PAZIA 3
JF-Expert Member
- Jan 30, 2018
- 1,102
- 1,919
Habari za uzima watu wote?
Nimekuja tena kuleta wazo litakaloweza kuibua au kuchochea maendeleo katika jamii zetu bila kuacha kundi lolote kwenye jamii zetu.
Bila shaka utakubaliana nami kwamba, mpaka Sasa, wataalamu wa TEHAMA wameshindwa kabisa kutuletea vifaa na programs zenye uwezo wa kushirikisha makundi yote ya jamii zetu ikiwemo watu wenye mahitaji maalumu kama vile watu wenye upofu, viziwi na wasioweza kuongea ( bubu).
Yaani, mpaka Sasa, bubu, kiziwi na kipofu hawana platforms nzuri zitakazowafanya wachangie maendeleo katika jamii zetu kupitia matumizi ya TEHAMA. Pamoja na kuwa, tupo katika ulimwengu wa TEHAMA, lakini bado Kuna gepu kubwa kwenye kundi la watu wasiokuwa na uwezo wa Moja kwa Moja kutumia program na vifaa vya TEHAMA.
Sisi kama nchi, kwa kutumia wataalamu wetu, au hata wataalamu wa kutoka nje ya nchi, hebu tuunde programs kama vile apps na vifaa design ya simu ambavyo, hata ndugu zetu, wenye mahitaji maalumu wawe na uwezo wa kuchangia maoni Yao katika kukimbiza gurudumu la maendeleo katika jamii zetu. Haiwezekani tuwe na kundii hili, na wakati mwingine serikali inatumia gharama kubwa kuwasomesha wenzetu hawa, Kisha wakishasoma, utaalamu wao wanabaki nao kichwani mwao. Tunahitaji mawazo Yao kwenye uchumi, Siasa, michezo, imani nk nk, wenzetu hawa wapo Kila mahali, njia pekee ya wao kishiriki mawazo Yao kwenye maendeleo ya nchi yetu, ni kupitia matumizi ya TEHAMA.
Hili linawezekana kwa kuweka offer au kuhamasisha kupitia mitandao ya kijamii na platform zingine kwamba, wataalamu wa TEHAMA watuletee either programs au vifaa kama simu zitakazowasaidia wenzetu kuchangia maoni Yao katika kuibua fursa za maendeleo kwenye jamii zetu. Mfano, tukipata application yenye design ya WhatsApp, iwe na uwezo wa kurekodi sauti, iwasaidie wasioona kutoa mawazo Yao.
Nimekuja tena kuleta wazo litakaloweza kuibua au kuchochea maendeleo katika jamii zetu bila kuacha kundi lolote kwenye jamii zetu.
Bila shaka utakubaliana nami kwamba, mpaka Sasa, wataalamu wa TEHAMA wameshindwa kabisa kutuletea vifaa na programs zenye uwezo wa kushirikisha makundi yote ya jamii zetu ikiwemo watu wenye mahitaji maalumu kama vile watu wenye upofu, viziwi na wasioweza kuongea ( bubu).
Yaani, mpaka Sasa, bubu, kiziwi na kipofu hawana platforms nzuri zitakazowafanya wachangie maendeleo katika jamii zetu kupitia matumizi ya TEHAMA. Pamoja na kuwa, tupo katika ulimwengu wa TEHAMA, lakini bado Kuna gepu kubwa kwenye kundi la watu wasiokuwa na uwezo wa Moja kwa Moja kutumia program na vifaa vya TEHAMA.
Sisi kama nchi, kwa kutumia wataalamu wetu, au hata wataalamu wa kutoka nje ya nchi, hebu tuunde programs kama vile apps na vifaa design ya simu ambavyo, hata ndugu zetu, wenye mahitaji maalumu wawe na uwezo wa kuchangia maoni Yao katika kukimbiza gurudumu la maendeleo katika jamii zetu. Haiwezekani tuwe na kundii hili, na wakati mwingine serikali inatumia gharama kubwa kuwasomesha wenzetu hawa, Kisha wakishasoma, utaalamu wao wanabaki nao kichwani mwao. Tunahitaji mawazo Yao kwenye uchumi, Siasa, michezo, imani nk nk, wenzetu hawa wapo Kila mahali, njia pekee ya wao kishiriki mawazo Yao kwenye maendeleo ya nchi yetu, ni kupitia matumizi ya TEHAMA.
Hili linawezekana kwa kuweka offer au kuhamasisha kupitia mitandao ya kijamii na platform zingine kwamba, wataalamu wa TEHAMA watuletee either programs au vifaa kama simu zitakazowasaidia wenzetu kuchangia maoni Yao katika kuibua fursa za maendeleo kwenye jamii zetu. Mfano, tukipata application yenye design ya WhatsApp, iwe na uwezo wa kurekodi sauti, iwasaidie wasioona kutoa mawazo Yao.
Upvote
2