Watanzania ilitokeaje mkaishia kubadilishiwa kibao na Barrick kwenye madini, hadi mkaangukia pua?

Hiyo pesa haikupotea siku moja, ni kwa kipindi cha miaka mingi kwa kupitia usafirishaji wa makinikia walikua wanadanganya kwamba ndani kuna kiasi kidogo cha madini kumbe ni kiasi kikubwa, ni kwa kipindi cha zaidi ya miaka kumi au zaidi, sio kwamba hiyo pesa wanayo.

Ni sawa na kumuweka mfanyakazi wako dukani na kila siku akawa anaiba mia tano, baada ya miaka kumi ukapiga hesabu ukakuta jumla ya pesa aliyoiba ni million 200, hiyo haina maana kwamba anazo hizo pesa, alikua anaiba na kuzitumia.
 

..Nilikwambia uchukue calculator ujaribu kucheza na numbers kidogo ili ujue uhusiano kati ya usd 191 billion vs usd 300 million. Did you do that? Kwasababu hapo ndipo msingi wa hoja ulipo; kama tumefanikiwa au tumelaliwa.

..Hoja ya pili ni mahusiano ya Barrick na Acacia. Ni makosa kuamini kwamba waliotuibia ni Acacia, wakati 64% ya kampuni hiyo inamilikiwa na Barrick. Serikali imekuwa ikiwapumbaza na kuwalaghai wananchi kuhusu suala hili.

..Hoja ya tatu ni kwamba hakuna mtu mwenye akili timamu dunia hii ambaye anaibiwa usd 191 billion halafu anakubali na anaridhika kulipwa usd 300 million. Malipo ya usd 300 million ni kidogo sana kama tuna uhakika na madai yetu ya awali.
 
Kwahiyo kama hawawezi kulipa ulitaka tufunge mgodi?, kama mfanyakazi wako alikuibia kidogo kidogo baada ya miaka kadhaa ukagundua ameiba pesa nyingi na hana uwezo wa kulipa utafunga biashara?. Kama ni wewe ndio rais ungechukua hatua gani?
 
Kwahiyo kama hawawezi kulipa ulitaka tufunge mgodi?, kama mfanyakazi wako alikuibia kidogo kidogo baada ya miaka kadhaa ukagundua ameiba pesa nyingi na hana uwezo wa kulipa utafunga biashara?. Kama ni wewe ndio rais ungechukua hatua gani?

..Barrick waliingia Tanzania mwaka 1999.

..Na ripoti ya kusema wameiba usd 191 billion ilitoka mwaka 2017.

..maana yake wizi huo umetokea ktk kipindi cha miaka 18.

..sasa ukichukua 191 billion ukagawanya kwa miaka 18 utapata usd 10.6 billion.

..hayo ni mahesabu ya kitoto kwamba tulikuwa tukiibiwa usd 10.6 billion kila mwaka.

..wewe kwa akili zako unaamini ni halali tulipwe usd 300 million?

NB:

..madai yetu yatakuwa ni ya kweli, au ni ya uongo.

..kama ni ya KWELI, basi we sent a very weak team to negotiate with Barrick.

..Na tunatakiwa tuunde timu nyingine, na majadiliano yaanze upya.

..kama madai yetu ni ya UONGO, tunatakiwa tuelezwe madai ya kweli.

..Na waliotoa madai ya uongo wachukuliwe hatua.

cc MK254
 
Baric hawakukataa hayo madai, wao wslichosema ni kwamba hiyo pesa sio rahisi kulipika ila watakachofanya ni kuwaondoa na kuvunja ubia waliokua nao na Acacia ambao ndio wahusika wakuu walifanya hilo kosa, wao kuonyesha kujutia hicho kitendo wakasema tutalipa $300 kama kutuomba msamaha sio "sio malipo ya hicho kiasi, ila ni kama ishara ya unyenyekevu na kuahidi kurekebisha na kuanza mahusiano mapya ya win win relationship.

Kitu kimoja lazima ukubali kwamba kuna wakati mwengine unalazimika kusamehe kilichopotea ili upate kinachokuja, tungeendeleza hayo malumbano ya kudai hizo $190B, hadi leo mgodi ungekuwa imefungwa hakina kinachoendelea na hizo pesa pia tusingezipata.

Tumeanza upya baada ya maridhiano, hiyo pesa hawana uwezo wa kulipa, let's move on, kumbuka huu wizi ulianza katika kipindi cha Mkapa, sio rahisi kurekebisha kila kitu kilichotendeka awamu za nyuma.
 
Umetoa maelezo mazuri sana. Hao vibaraka BBC leo wameingia cha kike wakamuhoji msemaji mkuu wa serikali. Hajawabakizia neno kawajibu yale majibu magumu hawajazoea kupewa.
 
Bila Shaka Leo jumatatu umemsikia msemaji wa serikali Hassan Abbas akihojiwa na Salim Kikeke wa hiyo hiyo BBC. Hako kachambuzi ka. Chadema hovyo kabisa.
 
Umetoa maelezo mazuri sana. Hao vibaraka BBC leo wameingia cha kike wakamuhoji msemaji mkuu wa serikali. Hajawabakizia neno kawajibu yale majibu magumu hawajazoea kupewa.
Ni kweli. Nimeyasikia pia maelezo ya serikali kupitia msemaji wake Hassan Abasi. Yule mchambuzi uchwara wa madini atakuwa amejificha uvunguni mwa kitanda, hovyo kabisa kamjamaa kale.
 

..kusamehe usd 191 billion na kukubali kulipwa usd 300 million ni UPUMBAVU.

..ukiniambia madai yale yalikuwa ya si ya kweli, hivyo ilibidi tuyaweke pembeni nitakuelewa.

..lakini kama unaendelea kusisitiza kwamba madai yale ni ya kweli, basi ni UPUMBAVU wa kiwango cha juu kabisa kuwasamehe barrick.

..semeni ukweli ndugu zangu, kwani ukweli utawaweka huru.
 
Inshort sakata hili limemalizika hivo ajili ya kusitiri aibu za watangulizi maana magufuli angeendelea na sakata hili ni kama kuwavua nguo watangulizi wake na kulitoboa jahazi analosafiria ndo maana busara zikatumika tofauti na hapo hao washenzi walikua wanafungasha virago.
 
Bila Shaka Leo jumatatu umemsikia msemaji wa serikali Hassan Abbas akihojiwa na Salim Kikeke wa hiyo hiyo BBC...hako kachambuzi ka. Chadema hovyo kabisa...

Sijamskliza labda nitapata clip, tusaidie kuelewa amepanguaje hoja ya namna mlivyokubali kulegeza kutoka kwa bilioni 191 hadi kuja kwa milioni 300 ambazo na zenyewe hampewi kwa mpigo.

Jinsi mlitoka kwa USD 191,000,000,000 ambayo ni Tshs 439,300,000,000,000
Na kukubali 300,000,000 ambayo ni Tshs 690,000,000,000

Hivi unafahamu hiyo 191B ni kama ujumuishe chumi za mataifa yote EAC.
 

We nduguyetu/ jirani tuhurumie tu

Acha kutonesha vidonda mkuu
 

..nadhani wengi unaojadiliana nao hawaelewi uzito wa hiyo figure, usd 191 billion.
 

..zile ripoti zilikuwa zimetiwa chumvi kuwalaghai waTz.

..ndiyo maana majadiliano yalichukua muda mrefu kumalizika.

..na barrick / acacia waliweka mguu chini mpaka Prof.Kabudi akaamua kujiuzulu.

..utakumbuka alisema kwamba kazi ilimshinda ila wenzake walimkatalia kujiuzulu.

..na katika timu ya majadiliano Prof.Mruma na Prof.Ossoro walikuwepo.
 
Upo huru kusema lolote unalofikiria kwasababu kila mtu ana mawazo yake, serikali baada ya kukaa na kufikiria kwa undani iligundua hakukuwa na jinsi ya uwezekano wa hizo pesa kupatikana, busara zikawatuma kuanza upya kwasababu pia nchi yetu ilihusika kufanya uzembe katika upotevu huo, usimamizi na sheria zetu hazikuwa vizuri.

Kwako wewe unahisi ni upumbavu, upo huru kufikiria hivyo, ila kuna wengine wanaofikiria kwamba, kuendelea kung'ang'ania kitu ambacho unajua hakiwezikani kupatikana, ni sawa na kuacha kuizika maiti kwa kutegemea kwamba itafufuka, kuwa makini isije ikawa wewe ndio mpumbavu.
 
Upo huru kufikiria na kutoa mawazo yako, hiyo haina maana kwamba upo sahihi, ila maisha lazima yaendelee, nchi lazima tuendelee mbele, kumbuka hadi sasa ni 4% tu ya deposite ya dhahabu ardhini ndio hadi sasa iliyochimbwa.

Yaliyopita si ndwele tugage yajayo kwasababu tumejipanga upya ili kuhakikisha makosa ya nyuma hayajirudii, wewe endelea kupiga kelele kusubiri embe chini ya mnazi. Yaliyotokea hatuwezi kuyarudisha, tugange yajayo.
 
Kuna mtu keshaijibu hiyo namna hii



Kama ndugu zetu wa Kenya mkishindwa kujenga uhusiano mzuri na sisi ndugu na majirani; tutawapiga ban tena. hatuwezi kuishi na watu ambao kila siku ni chockochoko.
 
Siwezi kujadili figures ambazo zimeletwa kihuni ni ajabu Sana namna unavyowasilisha hoja kishabiki. Nadhani I am just wasting my time here..you will never understand because you are bent to project negativity to any issue concerning Tanzania and your method being information spinning.
 

Mnachekesha ujue, hizo figures mlizitaja wenyewe, mkasema kila Mtanzania atapata noah, leo mnasema hiyo ni spinning haikuwepo.
 
Mnachekesha ujue, hizo figures mlizitaja wenyewe, mkasema kila Mtanzania atapata noah, leo mnasema hiyo ni spinning haikuwepo.

Siku ripoti zinawasilishwa ikulu kulikuwa mpaka na wasanii wa kuimba.

Hivi umeona wapi ripoti ya uchunguzi, ya kitaalamu, uwasilishaji wake unatanguliwa na nyimbo za wasanii?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…