Watanzania hawachukii ufisadi bali humuonea wivu anayekula

Watanzania hawachukii ufisadi bali humuonea wivu anayekula

... hiyo ni hulka ya binadamu sio watanzania tu; duniani kote binadamu ni wabinafsi sana. Kwa kutambua hulka hiyo ya kibinadamu; nchi zenye watu wenye akili huhakikisha wanaweka miundo ya kuwadhibiti wenye nafasi za kula ili wasile wakavimbiwa; tena imeandikwa "toshekeni na mishahara yenu". Kutoatoa vitamko vya "kuwakanya" walafi bila kuwa na strict measures hasaidii; binadamu ni viumbe wa ajabu. Nchi kama China wana measures zao tena ni kali kweli kweli.

... sisi sio lazima tufuate njia ya China au kwingineko wenye adhabu kali; bali tuanze kuboresha sheria mama - Katiba. Baadhi ya wenzetu hawataki kuona hilo linatokea; kwanini? Kwa sababu Katiba ilyopo inawahakikishia kufaya ufisadi bila bugudha; na hata akiingia mwingine kwa Katiba hii huenda akawa fisadi haswa! Katiba Mpya ni hatua muhimu ya kuanza nayo.
Kwahiyo sisi ni wadhaifu kiasi hadi tushindwe kutengeneza mifumo!??? Hadi aje mzungu atengeneze!?
 
Naunga mkono hoja...wapinga ufisadi ndio mafisadi wenyewe hawajapati mfereji tu...

Jitu linawasema wenzie au wezi wa serikalini wakati lenyewe kutwa kucha linadhurumu watu mtaani huku, linanunua vitu vya wizi,limission town, lijizi, linashangilia mafanikio ya mjomba ambaye ni fisadi serikalini tena na ada ya watoto linasaidiwa kulipiwa...

Tungekuwa wote tunauchukia ufisadi kwa dhati hapa Tanzania either usingekuwepo au ungekuwa negligible...
Braza natamani nikupe zawadi sema ndo hivo january hii sina kitu
 
Kwanini wasiandamane kudai sheria kali za kulinda mali zao badala yake wako kama mazombi!! Wanasubiri na wao waingie kwenye mrija wa kula sheria hizo hizo dhaifu ziwalinde!!! Wtz ni wezi sana
Sijui kwanini hawaandamani, ila ninachotaka kujua kuhusu hoja yako, ni kwamba mtu akiibiwa halafu akamchukia aliyemuibia, ni wivu? Sio?
 
Kwa hii Post Unakuwa umewakosea sana Heshima.watu waliotumikia hili taifa kwa uaminifu na bila kuiba ingwaje walikuwa kwenye nafasi za kufanya uovu huo. Kila mtumishi angekuwa fisadi kama hao mnaowapigia chapuo, hii nchi ingekuwa ya mwisho duniani. Isinge sogea hata hizi hatua tulizopiga. Usingeona hizi huduma zikisogea mpaka pale kijijini kwako. Amini kuwa kuna Wazalendo kindakindaki wa hili taifa wanaolipigania kila siku, wengine hata kuuwawa na hao mnaowapigia chapuo wasizomewe. Na Hoa wazalendo wa namna hiyo wameamua kukaa kimya kwakuwa kila wanapofungua mdomo, hugeukwa na watu kama nyinyi ulioandika post hii na kusema wana wivu ama wamekosa. #Wazalendo wa Taifa Hili wapo.
 
Watanzania hawachukii ufisadi na ukiona wanapiga kelele ujue ni wivu tu kwa mtu fulani, ukitaka kujua hilo mtafute mpiga kelele mmoja mpe nafasi uone maajabu!

Mtanzania na wizi ni mtu na Nduguye hawatengani, watz ndivyo tulivyo. Ni wezi hakuna mzalendo hata sisi tunaopiga kelele tunahitaji tu nafasi tupige. Tukipata nafasi hutatusikia tena!

CCM imetengeneza hilo kuwa kama mfumo wa nchi yaani "Piga kelele kama hujapata ukipata Nyamaza".
Ukweli mchungu,ndio maana na wao wakipata watafanya vilevile.

Afu huwa wanaona mtu akiwa kiongozi ni Halali kufanya ufisadi na upendeleo eti Kisa ni kiongozi na kasoma.

Huonaga hata mtu ana biashara nzuri ila utasikia napata shida kwa sababu sikusoma na kudhirisha hilo anapeleka watoto wake shule wasome na hawafundishi biashara.

Akimaliza akipata Kazi utasikia mwanangu kaajiriwa sehemu x and y na anajiskia fahari bila kujua kwamba kioato cha mwajiriwa ni kidogo Sana yaani biashara yake ni kubwa mmno.

Nadhani shida ni kuona biashara hazina security na yeye mwenyewe kuweka security kwa njia ya michango ya pension toka akianza.biashara.
 
Ni wivu ndy!!! Maana mlalamikaji nae akipata nafasi anakuwa mwizi vile vile!! Mtanzania ni mwizi sana
Sawa, wacha tuendelee kuwaonea wivu wanaotuibia, hata huko mtaani mwizi akikuibia usipate hasira na chuki kiasi mkaanza kumpiga, we muonee tu wivu huku ukimuacha anaondoka zake, maana huwezi kupiga mtu kisa unamuonea wivu
 
Ujue zamani nilikuaga mzalendo Sana ila baada ya kuwagundua jamii ya Tzn ilivyo nikasema kumbe ngoja nijipimie kwa urefu wa kamba yangu.

Tena jamii yetu ninya hovyo Sana ndio maana hata wakiona mgeni hakuna wa kustuka wala kumuuliza yaani hulka ya ubinafsi na kutojali wengine.

Hili ni tatizo la jamii yetu.
 
We ndo taahira kabisa ukiona mtu kakaa kimya ujue kalambishwa kitu tyr!!! Kama mzalendo kwanini asipaze sauti kwa kutoa ushahidi usiobakiza shaka!!!?
hatuwezi elewana coz hujawah fanya kazi yoyote serikalini, kuna watu ni waadilifu/wachamungu ukimambia habari ya dili hamuelewani kabisa, watu hawa hua wanakaa kimya kuepuka kufanyiwa fitna na watu wa madili bt wao hua hawachukui hata sent.
 
hatuwezi elewana coz hujawah fanya kazi yoyote serikalini, kuna watu ni waadilifu/wachamungu ukimambia habari ya dili hamuelewani kabisa, watu hawa hua wanakaa kimya kuepuka kufanyiwa fitna na watu wa madili bt wao hua hawachukui hata sent.
Hao ni maofisa wa chini wasio na access ya kupata pesa nje ya salary na posho zao.
 
Back
Top Bottom