Watanzania mnajua kuhusu Bandari mpya Bagamoyo?

Watanzania mnajua kuhusu Bandari mpya Bagamoyo?

BONGOLALA

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2009
Posts
16,508
Reaction score
11,897
Eneo litakalojengwa bandari mpya Bagamoyo ni lile lile ambalo chuo cha uvuvi mbegani kipo. Waalimu wanasema mamlaka ya bandari imeahidi kujenga chuo kingine eneo ambalo hawajajua ni wapi. Ikumbukwe kuwa chuo kile ni cha aina yake Afrika Mashariki, kati na Kusini, kuna wanafunzi toka nchi mbali mbali.

Pia chuo hicho kilijengwa mwaka 1972 na baadae wa Norway wakakikarabati kwa majengo ya kisasa na zana za kisasa za kufundishia kama boat za uvuvi na cold rooms. Je, leo hii wa Norway wakisikia chuo ambacho tulitumia maneno matamu kuomba msaada na wao wakatumia kodi za wananchi wao kutujengea, kimevunjwa na kupewa mchina kwa matumizi mengine watatuelewaje?

Na serikali imelisema hili kwa watanzania tukakubali chuo kuvunjwa? Ikumbukwe tunahitaji sana wataalamu wa mambo ya uvuvi kwani tuna ukanda mkubwa wa bahari na maziwa lukuki! Kwa nini huyo mchina asipewe eneo jingine aanze upya ujenzi wa miundombinu? Pale chuo kuna maji safi ya dawasco, kuna umeme mkubwa, kuna gati ndogo, pia kuna barabara ya lami toka main road ya kuelekea Bagamoyo-Dar, kuna nyumba za waalimu na madarasa, maabara, mabwawa ya samaki wa shamba darasa.

Yaani hapo mchina hatawekeza chochote zaidi ya kuweka mashine za upakuaji mizigo na kuanza kuvuna! Hii ni sawa na serikali ilipotaka kuuza jengo la mahakama ya rufaa ili kupisha ujenzi wa hotel-kempinsk. Wabunge, Wananchi tunalijua hili na tumeridhika na uamuzi huo wa kukiua chuo?

Ninavyo jua mamlaka ya bandari-TPA kujenga hicho chuo sehemu nyingine ni hadithi kwani vya kwao wenyewe vinakufa wameshindwa kuviendesha. Kama ni hivyo mchina ajenge kwanza chuo cha kisasa zaidi ya kile ndipo aende mbegani kuanza ujenzi wa bandari.

Mkataba unasemaje juu ya hili?

Nawasilisha.
 
Wewe unasema mambo ya chuo akipatikana hata mwekezaji wa kuhamisha Ikulu ya Magogoni mbona inawezekana tu. Lipo swali la kiuchokonozi, Tanzania imebarikiwa kuwa na kila kitu ispokuwa kitu kimoja tu Je wakijua hicho ni kitu gani

Tafakari!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Acha uchonganishi mkuu.
Hivi unaweza hamishwa kupisha ujenzi alafu usilipwe fiadia?tumia akiri kutupia bandiko!

Join Date : 20th February 2012
Posts : 2,899
Rep Power : 923
Likes Received304
Likes Given0

number of post @ sh. 7,000/=
2,899x 7,000= 20,293,000

Acha wenye uchungu wa rasilimali za nchi waanike uozo!!
 
Acha uchonganishi mkuu.
Hivi unaweza hamishwa kupisha ujenzi alafu usilipwe fiadia?tumia akiri kutupia bandiko!

kwani hakuna eneo jingine ktk bahari ya hindi mpaka chuo kivunjwe?watakao kosa elimu watalipwa kwa fidia?
 
kwani hakuna eneo jingine ktk bahari ya hindi mpaka chuo kivunjwe?watakao kosa elimu watalipwa kwa fidia?
Subiri bandari ianze kujengwa kwanza kisha njoo u post kama chuo kimejengwa kwingine au lah!

Usipandikize chuki kwa wananchi na serikali mkuu,Ebu tushirikiane kuilinda nchi yetu.
 
hyo ndiyo tz bwana wanauza hata ambavyo haviuziki. ngoja tusubili mana hii serikali ya bagamoyo yaweza kuwa kweli.
 
Subiri bandari ianze kujengwa kwanza kisha njoo u post kama chuo kimejengwa kwingine au lah!

Usipandikize chuki kwa wananchi na serikali mkuu,Ebu tushirikiane kuilinda nchi yetu.
Tuambie mkuu itajengwa eneo gani?mimi nipo hapa chuoni sasa hivi watu wanajipanga kuondoka
 
Hata mimi ningeenda kuomba hiyo kazi, hao wanalipwa 7000 kwa siku na number of posts...

Terms & condition utaziweza, mfano;
1. Kuwa mnafiki?
2. Mfitini
3. ujitoe kutetea Mafisadi kwa hali yoyote ile
4. ...............
5.................
6.................
7.................
8.................
9.................
10...............
 
We unaongelea kupewa eneo jingine? Me naongelea kuboresha bandari tulizo nazo. Hii ya Dar is just to the next door, tunahitaji nyingine hapo au tuendelee kuBWAGAMOYO?
 
Mie mamuzi ya baba mwanahasha yamenichosha kweli, yani huwa simwelewi kila kukicha zengwe analizua kwani mama cholo huwa hamshauri jamani hivi kweli amekosa pahala pa kujenga mpaka avunje chuo hicho majanga.
 
Bandari haiwezi jengwa popote, kwani hutegemeana na kina cha maji, na mambo mengine. bali chuo chaweza jengwa popote, hata SUA kuna kozi za ufugaji samaki wakati hawako ufukweni mwa bahari, ziwa wala Bwawa. tatizo sio chuo kuhama, mbona kambi ya jeshi Buhemba ilihama kupisha mgodi? tatizo ni pale ahadi za kujenga chuo kingine zisipotimia, na katika hilo hatuwezi kujadili sasa.
 
Unaongelea kuhamisha chuo watu wanahamisha kambi za jeshi na magereza sembuse CHUO

FEDHA ILIONGEA
 
Upanuzi wa bandari za Mtwara na Tanga zipo katika upembuzi yakinifu!ila Mh.Membe akiwa rais tutaanza kujenga Bandari ya Kilwa
 
Acheni bandari ijengwe ije ituletee faida baadae, chuo kitajengwa tu popote pale, kama chuo ni cha serikali basi for sure wanayo solution tayari. lakini kwa wale wa icho chuo kama wanajifunza uvuvi si waende kwa wakojani, mana wale jamaa wanavovua mpaka unashangaa!
 
Wewe unasema mambo ya chuo akipatikana hata mwekezaji wa kuhamisha Ikulu ya Magogoni mbona inawezekana tu. Lipo swali la kiuchokonozi, Tanzania imebarikiwa kuwa na kila kitu ispokuwa kitu kimoja tu Je wakijua hicho ni kitu gani

Tafakari!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Kuna haja ya KUTANGAZA INTERNATIONAL TENDER YA UONGOZI WA NCHI HII!!!! Kama zinavyotangazwa hizo tenda za WAWEKEZAJI WA NJEE ZINAZOTUCHANGANYA SASA
 
Back
Top Bottom