Watanzania hawana uhakika kuhusu matumizi ya mapato yatokanayo na Tozo

Watanzania hawana uhakika kuhusu matumizi ya mapato yatokanayo na Tozo

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Imeelezwa kuwa Wananchi wengi hawana uhakika kuhusu matumizi ya mapato yatokanayo na tozo kwani 42% wanasema kuwa hawajui yanatumikaje ikilinganishwa na 38% ya wanaosema wanajua namna mapato hayo yanavyotumika.

Hii ni kwa mujibu wa Ripoti mpya ya Shirika lisilo la Kiserikali la TWAWEZA ambalo limefanya uzinduzi wa matokeo ya utafiti mpya wa Sauti za Wananchi ambao umeangazia maoni ya Wananchi kuhusu uchumi kwa jumla na hasa tozo ya miamala ya pesa kwa njia ya simu.

Takwimu hizo ambazo zimekusanywa kutoka kwa wahojiwa 3,000 kuanzia Oktoba na Novemba 2021 na Juni na Julai 2022, pia zianaonesha kuwa Wananchi wanaonesha dalili kuwa wangeunga mkono zaidi Tozo hizo iwapo wangekuwa na taarifa kamili kuhusu matumizi ya Fedha zinazokusanywa.

Asilimia 63 wanasema wangekuwa tayari zaidi kulipa tozo iwapo wangeweza kufuatilia matumizi, huku asilimia 39 wanasema wanajua pesa zinatumikaje.

Je, unajua mapato ya Tozo yanapokwenda?
 
Tozo ni hela ndefu sana inakusanywa kwa mwezi nahisi zaidi ya billion 100! Cha ajabu utakuta 40B ndio inaenda kwenye serikali 60B inaenda uswizi! Ni ngumu sana kwa CCM kuongea ukweli
 
Jionee matumizi ya kodi ya mwananchi mlipa kodi wa France mwaka 1848 - 49 soma zaidi source : French Government Budgets 1848-49 | Online Library of Liberty

French Government Budgets 1848-49

1661424718094.png


Ikiwa kuna maandiko / machapisho ya taarifa toka mwaka 1848 kuhusu bajeti ya Ufaransa ingekuwa jambo jema pia media zetu zikachambua taarifa za NBS kuhusu keki ya taifa inavyoliwa kwa maandishi na taarifa-picha ili wananchi waelewe kodi yao inatumika vipi.

Ikiwa zoezi kubwa kama sensa limeweza kupewa nafasi kubwa ktk kutangazwa, basi ifuatwe na kila mwaka matumizi ya kodi ya mwananchi ijulikane asilimia ngapi imeenda ktk huduma gani n.k n.k

Picha: Sensa ya 2022 ikiendekea
tujitokeze kuhesabiwa

1661426063423.png
 
Naamini wasio na uhakika na mapato ya tozo yanapokwenda ni zaidi ya hiyo percentage waliyoweka, wameona aibu tu.

Mwanzo Mwigulu alikuwa anatuambia kila mwezi wamekusanya ngapi, na zitaenda wapi, kwa kazi gani, lakini siku hizi wanakusanya tu, hawatuambii kiasi walichokusanya kila mwezi wala wapi wanakozipeleka, huu ni wizi tu.

Halafu nimeona upande mwingine wanasema watanzania 39% hawapendi kulipa kodi, sasa kama hizo tozo wanazokata hawatuambii wanakozipeleka, hizo kodi ndio wataacha kuzichezea? haya yote wanayataka wenyewe wakina Mwigulu.
 
Tatizo kwenye matumizi na ufujaji wa fedha
SAHIVI INABIDI WANANCHI WAWE WANAHOJI WAKIONA NDIVYO SIVYO

ova
 
Tozo ni hela ndefu sana inakusanywa kwa mwezi nahisi zaidi ya billion 100! Cha ajabu utakuta 40B ndio inaenda kwenye serikali 60B inaenda uswizi! Ni ngumu sana kwa CCM kuongea ukweli
Duh !!!
 
Umasikini nchini Tanzania

1661426847335.png


Ramani inaonesha eneo kwa eneo kaya zilivyo masikini nchini Tanzania huku mkoa wa Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Kilimanjaro ikionesha kuwa na idadi ndogo ya kaya masikini kwa ujumla wake ikilinganishwa na mkoa wa Kigoma, Ruvuma au mikoa iliyo kanda ya ziwa yenye umasikini uliokithiri wa kujirudia kwa maana mtu anaweza kujinasua kutoka ktk lindi la umasikini uliikithiri lakini miaka mitano baadaye akajikuta tena amerejea ktk ule umasikini aliokuwa nao kabla.

There is substantial regional variation beyond Dar es Salaam. We visualize regional patterns in persistent poverty, vulnerability, and movements out of poverty with the help of maps.9 Figure 4 shows the spatial distribution of persistent poverty, which ranges between 4.40% in Kilimanjaro and 23.50% in Kigoma.

In general, the situation in the northwest of the country is more dramatic, with persistent poverty consistently above 15%, levels reached only in Singida (center) and Ruvuma (south) outside that area. On the contrary, Dar es Salaam, Pwani, and Morogoro are regions with a more favorable outlook, with persistent poverty rates below 10%.

Source: https://onlinelibrary.wiley.com/doi/full/10.1111/rode.12829
 
Katika utafiti uliofanywa na @Twaweza_NiSisi umeonyesha matatizo makubwa 3 yanayowakabili Watanzania ni
1. Kupanda kwa gharama za maisha
2. Ukosefu wa ajira na kipato
3. Ukosefu wa chakula hasa maeneo ya vijijini.

Screenshot_20220825-151256.jpg
 
Wengi wa wanaosema hawajui huwa hawatafuti taarifa kwa hiyo hakuna Serikali ya kuwapigia simu kuwaeleza matumizi yake kwa sababu matumizi yake yalishawekwa bayana.

Wengine ukiwaeleza Kazi Yao ni ubishi tu, sasa hili la ubishi ni ujinga wao hakuna wa kuhangaika na ujinga wenu..

Mwisho anayesema hajui hajaamua kujua.
 
Back
Top Bottom