MUTUYAMUNGU
JF-Expert Member
- Jan 25, 2014
- 1,825
- 4,374
- Thread starter
-
- #21
Kweli kabisa mkuu.Na exposure vile vile. Wakenya hadi wanaotoka vijijini utawakuta wametapakaa nchi mbalimbali duniani to tofauti na wabongo ambapo ukimkuta nchi za mbali basi atakuwa ametoka kwenye miji mikubwa. Halafu kumbuka mtu anakwenda kufundisha University sio vichocholoni hivyo hiyo English yake lazima iwe imenyooka kuanzia kwenye interview
Primary na secondary za Uganda na South Africa nyingi wanafundisha kiswahili sasa hivi. Wizara ya mambo ya nje na Wizara za kazi+uhamiaji wawawezeshe watanzania.Kiinglish hatujui kiswahili tabu....yani ni shida juu ya shida, wanaoharibu kiswahili wakabidhiwe kwa bwana nchemba atajua cha kuwafanya
Primary na secondary za Uganda na South Africa nyingi wanafundisha kiswahili sasa hivi. Wizara ya mambo ya nje na Wizara za kazi+uhamiaji wawawezeshe watanzania.Kiinglish hatujui kiswahili tabu....yani ni shida juu ya shida, wanaoharibu kiswahili wakabidhiwe kwa bwana nchemba atajua cha kuwafanya
Tanzania kupata tu hiyo passport utaita maji mmaa!Sio kibovu bali wenzetu wanacheza na fursa sisi tumelala!
Kuna oportunities nyingi sana za kufundisha kiswahili, kuna Nchi ambayo nipo, wakenya walikua wemeshikilia dept ya kiswahili lakini siku walipokutana na sisi Watanzania walisema nyinyi ndio mnajua kiswahili hadi leo wanaamini watamzania ndio tunaongea kiswahili fasaha na wanatafuta walimu sema sisi tumelala hatujiongezi!Tanzania kupata tu hiyo passport utaita maji mmaa!
Utaulizwa cheti cha kuzaliwa cha bibi yako na babu yako
Kweli mkuu tumelala sana. Ule moshi wa mwenge wa Uhuru umetupambaza sana. Uchawi wa Nyerere kibokoKuna oportunities nyingi sana za kufundisha kiswahili, kuna Nchi ambayo nipo, wakenya walikua wemeshikilia dept ya kiswahili lakini siku walipokutana na sisi Watanzania walisema nyinyi ndio mnajua kiswahili hadi leo wanaamini watamzania ndio tunaongea kiswahili fasaha na wanatafuta walimu sema sisi tumelala hatujiongezi!
Hujui tu! Tanzania hii kupata tu passport ni shughuli pevu,watu kukupa passport ni kama vile wanakupa roho!! Inakatisha tamaa hata pale watu wanapoamua kujiongezaKiingereza hatujui na lugha yetu adimu na adhimu kila siku tunaiharibu kwa kuingiza maneno ya kihuni. Tunakosa nafasi za kufundisha nje ya nchi pamoja na kazi za kutafsiri.
Tutumie lugha moja ili tupate nafasi za kufundisha Uganda, Rwanda, South Africa na kwingineko!
Uganda, Rwanda na South Africa waalimu wote wa kiswahili wanatoka Kenya!
Uchawi wa sisiemu!Kweli mkuu tumelala sana. Ule moshi wa mwenge wa Uhuru umetupambaza sana. Uchawi wa Nyerere kiboko
Tuwe aggressive kwenye kupambana kutafuta channels za nje!.tuaisubiri serikali ifanye kila kitu. Kama passport as long as wewe ni mtanzania utaipata tu.Kweli mkuu tumelala sana. Ule moshi wa mwenge wa Uhuru umetupambaza sana. Uchawi wa Nyerere kiboko
Kunana watu wana namba za NIDA tangu 2018 ila vitambulisho halisi hawajapewa hadi Leo. Hii ndio tzHujui tu! Tanzania hii kupata tu passport ni shughuli pevu,watu kukupa passport ni kama vile wanakupa roho!! Inakatisha tamaa hata pale watu wanapoamua kujiongeza
Apana/ HapanaAwezi/Hawezi
Atari/Hatari
Alusi/Harusi
Imehairishwa/imeahirishwa
L na R nazo huko ndio kuna hasara kubwa sana.
Balozi zetu kwa kweli hazitoi ushirikiano wa kutosha kwa Watanzania kuchangamkia fursa wamekazana na diplomasia tu.Ramaphosa katoa fursa kule South somo LA kiswahili lifundishwe ila balozi wetu kule MEJA JENERALI MILANZI anashangaa tu!
Siyo kulala kaka ,hizi ni kazi za Wizara ya Mambo ya Nje kupitia Balozi zetu, wewe umejua baada ya kwenda lakini kabla hujaenda hukujua, sasa ni Watanzania wangapi hatuzijui hizo nafasi, Wakenya wao walijua kupitia kwa watu wao.Kuna oportunities nyingi sana za kufundisha kiswahili, kuna Nchi ambayo nipo, wakenya walikua wemeshikilia dept ya kiswahili lakini siku walipokutana na sisi Watanzania walisema nyinyi ndio mnajua kiswahili hadi leo wanaamini watamzania ndio tunaongea kiswahili fasaha na wanatafuta walimu sema sisi tumelala hatujiongezi!
Nimekupata mkuu inaonekana kuna mambo mengi ya kubaniana nyuma ya pazia ila ni kawaida kwa ngozi nyeusi. Kikubwa ni kuendelea kupambana bila kutegemea wizara au serikali channels zipo na unaweza ukafanikiwa bila kutegemea mtu yoyote.Siyo kulala kaka ,hizi ni kazi za Wizara ya Mambo ya Nje kupitia Balozi zetu, wewe umejua baada ya kwenda lakini kabla hujaenda hukujua, sasa ni Watanzania wangapi hatuzijui hizo nafasi, Wakenya wao walijua kupitia kwa watu wao.
Tanzania kuna ukiritimba mkubwa mno kwenda nje kufanya kazi, vibali havitoki kwa wakati na kiurahisi. Roho mbaya na chuki binafsi zinaongoza kwenye ofisi nyingi hasa Wizarani. Chunguza chunguza ni nyingi kwa mtu anayekwenda nje kuliko anayeingia ndani.
Hakuna uwazi wa hizi nafasi pindi zinapotokea, wakati mwingine mtu anaona bora asiseme kwa kuwa hakuna mtu wake, wote wakose. Hii inapelekea kwenda kwa wengine.
Nikupe kisa. Kuna siku walikuja wageni katika Wizara moja hapa nchini wakihitaji wafanyakazi wa kwenda nao field kufanya nao kazi ya utafiti. Wakawaomba idadi wanayohitaji.
Wakawaonyesha scale ya mshahara wao. Aisee wale viongozi walipinga kwamba haiwezekani walipwe pesa yote hiyo kwasababu serikali hailipi hivyo. Wazungu wakashangaa na kusema hata kama ila sisi tumepangiwa tulipe hiki kiasi, kwahiyo siyo nyinyi mtalipa bali serikali yetu, wakaambiwa mkiwalipa pesa yote hii hawatafanya kazi watalewa tu.
Wazungu wakasema hatuwezi kurudisha pesa bila maandishi tutaonekana tumewadhulumu tupeni doc inayoonyesha kiwango hiki cha mshahara mmekipinga. Kweli bwana walipewa na pesa zikarudishwa.
Lengo la kufanyiwa mtima nyongo ni wivu kwasababu waliotakiwa kwenda field ni wafanyakazi wa ngazi za chini, hivyo basi waliona watalipwa pesa nyingi kuliko wao wakubwa. Ofisi nyingi wanafanya hivi, hiyo ni moja kwingine je penye ulaji mkubwa kukoje?
Ni kweli ngoja tupambane pasipo kukata tamaa yapo mambo huwa yanawezekana kwa kukomaa tu.Nimekupata mkuu inaonekana kuna mambo mengi ya kubaniana nyuma ya pazia ila ni kawaida kwa ngozi nyeusi. Kikubwa ni kuendelea kupambana bila kutegemea wizara au serikali channels zipo na unaweza ukafanikiwa bila kutegemea mtu yoyote.