Washauri wa Rais Magufuli, mshaurini aache kutumia Kiingereza kwenye hadhara

Washauri wa Rais Magufuli, mshaurini aache kutumia Kiingereza kwenye hadhara

Kuna mmiliki mwingine wa phd aliyesoma tokea secondary kingereza mpaka chuo kikuu masters mpaka kupata phd hajui kingereza? Kama yupo mtajeni jina lake
 
Tatizo ni phd Tatizo siyo polepole wala nini Tatizo ni mmiliki wa phd kutojua kingereza maana yake ni nini? aliyemuuzia vyeti alisahau kumfundisha kingereza?

Haya bwana mkubwa, nimekubali tunazungumzia kuhusu lugha , kuhusu PhD, mimi hainihusu kabisa na siwezi kusema chochote. Na siwezi shiriki kwa kuchangia chochote.
 
Huwa anamsikia tundu lissu anasema 'pipoz' Umma unaitikia 'pawa' hapo hata hajui kama amekosea,
Mkuu hiyo people's power na siyo people s power.
Hiyo inaonesha umiliki na siyo uwingi na umoja.

Nguvu ya umma au nguvu mikononi mwa umma sababu ya uwingi wao.
 
Mtaishia kuandika ujinga jamii forum wakati nchi inazidi kupaa. Watu wanazidi kufanya kazi yenye matokeo yenye kuonekana.
Matokeo yapi Mbona wewe ndiyo mjinga na unaandika ujinga hata kutetea phd asiyejua kingereza ni ujinga zaidi pengine wewe ndiyo mjinga kuliko wote huko CCM Nchi inapaa wapi? Watumishi wa umma miaka mitano pasipo nyongeza za mishahara hakuna maendeleo yeyote
 
Rais Magufuli ni mtu anayependa Kiswahili na huwa anapambana sana kukidumisha na kukikuza lakini cha ajabu anapokuwa na wageni wasiofahamu Kiswahili, ana hulka ya kuongea kiswa-nglish.

Kiingereza ni lugha ya malkia na ilikuja na meli kwahiyo ni vizuri akaongea lugha ya taifa inayoeleweka sababu wakalimani wapo.

Nukuu:
"We suppose to focus according our direction according our environment that's only way we can help our peoples no body should come and say that his there to save the problems of our peoples we are the one we are leader we suppose to change the direction"
Nyie watz hamna shukrani, mnasahau kwamba bila Magufuli taifa stars wasingeweza kucheza Afcon msimu uliopita, muwe na shukrani basi
 
Haya bwana mkubwa, nimekubali tunazungumzia kuhusu lugha , kuhusu PhD, mimi hainihusu kabisa na siwezi kusema chochote. Na siwezi shiriki kwa kuchangia chochote.
Mtafutie mwalimu wa kingereza toka Uganda au kenya muombee viza aishi pale chamwini au hata Ras simba ahamie ikulu ashinde nae ampe kozi ya kingereza kwa bidii ndani ya miezi mitatu ataongea kama Obama au akina Waziri mkuu wa Uingereza au aongee kama mseveni kingereza fasaha chenye lafudhi ya kinyankole kiganda
 
Nyie watz hamna shukrani, mnasahau kwamba bila Magufuli taifa stars wasingeweza kucheza Afcon msimu uliopita, muwe na shukrani basi
Hizo zilikuwa za makonda hata ndizi ikizaa kule kijijini alimshukuru magufuli
 
Sasa unasemaje hakusoma Advanced level!
Hajasoma Advance,huo ni utaratibu wa kuwawezesha kuweza kumudu masomo wanayoenda kufundisha. Najua unajaribu kumtetea,hao madogo aliowaita vilaza Udom walikuwa wanapitia mchakato kama wake.
 
Sasa hapo unaathirika na nini hasa? Kama kweli ww ni mzalendo basi ungejikita zaidi ktk kuguswa na kile Rais wako anafanya kwa nchi na sio wapi kaongea broken english. Ni kama vile mlio wengi mmesomeshwa na wazazi wasiojua kiingereza kabisa au kutokujua sana lakn hao wazazi si walitimiza wajibu wenu wa kuwalea,kuwatunza na kuwasomesha. Hasa hapo kutokujua kiingereza kwa mzazi wako kuliathiri vipi kukutunza au kukulea ww? Hamna tofauti na wale wakenya ambao hata mtanzania ashinde tuzo kimataifa watakimbilia kucheka na kubeza kwamba wa tz hatujui kiingereza badala ya ku focus kwenye achievement.
Mm kama mtanzania nina focus tu na utendaji wake wa kazi tu maana ndio unaonigusa kama mwananchi wa kawaida hayo mengine hayanisaidii mm.
 
Ni aibu kwa rais wa nchi kama Tanzania, ambaye amesoma mpaka chuo kikuu kwa kiingereza, akaishi Ulaya, akafanya Phd kwa kiingereza halafu hajui kuongea kiingereza fasaha.

Rais wa nchi ndio kioo cha nchi, kiingereza kibovu cha Rais wetu ni aibu kwetu sisi sote. Wasaidizi wa rais wako wapi kumsaidia kumfundisha kiingereza kizuri.
kwani kingereza kisaidia kujenga zahanati, au barabara ya lami japo nusu kilomita?
 
Mtafutie mwalimu wa kingereza toka Uganda au kenya muombee viza aishi pale chamwini au hata Ras simba ahamie ikulu ashinde nae ampe kozi ya kingereza kwa bidii ndani ya miezi mitatu ataongea kama Obama au akina Waziri mkuu wa Uingereza au aongee kama mseveni kingereza fasaha chenye lafudhi ya kinyankole kiganda
Badili kwanza jina lako kwani ni kielelezo cha ujinga wa maoni yako.
 
Matokeo yapi Mbona wewe ndiyo mjinga na unaandika ujinga hata kutetea phd asiyejua kingereza ni ujinga zaidi pengine wewe ndiyo mjinga kuliko wote huko CCM Nchi inapaa wapi? Watumishi wa umma miaka mitano pasipo nyongeza za mishahara hakuna maendeleo yeyote

Watumishi wa umma hawafiki laki sita nchi nzima wakati watanzania tupo milioni sitini.

Nani hapo ni muhimu zaidi, halafu unajikita kwenye kingereza cha rais wakati ujinga unaufuga kichwani!.
 
Mmekosa hoja....Nyie hata kiswahili hamjui sembuse kingereza....!!Upinzani wengi ni vijana mpechempeche marioo wa mjini wapenda vya bure,kingereza wamekijulia Kwenye movie na nyimbo za kina Cellin Dione...Wanaume wa kweli hawezi ongea hoja za kijinga kama hizi...!!
Tatizo we ni pisi mbovu na unayemtetea ni mshamba,in kindovu's voice
 
Ni aibu kwa rais wa nchi kama Tanzania, ambaye amesoma mpaka chuo kikuu kwa kiingereza, akaishi Ulaya, akafanya Phd kwa kiingereza halafu hajui kuongea kiingereza fasaha.

Rais wa nchi ndio kioo cha nchi, kiingereza kibovu cha Rais wetu ni aibu kwetu sisi sote. Wasaidizi wa rais wako wapi kumsaidia kumfundisha kiingereza kizuri.
Yule jamaa Ni jeuri,hafundishiki. Nasikia wasaidizi wake wakimuomba Ras Simba awasaidie kumfundisha,akagoma.
 
Ni aibu kwa rais wa nchi kama Tanzania, ambaye amesoma mpaka chuo kikuu kwa kiingereza, akaishi Ulaya, akafanya Phd kwa kiingereza halafu hajui kuongea kiingereza fasaha.

Rais wa nchi ndio kioo cha nchi, kiingereza kibovu cha Rais wetu ni aibu kwetu sisi sote. Wasaidizi wa rais wako wapi kumsaidia kumfundisha kiingereza kizuri.
Ras Simba anahitajika hapa
 
Mada ya kipumbavu, hatukumpigia kura aje atufundishe kingereza, tulimpigia kura aitekeleze ilani ya uchaguzi.

Tarehe 28 October atashinda tena kwa kutimiza kazi ya kutekeleza ilani aliyopewa.

Mwenye akili za kipuuzi za kitoto ndio atajikita kwenye masuala ya kingereza chake.
Kuwanyima nyongeza ya mshahara watumishi wa umma ipo kwenye ilani ya ccm?
 
Back
Top Bottom