimani.

Chikawe alisema kuwa mbali na suala hilo serikali ipo katika mchakato wa kutoa waraka wa serikali namba moja kuhusu marekebisho ya Sheria ya Ndoa na Sheria ya Mirathi na kwamba wizara yake imekuwa ikifanya kazi kutekeleza matamko ya ilani ya Chama Cha mapinduzi katika sekta ya sheria.

Alisema Sheria ya Ndoa, Sheria ya Mirathi na Urithi na Sheria ya Makosa ya Kujamiiana zimefanyiwa utafiti na kujadiliwa katika katika ngazi mbalimbali za kijamii na kiserikali.

Alisema ni jukumu la wizara yake kuhakikisha mfumo wa sheria uliopo unatoa fursa na haki sawa kwa raia wote mbele ya sheria na kwamba mfumo huo unatakiwa kuweka mazingira muafaka kwa taasisi zote za umma na za kiraia kuziwezesha kutekeleza majukumu yao.

Sheria nyingine zilizofanyiwa utafiti ni pamoja na Sheria ya Ulinzi wa Haki za Watu Wenye Ulemavu, Sheria ya Haki ya Ushindani wa Kibiashara, Sheria ya Usimamizi wa Haki za Ugunduzi na Uhamishaji wa Teknolijia na Sheria ya Kusimamia Matumizi ya Teknolojia ya Chembe za Asili za Urithi (DNA).

Source: Mwananchi Read News
 
nabet kwamba hakamatwi ngongoti huyu.
Ila nasema kwamba nchi ipo ktk hali mbaya kwani kila mtu sasa atafanya na kijifanyia kila analoona ni jema kwake.
 
Wakuu
Naomba mwenye profile ya Yusuph Mushi aiweke hapa jamvini.
 
Duh, Mbona siwaelewi?

Jamani Warioba aliwaita waandishi wa Habari ili awaeleze ufahamu wake kuhusu tuhuma zinazosemwasemwa mitaani na katika baadhi ya vyombo vya habari. Sasa alichokisema ndicho alichokuwa tayari kukisema. Ndio maana anasema, kama kuna kushitakiwa yuko tayari kujibu mashitaka hayo wakati wowote.

Ndugu zangu, Jaji Warioba ni mtu makini sana. NI mtu anaefikiri kabla ya kusema. Na anasema kinachojitosheleza. Anapotaja Makampuni yenye uwekezaji katika hiyo MWANANCHI Gold anajua anachokisema. Kama unavyojua, Kampuni ina wamiliki wake, na wamiliki wanaweza kuwepo leo, kesho wakauza share zao. Hawezi kutaja tu moja kwa moja wamiliki wa hizo kampuni bila kuwa makini. Yeye kama Jaji anajua umuhimu wa kuhifadhi taarifa za watu (Kama Waziri Mkuu mstaafu, anaijua Katiba). Haikuwa nia yake kwenye kikao kile kisema majina ya watu wowote.

Pili ushiriki wake na Kampuni yake ameusema bayana. Kama unavyojua, Memorandum and Articles of Association za Kampuni yoyote huandaliwa na wana sheria. Kampuni yake ilipewa kazi ya kufanya hivyo, pamoja na ushauri mwingine wa kisheria endapo utahitajika wakati wowote kabla na baada ya kuanzishwa kwa Kampuni hiyo (hii ameisema vizuri katika taarifa hapo juu Sijaona mahali anaposema alikuwa mwendeshaji wa Kapuni hiyo (labda kama kuna mtu anaweza kunisaidia hilo).

Wakuu, nadhani mnajua pia kuwa Serikali imepewa mamlaka na Katiba kupitia Bunge kuanzisha Taasisi, na taratibu zimewekwa za kufanya hivyo. Serikali pia inaweza kuwa na wabia wengine (binafsi au Taasisi za serikali) katika kufikia matarajio ya uanzishwaji wa Taasisi hizo.

Nilidhani mngeshitushwa zaidi na taarifa ya kudidimizwa kwa MWANCHI GOLD ambayo inaelekea ilikuwa na nia ya kuhakikisha rasilimali (madini) yetu yanasafishwa hapa hapa nchini na kutuhakikishia kuwa hatuporwi mali hizo. Mimi kwangu ni jambo la kushtua sana kusikia serikali inakusudia kwa nguvu zote kuua shirika/Kampuni muhimu kama hiyo.

Unajua mzee mimi sishangazwi na lolote isipokuwa kukurupuka kwa Jaji Warioba na kujitetea huku akishangaa namna Watanzania tulivyo wazuri katika kuwasulubu wenzetu kwa tuhuma na kuwatishia mashitaka. Ni Warioba huyu huyu alikuwa mstari wa mbele kumsulubu Mzee Ruksa kwa suala la OIC akizani yeye atakuwa tofauti na wengine. Kama inavyomkuta Mkapa na wengine Watanzania tutaendelea kusulubiana lilibaki ni Zamu tu.
 
FMES,
Mkuu hakuna sehemu nimesema Malecela alikuwa au ni Fisadi. Namheshimu sana mzee yule na hakika ni katika viongozi wachache walioweza kazi zao.. Warioba pia ni ktk kundi hili kwa hiyo sikusema kabisa kuwa Malecela ni fisadi isipokuwa nakumbuka Malecela ktk kikao cha CCM na sio bungeni aliaungumza against kina Dr. Slaa on Ufisadi... he was against the move kwa sababu yeye ni makamu mwenyekiti wa chama na wanachama wake ndio waliohusika..Kisiasa alikuwa na point lakini kwetu wananchi ilikuwa kutuvuruga..

Warioba alikanya tu kuwa swala la Mafisadi halitakiwi kukurupuka ovyo ni swala zito ambalo linataka subira na uangalifu laa sivyo linaweza kuhatarisha Usalama wa nchi.. Na moja wapo ya maneno yake ni pamoja na na shuku kama hizi hapa, unaona jinsi kina RA wanavyohema visogoni mwa watu kila siku wanatafuta scandals against watu clean..

Kuwa wakili wa shirika haina maana wewe pia ni mhusika as a fact kina Masha (mshikaji wako) ni wakili mwanasheria wa mashirika kibao ya uchimbaji dhahabu nchini ikiwa ni pamoja na TanGold, law firm yao imewawezesha Barricks kuchukua ardhi na mengineyo mengi tu dhidi ya wananchi na hasa maslahi ya Taifa, lakini siwezi kutumia uwakili wao kuwa kigezo cha kumshirikisha Masha na Ufisadi hata kidogo...Yeye ni wakili kisheria hata jambazi anaruhusiwa kuwa na wakili mwanasheria..

Hata wale mawakili wa O.J. ktk kesi ya mauaji Marekani siwezi kusema wao ni washiriki wa mauaji ati kwa sababu wamemwakilisha OJ mbele ya sheria.. haya ni makosa makubwa mshikaji.. Warioba katupa list ya watu wanaohusika na kwamba Mwananchi Gold ni shirika la serikali ambalo lilianzishwa na Mkapa na limevunjwa na Mkapa..Kama kuna maswali tumuulize Mkapa na hakika naomba Mungu Warioba afikishwe mahakanai, ndipo mtajua kilichomtoa kuku manyoya!..
Wewe binafsi mkuu wangu nakufahamu, anyone ambaye yuko au alikuwa na Nyerere bega kwa bega ni mbaya wako, sababu unazijua mwenyewe!..

Warioba ni kati wa watu CLEAN Tanzania ikiwa ni pamoja na Malecela...besides mkuu wangu sote tumekuwa na watoto wa hawa viongozi na hadi leo wanahesa kwa nguvu zao wenyewe..Warioba au Malecela wangekuwa mafisadi unafikiri tungekuwa tukiwaona watoto wao wakitafuta ajira za kukamatia..Tazama kina Lowassa, Yona, Mramba and the likes, fisadi hajifichi mkuu hata kidogo.
 
Je ni kweli warioba anapandishwa kizimbani, au ni mambo ya presha kupanda presha kushuka tu???
 
Nchi ishauzwa. Iko siku na sisi tutajikuta tumeushauzwa.

Kalaghabahooooooo!

./Mwana wa Haki
 
Back
Top Bottom