Uchaguzi 2020 Wasiwasi wangu ni hili 'Jeshi la akiba' muda huu wa kampeni

Uchaguzi 2020 Wasiwasi wangu ni hili 'Jeshi la akiba' muda huu wa kampeni

Hoja sio majina, kila eneo wanatohoa majina yao, Dar ni Ulinzi shirikishi. Hoja ni mgombea Urais asiyejua mifumo ya ulinzi wa nchi uliopo kisheria😬
Jeshi la M23 ya magu. Hapo hakuna jeshi la akiba. Hapo ukifanya upembuzi utakuta kumechanganyika na magwiji wenye mafunzo makali kabjsa ya kijeshi. Anatupiga changa la macho. Tumemshtukia. Intelijensia ya chadema ni kali sana.
 
Soma Katiba. Sura ya uanzishwaji wa majeshi ya ulinzi na usalama

Mkuu kama mayai yanapanda soma mchango wa Chief Kabikula #38 hapo utatoa tongotongo au kama nawe unayo nyingine weka hapa tuijadili
 
Tumeibiwa kuku, ng'ombe, mbuzi na kukwapuliwa simu hatujawahi kusikia wala kuona nguvu za jeshi la akiba. Kimsingi hawa sijui walikuwa wanaitwa Sungusungu au Mgambo lakini kwa nature ya kazi yao ilikuwa kupambana na uhalifu mdogo mdogo vijijini. Kwenye kampeni ziazoendelea jana wameibuka Shinyanga.

Swali la kujiuliza hivi polisi na jeshi la wanachi wamezidiwa hadi kuletwa jeshi la akiba. Tuko vitani na nani hadi sasa kuletwa jeshi lingine? Je, hii si mbinu ya kutengeneza makundi ya kijeshi ili kudhibiti upinzani na kuwatia watu hofu?

Hivi CCM kwanini wanataka kutuingiza katika sintofahamu? Mbona vyama vingine wao wamejikita kunadi sera na wao wanahaha kutafuta majeshi? Hofu ya CCM ni nini hasa?

Wito wangu ule msemo wa kufanya kampeni za kistaarabu kusiwe ni kupaka upepo matope bali uwe kwa vitendo. CCM wakinukisha hAta watoto wao nao watanukishiwa tu.

Janjajanja ndio maana Lissu na Membe wanakubalika.
Leteni tu vurugu tuwanyooshe
 
Vyombo hivi vipo miaka yote tena kisheria vikisimamiwa na jeshi la polisi maarufu kama Sungusungu au kwa Dar vinajulikana kama Ulinzi Shirikishi. Jeshi la Polisi kwa uchache wa askari haliwezi kuwa sehemu zote, hawa ni msaada mkubwa. Mfano ni wakati huu wa kampeni, Priority ya Polisi ni kulinda misafara na mikutano ya Magufuli ambaye mbali na ugombea yeye bado ni Rais
Sungusungu/ulinzi shirikishi "mnajioganizi"wenyewe kwenye mtaa wenu au kijiji na gharama mnazibeba wenyewe.Mgambo wameenda wapi?
 
Unajitah
Mkuu hiki Ni kikundi kilichoanzishwa na mbunge wa chadema Rachel Mashishanga kwa ajili ya kulinda usalama kwenye shughuli za chadema, Salome Makamba alivyoingia alikitelekeza, ndio kikaanza kufanyakazi huru, kimsingi Ni Mali ya chadema,
Unajitahidi kuwatetea Intarahamwe?Kama ni kikosi kilichoundwa na huyo MwanaCHADEMA uliyemtaja,ni sawa yeye kufanya hivyo?Sheria za nchi hii zinafanyaje kazi?Kila makosa yanayofanywa na watawala yakihojiwa mnayahusisha na wapinzani.Je,ndio wanaounda serikali inayohitajika kutupa ukweli wa yale tunayoulizia?
Hivyo vikosi vya Jeshi la Akiba ni haramu hata kama vimeundwa/kutumika na nani hapa nchini.Hawapo kisheria na tunapoulizia uwepo wao tupo sahihi na tunastahili kufahamishwa.Nimewaona wengine kwenye Canter nyeupe yenye Plate No.ya PT,yawezekana ni shopped photo?
 
Sungusungu/ulinzi shirikishi "mnajioganizi"wenyewe kwenye mtaa wenu au kijiji na gharama mnazibeba wenyewe.Mgambo wameenda wapi?
Hoja ni wapo kwa sheria? Rais ajaye alikuwa Ubelgiji hajui hilo. Waalipwa na nani sio hoja!! Kwani hao mgambo huwa wanalipwa na nani? Au vijana wanaojitolea wakirudi nyumbani wanalipwa na nani? Ndiyo maana ya Jeshi la Akiba.
 
Unajitah

Unajitahidi kuwatetea Intarahamwe?Kama ni kikosi kilichoundwa na huyo MwanaCHADEMA uliyemtaja,ni sawa yeye kufanya hivyo?Sheria za nchi hii zinafanyaje kazi?Kila makosa yanayofanywa na watawala yakihojiwa mnayahusisha na wapinzani.Je,ndio wanaounda serikali inayohitajika kutupa ukweli wa yale tunayoulizia?
Hivyo vikosi vya Jeshi la Akiba ni haramu hata kama vimeundwa/kutumika na nani hapa nchini.Hawapo kisheria na tunapoulizia uwepo wao tupo sahihi na tunastahili kufahamishwa.Nimewaona wengine kwenye Canter nyeupe yenye Plate No.ya PT,yawezekana ni shopped photo?
Red brigade iliasisiwa na mbowe na ndio hao wanamlinda yeye, mbona hahoji wanaomlinda Ni kea Sheria ipi?
 
Jeshi la M23 ya magu. Hapo hakuna jeshi la akiba. Hapo ukifanya upembuzi utakuta kumechanganyika na magwiji wenye mafunzo makali kabjsa ya kijeshi. Anatupiga changa la macho. Tumemshtukia. Intelijensia ya chadema ni kali sana.

Ukiwaza hivyo, hata Jeshi la JKT, JKU na Mgambo livunjwe maana wanafunzwa vikali ikiwemo matumizi ya silaha za Kivita na tunao mtaani. Kila nchi ina namna yake ya kudhibiti uhalifu. Kwa sera yetu ya ulinzi, Tanzania kila raia ni mlinzi wa nchi ndiyo maana kuna AMANI. Waliozaliwa 90's hawajui hili.
 
Hawa ni vijana wa ccm waliokuwa wamewekwa kambini mwaka jana na mwaka huu...karibia kila wilaya Tanzania imetoa vijana wake kujiunga na mafunzo ya ukakamavu na medani za vita
Hilo ni kundi kubwa na hatari kabisa na halipaswi kupuuzwa hata siku moja...wamefanyiwa brainwash ya kutosha sana kuhusu upinzani

Kulikuwa na ratiba na bajeti maalum kwa ajili ya hayo makundi na walipelekwa kwenye makambi ya siri kwa wiki tatu tatu ...mwezu na nk
Bajeti ilijumuisha
Malipo kwa ajili ya wakufunzi
Chakula
Malazi
Mavazi
Vinywaji
Posho nknk
Vyanzo vya mapato vilikuwa toka kwa wafanyabiashara na wenye viwanda vikubwa na vya kati...hawa walipelekewa barua za kuomba michango ya hali na mali pamoja na bajeti....chochote kilipokelewa na michango iliratibiwa na makada wa ccm toka makao...
Hao vijana ni kundi kubwa na wameiva hasa...kuna hao wenye uniform lakini nyuma yao wana backup ya wasio na uniform na wamefunzwa kuwasiliana kwa lugha ishara na wanatambuana kwa ishara na kila mmoja ana code number yake....

USINIULIZE NIMEJUAJE[emoji848][emoji2827][emoji848][emoji2827][emoji848][emoji2827][emoji848][emoji2827]
Hatari inainyemelea nchi yetu huku tunazuiwa hata kuhoji hali hiyo.Akijitokeza mtu wa kulizia hilo ataitwa CDM/Mpinzani.
 
Hakuna cha jeshi la akiba wala nini hao ni wahalifu wa "green guards" wapo kazini.

Hamna kitu hapo, huu ni uhuni mwengine wa ccm ktk sura hii.

Hao vijana wanatumika kwa namna ambayo wao hawajielewi... Ni sawa na wale wahuni waliotumwa kutupa mawe ktk mkutano wa TL...

Ni hatari kuwa na vikundi au majeshi yasiyo rasmi Kama hayo..
 
Tumeibiwa kuku, ng'ombe, mbuzi na kukwapuliwa simu hatujawahi kusikia wala kuona nguvu za jeshi la akiba. Kimsingi hawa sijui walikuwa wanaitwa Sungusungu au Mgambo lakini kwa nature ya kazi yao ilikuwa kupambana na uhalifu mdogo mdogo vijijini. Kwenye kampeni ziazoendelea jana wameibuka Shinyanga.

Swali la kujiuliza hivi polisi na jeshi la wanachi wamezidiwa hadi kuletwa jeshi la akiba. Tuko vitani na nani hadi sasa kuletwa jeshi lingine? Je, hii si mbinu ya kutengeneza makundi ya kijeshi ili kudhibiti upinzani na kuwatia watu hofu?

Hivi CCM kwanini wanataka kutuingiza katika sintofahamu? Mbona vyama vingine wao wamejikita kunadi sera na wao wanahaha kutafuta majeshi? Hofu ya CCM ni nini hasa?

Wito wangu ule msemo wa kufanya kampeni za kistaarabu kusiwe ni kupaka upepo matope bali uwe kwa vitendo. CCM wakinukisha hAta watoto wao nao watanukishiwa tu.

Janjajanja ndio maana Lissu na Membe wanakubalika.
Kwa hiyo chadema wanaogopa mgambo kuliko jeshi la police,
Pia wao hawaruhusiwi kusikiliza mkutano?
 
Hao vijana wanatumika kwa namna ambayo wao hawajielewi... Ni sawa na wale wahuni waliotumwa kutupa mawe ktk mkutano wa TL...

Ni hatari kuwa na vikundi au majeshi yasiyo rasmi Kama hayo..
Naam, CCM inawatumia kiutapeli. Zoezi la kukusanya hao vijana lilianza zaidi ya mwezi mmoja ulio pita. Wajumbe wa serekali za mitaa ndo wanaotumika kuwatafuta. Wanawaambia wazazi / walezi kuwa wanapelekwa jeshini, na vigezo ni umri wa miaka 18 na lazima wapewe kadi za ccm.
Huko Magu jamaangu kanambia zoezi hilo limehitimishwa juzi. Inshort ni mwendelezo wa utapeli wa ccm.
 
Tumeibiwa kuku, ng'ombe, mbuzi na kukwapuliwa simu hatujawahi kusikia wala kuona nguvu za jeshi la akiba. Kimsingi hawa sijui walikuwa wanaitwa Sungusungu au Mgambo lakini kwa nature ya kazi yao ilikuwa kupambana na uhalifu mdogo mdogo vijijini. Kwenye kampeni ziazoendelea jana wameibuka Shinyanga.

Swali la kujiuliza hivi polisi na jeshi la wanachi wamezidiwa hadi kuletwa jeshi la akiba. Tuko vitani na nani hadi sasa kuletwa jeshi lingine? Je, hii si mbinu ya kutengeneza makundi ya kijeshi ili kudhibiti upinzani na kuwatia watu hofu?

Hivi CCM kwanini wanataka kutuingiza katika sintofahamu? Mbona vyama vingine wao wamejikita kunadi sera na wao wanahaha kutafuta majeshi? Hofu ya CCM ni nini hasa?

Wito wangu ule msemo wa kufanya kampeni za kistaarabu kusiwe ni kupaka upepo matope bali uwe kwa vitendo. CCM wakinukisha hAta watoto wao nao watanukishiwa tu.

Janjajanja ndio maana Lissu na Membe wanakubalika.
Unazungumzia jeshi gani la wananchi inaonekana hata hajui mipaka ya majeshi yetu.
 
Hata mkitangaza kuongeza mishahara wakati wowote kuanzia sasa pasipo Bunge kupitisha,tutawapiga chini tu.
Maoni ya mdau wa jf
 
Mkuu kama mayai yanapanda soma mchango wa Chief Kabikula #38 hapo utatoa tongotongo au kama nawe unayo nyingine weka hapa tuijadili

Kimsingi, post #38 mchangiaji amenukuu National Defense Act ambayo inanazungumzia mamlaka ya Amiri Jeshi Mkuu katika kuanzisha majeshi wakati wa Vita.

Katiba katika Sura ya Unzishaji wa Majeshi, inazungumzia kwa ujumla mamlaka ya aliyopewa Amiri Jeshi Mkuu kuanzisha na kuunda majeshi.

Kwa hiyo, ukizingatia tafsiri ya National Defense Act kwamba Amiri Jeshi Mkuu ana mamlaka ya kuunda Jeshi wakati wa Vita pekee unakuwa unakiuka Katiba ya nchi na unapotosha.

Katiba haijasema kwamba Amiri Jeshi Mkuu ana mamlaka ya kuunda majeshi wakati wa Vita pekee, bali inasema Amiri Jeshi Mkuu ana mamlaka ya kuunda vikosi vya majeshi.
 
Back
Top Bottom