ChamaDola
JF-Expert Member
- Dec 23, 2016
- 3,431
- 2,804
Wakuu,
Unapofungua Agano Jipya,hasa katika zile Injili Nne,utakutana na uadui kati ya Wayahudi dhidi ya Wasamaria!
Ila ushawahi jiuliza chanzo cha ukinzani huu? Basi twende sote tupate kujua!
Ukirudi nyuma kidogo katika Agano la Kale utakutana na Mfalme Suleiman!
Baada ya kuikinikia hekima aliyoiomba na kupewa na Mungu,Mungu aliamua kuugawa
ufalme katika vipande viwili hasimu:Ufalme wa Yuda upande wa Kusini na Israel upande wa kaskazini!
Kwa kuwa Mungu hakutaka kuutia doa ufalme wa Suleiman ili kutokuvunja agano lake
aliloliweka na Mfalme Daudi,basi kumrundia heshima Daudi,alisubiri Suleiman afe, ndipo auchane pawili ufalme kama adhabu dhidi ya uasi wa Suleimani kwa Mungu kwa kuleta
ibada ya shetani na miungu ya kigeni kupitia mamia ya wake wa kigeni aliyowaoa!
Punde, Suleiman alipovuta pumzi ya mwisho,Israeli ikachanwa katikati! Makabila kumi yakaasi na kujiunga na Jeroboam na akaanzisha ufalme wake,huku makao makuu yakiwa katika mji wa Samaria! Makabila mawili yakajiunga na kutengeneza ufalme wa Yuda yakiongozwa na Rehoboam mtoto mkubwa wa Mfalme Suleiman!
Pia kumbuka,kabila pekee lilikokuwa na mamlaka ya kutoa mfalme lilikuwa la Yuda! Ila cha ajabu,Jeqoboam alikuwa wa kabila la Ephraim! Dharau namba moja! Kama haitoshi Hekalu la Suleiman lilikuwa Yerusalem kule Yuda, kwahyo kila mwaka Wayahudi wa Samaria wafunge safari ya kuja hekaluni! Jambo hili likamkera Mfalme Jeroboam! Naye pasipo kumuomba Mungu ushauri,akaamua kujitengenezea ndama wawili,katika mji wa Betheli ili Wayahudi wa Samaria wasiende Yerusalem! Jambo hili lilimkera Mungu sana! Uadui uliendelea!
Ila ulikua zaidi mwaka 722 Kabla ya Kristo,baada ya ufalme kupinduliwa na maelfu ya
waisraeli wa Samaria kubebwa utumwani na jeshi la Wassyria! Na mfalme aliyeshinda, akaamua kuleta watu wa mataifa mbali kutoka katika makoloni yake toka Ninawi mpaka Babylon ili wautunze mji na kuilima ardhi! Lengo lake ilikuwa ni kuzima jitihada zote za Wayahudi wa Samaria kujitutumua tena ili kupinga utawala wake! Na pia kutoa somo kwa makoloni madogo kuwa yasithubutu kuleta fyokofyoko! Lakini cha ajabu,nchi ya Samaria ikaanza kuvamiwa na Simba wala watu!
Baada ya watu kusosiwa kwa muda mrefu na taarifa kumfikia mfalme wa Assyria,ikabidi kuhani wa Kiyahudi atafutwe! Baada ya upepelezi,ikaonekana Yahweh hajapendezwa na
miungu ya wakazi wapya wa Samaria,hivyo kuhani akatumwa kwenda Samaria ili
kuwafundisha watu amri za Yahweh!
Baada ya hali kutulia,mwaka 586 Kabla ya Kristo ufalme wa kusini nao ukaanguka kwa mkono wa Nebukadneza! Wayahudi wa Samaria hawakuwahi kurudi Samari,na huo ukawa mwisho wa hayo makabila kumi! Ila yale makabila mawili ya kusini,yalirudi chini ya uongozi wa Nehemia na Ezra! Kwahyo mbele ya Wayahudi,hawa wakazi wapya
wa Samaria,na baadaye katika Agano Jipya wakiitwa walikuwa ni Walowezi,nusu watu na wa mataifa! Walikuwa na haki zote za kuwachukia! Japo Kristo aliwatendea vizuri, kama yule mwanamke msamaria pale kisimani,mpaka hekalu linavunjwa mwaka 70
Baada ya Kristo "bifu" liliendelea!
Unapofungua Agano Jipya,hasa katika zile Injili Nne,utakutana na uadui kati ya Wayahudi dhidi ya Wasamaria!
Ila ushawahi jiuliza chanzo cha ukinzani huu? Basi twende sote tupate kujua!
Ukirudi nyuma kidogo katika Agano la Kale utakutana na Mfalme Suleiman!
Baada ya kuikinikia hekima aliyoiomba na kupewa na Mungu,Mungu aliamua kuugawa
ufalme katika vipande viwili hasimu:Ufalme wa Yuda upande wa Kusini na Israel upande wa kaskazini!
Kwa kuwa Mungu hakutaka kuutia doa ufalme wa Suleiman ili kutokuvunja agano lake
aliloliweka na Mfalme Daudi,basi kumrundia heshima Daudi,alisubiri Suleiman afe, ndipo auchane pawili ufalme kama adhabu dhidi ya uasi wa Suleimani kwa Mungu kwa kuleta
ibada ya shetani na miungu ya kigeni kupitia mamia ya wake wa kigeni aliyowaoa!
Punde, Suleiman alipovuta pumzi ya mwisho,Israeli ikachanwa katikati! Makabila kumi yakaasi na kujiunga na Jeroboam na akaanzisha ufalme wake,huku makao makuu yakiwa katika mji wa Samaria! Makabila mawili yakajiunga na kutengeneza ufalme wa Yuda yakiongozwa na Rehoboam mtoto mkubwa wa Mfalme Suleiman!
Pia kumbuka,kabila pekee lilikokuwa na mamlaka ya kutoa mfalme lilikuwa la Yuda! Ila cha ajabu,Jeqoboam alikuwa wa kabila la Ephraim! Dharau namba moja! Kama haitoshi Hekalu la Suleiman lilikuwa Yerusalem kule Yuda, kwahyo kila mwaka Wayahudi wa Samaria wafunge safari ya kuja hekaluni! Jambo hili likamkera Mfalme Jeroboam! Naye pasipo kumuomba Mungu ushauri,akaamua kujitengenezea ndama wawili,katika mji wa Betheli ili Wayahudi wa Samaria wasiende Yerusalem! Jambo hili lilimkera Mungu sana! Uadui uliendelea!
Ila ulikua zaidi mwaka 722 Kabla ya Kristo,baada ya ufalme kupinduliwa na maelfu ya
waisraeli wa Samaria kubebwa utumwani na jeshi la Wassyria! Na mfalme aliyeshinda, akaamua kuleta watu wa mataifa mbali kutoka katika makoloni yake toka Ninawi mpaka Babylon ili wautunze mji na kuilima ardhi! Lengo lake ilikuwa ni kuzima jitihada zote za Wayahudi wa Samaria kujitutumua tena ili kupinga utawala wake! Na pia kutoa somo kwa makoloni madogo kuwa yasithubutu kuleta fyokofyoko! Lakini cha ajabu,nchi ya Samaria ikaanza kuvamiwa na Simba wala watu!
Baada ya watu kusosiwa kwa muda mrefu na taarifa kumfikia mfalme wa Assyria,ikabidi kuhani wa Kiyahudi atafutwe! Baada ya upepelezi,ikaonekana Yahweh hajapendezwa na
miungu ya wakazi wapya wa Samaria,hivyo kuhani akatumwa kwenda Samaria ili
kuwafundisha watu amri za Yahweh!
Baada ya hali kutulia,mwaka 586 Kabla ya Kristo ufalme wa kusini nao ukaanguka kwa mkono wa Nebukadneza! Wayahudi wa Samaria hawakuwahi kurudi Samari,na huo ukawa mwisho wa hayo makabila kumi! Ila yale makabila mawili ya kusini,yalirudi chini ya uongozi wa Nehemia na Ezra! Kwahyo mbele ya Wayahudi,hawa wakazi wapya
wa Samaria,na baadaye katika Agano Jipya wakiitwa walikuwa ni Walowezi,nusu watu na wa mataifa! Walikuwa na haki zote za kuwachukia! Japo Kristo aliwatendea vizuri, kama yule mwanamke msamaria pale kisimani,mpaka hekalu linavunjwa mwaka 70
Baada ya Kristo "bifu" liliendelea!