Wasaidizi wa Rais Samia warekebishe makosa aliyofanya katika mahojiano na BBC, vinginevyo ataonekana siyo muungwana

Wasaidizi wa Rais Samia warekebishe makosa aliyofanya katika mahojiano na BBC, vinginevyo ataonekana siyo muungwana

JokaKuu

Platinum Member
Joined
Jul 31, 2006
Posts
34,188
Reaction score
62,952
Hakuna binadamu aliye mkamilifu. Rais SSH alifanya makosa kwa kutoa kauli zisizo "sahihi" ktk interview yake na Salum Kikeke wa BBC.

Hilo siyo jambo geni kumtokea kiongozi yeyote yule. Kinachofanyika ktk mazingira kama hayo ni kiongozi mwenyewe, au wasaidizi wake, kujitokeza kuomba RADHI na kurekebisha makosa yaliyojitokeza.

Nashangaa kwanini mpaka sasa hivi hakuna mtu wa IKULU aliyejitokeza kurekebisha kauli alizotoa Rais. Ukimya huu wa Rais SSH, pamoja wasaidizi wake, unaweza kuleta hisia kwamba Rais hakukosea kibidamu, bali alifanya makusudi au alidhamiria kutoa majibu yale.

Zaidi ya kuharibu taswira ya Rais na kuporomosha heshima yake, hali hiyo inatoa mwanya kwa Rais kuitwa majina mabaya yenye kumvunjia heshima.

Hivi kweli Rais SSH ameridhika na majibu aliyotoa kwa BBC? Je, wasaidizi wake wanadhani Rais ametenda sawa, na kwa kukaa kimya wanamtendea haki Rais?

Nawasihi wasaidizi wa Rais wajitokeze kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza, na kuwaomba RADHI wananchi.

cc Richard, Nguruvi3 , Pascal Mayalla, Sesten Zakazaka
 
Wajitokeze kurekebisha? no way, haitasaidia kitu.

Hii ni awamu ya trial and error, toka siku ya kwanza Samia anakosea tu, hata wakirekebisha kesho watakosea tena.

Unavyoongea sasa, utadhan hata unaweza kuongoza hata Kijiji sembuse family yako basi kama unayo, unadhan kuongoza nchi ni jambo la masihara,watu Wana makarama yao
 
Mbona Mbowe hakujitokeza kumuomba msamaha Lisu na wengine kwa kitendo chake cha kuwalazimisha wasomi wazima washindwe kusimamia kauli zao wenyewe kuhusu Lowasa? Hii ni aibu kwao na magenge yao.

images (7).jpeg


images (11).jpeg


images (10).jpeg
 
Nimevunjika sana moyo.CCM tuandae mtu mwingine
... vp is a president on waiting! Haitakiwi kuwa suala la ushabiki hata kidogo kwenye kumpata mtu wa kukalia hicho kiti! Nireteeeni gwajiboy! Nireteeeeeeeni gwajiboy! Nireteeeeeeeeeeeeeeeeeni gwajiboy! Inaonesha jinsi busara na hekima ilivyokosekana kwenye mambo mengi; as a result ndicho kinachoonekana leo.
 
..hakuna binadamu aliye mkamilifu. Rais SSH alifanya makosa kwa kutoa kauli zisizo "sahihi" ktk interview yake na Salum Kikeke wa BBC.

..Hilo siyo jambo geni kumtokea kiongozi yeyote yule. Kinachofanyika ktk mazingira kama hayo ni kiongozi mwenyewe, au wasaidizi wake, kujitokeza kuomba RADHI na kurekebisha makosa yaliyojitokeza.

..Nashangaa kwanini mpaka sasa hivi hakuna mtu wa IKULU aliyejitokeza kurekebisha kauli alizotoa Rais. Ukimya huu wa Rais SSH, pamoja wasaidizi wake, unaweza kuleta hisia kwamba Raisi hakukosea kibidamu, bali alifanya makusudi au alidhamiria kutoa majibu yale.

..Zaidi ya kuharibu taswira ya Rais na kuporomosha heshima yake, hali hiyo inatoa mwanya kwa Raisi kuitwa majina mabaya yenye kumvunjia heshima.

..Hivi kweli Rais SSH ameridhika na majibu aliyotoa kwa BBC? Je, wasaidizi wake wanadhani Rais ametenda sawa, na kwa kukaa kimya wanamtendea haki Raisi?

..Nawasihi wasaidizi wa Raisi wajitokeze kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza, na kuwaomba RADHI wananchi.

cc Salary Slip, Erythrocyte , Pascal Mayalla
kama unaona alikosea kwa nn usimuambie kikeke afanye masahihisho?! au unataka interview irudiwe?
kuna mambo mengi ya msingi yanapaswa yashughulikiwe sio jambo hili ambalo haliongezi dawa mahospitalini wala haliongezi kodi ya nchi, wala haliongezi chanjo ya corona, wala halipunguzi maendeleo ya watanzania.
watanzania wenzangu nawaomba tujikite kujadili mambo ya msingi kwa taifa letu sio hoja ambazo hazina maana ambazo zinapoteza uwezo wetu wa kufikiria changamoto zinazo tukabili kama taifa.
 
kama unaona alikosea kwa nn usimuambie kikeke afanye masahihisho?! au unataka interview irudiwe?
kuna mambo mengi ya msingi yanapaswa yashughulikiwe sio jambo hili ambalo haliongezi dawa mahospitalini wala haliongezi kodi ya nchi, wala haliongezi chanjo ya corona, wala halipunguzi maendeleo ya watanzania.
watanzania wenzangu nawaomba tujikite kujadili mambo ya msingi kwa taifa letu sio hoja ambazo hazina maana ambazo zinapoteza uwezo wetu wa kufikiria changamoto zinazo tukabili kama taifa.

..Uungwana ni vitendo.

..Kuteleza sio kuanguka.

..Kauli za Rais SSH hazikuwa sahihi, hivyo ni busara wasaidizi wakajitokeza kuzirekebisha.
 
..It is never too late to apologize.

..Naamini Raisi akiomba RADHI atajizolea sifa lukuki.
Wafaransa hawaombi radhi hata kama ni kosa la wazi. Wanasema kuomba radhi ni sehemu ya kukubali udhaifu. Hiyo ni tabia ingawa siyo desturi ya wafaransa. Kule ni ubabe kwenda mbele!!!

Sisi mara nyingi twaomba radhi endapo tumefanya kosa kweli. Ingawa kundi fulani laweza kulazimika kuomba radhi hata kama halijakosa ili "yaishe".
====
Mkuu, kwanza orodhesha makosa yote yaliyotendwa ili tuwe na ujasiri wa kushauri hiyo radhi iombwe.
 
Unavyoongea sasa,utadhan hata unaweza kuongoza hata Kijiji sembuse family yako basi kama unayo,unadhan kuongoza nchi ni jambo la masihara,watu Wana makarama yao

..Rais au wasaidizi wanapaswa kuomba radhi.

..Nina hakika SSH atajizolea sifa kemkem za uungwana.
 
..Rais au wasaidizi wanapaswa kuomba radhi.

..Nina hakika SSH atajizolea sifa kemkem za uungwana.
Kazi ya Urais kwa nchi zetu za "Afrika" si kazi ya uungwana, Rais haombi msamaha....kiufupi raia hawana mamlaka ya kuombwa msamaha na Rais wao kwa sababu hawana mamlaka ya kuamua kumpa au kumnyang'anya nafasi ya Urais!
 
Back
Top Bottom