Watanzania mkifika nje ya nchi jiandikisheni Ubalozini. Ona lawama kibao kwa Serikali wakati Ubalozi haujui kuwa wengi mko Ukraine

Watanzania mkifika nje ya nchi jiandikisheni Ubalozini. Ona lawama kibao kwa Serikali wakati Ubalozi haujui kuwa wengi mko Ukraine

Kwani wakati wana ondoka wana pitia wapi serikali isijue? Ofisi za uhamiaji pale airport zina kazi gani? Mbona wana tuhoji paka jina la wife na watoto kijiji shughuri kwanini wasijue idadi ya watu. Serikali zetu hamna kitu kama vitamburisho vya taifa kutoa ni shida ndo waweze hilo.
Kwahiyo, kwa maelezo yako hayo ndo unatarajia nchi fulani kukitokea vita basi serikali ianze kupekua watu walipita kwenye airports zetu kwenda kwenye hizo nchi, ama?

Tuchukulie hii issue ya Ukraine kwa mfano... je, serikali ianze kupitia orodha ya miaka mingapi nyuma?! Na ukishapitia, utakuwa na uhakika gani kwamba bado wapo Ukraine?!

Hivi unajua unachokiongea?!

Na wakati mwingine, unakuta watu wametoka Bongo, say to Russia kwa ajili ya masomo. Wakimaliza masomo yao, wanajichanganya huko kwa huko... ndo hapo unakuta mtu kaondoka Bongo kuelekea Russia lakini baada ya kumaliza masomo yake, anaenda kutafuta maisha, say, Georgia au Maldova!!

Sasa watu kama hao unatapata wapi taarifa zao wasipoenda kuripoti ubalozini?
 
Kama si jukumu la ubalozi kupata ripoti ya raia was Tanzania walio tembelea nchi fulani basi jukumu hilo liongezwe haraka.
Na ukizingatia kwa sasa passports zimekuwa za kidijitali zaidi basi inakuwa rahisi kwa ofisi za ubalozi kusync taarifa kwa haraka na usahihi kabisa.

YEHODAYA hoja Yako ni nzuri but ni typical analog. Na ukizingatia umbali, muda, majukumu/dhumuni la safari na gharama mtu huwezi kwenda kujiandikisha ubalozini.
Imagine upo mji X na ubalozi wa Tanzania upo mji Z au nchi AA tofauti kabisa.
Hizo gharama nani anahusika??
Nchi zote raia ndo wajibu wa kwenda kujiandikisha kwenye ubalozi wao wa karibu!!!

Una-track track vipi as if mtu akisema kwa mfano anaenda UK, basi ndo atabaki hapo hapo UK maisha yake yote?

Mtu atatoka TZ hadi UK. Anaishi UK kwa miaka kadhaa anaamua kwenda kutafuta maisha sehemu nyingine, say Poland! Anapiga mishe zake akiona mambo hayasomeki, anaenda zake Russia, na baada ya muda huyooo, yupo Kyiv!!

Kwahiyo serikali ifanye kazi ya kuku-track kote kwa sababu zipi hasa?!

Kila mwenye akili timamu anaposafiri anajua akipata tatizo lolote sehemu anayotakiwa kukimbilia ubalozini! Sasa ikiwa hata mwenyewe hufahamu umuhimu wa ubalozi wako, nani afanye kazi ya kuku-track kila unapoenda kama Faru John wakati unajua umuhimu wa ubalozi wako?!
 
Nchi zote raia ndo wajibu wa kwenda kujiandikisha kwenye ubalozi wao wa karibu!!!

Una-track track vipi as if mtu akisema kwa mfano anaenda UK, basi ndo atabaki hapo hapo UK maisha yake yote?

Mtu atatoka TZ hadi UK. Anaishi UK kwa miaka kadhaa anaamua kwenda kutafuta maisha sehemu nyingine, say Poland! Anapiga mishe zake akiona mambo hayasomeki, anaenda zake Russia, na baada ya muda huyooo, yupo Kyiv!!

Kwahiyo serikali ifanye kazi ya kuku-track kote kwa sababu zipi hasa?!

Kila mwenye akili timamu anaposafiri anajua akipata tatizo lolote sehemu anayotakiwa kukimbilia ubalozini! Sasa ikiwa hata mwenyewe hufahamu umuhimu wa ubalozi wako, nani afanye kazi ya kuku-track kila unapoenda kama Faru John wakati unajua umuhimu wa ubalozi wako?!
(Usiwe unajibu kwa jazba utafikiri umekuwa forced kujibu).
Tuliza akili utaona logic. Fahamu tu kuwa Kila mtu anafahamu umuhimu wa ubalozi. Ninachokiona ubalozi ndo haufahamu umuhimu wa watu wao!
Mbona tuna uwezo wa ku-track watalii waingiao na kutoka nchini? Na nchi zao tunaorodhesha?? Siamini Tunashindwa kuwa na data kujua Watanzania wangapi wako Russia au Ukraine kwa sasa??
Passports zishie tu kufacilitate entry and exit.
We need to improve the way things work!!
 
Watanzania mkifika nje ya nchi jiandikisheni ubalozini ona sasa lawama kibao kwa serikali wakati ubalozi hauwajui wengi wenu kuwa mko Ukraine serikali iwasaidieje wakati mliingia kimya kimya kama vibaka.

Nchi za wenzetu wakifika wananchi walienda hutoa report ubalozini kuwa wako nchi hiyo si lazima waseme kwa shughuli gani wana report kuwa wapo mji fulani eneo fulani.

Kureport ni bure aweza report hata kwa Email ukiambstanisha copy ya Passport yako na contacts zako
Likitokea la kutokea Balozi wanajua afanyaje na awasilianaje na wewe

Watanzania lawama kibao kwa Serikali zimekuwa zikitolewa mfano mavurugu yalipotokea Afrika kusini serikali ililaumiwa na la Ukraine serikali inalaumiwa lakini ukienda register ya Watanzania waliojisajili ubalozini aweza ikuta tupu. Kelele zinalipuka tu nyumbani oh Serikali iokoe watanzania walioko Ukraine mbona nchi zingine wanaokoa.Nchi hizo zingine wana Rekodi za watu wao kule ndio maana rahisi

Sasa balozi mlitaka apite na gari ya matangazo mira ya Ukraine kutangaza kuwa kama kuna mtanzania aje gari ya matangazo yupo balozi hapa wakati mabomu ya Urusi yanarindima?

Tubadilike

Ubalozi Ukraine unajua uko wapi mjomba?
 
Hata ungekuwa mbali huwezi jiandikisha online kwa email?

Umeshawahi kufika au kuwasiliana na ofisi yoyote ya ubalozi wa tz kwenye nchi yoyote?

Unavijua vipaumbele vyao?

Hujawahi kusikia malalamiko dhidi yao?
 
Ngoja twende Taratibu unataka ubalozi ukupe inauli au? Ndugu zako Tanzania wote walifariki dunia hawawezi kuchangiana wakupe tickets au? Msaada gani unataka ubalozini ? Fafanua wazi
Huna akili, na unaonekana hujawahi kutoka nje ya TZ
 
Watanzania mkifika nje ya nchi jiandikisheni ubalozini ona sasa lawama kibao kwa serikali wakati ubalozi hauwajui wengi wenu kuwa mko Ukraine serikali iwasaidieje wakati mliingia kimya kimya kama vibaka.

Nchi za wenzetu wakifika wananchi walienda hutoa report ubalozini kuwa wako nchi hiyo si lazima waseme kwa shughuli gani wana report kuwa wapo mji fulani eneo fulani.

Kureport ni bure aweza report hata kwa Email ukiambstanisha copy ya Passport yako na contacts zako
Likitokea la kutokea Balozi wanajua afanyaje na awasilianaje na wewe

Watanzania lawama kibao kwa Serikali zimekuwa zikitolewa mfano mavurugu yalipotokea Afrika kusini serikali ililaumiwa na la Ukraine serikali inalaumiwa lakini ukienda register ya Watanzania waliojisajili ubalozini aweza ikuta tupu. Kelele zinalipuka tu nyumbani oh Serikali iokoe watanzania walioko Ukraine mbona nchi zingine wanaokoa.Nchi hizo zingine wana Rekodi za watu wao kule ndio maana rahisi

Sasa balozi mlitaka apite na gari ya matangazo mira ya Ukraine kutangaza kuwa kama kuna mtanzania aje gari ya matangazo yupo balozi hapa wakati mabomu ya Urusi yanarindima?

Tubadilike

Wewe ni mjinga kabisa unafikiri ofisi za uhamiaji kazi yake nini?
 
Kwa watanzania waliopo nje ya nchi, wanataka kufanya ujenzi na kusimamiwa ujenzi wao.
Basi wasiliana na Smart Ujenzi .

Tutakuandalia
1: Ramani za nyumba na majengo mbali mbali.
2:Tathmini nzima za gharama za ujenzi wako.
3. Tutakujengea na kusimamia ujenzi wako Kwa uaminifu na ubora.
4:Tutasimamia na kufuatilia Kila shughuli itayohitajika kwenye ujenzi wako.

Wasiliana nasi Whatsapp 0762-704-031 /0654-704-031.
Engineer Wilson M.M

Karibu ujenge nasi Leo.
 
Back
Top Bottom