Wasaidizi wa kazi kutembea na Baba wenye nyumba kuna madhara. Dada wa Arusha apokonyea Mwili wa marehemu

Certified copy unaipata hata mitandaoni, cheti cha kifo ni public document na ukifuata tarafibu unaipata copy au pia verification.
Pia mirathi inswekewa caveat bila kuwa na chochote zaidi ya sababu.
Tatu, hebu wewe fikiria mtu atapataje permit ya kuzika bila kuwa na cheti cha kifo? Si unapeleka court order tu unaipata cheti na permit ili Uzike.
 
Asante sana kwa kuelewa kua ili upate cheti cha kifo lazima ufuate utaratibu, siyo tu eti unachukua mtandaoni, tena ingekua kuchukua cheti tu mtandaoni, saa hizi ningekua napakua cheti chako cha kifo nikafunguwe mirathi yako ili nijipatie mali zako kwa njia ya udanganyifu!!
 
Unapakua mitandaoni kama ukitaka, miradi tu kiwe registered. Dakrari ana register hata elfu tano haifiki.
Copy kutoka RITA ni sawa na cheti original, same effect.
Halafu siyo udanganyifu maana kusimamia mirathi Haina maana mali ni zako, tofautisha Hilo.
 
Si haba
 
Taja specific provision(s) kama hutojali
The whole of Cap. 352 with the exception of Section 87 and part IX as per section 2 .
Kupunguza misunderstanding tafadhali soma interpretation of the "administrator".
 
Mwanamke amezaa nje ya ndoa lkn hata kaka enu si alizaa na akaleta watoto na akalea na akaona haitoshi akachukua na housegirl akamzalisha na kuishi nae yaliyotokea marehemu aliyataka mwenyewe,wanasema utavuna ulichopanda,ukipanda uharibifu utavuna uharibifu.By the way azae nje asizae sio juu yenu ndoa ilikuwa yao na sio yenu.Wakwanza kuside na michepuko ya kaka zenu na kusahau familia akifa mnajidai mlikuwa mnamjua marehem tulieni dawa iingie mke wa marehem kusanya hadi mia wakati unateseka na ndoa hakuna aliyekusaidia kati ya hao watu!
 
Unajua maana ya mke? Mke ni kwenye karatasi, ndio ushahidi unaompa uhalali kwenye kila kitu kuhusu mume wake,

Si lazima karatasi. Ndoa za kimila zina karatasi ??? Au hazitambuliki ?

Basi hao watoto wa pembeni wana stahiki zao kisheria, na mumo mumo ndo nyumba ndogo ataponea.

Hili ni funzo kwa wanaume, kulala lala na vimada kwa kigezo cha hana karatasi. Huwezi kumla mtu miaka 10, unazaa, halafu ukasema hana karatasi! Mahakama itakutoa kamasi!

Tena unambana mbavu kinyume na kisheria. If you know what I mean. There is a reason why mtu anapagawa, anahamia kwa hawara. Unachopata pembeni ni cha tofauti! Na ni stress-free. We understand all that. Lakini si cha bure mwisho wa siku.


Na usidhani hakuna ushahidi unaobaki huko pembeni. Umeacha ma fngerprint all over the crime scene, including your child!

Tamaa za mwanamme, na testasterone zake, zinahamishwaje kuwa tamaa za dada wa kazi ???? I just can't fathom this. Na tena hii mihimili ya nchi inazidi kutawaliwa na wanawake, majaji wa kike wataendelea kupindua mifumo dume. Wanamme waamke.
 
1. Huyu mubaba marehemu hakuwa na ndoa ya kimila, alioa mke wa karatasi. Tena huenda alibainisha ni ndoa ya mke 1. Pointi yako ya ndoa ya kimila haina mashiko kwa hii kesi. Mubaba angetaka angetoa talaka kwa mkewe

2. Uungwana wa Mke wa marehemu ndio pona ya watoto wa nje. Akikana na kudai sio watoto wa mume wake marehemu au ana mashaka mpaka itakapothibitishwa?

3. 'Ke wajiongeze, kama unajua unaiba mtu wa watu walau uhakikishe kuna vitu vipo kwa jina lako mwenyewe. Utalia peke yako, mahakamani vitu ni kwa ushahidi na sio hisia

4. Akae kwa kutulia avune alichopanda, dhambi ina washirika wawili. Mmoja ametangulia. Asilalamike sana, alijua alichokuwa anafanya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…