Wasiwasi wangu juu ya mradi wa Maabara ya akili bandia iliyozinduliwa UDOM

Je, haya mambo ya robotics hayatamaliza kabisa Ajira hata hizi chache zilizopo
Maan kama kitu kitaweza kufanya kazi kama binadamu maanake sasa kazi nyingi zitafanywa na robot
Au hii imekaaje wadau.
Behind the Robot Kuna Team Kubwa sana ya Operation, Ili huyo Robot aweze kufanya kazi, NI kama IT ilivyoingia tu, STill Kuna Watu wa Database, Application, Security, Bussiness Application hizo zote ni team tu Kubwa sana; So hata kama kutakuwa na Upungufu sio kwa kiwango kama ambavyo wengi wetu wanafikiri.
 
Hivi kuna graduate anawaza tena kuajiriwa baada ya Chuo? Labda kidogo waliosoma fani za Udaktari, Famasia, Nesi na ambazo ni very rare profession. Wengine mliobaki waza kujiajiri hata kwa biashara ya mtaji mdogo tu. Ukiwaza kuajiriwa na ukiikuta hali halisi miaka inasonga unatembeza CV na usaili wa watu 10,000 ndipo utaomba mama yako akumeze ili ubukie tumboni usizaliwe tena. Yaani narudia hakuna KAZI za kuajiriwa tena. The labour market is saturated.
 
Aaah asante sana kwa kunitoa wasiwasi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kwel mkuu lakin zana ya kujiajiri me nadhan inafaa kama umesoma IT basi jiajiri humo humo kwenye It lakin sio umesoma IT afu ufuge kuku hapo useme umejiajiri nakutokan na hilo ndo maan wasomi weng husubiri ajira tu za fani yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu temporarily unafuga kuku immediate ukimaliza Tu Chuo. Ukianza na kuku 200 wa chotara kununua ni 300,000 unalisha miezi 5-6 wanataga au wakifikisha miezi 4 unauza mmoja 10,000. Ukiondoa say vifo 10 then Una kuku 190×10,000= 1,900,000 ukiondoka na matumizi mengine then hukosi Faida 600,000 mpaka 1m. Ukifuga round 3 unapata mtaji unanunua vifaa vyako IT unasonga na unaweza pia ukaendekea na ufugaji taratibu mpaka upate mtaji wa kutosha . Hivyo hata Madaktari ukisubiri Ajira fuga au do a simple business. Ime work kwa watu ninaowafahamu.
 
Asante hapa nimekuelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
every thing has calculated all over the world
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…