Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Picha umepeleka wapiNaibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk Amon Mpanju amesema siku hizi wasimamizi wa ndoa wamekuwa ni fasheni na siyo wale wenye sifa ya kufanya kazi hiyo katika ndoa.
Sambamba na hilo amesema wakati mwingine wanakuwa ‘pisi kali’ kuliko bibi harusi mwenyewe.
Mpanju ameyasema hayo leo Ijumaa Novemba 25, 2022 katika uzinduzi wa maadhimisho ya siku 16 za uanaharakati dhidi ya ukatili wa kijinsia, yaliyofanyika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.
Amesema hii ni tofauti na huko nyuma ambapo msimamizi alipaswa kuwa mtu anayejua vizuri masuala ya ndoa na kutumika kama msuluhishi pindi kunapotokea changamoto.
Amesema hii imekuwa tofauti kwa sasa ambapo wasimamizi hao imekuwa ni fasheni na wanaangalia zaidi mvuto wa kimaumbile na sura na wengine wanakuwa hawajaingia kwenye ndoa hivyo kunavyotokea mtikisiko kwa wenye ndoa anashindwa kuwasaidia kwa kuwa hana uzoefu.
Hata hivyo, katika kuendelea na kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia vikiwemo vya ndani ya ndoa, katibu huyo amesema Serikali inaenda kushuka chini kwenye jamii ikiwemo kuwashirikisha viongozi wa dini makanisani misikitini na madrasa.
"Huko msikitini na makanisani kwa viongozi wa dini ndio watu wanaoweza kupata mafunzo ya uchaguzi mzuri wa mtu wa kuoa au kuolewa naye.
“Pia inatakiwa ifike mahali jamii itofautishe tendo la ndoa na taasisi ya ndoa ambayo ni kubwa kuliko mnavyofikiria hivyo katika mkakati ya kutokomeza ukatili wa kijinsia safari hii tunataka kumshirikisha kila mwanajamii wakiwemo viongozi hao wa dini,"amesema Mpanju.
Katika kukabiliana na vitendo vya vipigo katika ndoa, katibu huyo amesema kwa wale walio na mahusiano na wanaume wenye tabia ya kuwapiga wakati wakiwa kwenye uchumba wasitegemee mwanaume huyo akabadilika akiwa kwenye ndoa.
Ameeleza hiyo ni trela ndani akiingia atakuta mkanda wenyewe na kushauri waanze kuwaepuka mapema kabla ya kuja kufanyia madhara makubwa.
MWANANCHI
Ningekuwa Rwanda ningekufa kwa umalaya hii nchi imebarikiwa pisi kali
Siyo kipofu sema mtu asiyeona. Halafu kuujua uzuri wa mtu mpaka umuone kwa macho?Huyo Mpanju si anasema ni KIPOFU???
Kuna shida kwako nduguKipofu anazionaje pisikali?
Kwa miCCM ilivyo yawezekana Mpanju ni KIPOFU wa mchongo.Siyo kipofu sema mtu asiyeona. Halafu kuujua uzuri wa mtu mpaka umuone kwa macho?
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Uzuri wa mtu upo 'machoni' pa mtazamaji, hizi porojo za asiyeona sijui nini ni kipofu tu…. acha siasa.Siyo kipofu sema mtu asiyeona. Halafu kuujua uzuri wa mtu mpaka umuone kwa macho?
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Hii tu ndio nimeona point“Pia inatakiwa ifike mahali jamii itofautishe tendo la ndoa na taasisi ya ndoa ambayo ni kubwa kuliko mnavyofikiria hivyo katika mkakati ya kutokomeza ukatili wa kijinsia safari hii tunataka kumshirikisha kila mwanajamii wakiwemo viongozi hao wa dini,"amesema Mpanju.
Kazi kweli kweli
Unaposema wimbo mzuri je umeona? Uzuri una namna nyingi kuufahamu sio macho tu.Uzuri wa mtu upo 'machoni' pa mtazamaji, hizi porojo za asiyeona sijui nini ni kipofu tu…. acha siasa.
Weka picha mkuuNaibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk Amon Mpanju amesema siku hizi wasimamizi wa ndoa wamekuwa ni fasheni na siyo wale wenye sifa ya kufanya kazi hiyo katika ndoa.
Sambamba na hilo amesema wakati mwingine wanakuwa ‘pisi kali’ kuliko bibi harusi mwenyewe.
Mpanju ameyasema hayo leo Ijumaa Novemba 25, 2022 katika uzinduzi wa maadhimisho ya siku 16 za uanaharakati dhidi ya ukatili wa kijinsia, yaliyofanyika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.
Amesema hii ni tofauti na huko nyuma ambapo msimamizi alipaswa kuwa mtu anayejua vizuri masuala ya ndoa na kutumika kama msuluhishi pindi kunapotokea changamoto.
Amesema hii imekuwa tofauti kwa sasa ambapo wasimamizi hao imekuwa ni fasheni na wanaangalia zaidi mvuto wa kimaumbile na sura na wengine wanakuwa hawajaingia kwenye ndoa hivyo kunavyotokea mtikisiko kwa wenye ndoa anashindwa kuwasaidia kwa kuwa hana uzoefu.
Hata hivyo, katika kuendelea na kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia vikiwemo vya ndani ya ndoa, katibu huyo amesema Serikali inaenda kushuka chini kwenye jamii ikiwemo kuwashirikisha viongozi wa dini makanisani misikitini na madrasa.
"Huko msikitini na makanisani kwa viongozi wa dini ndio watu wanaoweza kupata mafunzo ya uchaguzi mzuri wa mtu wa kuoa au kuolewa naye.
“Pia inatakiwa ifike mahali jamii itofautishe tendo la ndoa na taasisi ya ndoa ambayo ni kubwa kuliko mnavyofikiria hivyo katika mkakati ya kutokomeza ukatili wa kijinsia safari hii tunataka kumshirikisha kila mwanajamii wakiwemo viongozi hao wa dini,"amesema Mpanju.
Katika kukabiliana na vitendo vya vipigo katika ndoa, katibu huyo amesema kwa wale walio na mahusiano na wanaume wenye tabia ya kuwapiga wakati wakiwa kwenye uchumba wasitegemee mwanaume huyo akabadilika akiwa kwenye ndoa.
Ameeleza hiyo ni trela ndani akiingia atakuta mkanda wenyewe na kushauri waanze kuwaepuka mapema kabla ya kuja kufanyia madhara makubwa.
MWANANCHI
Pisi kali ktk kusimamiaHalafu yeye ni kipofu aliwaonaje?