vampire_hunter007
JF-Expert Member
- Jul 25, 2015
- 1,034
- 2,624
Imekuwa mara nyingi watu wa jamii fulani wakijisifia pale mtu kutoka jamii yao anapokuwa maarufu kwa usanii au mengineyo....But sio wasanii wote walioweza kuzitambulisha sehemu wanazotoka....Wapo waliozitambulisha sehemu/Mitaa wanayoishi na wapo wale waliotambulisha sehemu walikozaliwa....Kwa haraka haraka wasanii ninaowakumbuka waliotambulisha sana maeneo yao ni hawa...
1. Juma Nature na Wanaume TMK - Temeke
Hawa jamaa walifanya temeke ijulikane Tanzania nzima...Kiasi watu wengi wa mikoani waliifahamu Temeke huku wengine wakiwa hata hawajui wilaya za mikoa yao....Jamaa waliwakilisha sana Temeke...
2. Crazy GK na East Coast - Upanga
Hawa nao walijitahidi kuitambulisha Upanga. Japo hawakufikia level ya TMK...Na watu wazima wenangu watakuwa wanakumbuka ushindani uliokuwepo baina ya makundi haya mawili...
3. Diamond Platnumz - Tandale
Dah jamaa kaiwakilisha sana Tandale...Mpaka nje ya Tanzania wanaijua Tandale... Baadhi ya wakenya huko wanadhani Tandale ni bonge la sehemuuuu........
4. Mangwea na Chamber Squad - Dom
Jamaa hawa nao waliipaisha Dodoma kimtindo...
5. Shilole - Igunga
Bibie naye hayupo nyumba kuiwakilisha Igunga..Huenda akizidisha vituko Igunga itakuwa maarufu sana siku zijazo....
6. Joh Makini na Weusi - A-town
Haya machalii ya Arusha nayo yanawakilisha vema pande zile....A-town imekuwa ikitrend sana haswa kama mji wa hip hop flani hivi....Wanajitahidi
7. Wagosi wa Kaya - Tanga
Wimbo maarufu wa Tanga kunani na lafudhi zao ziliifanya Tanga pia kujulikana kuwa kuna wasanii...Sijui siku hizi wapo wapi hawa jamaa....Huenda muda umewatupa mkono
8. Afande Sele na Stamina Sharo Bweeenz - Moro
Jamaa nae wameiwakilisha sana Moro town...
9. Fid Q aka Ngosha - Mwanza
Dah huyu jamaa sijui nilimsahau vipi....Ameweza sana
Kwa haraka haraka nnaowakumbuka ni hao...Wewe unadhani ni nani amewakilisha kitaa chake/ home town yake vya kutosha na kuifanya ikajulikana ....Karibuni
1. Juma Nature na Wanaume TMK - Temeke
Hawa jamaa walifanya temeke ijulikane Tanzania nzima...Kiasi watu wengi wa mikoani waliifahamu Temeke huku wengine wakiwa hata hawajui wilaya za mikoa yao....Jamaa waliwakilisha sana Temeke...
2. Crazy GK na East Coast - Upanga
Hawa nao walijitahidi kuitambulisha Upanga. Japo hawakufikia level ya TMK...Na watu wazima wenangu watakuwa wanakumbuka ushindani uliokuwepo baina ya makundi haya mawili...
3. Diamond Platnumz - Tandale
Dah jamaa kaiwakilisha sana Tandale...Mpaka nje ya Tanzania wanaijua Tandale... Baadhi ya wakenya huko wanadhani Tandale ni bonge la sehemuuuu........
4. Mangwea na Chamber Squad - Dom
Jamaa hawa nao waliipaisha Dodoma kimtindo...
5. Shilole - Igunga
Bibie naye hayupo nyumba kuiwakilisha Igunga..Huenda akizidisha vituko Igunga itakuwa maarufu sana siku zijazo....
6. Joh Makini na Weusi - A-town
Haya machalii ya Arusha nayo yanawakilisha vema pande zile....A-town imekuwa ikitrend sana haswa kama mji wa hip hop flani hivi....Wanajitahidi
7. Wagosi wa Kaya - Tanga
Wimbo maarufu wa Tanga kunani na lafudhi zao ziliifanya Tanga pia kujulikana kuwa kuna wasanii...Sijui siku hizi wapo wapi hawa jamaa....Huenda muda umewatupa mkono
8. Afande Sele na Stamina Sharo Bweeenz - Moro
Jamaa nae wameiwakilisha sana Moro town...
9. Fid Q aka Ngosha - Mwanza
Dah huyu jamaa sijui nilimsahau vipi....Ameweza sana
Kwa haraka haraka nnaowakumbuka ni hao...Wewe unadhani ni nani amewakilisha kitaa chake/ home town yake vya kutosha na kuifanya ikajulikana ....Karibuni