Wasomi elimu isiwapumbaze mnapishana na fursa nyingi

Wasomi elimu isiwapumbaze mnapishana na fursa nyingi

Vien

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2020
Posts
6,585
Reaction score
10,363
Happy Easter to everyone,

Nimeguswa ku share haya machache kuhusu hili kundi kubwa la watu (Wasomi) ambalo ndo linaongoza kulalamika huku mitandaoni kuwa maisha magumu na wengine wakienda mbali zaidi kuwa serikali yetu haiwajali.

Nimefuatilia kwa ukaribu wasomi wengi, kitu kinachowakwamisha ni wao wenyewe kujiona wao ni tofauti na watu wengine kwenye jamii na wanastahili kupewa heshima kubwa.

Huu mtazamo wenu wasomi ndo unawafanya mnapishana na fursa nyingi kwakua lazima tukubali hakuna serikali duniani iliyoweza kuwaajiri watu wake wote , hivyo basi ukiwa kama msomi na umekosa ajira cha kwanza kabisa kubali kujishusha kuendana na mazingira halisi ya mtaani.

Elimu uliyo nayo isikufanye uzubae tuu jichanganye na watu wa mtaani walioanza ujasiriamali hata kama wanafanya kwa kiwango cha chini, kupitia kujichanganya kwako kutakuongezea maarifa ambayo huna.

Elimu uliyo nayo isikufanye kujiona kuwa wewe ni mtu wa hadhi ya juu, huku huna source yoyote ya kukuingizia kipato. Kama huna means yoyote ya kuingiza kipato basi ujue kuna vingi sana huvijui unapaswa ujifunze.

Elimu uliyo nayo itakusaidia tuu endapo utakubali kubadilika kutokana na mazingira lakini pia kukubali uhalisia wa mambo coz huku mtaani mambo ni tofauti sana na vile wasomi wanavyochukulia pindi wakiwa vyuoni.

Elimu ulionayo ukiongeza na maarifa kidogo tuu utakayoyapata pindi ukijichanganya na watu mtaani itakua na faida sana, kuliko kusubiri ajira.

Elimu uliyo nayo bila kuwa na pesa tambua fika hakuna atakayekupa heshima kama wengi wenu mlivo na mawazo hayo ya kijinga.

Kushinda mitandaoni na kulalamika kuwa ajira ngumu tuu bila kuchukua hatua zozote ni ujinga ambapo ni wa kuacha mara moja.

Tunawategemea sana kuja kuleta ukombozi mtaani kutokana na elimu mlioipata, ila hii hali ya kulaumu tuu serikali inatupa sana mashaka kuwa kuna uwezekano tuna wasomi ambao hawajaelimika.
 
Binafsi naona kama kwa mbaaali akili zishawakaa, wengi sikuhizi washajua hakuna ajira, shida ipo tu kwenye kukubali huo ukweli...

BTW Msomi ni yupi? Maana naona kila yule anamuita mwenzake aliyejuu msomi..
Katika muktadha WAKO msomi ni yeyote aliyesoma anayetarajia elimu yake impe ajira..

Kesho mwingne atakuja na lake, atakuja kivyakee....
Wanaandamwa sana, kila uzi wasomi...wasomiii..

Lakini leo hii ajitokeze mmoja tuu hapa Aandike uzi ajiite msomi lets say wa Degree level, uone atakavyoandamwa, mara ooo
Degree yako moja unajiita msomi...
Wenye PHD wajiiteje..?
Tanzania kuna msomi....?
Wasomi hawaandiki hivyo...
Wasomi hawana mawazo hayo..

Hata kama ana kazi/bishara/ajira yake na maisha yakujimudu, atasimangwa kwa nini? kwa kujiita msomi,
Kumbe neno msomi lina sound pale linapobeba picha mbaya tuu..

Kumuita mtu msomi na amefanikiwa hio ni moja ya dhambi moja kubwa kwa mbumbu mmoja hawezi kuibeba

Kutokua na elimu sio sifa pia tukumbuke.
 
Happy Easter to everyone,

Nimeguswa ku share haya machache kuhusu hili kundi kubwa la watu (Wasomi) ambalo ndo linaongoza kulalamika huku mitandaoni kuwa maisha magumu na wengine wakienda mbali zaidi kuwa serikali yetu haiwajali

Nimefuatilia kwa ukaribu wasomi wengi , kitu kinachowakwamishwa ni wao wenyewe kujiona wao ni tofauti na watu wengine kwenye jamii na wanastahili kupewa heshima kubwa

Huu mtazamo wenu wasomi ndo unawafanya mnapishana na fursa nyingi kwakua lazima tukubali hakuna serikali duniani iliyoweza kuwaajiri watu wake wote , hivyo basi ukiwa kama msomi na umekosa ajira cha kwanza kabisa kubali kujishusha kuendana na mazingira halisi ya mtaani

Elimu uliyo nayo isikufanye uzubae tuu jichanganye na watu wa mtaani walioanza ujasiriamali hata kama wanafanya kwa kiwango cha chini , kupitia kujichanganya kwako kutakuongezea maarifa ambayo huna.

Elimu uliyo nayo isikufanye kujiona kuwa wewe ni mtu wa hadhi ya juu , huku huna source yoyote ya kukuingizia kipato. Kama huna means yoyote ya kuingiza kipato basi ujue kuna vingi sana huvijui unapaswa ujifunze

Elimu uliyo nayo itakusaidia tuu endapo utakubali kubadilika kutokana na mazingira lakini pia kukubali uhalisia wa mambo coz huku mtaani mambo ni tofauti sana na vile wasomi wanavyochukulia pindi wakiwa vyuoni..

Elimu ulionayo ukiongeza na maarifa kidogo tuu utakayoyapata pindi ukijichanganya na watu mtaani itakua na faida sana , kuliko kusubiri ajira

Elimu uliyo nayo bila kuwa na pesa tambua fika hakuna atakayekupa heshima kama wengi wenu mlivo na mawazo hayo ya kijinga.

Kushinda mitandaoni na kulalamika kuwa ajira ngumu tuu bila kuchukua hatua zozote ni ujinga ambapo ni wa kuacha mara moja

Tunawategemea sana kuja kuleta ukombozi mtaani kutokana na elimu mlioipata...ila hii hali ya kulaumu tuu serikali inatupa sana mashaka kuwa kuna uwezekano tuna wasomi ambao hawajaelimika
Udhaifu mkubwa wa sera ya Chama Cha Mapinduzi.

Yaani kule ulaya Kila mwezi wanatunza data za Unemployment rates na kupush vijana kwa kuwapa back-up inayoweza wasaidia eidha wajiendeleze au waishi wakisubiri ajira zingine.

Ila kwetu hakuna data za Unemployment rates za Kila mwezi, hatujui watu unemployed wako wangapi watengeneze sera za kuwaalika foreign investors wajenge viwanda vya kuwaajiri vijana, Leo hii kijana anatoka na 4.5 GPA tena honourable anakaa mtaani na ideas zake murua alizopambania miaka yote zikipotea bila matumizi yoyote alafu Serikali inashinda inanunua ma-V8 na kutengeneza miradi ambayo ndani yake kuna upigaji wa ajabu yalioanikwa na CAG, si Bora hizo pesa wawape vijana ambao hawaajajiliwa ila wanareport taarifa zao pale National Bureau of Statistics huku wakiendelea kusaka ajira zingine.

Hii kitu Cha "Kujiajiri isiwe ndo hoja ambayo Serikali inaitumia kupoteza vijana kufikia ndoto zao".
Imagine mtu anatoka chuo, anadaiwa almost 10 million na HESLB, Hana ajira, kaamua kujiajiri, bado hajakutana na wale wa TRA pasua kichwa, Kuna wengine wanatoka chuo hawana kitu, walikuwa wanalisha familia zao masikini, je mtawapa mtaji?

Mikopo hii ya Samia imejaa nepotism na corruption, kama wewe huna mtu wa CCM kama connection, hupati utapoteza muda sana.

SERIKALI IKAE CHINI NA KUANZA KUKUSANYA DATA WAONE UNEMPLOYED WANGAPI WAWEZE KULITATUA TATIZO, EIDHA WAPUNGUZE MAKODI YA AJABU WAWARUHUSU FOREIGN INVESTORS WAJE.
 
Udhaifu mkubwa wa sera ya Chama Cha Mapinduzi.
Yaani kule ulaya Kila mwezi wanatunza data za Unemployment rates na kupush vijana kwa kuwapa back-up inayoweza LOYED WANGAPI WAWEZE KULITATUA TATIZO, EIDHA WAPUNGUZE MAKODI YA AJABU WAWARUHUSU FOREIGN INVESTORS WAJE.
Thank you mkuu, Umechanganua vyema. kwa namna moja au nyingine uko sahihi pia
 
Back
Top Bottom