Wasomi wa Malawi waandika Kitabu kumhusu Magufuli

Wasomi wa Malawi waandika Kitabu kumhusu Magufuli

Kada ya wasomi wa kitanzania iliyojaa kijicho,majungu na kubezana hatuoni mazuri ya mtu Bali mabaya tuuuu(too biased) leo ,mustakabali wa usomi wetu tunavuliwa nguo na nchi mdogo kabisa ya nyasaland,hii Ina impact kubwa katika rank za usomi na taaluma kimataifa,tuna mfumo was elimu unatufanya tuwe vipofu zaidi,Malawi na udongo wake wanamfumo wa elimu unaowafanya wawe rational na waonaji!!!!! Tujitafakari,pamoja na kwamba anayeandikwa tuliishi nae tunajifanya tunamfahamu zaidi,kwa hiyo ufahamu wetu watz unaishia kwenye biasness?,tunashindwa kuwa rational hata kidogo,? Malawi wameenda kisomi zaidi kwa research huenda wamesoma taarifa za magufuli au wameingia nchini mwetu kufanya research,kwa hiyo wanatoa outcome ya researched paper yao, kinyume CHAKE sisi watz tumekalia keyboard,kubeza,kubagaza,kutukana,kusingizia,na Kila Aina ya uchafu,hizo ndo content za elimu yetu,wafuatiliaji wa Mambo internationally katika Kada tofauti,tofauti,Malawi utakuwa imeongeza credit nyingi,huku research data amezitoa Tanzania,n sisi watz,tumechagua kutumia,tuli,halafu anatokea mtu nje huko anaandika,tunaanza kukurupuka na kumtukana eti amtokea nchi masikini kwa hiyo Hana hoja,ndo hivi hivi watu wanachukua credit
 
upo TZ kwel au unaunafiki? au jamaa aliharibu maslahi yako?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio nipo Tanzania, Hujiulizi kwanini JPM alipoondoka ndio TRA inakusanya Mapato makubwa zaidi kuliko JPM alivyowahi kukusanya.

Jamaa Aliua uchumi ila sababu wengi ni darasa la 7 mkijengewa SGR kwa mkopo na Bwawa la Nyerere kwa mkopo mnaona jamaa kafanya muujiza.

Niambie apart from miundombinu kwa fedha za mikopo alifanikiwa kitu Gani zaidi? Na usije ukaniambia sijui ufisadi maana ripoti ya CAG imeonyesha madudu yaliyotokea huku yeye akiwa Rais.
 
He was a PATRIOT! Huwezi kumfananisha na Hawa sasa wsmechangamka Kuwauzia Waarabu maliasili yetu!
Samia is signing contracts with the Arabs from UAE without understanding the ramifications of those contracts to the long term wellbeing of the country!!
Understanding the content of the contracts is of prime importance.
Hakua na uzalendo wowote ule alikua opportunist na saddist tu aliyetamani kuona wenye nacho wanaporomoka. Hata aliowashughulikia ni wale tu alipokua na visasi nao na chuki kuona wamemzidi ushawishi.

Mfano Nchambi alikua na kesi ya ujangilli kwanini hakumfunga? Same to Mwanyika na wengine wote waliotajwa kwenye ripoti ya Makinikia. Ila Cha ajabu waliokua wanaokamatwa ni vyama vya upinzani na kupewa kesi nzito utadhani waliwahi kufanya ufisadi serikalini.

Kama ni mzalendo niambie kwanini hakuwahi kufunga mafisadi ya upande wa serikali kwenye kashfa za Tegeta Escrow, EGMA, Wezi wa Mali za CCM, Ripoti ya TAKUKURU kuhusu rushwa kwenye kampeni, ufisadi Electronic passports na kule NIDA!!

Huo uzalendo unapimwa wapi? Au ukifoka foka ndio uzalendo?
 
Ndio nipo Tanzania, Hujiulizi kwanini JPM alipoondoka ndio TRA inakusanya Mapato makubwa zaidi kuliko JPM alivyowahi kukusanya.

Jamaa Aliua uchumi ila sababu wengi ni darasa la 7 mkijengewa SGR kwa mkopo na Bwawa la Nyerere kwa mkopo mnaona jamaa kafanya muujiza.

Niambie apart from miundombinu kwa fedha za mikopo alifanikiwa kitu Gani zaidi? Na usije ukaniambia sijui ufisadi maana ripoti ya CAG imeonyesha madudu yaliyotokea huku yeye akiwa Rais.
Tuna miaka miwili sasa hakuna barabara mpya licha ya ukusanyaji mkubwa kutoka TRA ya sasa, hiyo ni nini?

Tunataka pia kubinafisisha Bandari zetu ili kujaribu kuokoa uchumi unaokufa, licha ya makusanyo makubwa unayosema

Tunatozo nyingi na kodi za ajabu kuliko wakati wowote ule, hizi pia huzioni kwamba zimeongeza hicho unachokiita ukusanyaji mkubwa wa pesa?

Kama tunakusanya pesa nyingi kuliko kipindi hicho, Huu ugumu wa maisha uliopo unatoka wapi?
 
Wewe uliyashuhudia? Tofauti yako na hao wasomi wa malawi ipo wapi? Unataka kila kiongozi afanye upendavyo? Huo ni ubinafsi uliokithiri.
Jifunze kupongeza vitu vizuri binadamu wenzio wakivifanya na jifunze kukosoa bila kunajisi utu wa wenzio waliokosea.
Ndio nimeyashuhudia, huku nakoishi hatukufanya uchaguzi kabisa kuanzia serikali za mitaa, udiwani na ubunge yaani walipita bila kupingwa. So hatukuwahi kuona kampeni kwenye kata yetu ila kwenye TV tu kwamba Kuna uchaguzi unaendelea!! Sasa mambo kama haya huyo Mmalawi anayajua?

Hivi Mmalawi anajua JPM alizuia kuajiri miaka 7 eti kwamba anajenga nchi ilihali pesa za mkopo.

Hivi Mmalawi anajua mishahara na madaraja hayakupanda miaka 7?!

Mmalawi anajua kwamba private sector ilikufa na data za NBS kuonyesha zaidi ya biashara kubwa elfu 2 zilikufa kufikia 2018?

Mmalawi anajua kwamba watu walikua wanaporwa fedha zao na Taskforce ya TRA kwa arrears za Kodi!! Yaani badala ya kupewa schedule ya kulipa mtu anaenda ku freeze tu akaunti.

Huyo Mmalawi hajui Kuna wapinzani zaidi ya 1000 walifungwa kipindi Cha uchaguzi mkuu and so far 460 wameachiwa. Na zaidi ya 60% kesi za uhujumu uchumi na mauaji!! Imagine.

Yule jamaa kitabu kiandikwe na waTanzania wenyewe maana tunamjua vizuri sio mtu amekaa huko porini anatafuta habari za JPM kupitia google basi anajifanya expert. Aje huku Tanzania apate facts za Moja kwa Moja.
 
Tuna miaka miwili sasa hakuna barabara mpya licha ya ukusanyaji mkubwa kutoka TRA ya sasa, hiyo ni nini?
Ufisadi huko CCM haujawahi kuisha tokea uhuru ila nyie mlidai JPM alizuia mianya ya ufisadi ndio maana Mapato yakapanda. Ndio nakuuliza Mama tunajua ni mpole, serikali imejaa ufisadi, mnadai pia watu wanakwepa Kodi Sasa jiulize kivipi makusanyo yawe makubwa kuliko ya JPM na JK? Means licha ya ufisadi ila uchumi umepanuka na ajira zimetengenezwa. Inaitwa Laffer's curve unaweza soma uelewe naongelea Nini.
Tunataka pia kubinafisisha Bandari zetu ili kujaribu kuokoa uchumi unaokufa, licha ya makusanyo makubwa unayosema
Uchumi unakufa wapi? hao wanataka kufanya partnership kama tu bandari ya Durban na Mombasa. Tatizo huwa ni jinsi mkataba unavyoandaliwa tu ila issue ya kushirikiana sio mpya, kwenye bandari mbona SGR mnajengewa kwa mkopo na Bado mkapangiwa mkandarasi ila hamkusema JPM kafilisika?

Tunatozo nyingi na kodi za ajabu kuliko wakati wowote ule, hizi pia huzioni kwamba zimeongeza hicho unachokiita ukusanyaji mkubwa wa pesa?
Sio kweli, hakuna serikali ilikua na Kodi kama ya JPM nadhani unakumbuka mpaka Online TV zikalipishwa million 1 kwa mwaka kusajiliwa. Hapo bado VAT ikawekwa kwenye utalii, Bado kukaletwa Kodi kwa wamachinga elfu 20 kwa mwaka, Bado bundle likaanzwa kukatwa tozo na TCRA since 2019 n.k hapo Bado mkaongeza Kodi kwenye saruji na mafuta.

Embu acheni kujitoa ufahamu
 
Kataa wivu ongeza wigo wa kuwakubali waliokuzidi na Mungu atakubariki
Wivu wa Nini Sasa kwani Mimi mwanasiasa au mgombea Urais? Ukweli lazima usemwe kwamba JPM was the worst president we've ever had in Tanzania and no Malawian can lecture us on the obvious facts.
 
Mimi siyo msomi lakini hata kama ningekuwa siwezi kufanya upuuzi wa namna hiyo.

Katika safari yangu ya kimaisha nina mashujaa ambao walikuwa watu wangu wa karibu (ndugu) walinifanyia mengi lkn sijawahi kuandika hata ukurasa mmoja kuwahusu wao ndo aje kuwa mtu asiye kuwa na undugu na mimi hata chembe!
Useme huna utaalam wa kuandika! Siyo Kila mmoja anaweza kuandika kitabu, na sisi tutakuelewa - sababu siyo Kwa kubwa JPM siyo ndugu yako!
 
Useme huna utaalam wa kuandika! Siyo Kila mmoja anaweza kuandika kitabu, na sisi tutakuelewa - sababu siyo Kwa kubwa JPM siyo ndugu yako!
Lete vya kwako ambavyo umemuandika.
Tusilazimishane kumuabudu mnae muabudu.
Kila mmoja ana mapungufu na mazuri yake,sasa ya nini unalazimishe kusifia?
Una wasiwasi na nini?

Hamna ya kuzungumzia?
Mlianza na mi5 tena,mkawa mnalazimisha wengine wawaunge mkono,leo hii mnatulazimisha kusifu mliyekuwa mnamsifia,ili iweje?
Kwa faida ya nani?
 
Wasomi wa malawi wasisingiziwe aliyegaramia kuandikwa kwa hcho kitabu tunamjua
 
Back
Top Bottom