Washauri wa Rais Magufuli, mshaurini aache kutumia Kiingereza kwenye hadhara

Washauri wa Rais Magufuli, mshaurini aache kutumia Kiingereza kwenye hadhara

Mmekosa hoja....Nyie hata kiswahili hamjui sembuse kingereza....!!Upinzani wengi ni vijana mpechempeche marioo wa mjini wapenda vya bure,kingereza wamekijulia Kwenye movie na nyimbo za kina Cellin Dione...Wanaume wa kweli hawezi ongea hoja za kijinga kama hizi...!!
Hii suala ni kubwa sana, haupaswi upanic
 
Ndugu yangu macho_mdiliko hata wewe hujaandika lugha sahihi hapo juu. Hakuna binadamu mkamilifu. Ila ujumbe umeshafika kwa walengwa na washauri wa mjomba Pombe.
Nani kasema kuna binadamu mkamilifu? Naomba tusichanganye mapungufu ya kibinadamu ya kawaida na u-kiazi wa darasani! Yaani mtu asome mpaka level ya Phd tena kwa kiingereza, halafu awe mwalimu afundishe kwa kiiingereza na kisha awe waziri kwa muda mrefu tu na bado simple english inamshinda kama mtoto wa darasa la saba? Hapana. Kuna kitu ambacho hakiko sawa kabisa kwenye mfumo wetu wa elimu. Na huyu tumebahatika kujua kwa sababu tu ni kiongozi. This is serious issue ndugu yangu.
 
Mmekosa hoja....Nyie hata kiswahili hamjui sembuse kingereza....!!Upinzani wengi ni vijana mpechempeche marioo wa mjini wapenda vya bure,kingereza wamekijulia Kwenye movie na nyimbo za kina Cellin Dione...Wanaume wa kweli hawezi ongea hoja za kijinga kama hizi...!!
Sasa kwanini msimshauri kutumia kiswahili badala ya kuliaibisha Taifa kiasi hiki?
 
Mmekosa hoja....Nyie hata kiswahili hamjui sembuse kingereza....!!Upinzani wengi ni vijana mpechempeche marioo wa mjini wapenda vya bure,kingereza wamekijulia Kwenye movie na nyimbo za kina Cellin Dione...Wanaume wa kweli hawezi ongea hoja za kijinga kama hizi...!!
Wewe kwa upeo wako ndiyo unaona ni hoja ya kijinga. Hapa tunazungumzia mtu aliyeandika thesis ya kitaalam ya kuhitimu Phd baada ya kufanya utafiti na baadae akawa mwalimu akifundisha kwa kutumia lugha ya kiingereza. Aliwezaje kumudu yote hayo wakati hawezi kuongea kiingereza ''cha kuridhisha''? Na wala siongei kile kizuri.

Nimekutana na wasomi wengi ambao english inawapiga chenga lakini wakizungumza unaona kabisa wana mwelekeo wa usomi na unaridhika. Hata maswali rahisi anashindwa kuelewa sembuse kujibu! Something very very wrong with his education!
 
"The Eclipse of the English Language" in the middle of native Local vernacular and overal national Swahili.

Kimalkia ni kigumu asikuambie mtu. Sisi tuliosoma before ni shida. Vijana wetu tumewapeleka international schools na kusomea nje ya nchi huwezi kuwalinganisha na sisi wa Kiingereza cha kukariri tulichoanza kusoma tukiwa darasa la 5. 😂😂😂🤣🤣🤣
 
Hahahahaaaa... (alisikika akicheka mtoto wa darasa la pili wa English medium). Anapenda sana kujifaragua na kutia watu million 60 aibu ya bure. Aongee tu Kiswahili.
"We suppose to focus according our direction, according our environment, that's only way we can help our peoples. No body should come and say that his there to save the problems of our peoples, we are the one we are leader we suppose to change the direction"
 
Ni aibu kwa rais wa nchi, ambaye amesoma mpaka chuo kikuu kwa kiingereza, akaishi ulaya, akafanya Phd kwa kiingereza halafu hajui kuongea kiingereza fasaha.​
Acha uongo. Magufuli hajawahi kuishi Ulaya.
 
Rais Magufuli ni mtu huru, ni fikra huru. Na hiki ndicho kinachomfanya awe rais bora miongoni mwa marais tuliowahi kuwa nao Tanzania. Anawaza kivyake, anasema anavyotaka iwe kingreza, kiswahili au kisukuma. Akosee au asikosee.

Rais wetu si mtumwa wa mtu yeyote, akili zake hajashikiwa na mtu yeyote. Anafanya anavyoona inafaa popote pale na muda wowote ule.

Ogopa kiongozi anayesema kwa staili ya ajili kuwaridhisha watu fulani au eti aendane na fikra fulani. Political correctness. Ni wabaya maana hawana ubunifu, hawawezi fanya maamuzi magumu, yaani wapo wapo tu kama maroboti ya kikundi fulani cha watu au fikra. Tulipopata uhuru kutoka kwa mkoloni maana yake ilikuwa ni uhuru kamili -- kimwili, kifikra na kimaamuzi.
 
Ndio hapo utashangaa ana mrukia Dkt Avemaria Semakafu aliye katika program ya kuinua walimu wa cheti kuwa na diploma kuwa ni mpumbavu sasa dunia ione Mpumbavu wa kweli no yupi hiyu mtu hashauriki ngoja tarehe 28/10 aumbuke ndipo siri zake za upumbavu wake utakavyo anikwa kwa speed ya moto wa petrol
 
Ni aibu kwa rais wa nchi kama Tanzania, ambaye amesoma mpaka chuo kikuu kwa kiingereza, akaishi ulaya, akafanya Phd kwa kiingereza halafu hajui kuongea kiingereza fasaha.

Rais wa nchi ndio kioo cha nchi, kiingereza kibovu cha rais wetu ni aibu kwetu sisi sote. Wasaidizi wa rais wako wapi kumsaidia kumfundisha kiingereza kizuri.
Usitujumuishe kwenye dhambi yako.

"Aibu kwetu sote" kivipi??
 
Back
Top Bottom