Tetesi: Wasafiri wamekwama porini kwa siku tatu, wanahitaji msaada wa haraka

Tetesi: Wasafiri wamekwama porini kwa siku tatu, wanahitaji msaada wa haraka

Criterion

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2008
Posts
11,797
Reaction score
11,891
Ndugu zangu, niaandika habari hii kwa uchungu nikiomba, kwa yeyeote atakayeisoma, afikishe habari hizi kwa wahusika ili hatua za haraka za uokozi zichukuliwe.


Kuna habari kwamba barabara inayotoka chunya kwenda manyoni imekatika na wasafiri wamekwama hapo porini maeneo ya ipole kwa siku tatu sasa.


Wito wangu ninaomba sana serikali iokoe hawa binadamu. pamoja na kuwapelekea askari wenye silaha (jambo ambalo ni jema), wawapelekee haraka huduma za kibinadamu. hawa watu watakufa porini.


Tunaomba chombo chochote chenye wepesi, kipeleke haraka chakula kama mikate white and brown, biscuits za sukari na zisizo na sukari, juice za sukari na zisizo, maji ya kunywa, huduma ya kwanza, dawa za kuzuia kuumwa na mbu, hata mablanketi ya kujifunika usiku ukizingatia pia njia hiyo huwa na tsetse flies.


Ombi lingine, kwa jinsi hali ya miuondo mbinu ilivyo kwa sasa, serikali ifanye juhudi za haraka za kutoa taarifa mapema pale kunapokuwa na barabara haipitiki ili watu wasiende kukwama maporini na kuhatarisha maisha. hii pia itasaidia watu kupanga route sahihi za kufika wanakotaka kwenda.


Habari nilizozipata ni kwamba daraja limekatika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha na hivyo hakuna uwezekano wa gari kupita ama kutoka manyoni kwenda chunya, ama kutoka chunya kwenda manyoni.


Habari zilizonifikia ni kwamba kuna abiria wamekwama hapo porini tangu juzi. ni porini ambapo hakuna duka, hakuna huduma za mpesa, hakuna hoteli wala huduma ya chakula, hakuna huduma ya afya hata duka la dawa, hakuna maji salama, hakuna hata kijiji kinachoweza kutoa msaada kwa hawa binadamu.


Nimeambiwa kwamba serikali ya mkoa wa tabora walikwenda ku survey eneo la tukio. wakati wanajiandaa kujenga daraja, ama kufanya utaratibu wa kuwezesha mahala pale papitike, wamepeleka askari kulinda usalama. hili ni jema, lakini naomba sana uhai wa hao binadamu uangaliwe.
 
Itaanza siasa kwanza waambieni Red Cross kuokota maisha fikiria watoto na wazee

Nitashukuru kama Red Cross watapata habari hii na waondoke mara moja kwenda eneo la tukio. Nina imani watakwenda na kila kitu muhimu. Kumbuka katika makundi ya binadamu kama hayo , kuna watu wenye allergy na kile na pengine kuna watu wako anaemic, wengine wangonjwa, wengine wako diabetic, wengine namna mbali mbali.

Mungu asaidie, binadamu wale waokolewe.
 
WASAIDIE KWANI WAO NDIO WAMELETA MAFURIKO??

Wanahitaji kuokolewa ili waishi, waendelee kutunza familia zao na kushiriki katika shughuli za maendeleo ambayo sote tunayahitaji ukibaki peke yako duniani hata wanyama wakali watakushambulia maana watakuvamia, hutaweza kujitosheleza katika mambo yote kwa kuwa wewe si mtaalamu wa kila kitu mafuriko yatakufuata nyumbani kwako na hutakuwa na hata mtaalamu wa kukuokoa kwa kuwa hiyo si fani yako.

Maisha bora na uhai wa binadamu mwenzako ni muhimu kwako kama ilivyo muhimu kwake!.
 
Gari limekwama wapi hasa? Umesema barabara tu lakini eneo hujasema. Taarifa haijakamilika kwa kutosema eneo halisi ili mamlaka zijue zinafanyeje na msaada wa haraka utoke wapi?
 
Gari haina reverse ?

Kuna magari mengi yamekwama pale, mengine yametoka Mbeya yanakwenda Tabora na mengine upande wa pili yanakwenda Mbeya ninaambiwa hata kule walikotoka ni shida.

Sina hakika kama ku reverse kunaweza kuwa na ahueni yoyote kumbuka njia ile ni mapori sana.
 
Gari limekwama wapi hasa? Umesema barabara tu lakini eneo hujasema. Taarifa haijakamilika kwa kutosema eneo halisi ili mamlaka zijue zinafanyeje na msaada wa haraka utoke wapi?

Ahsante Bazazi. Magari yamekwama maeneo ya "IPALE" kama na spell kwa usahihi. Ni karibu na kijiji cha IPALE".
 
Ndio najiuliza kwanini lisifanyike hili???

Ni rahidi magari yanayotokea Tabora kurudi Tabora kuliko yale yanayotokea Mbeya kurudi Mbeya maana hapo yalipo ni karibu na Tabora lakini wanapitaje?
 
Back
Top Bottom