Watanzania ilitokeaje mkaishia kubadilishiwa kibao na Barrick kwenye madini, hadi mkaangukia pua?

Watanzania ilitokeaje mkaishia kubadilishiwa kibao na Barrick kwenye madini, hadi mkaangukia pua?

..na tangu ccm wayalete hayo makampuni tumeibiwa kiasi gani?

rais anaposema tumeibiwa sababu mnamchukia mnapinga,kwamba ni uongo hawatuibii.

sijui hapa unauliza kitu gani!!!
 
rais anaposema tumeibiwa sababu mnamchukia mnapinga,kwamba ni uongo hawatuibii.

sijui hapa unauliza kitu gani!!!

..tumeibiwa chini ya uangalizi wa ccm.

..leo hii Deo Mwanyika ceo wa acacia amepitishwa na ccm kugombea ubunge jimbo la Njombe mjini.
 
Punguza jazba mkuu, BBC au mtangazaji Zuhura soon wataomba radhi kwa upotoshaji, nothing new but cheap propaganda 'been there done that' , Dr Dre🙂

..lazima tuwe na jazba.

..ccm mmeshirikiana na makampuni makubwa kuiba madini yetu.

..tunataka mtueleze usd 191 billion mlizosema tumeibiwa na acacia ziko wapi?
 
Mlitakeje kwani? yaendelee tu kupita bandarini na mkoa wetu ubakie mashimo.

Unataka kutuambia sasa hivi hayapiti? Hembu fungua hiyo link ya BBC uwakatalie kwa evidence
 
kwa upande mwingine yule mchambuzi alikua anachambua kishabiki sana,alionekana kama ameegemea upande flani wazi wazi

Hoja hujibiwa kwa hoja ni jukumu lako kuzipangua hoja zake kama aliyoyasema ni ya uwongo.
Hembu tusaidie katika haya aliyoyasema,
Je Mkataba ulijadiliwa na bunge?
Je makinikia yanasafirishwa kwa mabeberu au hayasafirishwi?
Je kinu cha kuchenjua kimeshajengwa?
Je tumepokea hata hiyo usd 300m?

Hayo tu machache ndo unapaswa kuyapangua
 
..tumeibiwa chini ya uangalizi wa ccm.

..leo hii Deo Mwanyika ceo wa acacia amepitishwa na ccm kugombea ubunge jimbo la Njombe mjini.

hata maendeleo kiduchu yaliyopo ni kwa usimamizi wa ccm hiyo hiyo.
 
kwa upande mwingine yule mchambuzi alikua anachambua kishabiki sana,alionekana kama ameegemea upande flani wazi wazi
Kale kachambuzi ni kachadema kale...kanasema kwa kejeli eti tunawapigia magoti mabeberu...very stupid...halafu mtangazaji Zuhura Yunus au aliyemwandalia hataki ku-balance...analeta Sera za madini za chadema na Act Wazalendo lakini wanaacha makusudi Sera za CCM...halafu kale kachambuzi uchwara kanatamba peke yake bila kuwepo na upande wa pili kwa maana kutoka serikalini au wizara ya madini....Zuhura Yunus anatumiwa na mabeberu na Kama hakuandaa yeye Bali anasoma tu basi lipo tatizo kwake...BBC stupid..a biased media...unprofessional ....always working against third world countries...
 
Kale kachambuzi ni kachadema kale...kanasema kwa kejeli eti tunawapigia magoti mabeberu...very stupid...halafu mtangazaji Zuhura Yunus au aliyemwandalia hataki ku-balance...analeta Sera za madini za chadema na Act Wazalendo lakini wanaacha makusudi Sera za CCM...halafu kale kachambuzi uchwara kanatamba peke yake bila kuwepo na upande wa pili kwa maana kutoka serikalini au wizara ya madini....Zuhura Yunus anatumiwa na mabeberu na Kama hakuandaa yeye Bali anasoma tu basi lipo tatizo kwake...BBC stupid..a biased media...unprofessional ....always working against third world countries...

Kuna hoja ya mdau hapo juu post number 47 huyo naye utsema katumwa na nani, maana huwa mnaona kila anayewazidi kwa hoja lazima katumwa, hamuna weledi wa kupambana point kwa point

Duh: Bandugu Watz ilitokeaje mkaishia kubadilishiwa kibao na Barrick kwenye madini, hadi mkaangukia pua - BBC
 
Kuna hoja ya mdau hapo juu post number 47 huyo naye utsema katumwa na nani, maana huwa mnaona kila anayewazidi kwa hoja lazima katumwa, hamuna weledi wa kupambana point kwa point

Duh: Bandugu Watz ilitokeaje mkaishia kubadilishiwa kibao na Barrick kwenye madini, hadi mkaangukia pua - BBC
Huyo Hana hoja labda wewe uwe mgeni naye...huyo ni paid stooge to tarnish the image of Tanzania...hakuna hoja kwa suala Zima....Kama kungekuwa na hoja hiyo documentary au news analysis ingekuwa balanced...timing yake ndiyo inayowaumbua pia...anasummarize Sera za madini za vyama viwili vya upinzani lakini anaacha makusudi Sera ya madini ya chama tawala...hiyo ndiyo inaitwa information spin...professionals wa news media wanafahamu hiyo...stupid BBC...
 
Mpaka Magufuli mwenyewe anaogopa kuiongelea hiyo issue kwenye kampeni zake. Yaani ni aibu, hakuna cha kupata Noah wala bibi yake Noah.

Mabeberu wana akili sana, walimuacha Meko abwabwaje weee, alipochoka wakamtandika za uso na kuzisahau hata sheria zake alizozitunga kihuni.

Endeleeni kuokoteza maneno ya mtaani
 
..umeona anavyojiuma-uma kwenye kuelezea "kishika uchumba" cha usd 300 million?

..serikali ilisema tumeibiwa usd 191 billion, sasa imekuwaje tumekubali kulipwa usd 300 million, tena tunalipwa kidogokidogo?
Tulisema Acacia ndio walioiba hizo pesa, tukasema wakitaka kuendelea lazima walipe, wangekuwepo tungekubaliana terms za malipo kwasababu hata serikali ya Marekani haiwezi kutoa hiyo pesa kwa pamoja.

Acacia hawakuweza kulipa ikabidi wafukuzwe nchini, BARIC wakaomba kama kuonyesha heshima na kuomba msamaha kutokana na kosa walilofanya wadogo zao, wakaomba kutuangukia kwa $300M.

Suala la kulipa kwa mafungu, hiyo sio hoja kwasababu hao BARIC sasa hivi ni wabia wetu katika uchimbaji dhahabu kupitia kampuni ya Twiga Gold.

Kwani kulipa zote na kulipa kidogo kidogo kuna athari gani kwa Tanzania?, kama tunafanya kazi kwa pamoja kama Partners na wameomba kulipa kwa mafungu, kuna ubaya gani au mnataka kuendelea uhasama kwa mtu mnayefaya kazi kama Partner?
 
Tulisema Acacia ndio walioiba hizo pesa, tukasema wakitaka kuendelea lazima walipe, wangekuwepo tungekubaliana terms za malipo kwasababu hata serikali ya Marekani haiwezi kutoa hiyo pesa kwa pamoja.

Acacia hawakuweza kulipa ikabidi wafukuzwe nchini, BARIC wakaomba kama kuonyesha heshima na kuomba msamaha kutokana na kosa walilofanya wadogo zao, wakaomba kutuangukia kwa $300M.

Suala la kulipa kwa mafungu, hiyo sio hoja kwasababu hao BARIC sasa hivi ni wabia wetu katika uchimbaji dhahabu kupitia kampuni ya Twiga Gold.

Kwani kulipa zote na kulipa kidogo kidogo kuna athari gani kwa Tanzania?, kama tunafanya kazi kwa pamoja kama Partners na wameomba kulipa kwa mafungu, kuna ubaya gani au mnataka kuendelea uhasama kwa mtu mnayefaya kazi kama Partner?

..sasa kama aliyetuibia ni acacia kwanini tulipwe na barrick?

..hapo ndipo waTz tulipoanza kudanganywa, na waliofanya hivyo ni viongozi wetu wenyewe.

..haiwezekani serikali iseme acacia wameiba usd 191 billion, halafu bila maelezo ya kutosha tunakubali kulipwa usd 300 million.
 
..sasa kama aliyetuibia ni acacia kwanini tulipwe na barrick?

..hapo ndipo waTz tulipoanza kudanganywa, na waliofanya hivyo ni viongozi wetu wenyewe.

..haiwezekani serikali iseme acacia wameiba usd 191 billion, halafu bila maelezo ya kutosha tunakubali kulipwa usd 300 million.
Unapaswa ujue uhusiano uliopo kati ya ACACIA na Baric, Baric walinunua Hisa 64% za Acacia Tanzania. Kwahiyo kosa la Acacia lingeigharimu sana BARIC Kama wangefukuzwa nchini. Baada ya Acacia kushindwa kulipa na kufungashwa virago, Baric ilibidi kuingilia kati ili wao ndio wawe ni waendeshaji hiyo Migodi wakishirikiana na serikali.

Kinyume na hapo maana yake ni kwamba migodi ilikua ifungwe, kwahiyo tukakubali hiyo $300 ila kuanzia sasa hivi tugawane faida 50/50, na hayo mambo mengine mengi tuliyokubaliana, tunaanza upya.
 
Haya ni matokeo ya kuwa na kiongozi asiyejua kizungu anajikuta hana cha kuzungumza beberu linapomuomba maelezo anaishia kusema yes no of course corruption is cancer na vijimaneno vingine vya kitoto.
 
Unapaswa ujue uhusiano uliopo kati ya ACACIA na Baric, Baric walinunua Hisa 64% za Acacia Tanzania. Kwahiyo kosa la Acacia lingeigharimu sana BARIC Kama wangefukuzwa nchini. Baada ya Acacia kushindwa kulipa na kufungashwa virago, Baric ilibidi kuingilia kati ili wao ndio wawe ni waendeshaji hiyo Migodi wakishirikiana na serikali.

Kinyume na hapo maana yake ni kwamba migodi ilikua ifungwe, kwahiyo tukakubali hiyo $300 ila kuanzia sasa hivi tugawane faida 50/50, na hayo mambo mengine mengi tuliyokubaliana, tunaanza upya.

..wewe ni kati ya waliodanganywa.

..barrick ndiyo walioanzisha/waliounda kampuni ya acacia.

..na walipounda kampuni hiyo waliuza hisa chache, wakabakiwa ya 64% ya hisa.

..kwa hiyo ulangai na ujanja-ujanja wa kwanza kabisa ni barrick kujidai wao ni wasafi na acacia ndio wezi au wachafu.

..na serikali ndiyo walikuwa vinara wa uongo na propaganda kwamba barrick wana nia njema na waTanzania.

..huwezi kusema acacia wameshindwa kulipa? How? serikali itueleze usd 191 billion walizoiba acacia zimekwenda wapi? hiyo siyo hela ya chenji inayoweza kupotea kirahisirahisi.

..sijui kama unaelewa tofauti kati ya usd 191 billion na usd 300 million. Nakuomba uchukue calculator yako ujaribu kulinganisha viwango hivyo viwili. Ukishindwa nitakusaidia kukuelewesha.
 
Back
Top Bottom