Wasomi wanavyosindwa kumwelewa "prof" Kishimba kuhusu elimu

Wasomi wanavyosindwa kumwelewa "prof" Kishimba kuhusu elimu

ego

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2013
Posts
1,620
Reaction score
1,407
Nimemsikiliza kwa makini sana Mbunge Kishimba na nimegundua mzee huyu anaongea mambo makubwa sana ambayo vyuo vyenye wataalamu wenye uelewa wangemtunuku mbunge huyu mwenye elimu ya darasa la saba uprofesa.

Mzee Kishimba anasema tuweke malengo ili elimu yetu iwe hivi

mtoto akimaliza kidato cha nne basi awe na basic knowledge ya maisha.

mtoto akijifunza plants basi ajue yafuatayo

Ajue kwa ufasaha faida za mimea katika maisha yetu, viumbe wengine na dunia kwa ujumla.
Mtoto aliyehitimu kidato cha nne atambue basic needs za mimea
Mtoto aliyehitimu kidato cha nne ajue kila hitaji la mmea linapatikanaje. Kama ni mwanga, kama ni maji, kama ni nutrients muhimu ajue ni kitu gani kinaathiri hivyo vitu.
Mtoto aliyehitimu kidato cha nne ajue kila hitaji likikosekana linaleta athari zipi katika mmea wenyewe na utoaji wa matunda.
Mtoto afundishwe dalili za ukosefu wa hivyo vitu muhimu ni nini, kama akiona mmea majani ni yanakosa rangi ya kijani ajue kuna tatizo la madini fulani, mtoto afundishwe mmea ukikosa maji ya kutosha unakuwaje, mtoto afundishwe mmea ukikosa mwanga unakuwaje.

Hii ndiyo maana ya basic knowledge au primary education.

Mzee kishimba anasema tuache kabisa kuwafundisha watoto wetu upuuzi usio na faida katika maisha yao. kwamba mtoto anamaliza kidato cha nne anajua kuchora section ya mmea na kulebo vitu vya kipuuzi

mfano
1652443372337.png



yaani elimu yetu ya sasa mtoto tunamkalilisha mtoto upuuzi huu, eti ndiyo primary education au secondary na Akimaliza shule akarudi mtaani uelewa wake katika mazingira ni sawa na mjinga ambaye hajasoma.

Mtu amemaliza kidato cha nne analima na akishindwa kuvuna anamtuhumu jirani yake kuwa karoga mazao yake. Mtu mwenye degree anapeleka mbegu za kupanda kanisani zikaombewe eti ndipo zitatoa mazao mengi.

Mzee kishimba anasema liwepo somo la biashara kwa watoto wote
watoto washundishwe misingi ya kufanya biashara kuwa ni ama kuwa mzalishaji, au kuwa mtu wa kati ukichuuza bidhaa za wengine au kutoa huduma.

Mtoto afundishwe miiko ya uzalishaji, mtoto afundishwe jinsi kitumia technolojia za kisasa katika uzalishaji kunavyoongeza tija na faida. Mtoto afundishwe umuhimu wa kuzalisha bidhaa zilizo bora ili kuteka soko, mtoto afundishwe umuhimu wa kulinda afya za wateja, mtoto aelezwe athari za kufanya udanganyifu katika biashara kama kuongeza uchafu katika bidhaa ili kuongeza kipimo jinsi inavyoharibu uaminifu, biashara na inaweza kupelekea kifungo.

Siyo mtu amehitimu kidato cha nne anashinda kwa waganga kusafishwa nyota ili afanikiwe.

Mtoto afundishwe mbinu za kubuni wazo la biashara, kama ni kilimo, kama ni uchuuzi au uzalishaji au utoaji wa huduma.

mtoto afundishwe mbinu za kutafuta mitaji, kama ni kudunduliza, au kumtumikia mtu kwa mkataba, au kukopa au kuingia ubia.

Mtoto afundishwe mbinu za kufanikiwa pale unapoanzisha biashara kama ni kutoa huduma bora, au kutoa huduma nafuu, kama ni kuweka mazingira bora ya huduma n.k

Mzee kishimba anasema tusiganganie kurundika mambo mengi na kumfundisha mtoto kwa kukimbia kimbia na mwisho unakuwa na wahitimu ambao ni "jerk of all trade, master of none"

elimu yetu ya sasa ni kama kokolo lenye vitu vingi lakini watoto wetu wanahitimu hawana uelewa wowote.

Tuwafundishe watoto wetu mambo machache na hayo machache wawe wabobezi katika elimu ile basic

kwamba mtoto akihitimu kidato cha nne akarudi kijijini awe ndiye wa kumweleza mzazi wake ambaye hakusoma kuwa tutavuna zaidi tukitumia mbolea au mimea yetu ni dalili za ukosefu wa nitrogen, au baba mimea yetu imebabanana sana na kukosa hewa ndiyo maana hatuvuni na siyo uchawi.

Mzee kishimba anasema tuache kuwaimbisha watoto wetu
sijui " Helo helena chinja lile beberu bora na ondoa figo " huu ujinga unamsaidia nini mtu aliyehitimu kidato cha nne. Mttalamu anayehitaji kujua periodic table atajifunza periodic table katika masomo ya taaluma yake.

Huu ushenzi wa kumweleza mtoto ukichanganya tindikali na besi unapata chumvi na maji

yaani tumekusanya vi taarifa vingi tu katika masomo mbalimbali na kuweka kama elimu but with no any beneficial gain kwa level husika.

Lazima tuwe na Level ya uelewa kwamba tunataka mtoto aliyemaliza darasa la saba awe na uelewa gani?

mtoto aliyehitimu kidato cha nne awe na uelewa gani?

na kadhalika
 
Kusema ukweli ni huyo Mzee tu ndiye huwa na-pay attention kumsikiliza.

Wengine huwa nawafatilia huku nafanya mambo yangu!
 
Wasomi viongozi ni wapumbavu sana
jamani jamani msituandame sisi wasomi, tumekuwa tukifanya kwa mujibu wa yale tuliyofundishwa. Kama tunatenda kinyume na matarjio yenu labda elimu mliyotupa haikuwa sahihi.

Hivyo tukae chini tutazame tunakwendaje lakini ni ngumu maana kudhania msomi aliyesoma elimu mbovu anaweza kuiboresha elimu hiyo ni sawa na kudhania mgonjwa anaweza kujitibu. Sisi wasomi ni tumelemazwa na elimu iliyokuwepo na bado fikra zetu tunaiona iko sahihi.

Tunahitaji dakitari kama mzee kishimba anayeweza kututazama akashangaa mbona aliyesoma na asiyesoma wanatenda sawa, wanawaza sawa?
 
Mh Kishimba popote ulipo WaTanzania wengi tunaokufuatilia tunakukubali sana. Tunakupenda kwa michango yako ya kuwainua hasa vijana wa nchi hii.
 
Kishimba wewe ni mtu na nusu,hajawahi kutokea mbunhe mwenye hoja za kueleweka kwenye elimubkama wewe sidhani kama atatokea mwingine mwenye hoja kama zako
Big up kishimba.
 
Ubora wa elimu haupimwi kwa kigezo cha ajira. Mana utasikia mtu anasema elimu haijawasaidia, ukiuliza kwa Nini atakujibu hawana ajira wako mtaani.

Napata mashaka na elimu yake, unless kama pia kaishia la saba no sahihi kuongea hivyo. Ubora wa elimu unaonekana kwa kias kidogo sana nchi za matakoni kwa Dunia sababu wengi wetu mawazo yameganda! Ya baridi na meusi Tiiii!.
 
Back
Top Bottom