Wasiomuelewa Hussein Bashe kwenye sukari waelewe swali la Dkt.Tulia

Wasiomuelewa Hussein Bashe kwenye sukari waelewe swali la Dkt.Tulia

Kiranja wa jamii

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2023
Posts
441
Reaction score
1,065
Kitu kitakachokumbukwa sana kwenye bunge la bajeti mwaka huu 2024 utakuwa mjadala wa sukari kati ya Mpina na Bashe.

Dkt. Tulia ameuliza swali la msingi sana kuhusu muda ambao viwanda vyetu vinahitaji ili viweze kuzalisha sukari kwa utoshelevu na hatimaye bei iwe sawa na nchi zilizotuzunguka

Wawekezaji wengi wanaowekeza Tanzania wamekuwa wakitumia mbinu chafu kuwanyonya wananchi kwa muda mrefu sana kwa kisingizio cha kuzalisha kwa hasara

Viwanda vya sukari vipo kwa muda mrefu sana na uzalishaji umeendelea kuwa wa kusua sua na sasa hawataki serikali ihifadhi sukari ili kudhibiti upandaji holela wa sukari. Hii ni tafsiri kuwa wao wanataka waendelee kunufaika na uhaba wa sukari nchi hii hivyo hakuna siku watataka kuongeza uzalishaji wao kwani hilo sio lengo lao. Ni lazima wabanwe ili wajitutumue

Hali hii haipo kwenye sukari pekee. Hapo nyuma tumekuwa tukisikia mambo ya Tax exemption kwa makampuni kadhaa kwa visingizio vya kutopata faida katika uwekezaji wao. Ifike mahali mambo kama haya yaishe anayeshindwa ampishe mwingine. Dunia ni ya ushindani sio ya kubembelezana

Unaweza kushuhudia makampuni kama ya simu yanavyotengeneza pesa kwenye kila angle. Lakini serikali ikipeleka tozo wanazileta kwa walaji. Haya mambo hadi lini?

Leo tumeona taarifa ya Makamba kutaka kuonana na mabalozi ambao wawekezaji wao wanalalamikia kodi za TRA. Si ajabu nao ni wababaishaji tu. Hayo tumeyaona kwenye makampuni ya madini

Namna Dkt. Tulia alivyoendesha mjadala wa sukari imetoa picha kuwa kumbe viongozi wa nchi hii wanajitoa ufahamu. Wakiamua kuisaidia nchi ipige hatua wanaweza. Siasa za vyama na uchawa ndio mchawi wa maendeleo ya nchi hii.

Atakaye ikomboa nchi hii ni atakayeweza kufuta mind set ya wanasiasa kutanguliza vyama vyao na uchawa kwa viongozi kabla ya maslahi ya nchi. Hiki ndicho kinawatafuna CCM na hatimaye wanadumaza nchi
 
Kitu kitakachokumbukwa sana kwenye bunge la bajeti mwaka huu 2024 utakuwa mjadala wa sukari kati ya Mpina na Bashe.

Dkt. Tulia ameuliza swali la msingi sana kuhusu muda ambao viwanda vyetu vinahitaji ili viweze kuzalisha sukari kwa utoshelevu na hatimaye bei iwe sawa na nchi zilizotuzunguka

Wawekezaji wengi wanaowekeza Tanzania wamekuwa wakitumia mbinu chafu kuwanyonya wananchi kwa muda mrefu sana kwa kisingizio cha kuzalisha kwa hasara

Viwanda vya sukari vipo kwa muda mrefu sana na uzalishaji umeendelea kuwa wa kusua sua na sasa hawataki serikali ihifadhi sukari ili kudhibiti upandaji holela wa sukari. Hii ni tafsiri kuwa wao wanataka waendelee kunufaika na uhaba wa sukari nchi hii hivyo hakuna siku watataka kuongeza uzalishaji wao kwani hilo sio lengo lao. Ni lazima wabanwe ili wajitutumue

Hali hii haipo kwenye sukari pekee. Hapo nyuma tumekuwa tukisikia mambo ya Tax exemption kwa makampuni kadhaa kwa visingizio vya kutopata faida katika uwekezaji wao. Ifike mahali mambo kama haya yaishe anayeshindwa ampishe mwingine. Dunia ni ya ushindani sio ya kubembelezana

Unaweza kushuhudia makampuni kama ya simu yanavyotengeneza pesa kwenye kila angle. Lakini serikali ikipeleka tozo wanazileta kwa walaji. Haya mambo hadi lini?

Leo tumeona taarifa ya Makamba kutaka kuonana na mabalozi ambao wawekezaji wao wanalalamikia kodi za TRA. Si ajabu nao ni wababaishaji tu. Hayo tumeyaona kwenye makampuni ya madini

Namna Dkt. Tulia alivyoendesha mjadala wa sukari imetoa picha kuwa kumbe viongozi wa nchi hii wanajitoa ufahamu. Wakiamua kuisaidia nchi ipige hatua wanaweza. Siasa za vyama na uchawa ndio mchawi wa maendeleo ya nchi hii.

Atakaye ikomboa nchi hii ni atakayeweza kufuta mind set ya wanasiasa kutanguliza vyama vyao na uchawa kwa viongozi kabla ya maslahi ya nchi. Hiki ndicho kinawatafuna CCM na hatimaye wanadumaza nchi

Una uelewa mdogo sana kwenye mambo haya!!

Anayesababisha bei kuwa kubwa kwa sukari na bidhaa zote Tanzania ni Serikali iliyorundika kodi nyingi. Fikiria kwenye diesel na petrol serikali imeweka tozo na kodi zinazofikia 14. Ndiyo maana mafuta Zambia kwa hela ya kwetu kwa lita ni sh 2,500 lakini kwa Tanzania ni kati ya sh 3,200 mpaka 3,500.

Viwanda Tanzania vinatozwa kodi na tozo jumla zote ni 38, nchi kama Botswana ni kodi na tozo 6 tu.

Halafu huelewi hata misamaha ya kodi ilivyokuwa ikitolewa. Haikuwa inatolewa kwa sababu mwingizaji wa bidhaa alikuwa hapati faida, bali misamaha ilikuwa kwa malighafi na mitambo ya uzalishaji. Na sababu ni wazi kuwa mitambo ya uzalishaji na malighafi hazistahili kutozwa kodi, kwa sababu kodi itatozwa kwenye bidhaa itakayozalishwa. Labda kama malighafi hiyo au hiyo mitambo inaletwa kwaajili ya kuuzwa na siyo kwaajili ya uzalishaji kwenye kiwanda au kwenye mradi.
 
Kitu kitakachokumbukwa sana kwenye bunge la bajeti mwaka huu 2024 utakuwa mjadala wa sukari kati ya Mpina na Bashe.

Dkt. Tulia ameuliza swali la msingi sana kuhusu muda ambao viwanda vyetu vinahitaji ili viweze kuzalisha sukari kwa utoshelevu na hatimaye bei iwe sawa na nchi zilizotuzunguka

Wawekezaji wengi wanaowekeza Tanzania wamekuwa wakitumia mbinu chafu kuwanyonya wananchi kwa muda mrefu sana kwa kisingizio cha kuzalisha kwa hasara

Viwanda vya sukari vipo kwa muda mrefu sana na uzalishaji umeendelea kuwa wa kusua sua na sasa hawataki serikali ihifadhi sukari ili kudhibiti upandaji holela wa sukari. Hii ni tafsiri kuwa wao wanataka waendelee kunufaika na uhaba wa sukari nchi hii hivyo hakuna siku watataka kuongeza uzalishaji wao kwani hilo sio lengo lao. Ni lazima wabanwe ili wajitutumue

Hali hii haipo kwenye sukari pekee. Hapo nyuma tumekuwa tukisikia mambo ya Tax exemption kwa makampuni kadhaa kwa visingizio vya kutopata faida katika uwekezaji wao. Ifike mahali mambo kama haya yaishe anayeshindwa ampishe mwingine. Dunia ni ya ushindani sio ya kubembelezana

Unaweza kushuhudia makampuni kama ya simu yanavyotengeneza pesa kwenye kila angle. Lakini serikali ikipeleka tozo wanazileta kwa walaji. Haya mambo hadi lini?

Leo tumeona taarifa ya Makamba kutaka kuonana na mabalozi ambao wawekezaji wao wanalalamikia kodi za TRA. Si ajabu nao ni wababaishaji tu. Hayo tumeyaona kwenye makampuni ya madini

Namna Dkt. Tulia alivyoendesha mjadala wa sukari imetoa picha kuwa kumbe viongozi wa nchi hii wanajitoa ufahamu. Wakiamua kuisaidia nchi ipige hatua wanaweza. Siasa za vyama na uchawa ndio mchawi wa maendeleo ya nchi hii.

Atakaye ikomboa nchi hii ni atakayeweza kufuta mind set ya wanasiasa kutanguliza vyama vyao na uchawa kwa viongozi kabla ya maslahi ya nchi. Hiki ndicho kinawatafuna CCM na hatimaye wanadumaza nchi
Umesahau kuwa RRRR ndiyo zinazofanya mabadiliko yote hayo.

Unazijuwa maana yake?
 
Dr Tulia kajiharibia sana kwenye sakata la Mpina, hana credibility tena kwenye jamii.

Ni mtu wa hovyo.
Si kweli, mimi naona kajipaisha kwa kuwa upande wa wanachi, badala ya yule juha mpina kuwa upande wa wapandisha bei kwa thamani ndogo.
 
Si kwewli, mimi naona kajipaisha kwa kuwa upande wa wanachi, badala ya yule juha mpina kuwa upande wa wapandisha bei kwa thamani ndogo.
Inawezekana kabisa Bashe alikuwa na majibu ya hoja zote za Mpina (he is a good debator after all.)

Kitendo cha speaker kuuzima mjadala bila ya serikali kujibu hoja. Huko ni kuuonyesha umma CCM na serikali inalea mafisadi. Hasa ukizingatia michango ya mapoyoyo waliomshambulia Mpina.

Mpina kaleta facts based on what transpired from original sources, angeachwa Bashe ajibu knowing him he is capable.

Kitendo cha kukingiwa kifua ndio kinamfanya speaker aonekane mtu wa hovyo na Bashe ni fisadi (kwa sababu ajatolea justification hoja za Mpina)

Mapoyoyo kama Kibajaji, Msukuma na wengine wa hovyo hawaku address hoja za Mpina zaidi ya kufanya personal attack na uchawa tu kwa speaker ambae kwa sasa hana credibility kwenye jamii.
 
Inawezekana kabisa Bashe alikuwa na majibu ya hoja zote za Mpina (he is a good debator after all.)

Kitendo cha speaker kuuzima mjadala bila ya serikali kujibu hoja. Huko ni kuuonyesha umma CCM na serikali inalea mafisadi. Hasa ukizingatia michango ya mapoyoyo waliomshambulia Mpina.

Mpina kaleta facts based on what transpired from original sources, angeachwa Bashe ajibu knowing him he is capable.

Kitendo cha kukingiwa kifua ndio kinamfanya speaker aonekane mtu wa hovyo na Bashe ni fisadi (kwa sababu ajatolea justification hoja za Mpina)

Mapoyoyo kama Kibajaji, Msukuma na wengine wa hovyo hawaku address hoja za Mpina zaidi ya kufanya personal attack na uchawa tu kwa speaker ambae kwa sasa hana credibility kwenye jamii.
Hjauzima mjadala, mpina kaambiwa athibitishe uongo aliousema Bashe. Matokeo unayajuwa. Badala ya kupeleka hoja kwa Spika ijadiliwe, yeye kakimbilia kuupeleka uongo wake kwa waandishi wa habari waufikishe kwa wananchi. Matokeo, kapigwa 18 -0 na Bashe, akapigwa nyundo ya kichwa na wabunge waliomuona poyoyo.

Sasa augulie maumivu, na akirudi bungeni ajuwe sasa kajigeuza pweza.
 
Hjauzima mjadala, mpina kaambiwa athibitishe uongo aliousema Bashe. Matokeo unayajuwa. Badala ya kupeleka hoja kwa Spika ijadiliwe, yeye kakimbilia kuupeleka uongo wake kwa waandishi wa habari waufikishe kwa wananchi. Matokeo, kapigwa 18 -0 na Bashe, akapigwa nyundo ya kichwa na wabunge waliomuona poyoyo.

Sasa augulie maumivu, na akirudi bungeni ajuwe sasa kajigeuza pweza.
Una namna yako ya kufikiria kiongozi.

Kwa sababu lishapita ngoja nikuache.

Mimi sipo kwa mahaba sawa ni sawa;; kosa ni kosa.
 
Hjauzima mjadala, mpina kaambiwa athibitishe uongo aliousema Bashe. Matokeo unayajuwa. Badala ya kupeleka hoja kwa Spika ijadiliwe, yeye kakimbilia kuupeleka uongo wake kwa waandishi wa habari waufikishe kwa wananchi. Matokeo, kapigwa 18 -0 na Bashe, akapigwa nyundo ya kichwa na wabunge waliomuona poyoyo.

Sasa augulie maumivu, na akirudi bungeni ajuwe sasa kajigeuza pweza.

Wewe ni poyoyo kabisa.

Bunge bandia na spika wao hawana thamani tena mbele ya Watanzania wema na wanaolipenda Taifa lao.

Kwenye kundi lile la wabunge mapoyoyo wapiga kelele, hakuna mbunge hata mmoja aliyeweza kujibu hoja za Mpina zaidi ya kupiga kelele za kusema Mpina amemdharau spika na bunge kwa kuongea na wananchi lakini hawakujadili hoja ya Mpina. Inaonekana mafisadi waliona wakazanie tu kusema amekiuka utaratibu kama njia ya kuikwepa hoja ya msingi.

Tulia anafahamika, wakati wote amesimama na kutumika na mafisadi yaliyohazana Serikalini. Hata kwenye report ya CAG ulioyojaa ufisadi, baadhi ya wabunge walipotaka ijadiliwe kama suala la dharula, alizuia hoja kujadiliwa kwa madai kuwa itajadiliwa mwezi September. Na huo muda wa ukimya mafisadi waliutumia kuwahonga wabunge walioonekana viherere. Huyu spika yupo pale kutumika na mafisadi, hakuna jema linalotegemewa kutoka kwake.

Ufisadi wa Bashe wa shilingi biliobi 36 alizozipata kupitia makubaliano na waagizaji, wa sh 100 kwa kila kilo kwenye kilo 360,000 walizoagiza, watu wanaufahamu inside out, muda ukifika, kila kitu kitawekwa wazi.

Ninyi watetezi wa mafisadi, mtambue kuwa hao watoa pesa, japo wanakuwa wametengeneza utajiri mkuu kupitia hiyo mikataba ya kifisadi, msidhani wanafurahia kutoa pesa yao na kumpa waziri ambaye hajaitolea jasho bali anaipata kwa kupitia nafasi yake. Waliomlipa ndio hao hao watoa taarifa.
 
Kitu kitakachokumbukwa sana kwenye bunge la bajeti mwaka huu 2024 utakuwa mjadala wa sukari kati ya Mpina na Bashe.

Dkt. Tulia ameuliza swali la msingi sana kuhusu muda ambao viwanda vyetu vinahitaji ili viweze kuzalisha sukari kwa utoshelevu na hatimaye bei iwe sawa na nchi zilizotuzunguka

Wawekezaji wengi wanaowekeza Tanzania wamekuwa wakitumia mbinu chafu kuwanyonya wananchi kwa muda mrefu sana kwa kisingizio cha kuzalisha kwa hasara

Viwanda vya sukari vipo kwa muda mrefu sana na uzalishaji umeendelea kuwa wa kusua sua na sasa hawataki serikali ihifadhi sukari ili kudhibiti upandaji holela wa sukari. Hii ni tafsiri kuwa wao wanataka waendelee kunufaika na uhaba wa sukari nchi hii hivyo hakuna siku watataka kuongeza uzalishaji wao kwani hilo sio lengo lao. Ni lazima wabanwe ili wajitutumue

Hali hii haipo kwenye sukari pekee. Hapo nyuma tumekuwa tukisikia mambo ya Tax exemption kwa makampuni kadhaa kwa visingizio vya kutopata faida katika uwekezaji wao. Ifike mahali mambo kama haya yaishe anayeshindwa ampishe mwingine. Dunia ni ya ushindani sio ya kubembelezana

Unaweza kushuhudia makampuni kama ya simu yanavyotengeneza pesa kwenye kila angle. Lakini serikali ikipeleka tozo wanazileta kwa walaji. Haya mambo hadi lini?

Leo tumeona taarifa ya Makamba kutaka kuonana na mabalozi ambao wawekezaji wao wanalalamikia kodi za TRA. Si ajabu nao ni wababaishaji tu. Hayo tumeyaona kwenye makampuni ya madini

Namna Dkt. Tulia alivyoendesha mjadala wa sukari imetoa picha kuwa kumbe viongozi wa nchi hii wanajitoa ufahamu. Wakiamua kuisaidia nchi ipige hatua wanaweza. Siasa za vyama na uchawa ndio mchawi wa maendeleo ya nchi hii.

Atakaye ikomboa nchi hii ni atakayeweza kufuta mind set ya wanasiasa kutanguliza vyama vyao na uchawa kwa viongozi kabla ya maslahi ya nchi. Hiki ndicho kinawatafuna CCM na hatimaye wanadumaza nchi
Shamba la bibi
 
Una uelewa mdogo sana kwenye mambo haya!!

Anayesababisha bei kuwa kubwa kwa sukari na bidhaa zote Tanzania ni Serikali iliyorundika kodi nyingi. Fikiria kwenye diesel na petrol serikali imeweka tozo na kodi zinazofikia 14. Ndiyo maana mafuta Zambia kwa hela ya kwetu kwa lita ni sh 2,500 lakini kwa Tanzania ni kati ya sh 3,200 mpaka 3,500.

Viwanda Tanzania vinatozwa kodi na tozo jumla zote ni 38, nchi kama Botswana ni kodi na tozo 6 tu.

Halafu huelewi hata misamaha ya kodi ilivyokuwa ikitolewa. Haikuwa inatolewa kwa sababu mwingizaji wa bidhaa alikuwa hapati faida, bali misamaha ilikuwa kwa malighafi na mitambo ya uzalishaji. Na sababu ni wazi kuwa mitambo ya uzalishaji na malighafi hazistahili kutozwa kodi, kwa sababu kodi itatozwa kwenye bidhaa itakayozalishwa. Labda kama malighafi hiyo au hiyo mitambo inaletwa kwaajili ya kuuzwa na siyo kwaajili ya uzalishaji kwenye kiwanda au kwenye mradi.
Kama wanatozwa kodi nyingi na nikikwazo kwa wao kukua kwanini hawafungi viwanda vyao wakaenda kuwekeza maeneo yasiyo na kodi nyingi?

Je, kuna sheria inawabana kwamba wakifunga viwanda watashitakiwa mahakamani?

Nieleweshe wewe mwenye uelewa mkubwa wa mambo haya
 
Inawezekana kabisa Bashe alikuwa na majibu ya hoja zote za Mpina (he is a good debator after all.)

Kitendo cha speaker kuuzima mjadala bila ya serikali kujibu hoja. Huko ni kuuonyesha umma CCM na serikali inalea mafisadi. Hasa ukizingatia michango ya mapoyoyo waliomshambulia Mpina.

Mpina kaleta facts based on what transpired from original sources, angeachwa Bashe ajibu knowing him he is capable.

Kitendo cha kukingiwa kifua ndio kinamfanya speaker aonekane mtu wa hovyo na Bashe ni fisadi (kwa sababu ajatolea justification hoja za Mpina)

Mapoyoyo kama Kibajaji, Msukuma na wengine wa hovyo hawaku address hoja za Mpina zaidi ya kufanya personal attack na uchawa tu kwa speaker ambae kwa sasa hana credibility kwenye jamii.
Kati ya waliokuwa hawataki kuagiza sukari ili ku control bei ya sukari (wenye viwanda) na aliyeruhusu watu wengine kuagiza kwa mpango wa dharula (Bashe) nani ni fisadi?

Ni mara ngapi hawa wenyeviwanda wamekuwa "wanatengeneza" upungufu wa sukari nchi ili kupandisha bei hadi kupelekea kulazimishwa kuitoa kwenye magodauni yao kwa mtutu wa bunduki? Hii ni sahihi?

Toka lini jambo lililokosea utaratibu (tena kwa makusudi na dharau) linaruhusiwa kujadiliwa? Mahakamani kesi inapofunguliwa ikaonekana vifungu vimekosewa hiyo kesi huwa inaamuliwaje?

Huenda kweli Mpina alikuwa na hoja, lakini hii haihalalishi kuvunja utaratibu na kudhihaki mamlaka. Hoja za kisheria zinatatuliwa kwa utaratibu. Bungeni sio kwenye social media ambapo yoyote yuko huru kusema chochote kivyovyote

Na usisahau pia kuwa hata kama hoja za Mpina ni za kweli, haiondoi ukweli kwamba katika hoja zile wenye viwanda walikuwa nyuma yake. Sasa tujiulize kama walikuwa nyuma yake kwa maslahi ya walaji au yao binafsi?

Hili la mwisho ndilo linalonifanya niwe upande wa Bashe na Spika hata kama inasemwa wamenufaika kwa uagizaji wa dharula walioufanya (kupata kamisheni) haiondoi ukweli kuwa wamesaidia kushusha bei ya sukari.
 
Wewe ni poyoyo kabisa.

Bunge bandia na spika wao hawana thamani tena mbele ya Watanzania wema na wanaolipenda Taifa lao.

Kwenye kundi lile la wabunge mapoyoyo wapiga kelele, hakuna mbunge hata mmoja aliyeweza kujibu hoja za Mpina zaidi ya kupiga kelele za kusema Mpina amemdharau spika na bunge kwa kuongea na wananchi lakini hawakujadili hoja ya Mpina. Inaonekana mafisadi waliona wakazanie tu kusema amekiuka utaratibu kama njia ya kuikwepa hoja ya msingi.

Tulia anafahamika, wakati wote amesimama na kutumika na mafisadi yaliyohazana Serikalini. Hata kwenye report ya CAG ulioyojaa ufisadi, baadhi ya wabunge walipotaka ijadiliwe kama suala la dharula, alizuia hoja kujadiliwa kwa madai kuwa itajadiliwa mwezi September. Na huo muda wa ukimya mafisadi waliutumia kuwahonga wabunge walioonekana viherere. Huyu spika yupo pale kutumika na mafisadi, hakuna jema linalotegemewa kutoka kwake.

Ufisadi wa Bashe wa shilingi biliobi 36 alizozipata kupitia makubaliano na waagizaji, wa sh 100 kwa kila kilo kwenye kilo 360,000 walizoagiza, watu wanaufahamu inside out, muda ukifika, kila kitu kitawekwa wazi.

Ninyi watetezi wa mafisadi, mtambue kuwa hao watoa pesa, japo wanakuwa wametengeneza utajiri mkuu kupitia hiyo mikataba ya kifisadi, msidhani wanafurahia kutoa pesa yao na kumpa waziri ambaye hajaitolea jasho bali anaipata kwa kupitia nafasi yake. Waliomlipa ndio hao hao watoa taarifa.
Siku bei ya sukari itakapokuwa stable na wenye viwanda kuwa na adabu ndio mtamkukumbuka Bashe alikuwa anapigania nini
 
Kati ya waliokuwa hawataki kuagiza sukari ili ku control bei ya sukari (wenye viwanda) na aliyeruhusu watu wengine kuagiza kwa mpango wa dharula (Bashe) nani ni fisadi?

Ni mara ngapi hawa wenyeviwanda wamekuwa "wanatengeneza" upungufu wa sukari nchi ili kupandisha bei hadi kupelekea kulazimishwa kuitoa kwenye magodauni yao kwa mtutu wa bunduki? Hii ni sahihi?

Toka lini jambo lililokosea utaratibu (tena kwa makusudi na dharau) linaruhusiwa kujadiliwa? Mahakamani kesi inapofunguliwa ikaonekana vifungu vimekosewa hiyo kesi huwa inaamuliwaje?

Huenda kweli Mpina alikuwa na hoja, lakini hii haihalalishi kuvunja utaratibu na kudhihaki mamlaka. Hoja za kisheria zinatatuliwa kwa utaratibu. Bungeni sio kwenye social media ambapo yoyote yuko huru kusema chochote kivyovyote

Na usisahau pia kuwa hata kama hoja za Mpina ni za kweli, haiondoi ukweli kwamba katika hoja zile wenye viwanda walikuwa nyuma yake. Sasa tujiulize kama walikuwa nyuma yake kwa maslahi ya walaji au yao binafsi?

Hili la mwisho ndilo linalonifanya niwe upande wa Bashe na Spika hata kama inasemwa wamenufaika kwa uagizaji wa dharula walioufanya (kupata kamisheni) haiondoi ukweli kuwa wamesaidia kushusha bei ya sukari.
Kiongozi

Ukisoma ulichoandika wewe ndio lawyer, judge and jury na kuhitimisha unavyotaka.

Hipo hivi

Priority ya nchi kwenye nchi uzalishaji wa sukari na upatikanaji wake ni jukumu la wazalishaji wa ndani.

Given their production capacity na mahitaji ya nchi kuna shortage of supply.

To fill the shortage gap nchi lazima iagizre.

By law ilikuwa wanaotakiwa kupewa vibali vya kuagiza ni wazalishaji wa sukari.

Wenye jukumu la kuhakikisha nchi aikosi sukari (ni body ya sukari) hiyo mission inataka kujua current production frontier (possibilities) na amount of buffer stock needed.

Body ya sukari pia ni responsible kufanya risk assessment na kuwa na mitigation staretegy.

Sasa kama utamsikiliza Mpina given the situation ndio utaona msingi wa hoja yake.

Ili nielezee kwa kina kama yeye, inabidi nilale niamke. Mtu sahihi wa kumjibu ilikuwa Bashe; kiherere cha spika kimefanya serikali iwe ye hovyo.

Good morning
 
Back
Top Bottom