Wasaidizi wa Rais Samia warekebishe makosa aliyofanya katika mahojiano na BBC, vinginevyo ataonekana siyo muungwana

..jamani tusijadili jinsia yake.

..tujadili kauli na matendo yake.

..na wewe unapaswa kuomba radhi.
Ndugu, wajitahidi kumsetiri, lakini huyu Mama alijianzishia mwenyewe, mara baada ya kuapishwa. Mwenyewe ndie aliyalitaka sijui alidhani litamjenga? Kwa kukosa busara/hekima kalikoroga swala ambalo kamwe hatoweza kulifuta hata ukimwombea radhi.
 
Porojo tu hizi, ulitaka aseme nn labda?

Siku ukijua nchi inaendeshwa kwa gharama kubwa kiasi gani, na maliasili zetu bado haziwezi kutunufaisha kwa kiwango tunachohitaji kwasababu wawekezaji wengi wanakuja na masharti ya kujinufaisha wao kwa kiasi kikubwa Basi utaacha mara moja kulalamika kama mjane
 
Unavyoongea sasa, utadhan hata unaweza kuongoza hata Kijiji sembuse family yako basi kama unayo, unadhan kuongoza nchi ni jambo la masihara,watu Wana makarama yao
Nimeandika sijaongea, mmoja kuwa legelege sio wote wako hivyo.
 

..mikataba yote ya kinyonyaji imesainiwa na viongozi wa ccm.

..tunatumia trillion 2 kununua ndege toka kwa wazungu wakati watoto wanakaa kwenye sakafu mashuleni.

.
 
..mikataba yote ya kinyonyaji imesainiwa na viongozi wa ccm.

..tunatumia trillion 2 kununua ndege toka kwa wazungu wakati watoto wanakaa kwenye sakafu mashuleni.

.
Kabla hujazitaja ndege lazima ujue lengo ni lipi?

Mbona ni mambo ya kawaida tu ambayo hayahitaji hata kusumbuka, kama unauliza habari za ndege Basi utauliza kwann mtu afungue biashara akati pesa iyo inatosheleza kujenga.

Uwekezaji si hadi uhakikishe umetimiza mahitaji yako yote, kwa kufanya ivo utachelewa sana.
 
Asante sana. Hii ndiyo shida ya kutunga sheria ili kumkomoa mtu badala ya kuangalia hali halisi. Sheria za namna hii zimekuwa zinatungwa sana na CCM kulenga wapinzani.
 
Raisi hatakiwi kuomba radhi kamwe.huo ni bonge la udhaifu.kinachotakiwa ni kufafanua kile ambacho hakikueleweka kwenye statement yake.Raisi atoke hadharani aanze kusema ohooo nilighafirika sababu nilikuwa na hofu ya camera,what?Hayo atatafanya kwa mumewe tu.Akiomba radhi ataonyesha dhaifu kabisa kwamba huwa analopoka lopoka hovyo bila mpango.
 
Nilikuwa naitafuta kauli kama hii; aonyeshe makosa ili na wengine tuyafahamu kwa kuwa watu wana mitazamo tofauti. Unaweza kuona hapa kajibu vibaya mwingine akaona amejibu vizuri hivyo anayesema kajibu vibaya basi ana wajibu wa kuonyesha huo ubaya badala kuandika tu kwa ujumla! Ukiandika kwa ujumla bila kudadavua nawe unakuwa umeandika vibaya na una wajibu wa kuomba radhi.
 
..kasikilize interview yake na Salum Kikeke wa BBC.
hajakosea popote, na sijawahi kusikia Rais yoyote akiomba radhi
mngemdanganya Trump akarekebisha Hotuba zake na tweeter alizozitoa enzi hizo,
JokaKuu wakati wa safari ya miguu ukienda kazini au kwenye biashara zako usisikilize mbwa wanavyobweka hutafika asilani, CHUKUA FIMBO /GONGO saonga mbele mbwa watanyamaza wote
tunataka maendeleo km hizo barabara tulizolipia TOZO kwa sasa, Siasa bado
Mama chapa lapa chapa fimbo
 
samia suluhu ni gaidi kaa magaidi wengine wa ccm, huyu mama hajui mbere au nyuma, hajielewi kabisa, hata akili hana kabisa, kasema uongo mtupu mbere ya dunia, kaa ni kwingine angekuwa amejiuzulu kufikia sasa
 
Unavyoongea sasa, utadhan hata unaweza kuongoza hata Kijiji sembuse family yako basi kama unayo, unadhan kuongoza nchi ni jambo la masihara,watu Wana makarama yao
Umempa nafasi ukaona hawez ongoza yaan unamuhukumu mtu usiyemjua na haujampa nafasi
 
Hakuna kauli iliyoniuzi Kama kusema kuwa wananchi wameridhika na tozo!! Hivi kwa nin mheshiwa sulululu anatukejeli kiasi kile jamani,, kweli maumivu hayaaa anyway
 
Nafikiri wewe ndiye mwenye hoja za hovyo na mtazamo wa mtu asiyetumia akili hata kama hajasoma hoja tunqzoziangalia hapa ni za msingi sana raisi wa nchi kutoa kauli za uongo ni hatari sana kwa nchi, kuminya democrasia kusingizia watu kesi za uongo kukumbatia washauri wabaya kupinga katiba isiyokidhi muda na hali halisi ya nchi hayo yote yana madhara ya moja kwa moja na mahitaji unayotaka tuyajadili.
 
Mbona tunaambiwa nchi inaongoza kwa rasilimali Africa nzima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…