"WATANIONAJE" imeharibu maisha ya watu wengi sana kimaendeleo

"WATANIONAJE" imeharibu maisha ya watu wengi sana kimaendeleo

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Kijana amemaliza degree yake karudi mitaa aliyokulia, yupo bize kuomba kazi na kutembeza bahasha bila mafanikio, kujitolea kwenye taasis kwa mshahara wa laki 1, n.k. Hawezi kufungua sehemu ya kunyoa nywele, kuwa seremala, kuuza mgahawa, n.k. kuna hofu ya watanionaje

Mchezaji wa mpira, msanii, muigizaji, n.k, alikuwa na mfanikio makubwa kapanga nyumba nzuri, gari kali, anavaa fresh, n.k. ghafla soko linamstaafisha, anaendelea kuishi maisha yale yale ya gharama pesa zinaisha, anaanza kukopa mpaka hakopesheki, hofu ya watanionaje ipo kwa kuogopa kuishi maisha ya chini, hakufanya uwekezaji wa maana akiwa kwenye ubora wake kinachobaki ni kuwa mpiga vizinga, uraibu wa madawa ya kulevya, punda wa kubeba madawa, uhalifu, n.k. anaona soo kufanya shughuli za kawaida kwasababu anajiona staa,

Mfanyabiashara alikuwa na mafanikio makubwa ghafla kapigwa na kitu kizito, jawezo kuishi maisha ya chini anaogopa kuchekwa, anaendelea na lifestyle ile ile kutembelea gari linalohitaji mafuta mengi, kuweka heshima bar, kusomesha watoto private za milioni 3, n.k. anakopa pesa aingize kwenye biashara lakini pesa hizo zinaishia kwenye maisha yake ghali kwasababu kakataa kuishi maisha ya chini, matokeo yake anakuwa mdaiwa sugu, kwenye biashara anataka kurudi kwa kasi badala ya kidogo kidogo, biashara zenye faida kidogo kidogo haziwezi kwasababu inabidi ajibane, matokeo yake anaingia biashara haramu za faida chap chap anapigwa na kitu kizito zaidi
 
Nidhamu ya fedha ni kitu muhimu sana kwenye utafutaji usisahau kuwekeza na kusave mambo yanapokuwa mazuri,

Wanachuo someni vyuo vya nje ya mkoa, mkimaliza bakini huko huko, hakuna aibu kwa mishe yoyote halali utayoifanya tofauti na kusomea chuo sehemu uliyokulia
 
Ni suala la mindset, naamini unaweza kufanikiwa popote pale kama tu utakuwa na utulivu wa fikra, kujua unataka Nini na unataka kufika wapi... Pesa hazipatikani kirahisi kabisa, ni process ndefu inayohitaji vitu vingi hasa kama umeamua kujiajiri from scratch kabisa.
 
Ni suala la mindset, naamini unaweza kufanikiwa popote pale kama tu utakuwa na utulivu wa fikra, kujua unataka Nini na unataka kufika wapi... Pesa hazipatikani kirahisi kabisa, ni process ndefu inayohitaji vitu vingi hasa kama umeamua kujiajiri from scratch kabisa.
Nakazia ujumbe wako mkuu
 
Hicho kitu ni kibaya sana. Unakutwa na janga, au failure fulani halafu unajiweka katikati ya jamii. No
 
Watanionaje.

Nafkir hii imekuja zaidi baada ya maendeleo ya Mitandao ya Kijamii, hii ndio inaleta watu kuwa na depression na matumizi mabaya ya fedha ili kuimpress watu ambao hata hajawahi kuwaona.

Waathirika wakubwa ni Wanawake.
 
Ni kweli kabisa unaogopa watanionaje wakati hawakupi hata mia ya kula
Tujufunze na tubadilike
 
Ni suala la mindset, naamini unaweza kufanikiwa popote pale kama tu utakuwa na utulivu wa fikra, kujua unataka Nini na unataka kufika wapi... Pesa hazipatikani kirahisi kabisa, ni process ndefu inayohitaji vitu vingi hasa kama umeamua kujiajiri from scratch kabisa.
Upo sahihi
 
Back
Top Bottom