Uchaguzi 2020 Wasiwasi wangu ni hili 'Jeshi la akiba' muda huu wa kampeni

Uchaguzi 2020 Wasiwasi wangu ni hili 'Jeshi la akiba' muda huu wa kampeni

onjwayo

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2020
Posts
1,356
Reaction score
1,309
Tumeibiwa kuku, ng'ombe, mbuzi na kukwapuliwa simu hatujawahi kusikia wala kuona nguvu za jeshi la akiba. Kimsingi hawa sijui walikuwa wanaitwa Sungusungu au Mgambo lakini kwa nature ya kazi yao ilikuwa kupambana na uhalifu mdogo mdogo vijijini. Kwenye kampeni ziazoendelea jana wameibuka Shinyanga.

Swali la kujiuliza hivi polisi na jeshi la wanachi wamezidiwa hadi kuletwa jeshi la akiba. Tuko vitani na nani hadi sasa kuletwa jeshi lingine? Je, hii si mbinu ya kutengeneza makundi ya kijeshi ili kudhibiti upinzani na kuwatia watu hofu?

Hivi CCM kwanini wanataka kutuingiza katika sintofahamu? Mbona vyama vingine wao wamejikita kunadi sera na wao wanahaha kutafuta majeshi? Hofu ya CCM ni nini hasa?

Wito wangu ule msemo wa kufanya kampeni za kistaarabu kusiwe ni kupaka upepo matope bali uwe kwa vitendo. CCM wakinukisha hAta watoto wao nao watanukishiwa tu.

Janjajanja ndio maana Lissu na Membe wanakubalika.
 
Jeshi la akiba
IMG_20200903_045252.jpg
IMG_20200903_045307.jpg
 
Vyombo hivi vipo miaka yote tena kisheria vikisimamiwa na jeshi la polisi maarufu kama Sungusungu au kwa Dar vinajulikana kama Ulinzi Shirikishi. Jeshi la Polisi kwa uchache wa askari haliwezi kuwa sehemu zote, hawa ni msaada mkubwa. Mfano ni wakati huu wa kampeni, Priority ya Polisi ni kulinda misafara na mikutano ya Magufuli ambaye mbali na ugombea yeye bado ni Rais
 
Kampeni za kistaarabu ni kwa ajili ya upinzani nadhani ni maelekezo ya viongozi wa dini na tume maana mpaka sasa hawajakemea chochote kuhusu kuingiza majeshi kwenye mikutano ya kampeni
 
Vyombo hivi vipo miaka yote tena kisheria vikisimamiwa na jeshi la polisi maarufu kama Sungusungu au kwa Dar vinajulikana kama Ulinzi Shirikishi. Jeshi la Polisi kwa uchache wa askari haliwezi kuwa sehemu zote, hawa ni msaada mkubwa. Mfano ni wakati huu wa kampeni, Priority ya Polisi ni kulinda misafara na mikutano ya Magufuli ambaye mbali na ugombea yeye bado ni Rais

Kama ni hivo kwa nini wasiitwe kwa jina lao sungusungu?
 
Kama ni hivo kwa nini wasiitwe kwa jina lao sungusungu?
Hoja sio majina, kila eneo wanatohoa majina yao, Dar ni Ulinzi shirikishi. Hoja ni mgombea Urais asiyejua mifumo ya ulinzi wa nchi uliopo kisheria😬
 
Mimi mtazamo wangu ni kuwa either majeshi ya mjibu wa sheria yameonyesha kuwa yanaweza pindua Meza kwenye kura mana upinzani unasera znazogusa jamii kwa mapana yake ikiwemo majeshi yenyewe !!!
Pili huenda hicho kikundi japo kuwa halijawahi sikika ni mbadala wa police!
Tatu huenda ni Jeshi la Chama fulani..rangi ya jezi zao ni danganya toto ila mfadhir ni Chama fulani.
Note:
Kwa level ya Lisu msje mkafikilia kuwa amepga porojo..ila atakuwa amepata taarfa rasm kutoka vianzo rasmi ndy mana ameamua kuongelea hadharani.
Lakini tujiulize je Police wameshindwa kazi yao mpaka waletewe vikundi hivi?mbona miaka mingine hutajawahi kuona?

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Chadema wanajua kweli kufukuza wapiga kura. Kwani asingewasema akaomba kura zao na za familia zao angekuwa kapungukiwa nini?

Chadema Huyo Lisu wenu hashauriki anafukuza wapiga kura. HIVI kwa jinsi alivyowadharau unategemea wao na familia zao watampa kura? Kaenda shinyanga kufukuza wapiga kura au kuomba kura? Chadema Huyo mtu wenu kichwani hayuko sawa
 
Ni tabia yakutaka kuonyesha wana misimamo, misimamo isiyo na mashiko. Unadhani walipowafukuza TBC Mbagala hawakujua kuna sheria ya Maudhui inayobana vyombo vyahabari kurusha maudhui yanayoashiria uchochezi na kuvunja amani?. Lossu anajua kuna People's Militia Act na imeorodheshwa hadi vikundi vya jadi.

Tona mkoa wa shinyanga vinafanya kazi nzuri sana kusaidiana na Polisi. Amefukuza watu ambao kesho wangejivunia kwa kuweka historia ya kushiriki ulinzi wa mikutano ya Rais. Amewadharirisha na kupoteza kura.
 
Ni tabia yakutaka kuonyesha wana misimamo, misimamo isiyo na mashiko. Unadhani walipowafukuza TBC Mbagala hawakujua kuna sheria ya Maudhui inayobana vyombo vyahabari kurusha maudhui yanayoashiria uchochezi na kuvunja amani?. Lossu anajua kuna People's Militia Act na imeorodheshwa hadi vikundi vya jadi. Tona mkoa wa shinyanga vinafanya kazi nzuri sana kusaidiana na Polisi. Amefukuza watu ambao kesho wangejivunia kwa kuweka historia ya kushiriki ulinzi wa mikutano ya Rais. Amewadharirisha na kupoteza kura.
Sheria ipo ndy..lakini ni sheria kandamizi inaskitisha vyombo vinavyoendeshwa kwa kodi za wananchi tena wanyonge vinageuka kutotumikia wanyonge!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Sheria ipo ndy..lakini ni sheria kandamizi inaskitisha vyombo vinavyoendeshwa kwa kodi za wananchi tena wanyonge vinageuka kutotumikia wanyonge!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
Mgombea wenu hajui kama kuna sheria ya People's militia, hata hivyo kusaidia ulinzi wa mkutano wako ni kukandamiza wanyonge? Wakiwepo Polisi mkutanoni anawatukana ati wanatumika, wamemletea vijana wa jeshi la akiba wasio na silaha wawasaidie nao anawafukuza
 
Hoja sio majina, kila eneo wanatohoa majina yao, Dar ni Ulinzi shirikishi. Hoja ni mgombea Urais asiyejua mifumo ya ulinzi wa nchi uliopo kisheria[emoji51]

Ok shinyanga wametohoa jina gani?
 
Back
Top Bottom