Wassira: Hati ya Muungano imesha fika Dodoma leo!

Wassira: Hati ya Muungano imesha fika Dodoma leo!

Wakati mwingine tuwe na heshima kwa viongozi waliotuongoza miaka ya zamani ambapo hapakuwa na komputa. Kudai kuwa viongozi wa Zanzibar wote waliotumikia serikali ya Nyerere, hasa wale wa kwanza kutoka kwenye baraza la mapinduzi akina Babu, Jumbe, Hanga, Karume, Moyo na wengine walikuwa ni wajinga sana kutumikia serikali ya Muungano ambao hawakuwa wameuafiki kweli ni kuwadhalilisha sana viongozi hao ambao wengi wao wameshatangulia mbele ya haki.

Ni afadhali tujadiliane kuwa Muungano huu ambao wazee wetu waliafikiana wakati huo sisi hatuuhitaji leo kwa hiyo tuachane nao kuliko kuelata maswali yasiyo kuwa na maana kama vile hati ya muungano ina walakini, sahihi haikukaaa sawa na upuuzi wa namna hiyo tuachane na hayo tuangalie tu kama Muungano kweli unatufaa. Mimi sasa hivi nina imani kabisa kuwa Muungano huo hautufai tena, ndiyo maana ninapenda kuona Tanganyika inarudi tena. Wenzetu waliahi kusema kuwa "you don't know its value until you miss it." Nitakapo-miss muungano labda ndipo nitajiangalia tena ila kwa sasa nasema "enough is enough" Muungano huu uvunjwe. Nchi yenyewe imekuwa haina mwelekeo tena kwa hiyo ni afadhali tuanze upya tu.

Hatuwezi kufikia kuamua kuuvunja muungano, bila kukiri kuwa makubaliano yaliyofanywa yalikuwa na kasoro. Kadhalika , hatuwezi kukubali kasoro zilizokuwepo halafu tukajifanya hatujui waliozisababisha. Hii ndiyo maana kila siku napiga kelelele humu kwa watu kuacha ushabiki wa kipuuzi na kuangalia ni hoja ipi ina ukweli na ni ipi inabeba maslahi ya nchi, na siyo hoja ipi imesemwa na nani na kama ni mCCM au mCHADEMA! Ni kwa sababu historia ndivyo inavyoandikwa. Kwa hiyo pale ambapo viongozi wetu tuliowachagua waliandikisha historia ya ovyo kabisa, ni vizuri tukakiri hilo, bila kigugumizi wala kupepesa macho.Na historia ituhukumu hivyo, kuwa sisi, baada ya kuangalia na kutafakari kwa kina, tuligundua kuwa viongozi wetu walifanya jambo la ovyo kabisa. Halafu tuwaambie watoto wetu ni kipi kilikosewa ili wao wapate kurekebisha. Vinginevyo kugundua makosa na kuendelea kuyapaka mafuta, ni kuhalalisha watoto na wajukuu zetu (taifa la kesho) kuishi kwenye uwongo ulioanzishwa na hao marehemu, ambapo tutakuwa hatuna tofauti nao kama tutashindwa kusema hilo lina makosa.

Kuhusu kuuvunja au kuunusuru, mimi nadhani ni mapema kufika huko. Kwanza tuone uhalali wa makubaliano yale, halafu tuone kama bado tuna sababu (kwa leo) za kuwa na makubaliano ya aina hiyo. Kisha kama tutaona inafaa tuendelee au kama haifai turekebishe makubaliano au kama haiwezekani basi tuuvunje! hili ni swala linalohitaji maamuzi ya wananchi wenyewe, na siyo viongozi kuamua kama walivyofanya kipindi kile na kama ambavyo wanalazimisha kufanya leo!
 
teh! ccm ni wahuni wa stendi inachezea vichwa vya waandishi wa hbr watakavyo wakibanwa na mambo wanawaita,wakati wa kuchezesha dili zao kwenye vikao vya kamati hawataki kusikia harufu ya mwandishi wa habari.
 
Kwakweli Wassira umedhihirisha kuwa wewe ni kiongozi imara, Hongera kwa kuiwakilisha dola.
 
hiyo hati ya magumashi, kuileta hati mwezi mzima?
 
Wote mlio changia hapo juu mnajikuta mnaleta umbea tu. Subirini tupewe hati tutaichunguza baada ya kupewa. Na mnaobeza na kusema feki kwani origina mkonayo na kama mnayo wasilisheni..... wasira a.k.a SIMBA WA YUDA.

Acha madharau, hiyo sentesi uliyotimia herufi kubwa haiakisi uwezo Wa kiumbe ulichokitaja! Tuheshimiane bwana!
 
Wote mlio changia hapo juu mnajikuta mnaleta umbea tu. Subirini tupewe hati tutaichunguza baada ya kupewa. Na mnaobeza na kusema feki kwani origina mkonayo na kama mnayo wasilisheni..... wasira a.k.a SIMBA WA YUDA.

Wambea akina nani? ngoja muumbuke na wassira wako
 
Mbona ina date of transimision kwa fax? Si ilikuwa Og. wanahabari walipewa?
 
Lissu Kiboko yao kunguruma jana tuu Hati imepatikana kitu ambacho hata mahakama kuu zanzibar haikupelekewa
 
Certified true copy my foot- nani kadhibitisha? Usanii unaendelea.
 
Iweke hapa janvini tuone uchakachuaji, na hata kama ipo imefikia ukomo wake sasa tunaandika katiba mpya hiyo ni zilipendwa
 
Hongera sana Tundu Lisu kwa kuilazimisha serikali kuleta hati ya muungano japo feki ni kwamba wamesikia unachotaka.
Ikumbukwe kuwa Mbatia alihitaji curriculum ya elimu wakaleta feki ila badaye walisikia hitaji lake kwa kufutwa kwa EMAC.
Bila CHADEMA, Inamaana CCM mngefanya yale ya Bogus mind enzi ya ukoloni.
 
WanaJF wenzangu naomba tutafakari kwa makini juu ya tukio hili la suala la Hati ya Muungano Katika taratibu za uwekaji wa Saini nyaraka muhimu uwa lazima zisainiwe nyaraka zaidi ya moja ili kila upande unaohusika uweze kuwa na nyaraka yake. kwa hiyo katika nyaraka hii yaani HATI YA MUUNGANO ni lazima zilisainiwa HATI zaidi ya 3 yaani moja ilitakiwa iwepo kama kumbukumbu ya Serikali ya Tanganyika, Nyingine Serikali ya Zanzibar na nyingine UN na moja kuwepo kwenye hii serikali ya Muungano. Tumeweza kuonyeshwa hiyo moja je hizi zingine ziko wapi tunaomba tuonyeshwe ili tujiridhishe uhalali wa hii iliyopo.
 
Habari za muda huu waungwana!
Mimi naomba kuuliza maswali yangu yanaoniumiza kichwa tangu jana ilipotolewa au kuonyeshwa kwa Hati ya Muungano jana Ikulu kupitia katibu mkuu Ombeni Sefue
swali langu la kwanza 1-kwann serikali iliicherewesha Hati mpaka mvutano mkubwa bungeni, Je serikali ilikuwa inawadhihaki wajumbe wa bunge maalumu la katiba na waTanzania kwa ujumla kuwasilisha Hati yenye utata wa sahihi ambapo wajumbe wengine walisema ni feki ??

2-Nakumbuka mwandishi wa radio uhuru(jina limenitoka) aliuliza kumekuwepo na marumbano au mzozo wa kuwa Hati ilisainiwa na watu wachache bila kushirikisha watu nk. nk. nk kama sijakosea swali lkn pia alikuwa mwandishi wa gazeti ambaye pia aliuliza swala hati kuwa haitambuliki UN na swali la kuhusu mafuriko ya Dar Ikulu inalisemeaje hilo swala wakati waathirika kuwa serikali imesahau. Nk
lkn katibu mkuu alijibu hayo maswali waposemaji yeye kaja kuonyesha Hati ya muungano tu! Swali ni
Je, kulikuwa na haja gani ya Katibu Mkuu ndg. Ombeni Sefue kuruhusu maswali kwa waandishi wa habari wakati yeye kuionyesha na kuielezea tu????

3-kuna nini kilicho nyuma ya pazia/siri gani kuhusu hati ya Muungano(kutona na yoote niliyauliza kwenye swali no.1)

nipo free kabisa kusahihishwa ktk maswali niliouliza lkn lililo muhimu kwangu ni kusaidiwa haya maswali.
Asante nawasilisha
-Gody
 
Hati iliyotolewa ni batili ccm wamekosa hoja kweli sasa tuamini sahihi gani hapa,acheni upuuzi nyie wapuuzi,tunachosema ni kuwa muungano huu ni batili na tunaitaka tanganyika,watanzania acheni uoga tanganyika inamashujaa wengi waliopigania uhuru na tanganyika ikawepo amini nawaambia tanganyika huru utapatikana kwa gharama yoyote.
 

Attachments

  • 1397552203466.jpg
    1397552203466.jpg
    40.3 KB · Views: 732
Naunga mkono hoja, kama hiyo sito ya kutengeneza, tuone ya Zenji, Tanganyika, JMT na UN
 
ndio tunataka hati ya pili original km hii ya jana kutoka zanzibar,
 
Back
Top Bottom