Wasifu wa Rais Samia Suluhu Hassan

Wasifu wa Rais Samia Suluhu Hassan

Nataka tuingie karne ya 21 lakini bado tunaishi maisha waliyoishi wenzetu karne ya 18. Sasa hao wasomi wana faida gani?
Hata kufikiri kidogo huwezi? Hao "wenzenu wa karne ya 18" hata hujui iliwachukuwa muda gani kufikia hapo walipofika?

Wewe unadhani ilitokea tu mara vuuu, wakawa kama walivyo leo?
 
Tanzania anastahiki kumpata rais anayekubalika na kuwafanyia kazi waTanzania, siyo mataifa ya huko unayoyatafuta wewe.
Samia hana uwezo. Hadi 2025 Tanzania itakuwa ni jalala la uchafu wa hao unaowaita watu wa nje wanaomkubali yeye.

Na zaidi ya yote, na pengine ndiyo chanzo cha ubovu wa uongozi wake, Samia hana maslahi ya nchi hii moyoni mwake.
Huwezi kuwakwepa watu wa nje hilo ndio tatizo. Alishindwa Nyerere na uwezo wake wote wa kufikiri na kujenga hoja hatakuja kuweza rais mwingine yoyote.

Na huwezi kuishi kwa kujitenga, utakosa fursa nyingi za uwekezaji. Utalii unaongezeka sana baada ya Royal Tour.
 
Tofautisha utajiri na kuiongoza serikali. Mikataba unaijua? Sera na sheria? Huwezi kuwahimiza wananchi wajitutumue kutafuta kisomo, tena kwa gharama kubwa, ilhali wewe huoneshi mfano.

President anapaswa kuwa kielelezo ladhimu (impeccable role model) almost katika kila nyanja za bora.
Rais Samia ni msomi mzuri tu, huu uzi umeandikwa na wale wenye donge wanapomuona mwanamama ana cheo cha juu kabisa Tanzania.
 
Rais Samia ni msomi mzuri tu, huu uzi umeandikwa na wale wenye donge wanapomuona mwanamama ana cheo cha juu kabisa Tanzania.
Hapo sawa, kama ni hivyo. Lakini mbona uendeshaji wake wa serikali una tashwishi nyingi? Mbona hajiamini? Kwa nini haamini kwamba Tanzania itafanikiwa tu kwa kutumia siasa na sera za maendeleo ya kujitegemea, na wala siyo kujikomba ughaibuni akitafuta hisani, fadhila, misaada na mikopo, huku kuwadhalilisha Watanzania, na mwishowe taifa kuishia kunyonywa zaidi?

Ndiyo maana wazalendo bila shaka wameamua kuhoji kiwango na ubora wa elimu yake.
 
Huyu na Magufuli na Kikwete wote elimu Yao ni ya kuunga unga tu kwahiyo hawana usomi wowote tena Bora na Kikwete kidogo.
Lakini lazima turejee maana halisi ya elimu ya kweli. Wakati ambapo mie ni mdau, mbia, na msoda wa elimu, sina mahaba na elimu tu ya darasani ambayo haijipambanui katika ufanisi wa maisha halisi na utendaji.

Nadhani mtihani wa kweli unaoonesha kwamba mtu ana elimu, amesoma na kupata maarifa yenye tija, ni matumizi ya elimu husika uraiani.

JK, JPM, na SSH (plus wengineo), wanaweza tu kupimwa kihalali kwa kigezo hiki.

Angalia mfano mmoja tu kuhusu wasaidizi wa SSH. Hivi unaanzaje kumtoa kiongozi hodari kama Lukuvi kwenye Wizara ya Ardhi? Hata kama, tuseme, kwa kukiakiza hoja, Lukuvi angekuwa na makosa 99 kwa 100, bado angefaa saa kuendelea na wizara husika.

^Elimu^

^Elimu^

^Elimu^~ Alisema ENL.

Inaweza isiwe elimu ya makaratasi fulani-fulani, per se, anayokosa Bibie, lakini elimu ya uzalendo, elimu ya kutambua kwamba zaidi ya 80% ya Watanzania ni fukara, elimu ya kutambua kwamba UJINGA, MARADHI, na UMASKINI--maadui aliopambana sana JKN ili kuwatokomeza, hivi sasa wameshamiri kama jana!

Elimu ya kutambua kwamba hakuna mjomba wala shangazi atakayetoka Ulaya ili kuyapambania maendeleo ya nchi yetu.

Narudia tena, kuna ukasisi mkubwa kuhusu elimu kwa mtu mwenye akili timamu asiyetambua na kutumikia mahitaji mahususi ya wananchi. Hivi unawezaje hata kufurahia kiti cha urais ilhali wapo mamilioni ya watu wako kila kona ambao hata hawajui watakula nini leo mchana? Maji? Afya? Elimu yao? Furaha? Maendeleo kijumla?

Nasema hivi, hakuna elimu hapo. Hiko ni kitu kingine, siyo elimu. Nyerere alisema elimu inakomboa fikra na utu na kuleta maendeleo himilivu. Kwetu hapa Tanzania, elimu inafanya kinyume cha haya. Halafu mnaleta habari za CV? Nonsense!
 
Bi Samia Suluhu alizaliwa Januari 27, 1960 visiwani Zanzibar. Alisomea shule za msingi za Chawaka (Unguja), Ziwani (Pemba) na Mahonda (Unguja) na kati ya 1966 na 1972 na kisha akasomea masomo ya upili Ngambo, Unguja (1973-1975) na Lumumba, Unguja (1976).

Alisomea kozi mbalimbali hadi akafikia kupata shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Southern New Hampshire nchini Marekani.

Kazi
Aliajiriwa kama mchapishaji katika serikali ya Zanzibar mwaka 1977 na akapanda ngazi hadi kuwa afisa wa mipango serikalini kati ya 1987 na 1988.

Alihudumu pia kama meneja wa mradi wa Shirika la Chakula Duniani (WFP) Zanzibar kati ya 1985 na 1997, na pia kama meneja mkurugenzi wa Mwamvuli wa NGO 1998 hadi 1999.

Bi Samia anasema kuwa njia yake ya ufanisi haijakuwa rahisi kama inavyodhaniwa.

''Safari yangu katika siasa imekuwa njia ndefu na yenye tija.''

Kimsingi ufanisi wangu katika siasa za Tanzania umetokana na uweledi na umakini katika kila jambo ninalolifanya.''

''Sio rahisi kuwajibikia familia yako wakati huohuo ukiendelea na maisha ya siasa elimu na majukumu mengine ya kikazi," anasema Bi Samia.

Familia
Aliolewa mwaka wa 1978, kwa Bw Hafidh Ameir, ambaye wakati huo alikuwa afisa wa Kilimo .

Walijaliwa watoto wanne.

Mmoja kati ya wanawe Wanu Hafidh Ameir (1982), ni mwakilishi maalum katika bunge la Zanzibar

Siasa
Alijiunga na siasa mwaka wa 2000.

Wakati huo alijiunga na bunge la wawakilishi la Zanzibar kama mjumbe maalum.

Haikuchukua muda mrefu nyota yake ikaanza kung'aa na akateuliwa kuwa waziri na rais Amani Karume, akipewa wadhifa wa Waziri wa Leba, Jinsia na Watoto.

Alitumikia taifa hadi mwaka wa 2005 alipochaguliwa tena na kuteuliwa upya kama waziri, wakati huu akipewa wizara ya Utalii, Biashara na Uwekezaji katika serikali ya visiwani.

Mwaka wa 2010 alichaguliwa kuwa mwakilishi wa jimbo la Makunduchi.

Punde tu akateuliwa na rais Jakaya Kikwete kuwa waziri wa maswala ya muungano katika serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akihudumu chini ya Makamu wa Rais Mohamed Gharib Bilal.

Machi mwaka 2014, aliwania na kuchaguliwa kuwa makamu mwenyekiti wa Bunge maalum la Katiba nmjini Dodoma. Bi Hassan alichaguliwa kwa kura 390 sawa na asilimia 74.6 na kumshinda mpinzani wake Amina Abdalla Amour ambaye alipata kura 126 sawa na 24%.

Julai mwaka 2015, Dkt John Magufuli alimteua kuwa mgombea mwenza.
===
First Name: Samia
Middle Name: Hassan
Last Name: Suluhu
Member Type: Elected Member
Political Party: Chama Cha Mapinduzi
Office Location: P.O. Box 3021, Dar Es Salaam
Office Phone: +255 774 010 203/+255 784 717 712 Office Fax:
Date of Birth 27 January 1960

EDUCATION
  • School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
  • Ziwani Primary School, Pemba CPEE 1970 - 1971 Primary School
  • Mahonda Primary School, Unguja CPEE 1972 - 1972 Primary School
  • Chwaka Primary School, Unguja CPEE 1966 - 1968 Primary School
  • Ngambo SecondarySchool, Unguja CSEE 1973 1975 Secondary School
  • Lumumba Secondary School, Unguja CSEE 1976 1976 Secondary School
  • National Institute of Public Administration, Lahore Pakistan Course 1989 1989 Certificate
  • Institute of Management for Leaders, Hyderabad, India Management Course 1991 1991 Certificate
  • Zanzibar Institute of Financial Administration, ZIFA Statistics 1983 1983 Certificate
  • Institute of Development Management, IDM, Mzumbe (Morogoro) Advanced Diploma 1983 1986 Advanced Diploma
  • Manchester University, London Postgraduate 1992 1994 Postgraduate Diploma
  • Open University Southern New Hampshire, USA M.A 2004 2005 Masters Degree

EMPLOYMENT HISTORY
  • Company Name Position From To
  • The Parliament of Tanzania Member - Makunduchi Constituency 2010 2015
  • Ministry of Tourism, Trade and Investment, Zanzibar Minister 2005 2010
  • Ministry of Labour, Gender Development and Children Minister 2000 2005
  • Mwamvuli wa NGO Managing Director 1998 1999
  • Revolutionary Government of Zanzibar Planning Officer 1987 1988
  • World Food Programme, WFP - Zanzibar Project Manager 1985 1997
  • Revolutionary Government of Zanzibar Typists (Typing Pool) 1977 1986

POLITICAL EXPERIENCE
  • Ministry/Political Party/Location Position From To
  • Chama Cha Mapinduzi, CCM Guardian (Warden) - North Unguja Region 2009 Todate
  • Chama Cha Mapinduzi, CCM Guardian (Warden) - North Pemba Region 2004 2007
  • Chama Cha Mapinduzi, CCM Member - National Executive Committee (NEC) 2002 Todate
Born 60 .. kazi 77 ...akiwa na miaka 17 tayari ajira serikalini na bado unasema alisoma kozi mbali mbali ... zilikuwa kozi za week week nini
 
Hapo sawa, kama ni hivyo. Lakini mbona uendeshaji wake wa serikali una tashwishi nyingi? Mbona hajiamini? Kwa nini haamini kwamba Tanzania itafanikiwa tu kwa kutumia siasa na sera za maendeleo ya kujitegemea, na wala siyo kujikomba ughaibuni akitafuta hisani, fadhila, misaada na mikopo, huku kuwadhalilisha Watanzania, na mwishowe taifa kuishia kunyonywa zaidi?

Ndiyo maana wazalendo bila shaka wameamua kuhoji kiwango na ubora wa elimu yake.
Hakuna nchi inayoweza kuwa kama kisiwa, siasa za hayati JPM zilikuwa na matatizo.

Ukiongelea sana kujitegemea pia unakuwa unaficha ubaguzi ule ule walionao wazungu kwa kigezo cha kutukuza uafrika wako.

Samia alikuwa mwerevu kwa kumpa yule mama wizara ya mambo ya nje, kuifufua diplomasia ya kiuchumi tofauti kabisa na Profesa Kabudi.
 
Hata kufikiri kidogo huwezi? Hao "wenzenu wa karne ya 18" hata hujui iliwachukuwa muda gani kufikia hapo walipofika?

Wewe unadhani ilitokea tu mara vuuu, wakawa kama walivyo leo?

Nyerere si alisema siye tunakimbia wengine wanatembea? Hizo mbio zote za miaka 60 tangu tupate uhuru tumeshindwaje kuwafikia wanaotembea?
 
Bi Samia Suluhu alizaliwa Januari 27, 1960 visiwani Zanzibar. Alisomea shule za msingi za Chawaka (Unguja), Ziwani (Pemba) na Mahonda (Unguja) na kati ya 1966 na 1972 na kisha akasomea masomo ya upili Ngambo, Unguja (1973-1975) na Lumumba, Unguja (1976).

Alisomea kozi mbalimbali hadi akafikia kupata shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Southern New Hampshire nchini Marekani.

Kazi
Aliajiriwa kama mchapishaji katika serikali ya Zanzibar mwaka 1977 na akapanda ngazi hadi kuwa afisa wa mipango serikalini kati ya 1987 na 1988.

Alihudumu pia kama meneja wa mradi wa Shirika la Chakula Duniani (WFP) Zanzibar kati ya 1985 na 1997, na pia kama meneja mkurugenzi wa Mwamvuli wa NGO 1998 hadi 1999.

Bi Samia anasema kuwa njia yake ya ufanisi haijakuwa rahisi kama inavyodhaniwa.

''Safari yangu katika siasa imekuwa njia ndefu na yenye tija.''

Kimsingi ufanisi wangu katika siasa za Tanzania umetokana na uweledi na umakini katika kila jambo ninalolifanya.''

''Sio rahisi kuwajibikia familia yako wakati huohuo ukiendelea na maisha ya siasa elimu na majukumu mengine ya kikazi," anasema Bi Samia.

Familia
Aliolewa mwaka wa 1978, kwa Bw Hafidh Ameir, ambaye wakati huo alikuwa afisa wa Kilimo .

Walijaliwa watoto wanne.

Mmoja kati ya wanawe Wanu Hafidh Ameir (1982), ni mwakilishi maalum katika bunge la Zanzibar

Siasa
Alijiunga na siasa mwaka wa 2000.

Wakati huo alijiunga na bunge la wawakilishi la Zanzibar kama mjumbe maalum.

Haikuchukua muda mrefu nyota yake ikaanza kung'aa na akateuliwa kuwa waziri na rais Amani Karume, akipewa wadhifa wa Waziri wa Leba, Jinsia na Watoto.

Alitumikia taifa hadi mwaka wa 2005 alipochaguliwa tena na kuteuliwa upya kama waziri, wakati huu akipewa wizara ya Utalii, Biashara na Uwekezaji katika serikali ya visiwani.

Mwaka wa 2010 alichaguliwa kuwa mwakilishi wa jimbo la Makunduchi.

Punde tu akateuliwa na rais Jakaya Kikwete kuwa waziri wa maswala ya muungano katika serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akihudumu chini ya Makamu wa Rais Mohamed Gharib Bilal.

Machi mwaka 2014, aliwania na kuchaguliwa kuwa makamu mwenyekiti wa Bunge maalum la Katiba nmjini Dodoma. Bi Hassan alichaguliwa kwa kura 390 sawa na asilimia 74.6 na kumshinda mpinzani wake Amina Abdalla Amour ambaye alipata kura 126 sawa na 24%.

Julai mwaka 2015, Dkt John Magufuli alimteua kuwa mgombea mwenza.
===
First Name: Samia
Middle Name: Hassan
Last Name: Suluhu
Member Type: Elected Member
Political Party: Chama Cha Mapinduzi
Office Location: P.O. Box 3021, Dar Es Salaam
Office Phone: +255 774 010 203/+255 784 717 712 Office Fax:
Date of Birth 27 January 1960

EDUCATION
  • School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
  • Ziwani Primary School, Pemba CPEE 1970 - 1971 Primary School
  • Mahonda Primary School, Unguja CPEE 1972 - 1972 Primary School
  • Chwaka Primary School, Unguja CPEE 1966 - 1968 Primary School
  • Ngambo SecondarySchool, Unguja CSEE 1973 1975 Secondary School
  • Lumumba Secondary School, Unguja CSEE 1976 1976 Secondary School
  • National Institute of Public Administration, Lahore Pakistan Course 1989 1989 Certificate
  • Institute of Management for Leaders, Hyderabad, India Management Course 1991 1991 Certificate
  • Zanzibar Institute of Financial Administration, ZIFA Statistics 1983 1983 Certificate
  • Institute of Development Management, IDM, Mzumbe (Morogoro) Advanced Diploma 1983 1986 Advanced Diploma
  • Manchester University, London Postgraduate 1992 1994 Postgraduate Diploma
  • Open University Southern New Hampshire, USA M.A 2004 2005 Masters Degree

EMPLOYMENT HISTORY
  • Company Name Position From To
  • The Parliament of Tanzania Member - Makunduchi Constituency 2010 2015
  • Ministry of Tourism, Trade and Investment, Zanzibar Minister 2005 2010
  • Ministry of Labour, Gender Development and Children Minister 2000 2005
  • Mwamvuli wa NGO Managing Director 1998 1999
  • Revolutionary Government of Zanzibar Planning Officer 1987 1988
  • World Food Programme, WFP - Zanzibar Project Manager 1985 1997
  • Revolutionary Government of Zanzibar Typists (Typing Pool) 1977 1986

POLITICAL EXPERIENCE
  • Ministry/Political Party/Location Position From To
  • Chama Cha Mapinduzi, CCM Guardian (Warden) - North Unguja Region 2009 Todate
  • Chama Cha Mapinduzi, CCM Guardian (Warden) - North Pemba Region 2004 2007
  • Chama Cha Mapinduzi, CCM Member - National Executive Committee (NEC) 2002 Todate
"Walijaliwa watoto wanne.

Mmoja kati ya wanawe Wanu Hafidh Ameir (1982), ni mwakilishi maalum katika bunge la Zanzibar".
Ni nani mwenye jukumu la ku update hii CV humu jukwaani!!?
Mbona hao watoto wengine haisomeki wapo wapi/ wana nafasi gani!!??
Ritz tafadhali njoo uipange upya huu wasifu uliouanzisha hapa jukwaani ili uweke rekodi sawa.
 
Born 60 .. kazi 77 ...akiwa na miaka 17 tayari ajira serikalini na bado unasema alisoma kozi mbali mbali ... zilikuwa kozi za week week nini
Kumbuka tu kwamba miaka ile ya 70 ukimaliza form 4 tu kazi ziko tayari. Kujiendeleza inakuja baadae ukiwa kazini.

Mbona hata mimi nilimaliza form 6 nikiwa miaka 17 na miaka 18 nimeanza kazi baadae ndiyo nikaenda University.
 
Huwezi kuwakwepa watu wa nje hilo ndio tatizo. Alishindwa Nyerere na uwezo wake wote wa kufikiri na kujenga hoja hatakuja kuweza rais mwingine yoyote.

Na huwezi kuishi kwa kujitenga, utakosa fursa nyingi za uwekezaji. Utalii unaongezeka sana baada ya Royal Tour.
Nani kasema kuishi kwa kujitenga kama siyo kutafuta upotoshaji wa hoja.

Nyerere alishindwa nini, kwenda nje, mbona kama unajichanganya mweyewe!

Nyerere hakwenda nje kutafuta watu wa nje walete maendeleo Tanzania.
 
Nyerere si alisema siye tunakimbia wengine wanatembea? Hizo mbio zote za miaka 60 tangu tupate uhuru tumeshindwaje kuwafikia wanaotembea?
Hivi hukuona tulipoanzia 1961, au hata historia huwezi ukaisoma na kuielewa?
 
Nani kasema kuishi kwa kujitenga kama siyo kutafuta upotoshaji wa hoja.

Nyerere alishindwa nini, kwenda nje, mbona kama unajichanganya mweyewe!

Nyerere hakwenda nje kutafuta watu wa nje walete maendeleo Tanzania.
Sera za Nyerere zilikufa kitambo tu. Kubali au kataa huwezi kuendesha uchumi kwa kutegemea nguvu kazi hii ya kibongo peke yake.

Tungekuwa na jeuri ya kujitegemea tusingetaifisha mashirika ya umma zaidi ya 50. Tusingekuja na dhana hizi za kuingia ubia.
 
Sera za Nyerere zilikufa kitambo tu. Kubali au kataa huwezi kuendesha uchumi kwa kutegemea nguvu kazi hii ya kibongo peke yake.

Tungekuwa na jeuri ya kujitegemea tusingetaifisha mashirika ya umma zaidi ya 50. Tusingekuja na dhana hizi za kuingia ubia.
Mbona ni kama huelewi, au unapenda sana kupotosha uonekane una hoja?

Nani kasema "tutegemee nguvu kazi hii ya kibongo pekee", na ni wapi uliposikia Nyerere akisema hatuwezi kushirikiana na watu wengine toka nje katika maendeleo yetu?

Lakini jukumu ni letu, na hatuwezi kamwe kutegemea kupata maendeleo kwa kwenda huko kuyatafuta yaletwe hapa.

Hilo swala la mashirika unalitumbukiza hapa pasipo kujua maana yake ni nini. Kwani ni Tanzania pekee ndiko mashirika ya umma yalipokuwa?
 
Mbona ni kama huelewi, au unapenda sana kupotosha uonekane una hoja?

Nani kasema "tutegemee nguvu kazi hii ya kibongo pekee", na ni wapi uliposikia Nyerere akisema hatuwezi kushirikiana na watu wengine toka nje katika maendeleo yetu?

Lakini jukumu ni letu, na hatuwezi kamwe kutegemea kupata maendeleo kwa kwenda huko kuyatafuta yaletwe hapa.

Hilo swala la mashirika unalitumbukiza hapa pasipo kujua maana yake ni nini. Kwani ni Tanzania pekee ndiko mashirika ya umma yalipokuwa?
Anaendelea kuupiga mwingi sisi tuendelee kukosoa na kulalama.
 
Back
Top Bottom