Wasanii wa Tanzania wameshindwa kuhudhuria msiba wa mama yake Sugu kwa sababu za kiitikadi?

mr mkiki

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2016
Posts
5,588
Reaction score
11,668
Wadau.

Roho imeniuma sana yani kama imefika hatua mpaka watu wanaogopa kwenda kwenye misiba ya wapinzani eti kisa wanamuogopa mtu mmoja.

Ubaguzi wa kiitikadi unalitafuna taifa letu tusipokemea itafika mahali mtu atakuta mtu ambae sio wa chama chake kapata ajali atashindwa kumsaidia

Yani sugu pamoja na heshima aliyonayo kwenye mziki wa bongo flavor leo kafiwa na mzazi mmeshindwa hata kwenda msibani

Asante suma G, Kala Jeremiah, papi choka na Nguza Viking kwa kushiriki ibada ya kumuombea mama yetu

Nasema kuna maisha baada ya unafiki.

mr mkiki



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa nini unawalaumu bongo flava peke yao?

Umewaona wabunge wote wa CHADEMA wameenda kwenye huo msiba achilia mbali wabunge wote wa Tanzania?

Ukiangalia hata viongozi wote wakuu wa CHADEMA hawakuepo kwenye msiba!

Unachofanya ni selective blaming kwa faida ambayo unaijua!

Tusipangie watu nini cha kufanya kwa sababu kufanya hivyo ni aina fulani ya udikteta.
 
Wasanii walimwambiaga mh mbona ututetei bungeni akawajibu Mimi siyo mbunge wa wasanii, miye ni mbunge wa wana mbeya akaongeza pia kuwa kipindi anaomba ubunge uko mbeya wasanii hawakwenda masapoti kwaiyo wamuache

My take

Msitusumbue wasanii sugu alishaga tukataa wenzake alisema yeye ni mbunge wa mbeya so ngoja afike mbeya wanainchi watajaa kwake kwa wing tu.
 
Rubbish! Kuna watu humu unawafikira (maana huwajui) kama reasonable people kumbe Mhhhh! Is it healthy Mkuu kutotuma rambirambi? Unalisemeaje hilo!
 
Acha siasa za kijinga kwenye msiba hakuna siasa.
 
Magigizi nimewasema wasani kwa maana yule ni msani mwenzeo, Kama unaweza kuwa na ushaidi unaweza kuongea kwanini chama chake hawakuenda, sina details nao mimi nasema ninacho kiona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Najilaumu kwa nini nimefungua na kusoma hii mada ya kipumbavu.
 
Kwanza nimshukuru sana Mungu kwa kuzuia wanafiki wenye akili za kichawi kutoka ccm kwenda kwenye msiba huu , hii ni baraka kwa mama yetu , Msiba ukihudhuriwa na wachawi roho ya marehemu huishia ardhini tu .
 
Usimpangie mtu kitu cha kufanya kila mtu ana busara zake mi sidhani kama kutokwenda eti kuna mtu wanamuogopa nadhani sometimes tufikirie pande zote mbili tusije kufikiria upande mmoja tu wa siasa
 
Kwani nao wameogopa kwenda? Ishu ya wasanii ni kweli kabisa

Jr[emoji769]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…