Wasichana wa kiislamu wamekamatwa wakiwa wamefungiwa kwenye nyumba Dodoma, inayosadikika kupewa elimu ya dini

Hilo ni soko la binadamu, ambapo wanaandaliwa kwenda kuuzwa kwa waume zao nje ya nchi
 
Shot...
Nimefika MUM nimepokelewa na Prof. Mussa Assad na Prof. Hamza Njozi.

Nimewahi halikadhalika kuwa kwenye mradi wa utafiti na Prof. Ibrahim Juma kutoka MUM.

Nashangaa kuwa hawapo kwenye hiyo orodha.

Nakumbuka pia alikuwako Prof. kutoka Malaysia lakini alikwenda likizo kwao na hakurejea kwa sababu za corolla.
 
Hongera watu usalama kwa kuwahi maana walikuwa wanaandaliwa kuwa watu hatari
Ash...
Hapakuwa na tishio la usalama.
Ingekuwa hilo limethibiti Sheikh Yusuf Muhammad angefikishwa mahakamani kujibu mashtaka.

Ugonjwa ni ule ule wa kuogopa Uislam uwe ni historia yao katika kupigania uhuru wa Tanganyika au kujenga taasisi zao huru.
 
Naijua sana historia ya uhuru wa Tanganyika, lakini narudia Tena wakati wa TAA na hatimaye kuundwa kwa TANU mwenye elimu ngazi ya Digrii alikuwa ni Kambarage tu na mwenye hela kuwazidi wote alikuwa John Rupia. Wengine walikuwa na elimu ya kawaida na hela kiduchu.
 
Hilo dini linafundisha chuki bwana unafikir hatujui
 
Niz...
Hapana huijui sana historia ya uhuru wa Tanganyika.
Mimi naijua sana kiasi nimeandika kitabu cha historia hii.

Kitabu hiki kimebadili historia iliyokuwapo ya TANU na historia ya Julius Nyerere.

Kitabu kinakwenda chapa ya nne.
Kimepokelewa vyema ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.

Umuhimu wa kitabu hiki ni kule kueleza yale ambayo hayakupata kuandikwa kabla.

Ungekuwa unaijua historia ya TANU ungejua kuwa TANU ilikuwa na wafadhili wanne matajiri: John Rupia, Dossa Aziz na Abdulwahid na Ally Sykes ndugu wawili.

Dossa Aziz alikuwa na malori saba ya mchanga na kokoto aliyorithi kutoka kwa baba yake Aziz Ali pamoja na kampuni ya ujenzi wa majumba.

Dossa aliipa TANU gari yake ya kwanza iliyokuwa ikitumiwa na Nyerere.

Utajiri wa Sykes unafahamika na umedumu hadi leo.

Iko siku nitakuwekea hapa kisa cha kabati la fedha la Abdul Sykes lililokuwa liko wazi kwa TANU kuanzia 1954 hadi uhuru unapatikana.

Huyu Abdul Sykes ndiye aliyeishi na Nyerere nyumbani kwake Nyerere alipoacha kazi ya ualimu baada ya safari ya UNO 1955.

Mipango yote ya safari ikifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu.

Angalia picha ya nyumba hiyo ya Abdul Sykes iliyojengwa 1942 na hii iliyojengwa sasa.

(Hiki ndicho kilikuwa kituo cha mikutano yote ya siri ya TANU toka enzi za TAA).

Degree isingeweza kufanya haya na kuunda chama cha African Association 1929 na kuunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) 1933.

Wazalendo katika vyama hivi walianza harakati dhidi ya Waingereza miaka hiyo.

Sitaki kujirudia nimekueleza vipi Nyerere alichaguliwa na sababu zake.

Ikiwa huamini hakuna tatizo.
Nikueleze upate kujua.

Abdul Sykes 1953 alikuwa amekubaliwa kujiunga na Princeton University, New Jersey.


Nyumba ya Abdul Sykes aliyosihi Nyerere 1955

Nyumba ya Abdul Sykes kama ilivyo hivi sasa
 
Hilo dini linafundisha chuki bwana unafikir hatujui
Ash...
Uislam ungefundisha chuki Nyerere asingekuwa kiongozi wa TANU.

Angalia picha hizo hapo chini Nyerere yuko na watu gani na ikiwa huwajui hao ni nani uliza.

Unaona chuki na uadui hapo?


Baraza la Wazee wa TANU 1957

Safari ya kwanza UNO 1955

Wakati wa kupigania uhuru miaka ya 1955/56 Dodoma
 
Walianzisha harakati za kudai uhuru sawa lakini hawakuwa na elimu Dunia ndio maana wakamhitaji mtu anayeona mbali mwenyeelimu ya kutosha yaani Kambarage wa Butiama
Usijidanganye.

Elimu yoyote ile ni ya duniani.

Akhera kuna moto au pepo kwa utayoyachuma duniani.
 
Wapi habari imetaja 200?

Hiyo ni sifa kubwa tena kubwa sana mabinti kutunzwa na kusomeshwa dini na bikra zao. Au Ulitaka wasiwe bikra?
 
Hawa wengi wao wanawatoa Kondoa .. Kuna maeneo kule watu hawajui chochote Cha Dunia zaidi ya Uislam.. hata wakiona mtu wa Dini nyinginewanadhangaa mno..
Kuna Mwalimu Mkristu alipangwa kufundisha huko alipata shida sana!
Kuna chema cha dunia zaidi ya Uislam?

Au kwako wewe masomo ya kufundisha watoto namna ya kuvalisha wanaume kondom kuanzia shule ya msingi ndio ya maana?
 
Hata mimi nimesikitika dana mabinti kuwachishwa masomo ya dini yao kabla hawajahitimu.
Mabikra waachwe wasome ilm zote, ilm duniya na ilm akhera. Tatizo ni pale maustadh wanapolazmisha wapate ilm akhera pekee.
 
Wapi habari imetaja 200?

Hiyo ni sifa kubwa tena kubwa sana mabinti kutunzwa na kusomeshwa dini na bikra zao. Au Ulitaka wasiwe bikra?
Pitia youtubue, nikiwaka hapa mods wanaondoa, labda issue za copyrights.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…