Wasomi elimu isiwapumbaze mnapishana na fursa nyingi

Wasomi elimu isiwapumbaze mnapishana na fursa nyingi

Udhaifu mkubwa wa sera ya Chama Cha Mapinduzi.
Yaani kule ulaya Kila mwezi wanatunza data za Unemployment rates na kupush vijana kwa kuwapa back-up inayoweza wasaidia eidha wajiendeleze au waishi wakisubiri ajira zingine.
Ila kwetu hakuna data za Unemployment rates za Kila mwezi, hatujui watu unemployed wako wangapi watengeneze sera za kuwaalika foreign investors wajenge viwanda vya kuwaajiri vijana, Leo hii kijana anatoka na 4.5 GPA tena honourable anakaa mtaani na ideas zake murua alizopambania miaka yote zikipotea bila matumizi yoyote alafu Serikali inashinda inanunua ma-V8 na kutengeneza miradi ambayo ndani yake kuna upigaji wa ajabu yalioanikwa na CAG, si Bora hizo pesa wawape vijana ambao hawaajajiliwa ila wanareport taarifa zao pale National Bureau of Statistics huku wakiendelea kusaka ajira zingine.
Hii kitu Cha "Kujiajiri isiwe ndo hoja ambayo Serikali inaitumia kupoteza vijana kufikia ndoto zao".
Imagine mtu anatoka chuo, anadaiwa almost 10 million na HESLB, Hana ajira, kaamua kujiajiri, bado hajakutana na wale wa TRA pasua kichwa, Kuna wengine wanatoka chuo hawana kitu, walikuwa wanalisha familia zao masikini, je mtawapa mtaji?
Mikopo hii ya Samia imejaa nepotism na corruption, kama wewe huna mtu wa CCM kama connection, hupati utapoteza muda sana.
SERIKALI IKAE CHINI NA KUANZA KUKUSANYA DATA WAONE UNEMPLOYED WANGAPI WAWEZE KULITATUA TATIZO, EIDHA WAPUNGUZE MAKODI YA AJABU WAWARUHUSU FOREIGN INVESTORS WAJE.
Kweli mkuu , inaumiza sana ajira za kupigiana magoti .
 
Happy Easter to everyone,

Nimeguswa ku share haya machache kuhusu hili kundi kubwa la watu (Wasomi) ambalo ndo linaongoza kulalamika huku mitandaoni kuwa maisha magumu na wengine wakienda mbali zaidi kuwa serikali yetu haiwajali

Nimefuatilia kwa ukaribu wasomi wengi , kitu kinachowakwamishwa ni wao wenyewe kujiona wao ni tofauti na watu wengine kwenye jamii na wanastahili kupewa heshima kubwa

Huu mtazamo wenu wasomi ndo unawafanya mnapishana na fursa nyingi kwakua lazima tukubali hakuna serikali duniani iliyoweza kuwaajiri watu wake wote , hivyo basi ukiwa kama msomi na umekosa ajira cha kwanza kabisa kubali kujishusha kuendana na mazingira halisi ya mtaani

Elimu uliyo nayo isikufanye uzubae tuu jichanganye na watu wa mtaani walioanza ujasiriamali hata kama wanafanya kwa kiwango cha chini , kupitia kujichanganya kwako kutakuongezea maarifa ambayo huna.

Elimu uliyo nayo isikufanye kujiona kuwa wewe ni mtu wa hadhi ya juu , huku huna source yoyote ya kukuingizia kipato. Kama huna means yoyote ya kuingiza kipato basi ujue kuna vingi sana huvijui unapaswa ujifunze

Elimu uliyo nayo itakusaidia tuu endapo utakubali kubadilika kutokana na mazingira lakini pia kukubali uhalisia wa mambo coz huku mtaani mambo ni tofauti sana na vile wasomi wanavyochukulia pindi wakiwa vyuoni..

Elimu ulionayo ukiongeza na maarifa kidogo tuu utakayoyapata pindi ukijichanganya na watu mtaani itakua na faida sana , kuliko kusubiri ajira

Elimu uliyo nayo bila kuwa na pesa tambua fika hakuna atakayekupa heshima kama wengi wenu mlivo na mawazo hayo ya kijinga.

Kushinda mitandaoni na kulalamika kuwa ajira ngumu tuu bila kuchukua hatua zozote ni ujinga ambapo ni wa kuacha mara moja

Tunawategemea sana kuja kuleta ukombozi mtaani kutokana na elimu mlioipata...ila hii hali ya kulaumu tuu serikali inatupa sana mashaka kuwa kuna uwezekano tuna wasomi ambao hawajaelimika
kama vijana wa kitanzania tupoteali serikal ituuze mataifa mengine ambayo yana nguvu kazi ndogo ili kutajipatie lizki uko uko kama serikali ina uhusiano mzuri na mataifa yaliyo endelea bora iwafanyie vijana mpango kuliko wa vijana baki TZ na waendelee kubet [emoji3][emoji28]
 
kama vijana wa kitanzania tupoteali serikal ituuze mataifa mengine ambayo yana nguvu kazi ndogo ili kutajipatie lizki uko uko kama serikali ina uhusiano mzuri na mataifa yaliyo endelea bora iwafanyie vijana mpango kuliko wa vijana baki TZ na waendelee kubet [emoji3][emoji28]
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] hali ni mbaya mno
 
Umeeleza vyema sana. Unakutana na msomi anakuambia yeye hawezi fanya kazi nje ya alichosomea, anapiga teke fursa zinazomzunguka huku akiwa hana chochote afanyacho, umri unasogea+majukumu. Siku akija kushtuka anakua kashachelewa.

Kitu ambacho wasomi huweza kufanya mtaani ni kuilaumu serikali.
 
Narudia tena, kuna dada mmoja alimaliza degree yake pale mlimani, badala ya kutembea na CV yake maofisini kuomba kazi, alifanya kazi ya kuuza uji wa ulezi. Anatembeza na chupa yake kubwa ya uji na kuuza uji na ucheshi mzuri. Sasa hivi amefungua saloon yake kwa kutumia kipato cha kuuza uji na mambo yake ni mazuri. Kazi ni kazi, ili mradi ujue kwa siku unaingiza ngapi.
 
Umeeleza vyema sana. Unakutana na msomi anakuambia yeye hawezi fanya kazi nje ya alichosomea, anapiga teke fursa zinazomzunguka huku akiwa hana chochote afanyacho, umri unasogea+majukumu. Siku akija kushtuka anakua kashachelewa.

Kitu ambacho wasomi huweza kufanya mtaani ni kuilaumu serikali.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] kulaumu na kujipa u special ..hakika ni ulimbukeni wa hali ya juu
 
Siku hizi mchawi HR HR akikukubari kazi IPO kiganjani mwako, nazungumzia Private Sector sio Government's
Huna connection kwa zama hizi ni kilio utazunguka sana na bahasha. Nna jamaa yangu mtaji wa biashara kamalizia kwenye kuzungukia interviews ambazo hazijazaa matunda. Now anajilaumu sana angefocus na biashara angekuwa mbali.
 
Narudia tena, kuna dada mmoja alimaliza degree yake pale mlimani, badala ya kutembea na CV yake maofisini kuomba kazi, alifanya kazi ya kuuza uji wa ulezi. Anatembeza na chupa yake kubwa ya uji na kuuza uji na ucheshi mzuri. Sasa hivi amefungua saloon yake kwa kutumia kipato cha kuuza uji na mambo yake ni mazuri. Kazi ni kazi, ili mradi ujue kwa siku unaingiza ngapi.
Very true mkuu [emoji817]
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] kulaumu na kujipa u special ..hakika ni ulimbukeni wa hali ya juu
Ulimbukeni haswa, matarajio yanawafanya wengi wasitimize na kuishi ndoto zao. Mtu anaona ni aibu kufanya kazi ya nguvu inayomuingizia 10K-15k ili hali hana chochote anachofanya. Na kauli zao "mimi msomi mzima bhana nna degree yangu siwezi kufanya kazi za nguvu".

Wengi wasichojua ni kuwa bills na mahitaji hayaitaji level yako ya elimu, yanahitaji pesa bila kujali imepatikana kwa njia gani.
 
Back
Top Bottom