Wassira: Hati ya Muungano imesha fika Dodoma leo!

Wassira: Hati ya Muungano imesha fika Dodoma leo!

WanaJF wenzangu naomba tutafakari kwa makini juu ya tukio hili la suala la Hati ya Muungano Katika taratibu za uwekaji wa Saini nyaraka muhimu uwa lazima zisainiwe nyaraka zaidi ya moja ili kila upande unaohusika uweze kuwa na nyaraka yake. kwa hiyo katika nyaraka hii yaani HATI YA MUUNGANO ni lazima zilisainiwa HATI zaidi ya 3 yaani moja ilitakiwa iwepo kama kumbukumbu ya Serikali ya Tanganyika, Nyingine Serikali ya Zanzibar na nyingine UN na moja kuwepo kwenye hii serikali ya Muungano. Tumeweza kuonyeshwa hiyo moja je hizi zingine ziko wapi tunaomba tuonyeshwe ili tujiridhishe uhalali wa hii iliyopo.

kwani zipo ,,ngapi?
Na nchi zipo ngapi?
 
attachment.php
 
Tukiwabana sana, mwisho wa siku watatuambia kwamba, hati ya muungano ni ule udongo aliouchanganya Nyerere peke yake!~
 
Tukiwabana sana, mwisho wa siku watatuambia kwamba, hati ya muungano ni ule udongo aliouchanganya Nyerere peke yake!~

Mkuu,

Umenikumbusha!

Halafu ule udongo aliouchanganya Mwl Nyerere peke yake ndio wanasema tukautafute baharini?

Hv nani anajua ulitoka Zanzibar na Tanganyika na haukutoka Butiama na Chalinze?

MTANGANYIKA DAIMA!
 
Tusuburi labda atakuja na hati tofauti na hiyo iliyoonyeshwa waandishi WA Habari.
 
Mkuu umechnganya mambo hapo...Kuna hati ya Mauungano na sheria ya Muungano ambayo Nyerere alii-assent.
 
ccm wahuni na washenzi wakubwa hiyo hati siyo yenyewe saini wamebushi
 
Naona uelekeo wa Bunge la Katiba unayumbishwa yumbishwa kila mara...
 
ni vigumu kuelewa kinachoendelea , mbona Nyerere anazalilishwa kiasi hicho ina maanisha alikuwa hawezi kusaini mbona kila saini iko tofauni na nyingine
 
jana tumemsikia katibu mkuu kiongozi akisema kuna hati nyeti za taifa kama ile ya muungano na ile ya uhuru wa tanganyika ni nyeti sana kiasi kwamba hawawezi kuzitoa, hivi muungano wetu una usiri gani,hati ya uhuru wa tanganyika ina usiri gani? uzalendo wa nchi utajengwaje? vijana wamecheleweshwa kufunzwa muungano ndio maana leo serikali inatumia nguvu kuulinda, wakati ingeingizwa kwenye mitaala ya elimu, ni nchi iliyojaa ujinga mkubwa hasa kwa ccm na viongozi wake
 
Wote mlio changia hapo juu mnajikuta mnaleta umbea tu. Subirini tupewe hati tutaichunguza baada ya kupewa. Na mnaobeza na kusema feki kwani origina mkonayo na kama mnayo wasilisheni..... wasira a.k.a SIMBA WA YUDA.

Mjinga Wasira anawezaje kuwa Mungu? Acha kukufuru, na serikali yenu ya uongo uongo, serikali ya ujanja ujanja.
 
Serikali mbili HAZIKUBALIKI!

MTANGANYIKA DAIMA!

kuna maswali najiuliza, kulingana na yanayoendelea mjengon, bila shaka watatoka na serikali 2, ndizo zitakazopigiwa kura kama itakuwa no tutaendelea na ya zaman, je kulingana na maswali ya Tundu Lisu, hati ya muungano ipo? kama ipo ni sahihi? kama ni sahihi je muungano ni halali, kwenye swali la tatu kama muungano c halali kitu gan kitakachofanyika?
 
Tukiwabana sana, mwisho wa siku watatuambia kwamba, hati ya muungano ni ule udongo aliouchanganya Nyerere peke yake!~

Kwa nn Nyerere alikamata zile chupa peke yake?
 
Baada ya mh. Wassira kutoa kauli na kuwahakikishia watanzania kuwa hati ya muungano ipo na ataiwasilisha ndani ya siku mbili.

Taarifa zenye uhakika kabisa kuwa hati imeshawasili Dodoma kwa maana ya nakala/copy na asubuhi itawasilishwa nakala iliyothibitishwa/certified true copy na kila mjumbe wa bunge la katiba atapewa nakala yake kama kumbukumbu.

WAKUU, Hati ya Muungano ilotolewa jana na Ikulu ni Kiini macho kingine kutoka CCM. Au ndo kazi ya mjumbe wa Katiba kwa Tiketi ya Waganga wa Kienyeji? Hati gani ambayo kwa mujibu wa Sefue hutunzwa kama mboni ya jicho, imechakaa hivyo mpaka kufungwa kwa cellotape kwa kitabu cha kiada kutoka maktaba ya sekondari ya Kata? TUTAFAKARI!!!
 
Back
Top Bottom