Money Stunna
JF-Expert Member
- Aug 9, 2011
- 13,053
- 6,304
Kuna watu humu wanaleta matangazo ya Semina za siku moja kupata Masoko kwa gharama za Dola 700, zaidi ya Tshs. 1,260,000/=. Hawa watu hawana tofauti na matapeli wakubwa wanaotaka kupata utajiri wa siku moja kupitia kuwakamua nyie pesa zenu bila huruma kabisa.
Hizi Semina za biashara gharama inabidi ikiwa kubwa iwe 30,000/= - 50,000/= Tshs. mwisho, isizidi hapo. Lakini ukiona mtu anawambia Dola 700, ujue huyo ni 419 anayetaka kupata utajiri mkubwa kupitia pesa zenu na wengi wanakuwa hawana hata biashara zaidi ya kutapeli.
Hata hao wenye biashara pia wanaowakamua hizo Dola, ujue utajiri wao wa mashaka ni 419. Utatozaje mtu pesa yote Hiyo!? Huo ni mtaji kabisa!
Kuweni makini, ni hayo tu..
Hizi Semina za biashara gharama inabidi ikiwa kubwa iwe 30,000/= - 50,000/= Tshs. mwisho, isizidi hapo. Lakini ukiona mtu anawambia Dola 700, ujue huyo ni 419 anayetaka kupata utajiri mkubwa kupitia pesa zenu na wengi wanakuwa hawana hata biashara zaidi ya kutapeli.
Hata hao wenye biashara pia wanaowakamua hizo Dola, ujue utajiri wao wa mashaka ni 419. Utatozaje mtu pesa yote Hiyo!? Huo ni mtaji kabisa!
Kuweni makini, ni hayo tu..