Watanzania hawachukii ufisadi bali humuonea wivu anayekula

Watanzania hawachukii ufisadi bali humuonea wivu anayekula

Kwenye mojawapo ya kesi fulani ya miaka ya nyuma ya maswala ya fedha za Serikali kuchotwa kinyemela, nilijaribu kufanya utafiti wa juu juu kuhusinana na watu waliokuwa wanalalamika kuhusiana na fedha hizo kupotea.

Nilichokuja kubaini ni kuwa wachache sana walikuwa wameumizwa na issue nzima ya hela hizo za umma kupotea, lakini wengi wao malalmiko yao yalikuwa yamejikita katika kulalamikia issue nzima ya kwa nini zilipita kwenye mikono ya makanyaga na siyo kwenye mikono yao wenyewe.

Yaani walikuwa wanalalamika kwa sababu walitamani ziwe zimepita kwenye mikono yao walalamikaji hao
Ili ni kweli kabisa.
Hili ni tatizo kabisa.
Mtza kwa pesa za upigaji afai kabisa.
Unakamatwa na rushwa unatoa rushwa kesi inatupwa.
Ni nadra kukuta akufatiliaye eti umekwapua nae ukamp mgao wake akaendelea kukufatilia.
 
Sheria za Tza hazina uwezo wa kumfunga fisadi.Bali vibaka wadokozi.
Wadokozi upigwa miaka mingi fisadi afungwi ulipa faini kiduchu au miaka michache jela.
 
Kweli kabisa kwenye hilo ni kama sote tupo sawa ila sasa utofauti unakuja hapa..

Kuna wale wezi ambao huiba kwa akili na wasistukiwe na wananchi (kama mimi endapo nitapata nafasi) , na pia kuna wale wezi wa waziwazi, watumia mabavu pasipohitajika, wanyang'anyi na mostly hawatumii akili (sabaya, bashite nk nk.)
 
Watza wengi ni wezi.uiba ofisini uleta nyumbani,kina mama uachiwa pesa za chakula uwalisha watoto viporo nao ubana wanatuma kwao na kucheza vikoba,dada wa Kazi nao uzidisha bei ya vitu wakitumwa dukani sokoni.
Maadamu KILA mtu mwizi sio raisi sio mkuu sijui wa nn sio mfagizi KILA mmoja ula urefu wa kamba yake.
Mzungu kutengeneza control number lakini haijamzuia mswahili kuiba.
 
Kweli kabisa kwenye hilo ni kama sote tupo sawa ila sasa utofauti unakuja hapa..

Kuna wale wezi ambao huiba kwa akili na wasistukiwe na wananchi (kama mimi endapo nitapata nafasi) , na pia kuna wale wezi wa waziwazi, watumia mabavu pasipohitajika, wanyang'anyi na mostly hawatumii akili (sabaya, bashite nk nk.)
Hawa chawa walijua baba yao ataishi milele wakaamua kuwatenda watz.
 
... hiyo ni hulka ya binadamu sio watanzania tu; duniani kote binadamu ni wabinafsi sana. Kwa kutambua hulka hiyo ya kibinadamu; nchi zenye watu wenye akili huhakikisha wanaweka miundo ya kuwadhibiti wenye nafasi za kula ili wasile wakavimbiwa; tena imeandikwa "toshekeni na mishahara yenu". Kutoatoa vitamko vya "kuwakanya" walafi bila kuwa na strict measures hasaidii; binadamu ni viumbe wa ajabu. Nchi kama China wana measures zao tena ni kali kweli kweli.

... sisi sio lazima tufuate njia ya China au kwingineko wenye adhabu kali; bali tuanze kuboresha sheria mama - Katiba. Baadhi ya wenzetu hawataki kuona hilo linatokea; kwanini? Kwa sababu Katiba ilyopo inawahakikishia kufaya ufisadi bila bugudha; na hata akiingia mwingine kwa Katiba hii huenda akawa fisadi haswa! Katiba Mpya ni hatua muhimu ya kuanza nayo.
Hapa kwenye upigaji ishu sio katiba ni tabia yetu halisi.
Watz wengi wamewapiga wawekezaji unawajua wale mapapaa wa mjini Magufuli aliwapukutusha wote wengine wakakimbia nje kina papa msofe,jack pemba nk ni wapigaji wa kimataifa.
China au ulaya ukifanya ufisadi umepotea sheria zao ni kali.
Kama makengeza anatamba wa kumkamata wapo wa kumfunga hayupo si kaona udhaifu wa sheria zetu, thus KILA dili kubwa yupo hadi ukawepo msemo ukitaka kupiga dili kubwa piga na chenge utakuwa salama.
 
Hapa kwenye upigaji ishu sio katiba ni tabia yetu halisi.
Watz wengi wamewapiga wawekezaji unawajua wale mapapaa wa mjini Magufuli aliwapukutusha wote wengine wakakimbia nje kina papa msofe,jack pemba nk ni wapigaji wa kimataifa.
China au ulaya ukifanya ufisadi umepotea sheria zao ni kali.
Kama makengeza anatamba wa kumkamata wapo wa kumfunga hayupo si kaona udhaifu wa sheria zetu, thus KILA dili kubwa yupo hadi ukawepo msemo ukitaka kupiga dili kubwa piga na chenge utakuwa salama.
... tabia ni lazima ziwe na namna ya kuzidhibiti zisivuke mipaka iliyokubalika katika jamii. Tool ya kudhibiti tabia kiserikali ni sheria na Katiba ni sheria mama.
 
Na ni nini kinakwamisha wote wasile labda.......au umehalalisha wengine kufa njaa.
 
... tabia ni lazima ziwe na namna ya kuzidhibiti zisivuke mipaka iliyokubalika katika jamii. Tool ya kudhibiti tabia kiserikali ni sheria na Katiba ni sheria mama.
Walinda sheria ndio wavunja sheria tutawajibisha vipi walinde sheria!
 
Kwa hii Post Unakuwa umewakosea sana Heshima.watu waliotumikia hili taifa kwa uaminifu na bila kuiba ingwaje walikuwa kwenye nafasi za kufanya uovu huo. Kila mtumishi angekuwa fisadi kama hao mnaowapigia chapuo, hii nchi ingekuwa ya mwisho duniani. Isinge sogea hata hizi hatua tulizopiga. Usingeona hizi huduma zikisogea mpaka pale kijijini kwako. Amini kuwa kuna Wazalendo kindakindaki wa hili taifa wanaolipigania kila siku, wengine hata kuuwawa na hao mnaowapigia chapuo wasizomewe. Na Hoa wazalendo wa namna hiyo wameamua kukaa kimya kwakuwa kila wanapofungua mdomo, hugeukwa na watu kama nyinyi ulioandika post hii na kusema wana wivu ama wamekosa. #Wazalendo wa Taifa Hili wapo.
Mungu awapiganie kama wapo!!!
 
Sawa, wacha tuendelee kuwaonea wivu wanaotuibia, hata huko mtaani mwizi akikuibia usipate hasira na chuki kiasi mkaanza kumpiga, we muonee tu wivu huku ukimuacha anaondoka zake, maana huwezi kupiga mtu kisa unamuonea wivu
Sasa kama wewe tabia zako ni mwizi kwanini umsulubu mwizi mwenzio!!?
 
Back
Top Bottom